Ni kanuni tu!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,419
21,243
Ni kanuni tu!

Wangefuata kanuni, yasingewakuta haya! Talaka ni issue ambayo imejikita katika suala la maadili na uadilifu.
Maisha ya binadamu yametawaliwa na kanuni (standards/discipline) na bila kufuata hizi kanuni basi kila mmoja hufanya anavyotaka na matokeo yake ni maafa.

Kuna standards za ujenzi,
biashara,
uhasibu,
elimu nk na zikiwe implemented vizuri kila kitu huenda vizuri.
Nyumba iliyojengwa kwa kufata standards za ujenzi haiwezi kuporomoka kwani imejengwa kwa kuzingatia standards zinazotakiwa.

Katika serikali ya Mungu kuna standards zilizowekwa ambazo binadamu anatakiwa kuzifuata, hata hivyo wengi hawataki kuishi katika standards za kimungu.
Tumekuwa na man-made standards ambazo tunadhani ni msaada zaidi kitu ambacho si kweli.

Standards ambazo zimewekwa na Mungu ni Baraka kwa jamii ya binadamu na hazibadiliki na hazijawahi kubadilika na Mungu hajatoa tangazo lolote kwamba sasa standards za kuishi duniani ambazo aliziweka kama msingi zimebadilika.

Katika ndoa Mungu ameweka standards wazi na halisi ambazo binadamu anatakiwa kuzifuata ili aishi maisha ya Baraka leo na hata milele.

MFANO WA KANUNI ZA MUNGU KWA NDOA
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikjitenganishe.
(Mathayo 19:6)
Hilo ni wazo la Mungu tangu mwanzo.

Ndoa ni zaidi ya mkataba, ndoa ni agano (covenant) ambalo Mungu aliweka hata kabla ya sheria ambazo tunatumia wakati wa kupeana talaka zilikuwa hazipo.
Ndoa ni union ya watu wawili kuwa mmoja, ni muujiza ambao ni Mungu tu anaweza yaani mtu mmoja kuwa wawili (Adam katika usingizi na Eva akaumbwa) na wawili kuwa mmoja (Adam na Eva kuwa mwili mmoja).
Je, kuna binadamu duniani anaweza kufanya hivyo?
HAKUNA KUBWA!


Hivyo ni kifo tu huweza kutenganisha na talaka haiwezi kutenganisha wawili walioana na kupeana ahadi ya kuishi pamoja hadi kifo mbele za Mungu.

Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mumewe wakati akiwa hai, lakini yule mume akifa, yule mwanamke amefunguliwa kutoka katika sheria ya ndoa.
Hivyo basi, kama huyo mwanamke ataolewa na mwanaume mwingine wakati mumewe akiwa bado yuko hai, ataitwa mzinzi.
Lakini kama mumewe akifa, mwanamke huyo hafungwi tena na sheria ya ndoa, naye akiolewa na mtu mwingine haitwi mzinzi.
(Warumi 7:2-3)
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom