Ni kifaa gani kinatumika kupima haya Magonjwa?

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,373
Habari wakuu,

Kwa miaka ya karibuni kumekuwa na mlipuko wa magonjwa mbalimbali ambayo katika jamii zetu hayakuzoeleka hivyo yanapotokea huleta shida tangu hatua za kugundua na matibabu yake na hivyo kuwagharimu wagonjwa pesa nyingi.

Swali langu ni Je magonjwa haya ambayo yote huenezwa na mbu na tayari yamesharipotiwa kutokea hapa Tanazania katika vipindi tofauti yanagundulika kwa kutumia vifaa gani?( diagnostic)

Tunajua malaria inapimwa kwa darubini na njia nyingine ambayo wataalam wanajua

Je ugonjwa wa Chikungunya na Dengue wanapima kwa kutumia kifaa gani maana kuna kipindi mtu akipata dengue ilikuwa anatoa hadi 50,000 kupata kipimo tena kwenye baadhi tu ya hospitali mjini.

Lengo ni kujua namna gani vijijini watapata huduma kama hii maana mtu anaweza kuugua mfano Chikungunya halafu akakosa vipimo au akanunua dawa akidhani ni malaria ambayo imezoeleka matokea yake ikamuathiri

Karibuni wataalamu.
download.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chikunganya na dengue ni magonjwa ambayo yanafanana dalili na ni vigumu kuyatofautisha

Dalili zake
Homa,kuumwa kichwa na joints

Magonjwa hayo yote yanasababishwa na virus na kuenezwa na mbu

Vipimo vyake

Kwa kawaida virusi anaposhambulia mwili,mwili hutengeneza kinga kitaalamu wanaita antibodies,na kila antibody iko special kwa ugonjwa Fulani,kwahy ndyo hii antibody Amby hupimwa kupitia damu ambapo hupata Immunoglobulin (M) kama ushahidi wa kuwa na maambuzi kipimo kingine ni kuangalia viral nucleic acid kupitia damu pia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chikunganya na dengue ni magonjwa ambayo yanafanana dalili na ni vigumu kuyatofautisha

Dalili zake
Homa,kuumwa kichwa na joints

Magonjwa hayo yote yanasababishwa na virus na kuenezwa na mbu

Vipimo vyake

Kwa kawaida virusi anaposhambulia mwili,mwili hutengeneza kinga kitaalamu wanaita antibodies,na kila antibody iko special kwa ugonjwa Fulani,kwahy ndyo hii antibody Amby hupimwa kupitia damu ambapo hupata Immunoglobulin (M) kama ushahidi wa kuwa na maambuzi kipimo kingine ni kuangalia viral nucleic acid kupitia damu pia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa maelezo ya kitaalamu,sasa swali langu ni kwamba hio damu inapimwa kupitia kifaa gani?au ni darubini hizi wanazotumia kupima malaria?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom