Ni kifungu gani kinamlazimisha mwanaume wa kikristo kuwa na mke mmoja?

Hi Ladies, gentlemen and baharias
Naomba nieleweke kuwa lengo langu si kupingana na hili bali nataka tu kueleweshwa. Katika kusoma kwangu biblia sijaona sehemu inayozuia mtu kuwa na wake zaidi ya mmoja, hata katika kusikiliza na kusoma mafundisho mbalimbali sijawahi kuona hoja yenye uzito ila naamini hapa nitapata majibu....nitaweka hapa baadhi ya hoja ambazo huwa zinatolewa

1. Uumbaji. Ukisoma Mwanzo sura ya pili Mungu alipomuumba mwanadamu aliumba mwanaume kisha kutoka kwenye ubavu wa mwanaume akamuumba mwanamke kwa hiyo Mungu alimpa Adamu mke mmoja. Lakini je kulikuwa na haja ya kuumba wanawake wengine wakati wanaenda kuzaana? Ina maana alimaliza kila kitu kwenye hizo sample mbili, ndio maana hatuoni aliumba mzungu, mwarabu, mwafrika n.k Na kama jambo hilo ni haramu kiasi hicho mbele za Mungu kwa nini aliruhusu watakatifu wale wa zamani mf. Yakobo, Daudi na wengineo kuwa na wake zaidi ya mmoja?
2. Mafundisho ya Bwana Yesu. Baadhi ya mafundisho yanayorejewa ni

Mathayo 19:4, 5
4 Akawajibu: “Je, hamkusoma kwamba yule aliyewaumba tangu mwanzo aliwaumba mwanamume na mwanamkea 5 na kusema: ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’

Hapa Bwana Yesu alikuwa anajibu kuhusu talaka, lakini mimi nadhani mtu mmoja anaweza kuwa mwili mmoja na huyu na akawa mwili mmoja na mtu wa pili pia bila kuathiri muunganiko wa kwanza


3. Mafundisho ya Mtume Paulo
1 Wakorintho 7:2
2 lakini kwa sababu ya kuenea kwa uasherati,* kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewea na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.

Hapa kilichokatazwa ni uasherati, sioni uhusiano wa idadi ya wanawake na hili andiko maana hata ukiwa nao wawili bado ni wake zako mwenyewe.

1Timotheo 3
1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. 2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkarimu, ajuaye kufundisha; 3asiwe mtu wa kulewa, asiye dhalimu; bali awe mpole; asiwe mbishi wala asiwe mwenye kupenda fedha;.......
Hapa amezungumziwa askofu au mwangalizi wa kanisa, je kama sio askofu? KItu kingine kinachonitatiza hapa ni kuwa Paulo alikuwa anazungumzia watu wanaoamini (kanisa), anaposema askofu awe mwanaume wamke mmoja in maana katika kanisa kuna watu wenye wake zaidi ya mmoja? kwa sababu ni wazi askofu hawezi kutoka nje ya kanisa bali miongoni mwa haohao waumini.
Kama hawapo watu wasio na mke mmoja kwa nini aliweka hicho kigezo?

Samahani siko vizuri kwenye kuandika na kupangilia hoja lakini nadhani mmenielewa.

NB; Nimejikita upande mmoja wa wanaume ili tusitoke kwenye mlengo wa mada
shetani ame create id huku jf
 
Hapo Mathayo 19:5B umesema na hao wawili watakua mwili mmoja na sio hao watano au watatu.
 
Hapo Mathayo 19:5B umesema na hao wawili watakua mwili mmoja na sio hao watano au watatu.
Lakini wanaofanya makubaliano ya kuoana ni wawili ndio maana amesema na hao wawili. Kwa mfano ukioa mke wa kwanza ninyi wawili mnakuwa mwili mmoja na ukioa wa pili hivyo hivyo mnakuwa mwili mmoja, yaani mwili mmoja unahusisha ninyi mlioingia makubaliano ya kuoana hata kama mmojawapo yuko mwili mmoja na mtu mwingine. Samahani najaribu kutoa tu mawazo yangu....ni katika kujifunza tu zaidi
 
Zaman nilikuwa nikitaka kuongea na mtu anauliza maswali tashititi kama mtoa Uzi huu nilikuwa namuuliza alikuwa wangapi darasan. Yaan vifungu vyote vya biblia alivyonukuu vinampa majibu ya swali lake lakini bado eti haelewi.
1. Unasema Mungu akafanya mwanamke akamleta kwa Adam. Huo ndo mpango wa Mungu toka uumbaji mwanaume awe na make mmoja. Kwan alishindwa kumletea zaid?
2. Mwanaume atamuacha baba na mama anaambana na mkewe nao wanakuwa mwili mmoja. Mbona iko wazi wapi unakwama? Je Yesu hakujua wingi na umoja? Watu wameungana na kuwa mwili mmoja wanawezaje kuungana na watu na wanne nk.?
Kifupi nukuu zote hakuna sehemu anapoambiwa awe na wake wengi. Kwani mwenzetu unakwama wapi hasa
 
Zaman nilikuwa nikitaka kuongea na mtu anauliza maswali tashititi kama mtoa Uzi huu nilikuwa namuuliza alikuwa wangapi darasan. Yaan vifungu vyote vya biblia alivyonukuu vinampa majibu ya swali lake lakini bado eti haelewi.
1. Unasema Mungu akafanya mwanamke akamleta kwa Adam. Huo ndo mpango wa Mungu toka uumbaji mwanaume awe na make mmoja. Kwan alishindwa kumletea zaid?
2. Mwanaume atamuacha baba na mama anaambana na mkewe nao wanakuwa mwili mmoja. Mbona iko wazi wapi unakwama? Je Yesu hakujua wingi na umoja? Watu wameungana na kuwa mwili mmoja wanawezaje kuungana na watu na wanne nk.?
Kifupi nukuu zote hakuna sehemu anapoambiwa awe na wake wengi. Kwani mwenzetu unakwama wapi hasa
Hongera kwa kuwa na akili darasani
 
Ahsante mkuu lakini hivi ukisema huyu ni mwanangu mwenyewe maana yake yuko mmoja sio?
"Huyu ni mwanangu mwenyewe", kauli hii inaashiria umoja maana kama ingekuwa wingi, kunapaswa kuwa na neno 'wanangu' na sio 'mwanangu'.
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom