share
JF-Expert Member
- Nov 22, 2008
- 6,062
- 10,457
Ashakum si matusi. Hivyo, lile gari letu la mkaa limeshatoka garage? Nahofia mkaa unaharibika kwa mvua hizi za vuli.Wanabodi,
Nguvu ya Tundu lissu baada ya kusafiri kwa mtumbwi toka ukerewe si ya kawaida tena, ni kama sio yeye bali amevaa nguvu za maajabu na miujiza.
Mapigo ya Tundu Lissu Ukerewe, Mapigo ya simiyu huko bariadi yatosha kusema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza.
Ni uzalendo wetu ndani ya chama chetu cha mapinduzi ndio unatupa ganzi la moyo na ahueni huku tukijifariji lakini. Technically Tundu Lissu ana hoja na anashambulia ngome mfululizo bila aibu huku akiungwa mkono na umati ambao una uchungu na hasira kubwa.
Leo akiwa Simiyu na akinukuu wosia wa Baba wa Taifa wa mwaka 1995 kuhusu uhuru na maendeleo ya watu kwa mifano na akili kubwa hakika amenifanya nishindwe kuendelea kumchungulia kule "Youtube " anatuchezesha sindimba na Segere huku wengine wakisema Beat ya mdundo ina mikwaruzo.
Niliamini ni ndumba na uchawi unatumika ili kushawishi watu kwa maelfu kumshangilia Tundu lissu lakini nimegundua watu wanahitaji maendeleo ya mifukoni mwao yaani pesa. Anachokifanya ni kupigilia msumari wa hasira kwenye maisha na kuwatia watu uchungu unaopelekea kuambiana sera zake.
Tundu Lissu alifaa kuwa professor, Doctor, Mwanahistoria na Mwanamikakati anawajaza watu nguvu na morali ya kutokukata tamaa. Anawaaminisha watu kuwa nchi h ii Raia ndio mmiliki na anapaswa kupewa nguvu ya kuwasema watawala na kuwawajibisha wakikosea.
Tangu kuanza kampeni hakuna wakati au siku ambayo Tundu Lissu ameshambulia ngome kwa hoja kuanzia vitambulisho vya machinga ,Afya,Mfumo wa elimu yetu ya kujaza notes,Bei za mazao,Muundo wa uongozi mpaka ajira na mishahara kama leo
Nilijua labda naota lakini nikaamua kufuatilia habari zake kwenye television tofauti za online na zile za masafa saa mbili usiku huu nikagundua haikuwa ndoto nilipokuwa nachungulia "Youtube"bali ni anagonga hoja na watu zinawaingia kwa hasira kubwa
Yote haya yanayoendelea na mashambulizi yote lakini tutashinda kwa mbinu za kisasa na zilizoboreshwa zaidi.
Tundu Lissu kwenye kuelezea historia ya nchi hii tangu ukoloni mpaka sasa namfananisha na Rais mstaafu Jakaya Kikwete.
Tundu lissu na Jakaya Kikwete kwenye kuelezea matukio ya nchi hii tangu uhuru kwa mifano na kusisimua ninawakubali sana.
Tundu Lissu na Jakaya Kikwete wana uwezo wa kushusha nondo za nchi hii kwa kumbukumbu kubwa sana na ya kushawishi tumetoka wapi na tupo wapi