Uchaguzi 2020 Ni Kanda ya Ziwa ila maji tunapata kwa masaa na unataka tukupigie kura tena?

Kumbe Victorie nawe upo kwenye jiji hili! Huku kwetu Bwiru, maji, barabara usiseme. Lakini ukienda mikoa mingine wanaamini huku Kanda ya Ziwa tunapendelewa.

Jamani huku nako hamna kitu. Labda hizo teuzi za upendeleo ambazo nazo zinagusa watu wangapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Bukoba yenyew mji haunaga stendi Zaid ya kichochoro cha matope na soko kuu la mabati.

Watu wa Bukoba walishachoka Bora hata iddi Amin angeichukua sasa bukoba ingekuwa jiji sawa na kampala
 
Too Sad yaani Buhongwa tunaamka tunaona Ziwa huyoooo.Eti halafu kuna shida ya maji. Stupid policies.Halafu kutwa kunyooshea vidole mabeberu. Hivi mabeberu wanazuia msijenge mabomba na kuwa na huduma ya maji yasiyokatika katika ?

Hakuna kitu kinanikera na kunitia hasira kama kumekuwa na wawakilishi miaka na nenda rudi huko bungeni lakini maeneo mengi ya kanda ya ziwa hawana maji safi na salama ya kunywa. Maeneo ya kanda ya ziwa yote yalitakiwa yawe na maji safi na salama ya kunywa, maana chanzo cha maji kimewazunguka halafu wanaishi kwa shida shida. Na sasa hivi watapita tena kuwaomba kura halafu watawapa? Kweli akili zao zinafikiria vizuri? Kuna huduma za msingi kulingana na upatikanaji wake katika maeneo husika haitakiwi kuwa shida upatikanaji wake. Kwa kanda ya Ziwa upatikanaji wa MAJI, MAJI, MAJI, MAJI ,katika vijiji vyake vyote ni muhimu sana. Kuna mikoa mengine wanamito tu lakini maji karibia mkoa mzima yanapatikana.
 
Mimi ni mkazi wa Kanda ya Ziwa ila tunachangamoto kubwa ya maji.

Cha kwanza awamu hii gharama ya maji imepanda sana na maji yenyewe ni ya shida.

Hebu imagine ziwa lipo within 30 km ila maji mnapewa kwa mgao. Kunamaeneo mwanza hii maji yanapatikana usiku tu. Sasa afadhali na uko. Kuna pengine maji yanafunguliwa mara moja kwa wiki.

Hawa wabunge tuliochagua ndyo bure kabisa. Mbali na maji ila barabara vumbi ndyo hovyo kabisa.

Umekaribia uchaguzi ndyo wamezikwangua kihuni huni tu mvua imepiga mara moja tu kwisha mabonde kuinama kama kawaida.

Sasa ni hivi, kura mtapigiwa na mandege mliyonunua.
Unaongea mara moja kwa wiki, nakaa Buswelu manispaa ya Ilemela na sijapata maji ya bomba zaidi ya miezi mitatu.

Siwezi kuwapa kura CCM hata nikiwa mgonjwa wa akili
 
Hapa chato Hakuna maji ya bomba,watu wanachota maji ya matumizi kwenye ziwa Victoria .Katoro mjini ambayo upo buserere wilaya ya chato ,Hakuna maji ya bomba watu wanachota na kunywa maji ya visima vifupi naziwa Victoria lipo KMS chache tu,Ila hakuna maji.

Sembuse mwanza jiji kubwa. Kupiga Kura mwaka huu lazima mtanzania ujithadhimini Sana kabla hujapiga Kura , tunadanganywa na miradi mikubwa Ila wananchi wanateseka Sana kuanzia chato Hadi mtwara.
Wasiofika Mwanza wanaweza kushangaa km labda tunasingizia......
Sasa chato wanakubalije kujengewa uwanja wa kimataifa wa ndege hata maji kwao ni shida?

Watz bana ni watu wa ajabu sana
 
QUOTE="LadyRed, post: 36327345, member: 358507"]
Hahahah eti mandege
[/QUOTE]
Tangu 2015 Hadi Sasa mkoa wa Mara na wilaya zake serikali haikufika huko,mkoa wa kagera na wilaya zake serikali haikufika huko.Leo wanaotarajia kwenda huko kuomba Kura za ubunge ,uraia na udiwani. Kura kwa kipindi hiki zitatolewa Kama wajumbe walivyotoa Kura za maoni" nipe nikupe,hakuna Kura za bure October"
 
Unaongea mara moja kwa wiki, nakaa Buswelu manispaa ya Ilemela na sijapata maji ya bomba zaidi ya miezi mitatu.

Siwezi kuwapa kura CCM hata nikiwa mgonjwa wa akili
Buswelu ipo within 30 km from lake victoria north, west na est imezungukwa na ziwa victoria
 
Buswelu
Screenshot_20200812-184734_Maps.jpg
 
Mimi niko kata ya Kishili, naingia mwezi wa nne sasa bomba la maji la nyumbani halijatoa maji. Vyoo vya ndani bila huduma ya maji kweli!!! MWAUWASA wamenitumia bill ya July na ninashangaa kwa huduma ipi? Kipindi Corona inaanza March sisi huku tulikuwa na shida na maji ya kunawa. Kweli ulimwengu wa kati Afrika ni shiiiiidaaaa!!!
 
Mimi niko kata ya Kishili, naingia mwezi wa nne sasa bomba la maji la nyumbani halijatoa maji. Vyoo vya ndani bila huduma ya maji kweli!!! MWAUWASA wamenitumia bill ya July na ninashangaa kwa huduma ipi? Kipindi Corona inaanza March sisi huku tulikuwa na shida na maji ya kunawa. Kweli ulimwengu wa kati Afrika ni shiiiiidaaaa!!!
Kesho nakuja halo chadema kuangalia ndondo LA mashujaa vs Kishiri
 
Back
Top Bottom