Ni kero kubwa sana kwangu mtu kuongea na mimi huku ananigusa au kunisukuma...

adden

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
7,035
15,538
Habari za asubuhi wana..

Huku duniani kuna watu nahisi wana matatizo ya kiakili na wanahitaji kumuona daktari.

Kuna hizi tabia nachukia sana kama mtu kuongea na mimi hadi akusonge songe!!atakupiga piga au kukuskuma huku mkipiga stori kawaida tuu..

Mwingine unaongea nae unaona kama anakurusha mood ukifanya kumpotezea ndio anazidi kukulazmisha umskilize nachukia huwa natamani nimpe KELBU moja azimie...

Huwa nakereka balaa ni hizi tabia sijui hawa watu ni mimi tuu ndo huwa wananitokea au na nyie wenzangu huko kwenu wapo.
 
WANABOA SANA WATU HAO

Kuna wengine wananuka midomo akiongea anakusogezea mdomo karibu

Wengine wakiongea wanarusha mate usipoangalia uso wote unaloa
 
Mlevi anaongea kwa sauti ya juu lakini bado anakusogelea tena sikioni maamake
 
Yani mimi imenikuta jana natembea na mtu ananisogelea hadi nimekasirika ila nikatulia tu..,
 
Mara amekupiga kof began mara mgongon mara amekusuma wana kera sana aiseeeh
 
Halafu wanakuwaga na mikono ina nguvu sana hao mandezi, akikugusa mpaka unaumia ila yeye hashtuki anakazana kukupigapiga tuu
 
Back
Top Bottom