Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Amani iwe nanyi wadau,
Huko soko la dunia hapatoshi! Bei ya Mafuta na Gesi inazidi kupanda kwa Kiwango cha kutisha.
Haya yanatokea huku Ulaya na Marekani kukiwa na uhaba wa bidhaa hii adhimu kiasi kupelekea Makampuni ya Gesi na Mafuta kuamka mbio kutoka usingizini na kuanza kufufua zile fursa walizokuwa wamezitupa kando kwa miaka karibu 6 mpaka 7!
Ulaya walipokuwa wanategemea nishati mbadala sasa wameona hawawezi tena kwenda bila gesi! Baridi inayoongezeka Ulaya inafanya Gesi kuhitajika zaidi kuliko bidhaa zingine Kwa ajiri ya kupata nishati!
Ndo mana hivi Karibuni Makampuni Makubwa yameanza kujileta Tanzania! Wiki mbili zilizopita Makampuni ya Exon Mobil yalifanya kikao na Waziri Makamba.
Juzi hapa Mtendaji Mkuu wa Kampuni kubwa ya Gesi na Mafuta ya Shell ya Uholanzi kafanya kikao na Rais Samia.
Vikao hivi bila shaka ni vya makampuni haya kujaribu kupata nafasi ili yapewe nafasi ya kufanya biashara hii Tanzania. Kusema kweli huu ni upepo mzuri kwa Mama Samia maana haya yanatokea chini ya uongozi wake!
Rais Samia akikaa vizuri kwenye Mazungumzo na watu hawa na tukaingia mikataba mizuri nadiliki kusema Mradi huu wa LNG ndo utakuwa mradi wa kipekee na faida zaidi kwa Tanzania na Watanzania kuliko mradi wowote uliowai na utakaowai kuja kufanywa Tanzania.
Dunia inahitaji Kweli Gesi na wako kwenye panic state ya kupata fursa ya kuchimba na kuuza Gesi. Tanzania ikicheza vizuri hapa , hata Tozo za simu tutaachana nazo.
Huko soko la dunia hapatoshi! Bei ya Mafuta na Gesi inazidi kupanda kwa Kiwango cha kutisha.
Haya yanatokea huku Ulaya na Marekani kukiwa na uhaba wa bidhaa hii adhimu kiasi kupelekea Makampuni ya Gesi na Mafuta kuamka mbio kutoka usingizini na kuanza kufufua zile fursa walizokuwa wamezitupa kando kwa miaka karibu 6 mpaka 7!
Ulaya walipokuwa wanategemea nishati mbadala sasa wameona hawawezi tena kwenda bila gesi! Baridi inayoongezeka Ulaya inafanya Gesi kuhitajika zaidi kuliko bidhaa zingine Kwa ajiri ya kupata nishati!
Ndo mana hivi Karibuni Makampuni Makubwa yameanza kujileta Tanzania! Wiki mbili zilizopita Makampuni ya Exon Mobil yalifanya kikao na Waziri Makamba.
Juzi hapa Mtendaji Mkuu wa Kampuni kubwa ya Gesi na Mafuta ya Shell ya Uholanzi kafanya kikao na Rais Samia.
Vikao hivi bila shaka ni vya makampuni haya kujaribu kupata nafasi ili yapewe nafasi ya kufanya biashara hii Tanzania. Kusema kweli huu ni upepo mzuri kwa Mama Samia maana haya yanatokea chini ya uongozi wake!
Rais Samia akikaa vizuri kwenye Mazungumzo na watu hawa na tukaingia mikataba mizuri nadiliki kusema Mradi huu wa LNG ndo utakuwa mradi wa kipekee na faida zaidi kwa Tanzania na Watanzania kuliko mradi wowote uliowai na utakaowai kuja kufanywa Tanzania.
Dunia inahitaji Kweli Gesi na wako kwenye panic state ya kupata fursa ya kuchimba na kuuza Gesi. Tanzania ikicheza vizuri hapa , hata Tozo za simu tutaachana nazo.
Wito wangu kwa Mama Samia! Hii ni kete adhimu, una bahati sana, itumie vizuri hii nafasi na hutasahaulika kwa Watanzania vizazi na vizazi!