Ni kanda ya Magharibi pekee haijawahi kuwa na kiongozi wa kitaifa - wanasiasa mna majibu? Nielimisheni!

Wabobezi wa siasa, nijengeeni uwezo!

Kanda ya Magharibi - yenye mikoa ya Kigoma na Tabora ndiyo haijawahi kuwa na kiongozi wa kitaifa - nalenga Rais au Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.

(a). Orodha ya Marais tangu 1961 - 2021
= Mwl Julius K Nyerere (kanda ya ziwa); Mzee Ally Hassan Mwinyi (Zanzibar); Benjamin William Mkapa (Kusini); Jakaya Mrisho Kikwete (Mashariki); Dkt John Pombe Magufuli (Ziwa); na Samia Suluhu Hassan (Zanzibar).

(b). Makamu wa Rais
= Abeid Aman Karume (Zanzibar); Aboud Jumbe (Zanzibar); Ally Hassan Mwinyi (Zanzibar);

* Joseph Sinde Warioba (Ziwa); John Samwel Malecela (Kati); Cleopa Msuya (Kaskazini); Omary Ally Juma (Zanzibar); Ally Mohammed Shein (Zanzibar); Mohammed Gharib Bilali (Zanzibar); na Samia Suluhu Hassan (Zanzibar).

(c). Mawaziri Wakuu tangu 1961 - 2021
= Julius K Nyerere (Ziwa); Rashid Mfaume Kawawa (Mashariki); Edward Moringe Sokoine (Mashariki); Cleopa Msuya (Kaskazini); Edward Moringe Sokoine (Mashariki); Salim Ahmed Salim (Mashariki); Joseph Sinde Warioba (Ziwa); John Samwel Malecela (Kati); Cleopa Msuya (Kaskazini); Fredrik T Sumaye (Kaskazini); Edward Ngoyai Lowassa (Kaskazini); Mizengo Kayanza Peter Pinda (Nyanda za Juu Kusini); na Kasim Majaliwa Majaliwa (Kusini).

Kwa uchambuzi huo hapo juu inaonesha mikoa ya Kigoma na Tabora tangu Uhuru wa nchi yetu na baadae Muungano haijawahi kuwa na kiongozi wa kitaifa kwa nafasi za Rais, Makamu, au Waziri Mkuu. Mpo wabobezi na wachambuzi wa siasa na utawala - hebu njooni na kile mnachodhani ni chanzo cha sababu za kutokuwa na walau moja kati ya nafasi hizo.

Aidha, nimempigia saruti Hayati JPM kwani kwa uongozi wake aliliona hili ndipo akamteua Dkt Philipo I. Mpango (WF); Prof Joyce Ndalichako (WE).

Nahitimisha kwa kusema
"Hili ni taifa la watanzania kwa kuzingatia mipaka yake na kwa vyovyote vile watanzania wote tunazo sifa sawia".

Msakila M Kabende
Kakonko - Kigoma (Tanzania)

******************
Mhe Mama Samia, kigoma na kanda ya magharibi tunakupongeza kwa uteuzi huo - tunakuhakikishia ushirikino ktk chama na Serikali
Edward M. Sokoine -Mashariki??? Na umerudia Mara tatu

Salim Ahmed Salimu - Mashariki???
 
Wabobezi wa siasa, nijengeeni uwezo!

Kanda ya Magharibi - yenye mikoa ya Kigoma na Tabora ndiyo haijawahi kuwa na kiongozi wa kitaifa - nalenga Rais au Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.

(a). Orodha ya Marais tangu 1961 - 2021
= Mwl Julius K Nyerere (kanda ya ziwa); Mzee Ally Hassan Mwinyi (Zanzibar); Benjamin William Mkapa (Kusini); Jakaya Mrisho Kikwete (Mashariki); Dkt John Pombe Magufuli (Ziwa); na Samia Suluhu Hassan (Zanzibar).

(b). Makamu wa Rais
= Abeid Aman Karume (Zanzibar); Aboud Jumbe (Zanzibar); Ally Hassan Mwinyi (Zanzibar);

* Joseph Sinde Warioba (Ziwa); John Samwel Malecela (Kati); Cleopa Msuya (Kaskazini); Omary Ally Juma (Zanzibar); Ally Mohammed Shein (Zanzibar); Mohammed Gharib Bilali (Zanzibar); na Samia Suluhu Hassan (Zanzibar).

(c). Mawaziri Wakuu tangu 1961 - 2021
= Julius K Nyerere (Ziwa); Rashid Mfaume Kawawa (Mashariki); Edward Moringe Sokoine (Mashariki); Cleopa Msuya (Kaskazini); Edward Moringe Sokoine (Mashariki); Salim Ahmed Salim (Mashariki); Joseph Sinde Warioba (Ziwa); John Samwel Malecela (Kati); Cleopa Msuya (Kaskazini); Fredrik T Sumaye (Kaskazini); Edward Ngoyai Lowassa (Kaskazini); Mizengo Kayanza Peter Pinda (Nyanda za Juu Kusini); na Kasim Majaliwa Majaliwa (Kusini).

Kwa uchambuzi huo hapo juu inaonesha mikoa ya Kigoma na Tabora tangu Uhuru wa nchi yetu na baadae Muungano haijawahi kuwa na kiongozi wa kitaifa kwa nafasi za Rais, Makamu, au Waziri Mkuu. Mpo wabobezi na wachambuzi wa siasa na utawala - hebu njooni na kile mnachodhani ni chanzo cha sababu za kutokuwa na walau moja kati ya nafasi hizo.

Aidha, nimempigia saruti Hayati JPM kwani kwa uongozi wake aliliona hili ndipo akamteua Dkt Philipo I. Mpango (WF); Prof Joyce Ndalichako (WE).

Nahitimisha kwa kusema
"Hili ni taifa la watanzania kwa kuzingatia mipaka yake na kwa vyovyote vile watanzania wote tunazo sifa sawia".

Msakila M Kabende
Kakonko - Kigoma (Tanzania)

******************
Mhe Mama Samia, kigoma na kanda ya magharibi tunakupongeza kwa uteuzi huo - tunakuhakikishia ushirikino ktk chama na Serikali
Wazee wachawi wa Kigoma hawaruhusu maendeleo kanda hiyo. Ondokeni na ushirikina mambo yatakuwa shwari.
 
Back
Top Bottom