Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
Katika hoja zake Profesa Kitila Mkumbo, mwanachama mwenzangu wa kale wa Chadema amewahi kuandika "Kumuenzi Mwalimu Nyerere: Tufanye vita dhidi ya ulaghai wa kisiasa" na katika hoja yake hiyo Prof Kitila anaandika;
Katika kumalizia andiko lake baada ya aya kadhaa Profesa Kitila Mkumbo anaendelea kuandika akisema;
Binafsi nimevutiwa na maandiko haya ya Profesa huyu mchanga, maandiko yake haya bila shaka yametokana na ukweli kuwa si tu ni mtu mwenye taaluma kubwa na ueledi mpana kwenye masuala ya siasa za nchi hii bali ameyaishi maisha yaliyoguswa na ULAGHAI mkubwa uliopo katika vyama vya upinzani nchini.
Nadhani mimi nitaongeza jambo kuhusu ulaghai unaopaswa kupigwa vita ili kuimarisha demokrasia ya kweli nchini.
Ulaghai mwingine wa hovyo sana ni kule kujaribu kuwaaminisha watu kuwa upinzani wa kweli ni wa CHADEMA pekee na kwamba chama kingine chochote cha upinzani ambacho hakikubaliani na chadema hao ni CCM B na kwamba wanatumika na CCM. Iliwahi kuwa hivi kwa CUF pale Mheshimiwa TUNDU aliposimama na hoja yake maarufu bungeni "HAKUNA NDOA YA WANAUME WENGI" akiwatuhumu CUF kuwa wameolewa na CCM na kwamba ndoa yao hiyo inawaweka mbali na CHADEMA na kwamba chadema haiko tayari kushirikiana chochote na CUF katika kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni wakati huo. Ni kama vile leo ACT wazalendo wanavyozamishwa kwenye bahari hiyo ya U-CCM B kwa fikra, hila na ulaghai ule ule wa miaka 5 iliyopita.
Wakati mwingine nashawishika kuwa UCHAWI UPO na una nguvu kubwa sana katika siasa za nchi yetu. Maana kama si upungufu wa akili basi ni nguvu ya giza pekee ambayo inaweza kumfanya mtu kama TUNDU kusimama jukwaani kumnadi EDWARD LOWASSA kuwa ni mtu safi, hakuwahi kula rushwa na mwenye maamuzi ya kuwaletea mabadiliko watanzania....LOWASSA..eti Lowassa ni mwanamabadiliko anayesemewa na LISSU, MNYIKA, MDEE etc.
Katika Video Clip maarufu Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Freeman Mbowe anasikika akiapa kwa Mungu wake akisema "LOWASSA CHADEMA, yaani lowassa ajiunge na Chadema, OVER MY DEAD BODY"' lakini leo Lowassa sio tu ni mwanachama wa CHADEMA bali ndio KAULI KUU ya chadema, ndio mfanya tathimini na ndio mwenye maamuzi. Tusipopiga vita Ulaghai huu na UNAFIKI wa kiwango hiki, Taifa hili litaangamia.
Kimsingi nimekata tamaa na Vijana wa BAVICHA na supporters wa Chama hiki ambao watu wengine wanawaita majina mabaya ya wanyama fulani hivi, maana wao si watu wenye kuhoji na kutafakari, wanachoambiwa na wakubwa zao wao wanakibeba na kukinadi. Siku nikijiunga na CHADEMA hii (MUNGU wangu aepushie mbali) mtaona maajabu, maana Thread ya Kwanza hapa JF italetwa na John Heche yenye kichwa cha habari "JULIANA, MWAMBA USIOYUMBA" na wale waliokuwa wakikesha kuandika matusi hapa watakuwa wakwanza kuandika kwa mbwembwe za kunisifia...kama wamelogwa hivi.
TUACHE UNAFIKI WA NAMNA HII.
Pengine ulaghai mkubwa kabisa wa kisiasa kuwahi kutokea hapa nchini ni ule uliofanywa na chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA kwa kushirikiana na washirika wake katika vyama vinavyounda Ukawa
Baada ya kumnyanyasa, kwa miaka mingi, kwa kila aina ya kejeli na matusi, na kufanikiwa kuiaminisha jamii kwamba Edward Lowassa ndiye alikuwa taswira halisi ya ufisadi nchini, wakaibuka naye kuwa mgombea katika mchakato ambao wataalamu wa sayansi ya siasa watahitaji kuufanyia utafiti maalumu
Katika kumalizia andiko lake baada ya aya kadhaa Profesa Kitila Mkumbo anaendelea kuandika akisema;
Katika kitabu chake Mwalimu Nyerere anaita tabia hii katika uongozi kuwa ni unafiki. Kwamba kosa ni kosa likifanywa na mtu mwingine, lakini kosa hilo hilo linakuwa si kosa likifanywa na wewe au likifanywa na jamaa yako!
Binafsi nimevutiwa na maandiko haya ya Profesa huyu mchanga, maandiko yake haya bila shaka yametokana na ukweli kuwa si tu ni mtu mwenye taaluma kubwa na ueledi mpana kwenye masuala ya siasa za nchi hii bali ameyaishi maisha yaliyoguswa na ULAGHAI mkubwa uliopo katika vyama vya upinzani nchini.
Nadhani mimi nitaongeza jambo kuhusu ulaghai unaopaswa kupigwa vita ili kuimarisha demokrasia ya kweli nchini.
Ulaghai mwingine wa hovyo sana ni kule kujaribu kuwaaminisha watu kuwa upinzani wa kweli ni wa CHADEMA pekee na kwamba chama kingine chochote cha upinzani ambacho hakikubaliani na chadema hao ni CCM B na kwamba wanatumika na CCM. Iliwahi kuwa hivi kwa CUF pale Mheshimiwa TUNDU aliposimama na hoja yake maarufu bungeni "HAKUNA NDOA YA WANAUME WENGI" akiwatuhumu CUF kuwa wameolewa na CCM na kwamba ndoa yao hiyo inawaweka mbali na CHADEMA na kwamba chadema haiko tayari kushirikiana chochote na CUF katika kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni wakati huo. Ni kama vile leo ACT wazalendo wanavyozamishwa kwenye bahari hiyo ya U-CCM B kwa fikra, hila na ulaghai ule ule wa miaka 5 iliyopita.
Wakati mwingine nashawishika kuwa UCHAWI UPO na una nguvu kubwa sana katika siasa za nchi yetu. Maana kama si upungufu wa akili basi ni nguvu ya giza pekee ambayo inaweza kumfanya mtu kama TUNDU kusimama jukwaani kumnadi EDWARD LOWASSA kuwa ni mtu safi, hakuwahi kula rushwa na mwenye maamuzi ya kuwaletea mabadiliko watanzania....LOWASSA..eti Lowassa ni mwanamabadiliko anayesemewa na LISSU, MNYIKA, MDEE etc.
Katika Video Clip maarufu Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Freeman Mbowe anasikika akiapa kwa Mungu wake akisema "LOWASSA CHADEMA, yaani lowassa ajiunge na Chadema, OVER MY DEAD BODY"' lakini leo Lowassa sio tu ni mwanachama wa CHADEMA bali ndio KAULI KUU ya chadema, ndio mfanya tathimini na ndio mwenye maamuzi. Tusipopiga vita Ulaghai huu na UNAFIKI wa kiwango hiki, Taifa hili litaangamia.
Kimsingi nimekata tamaa na Vijana wa BAVICHA na supporters wa Chama hiki ambao watu wengine wanawaita majina mabaya ya wanyama fulani hivi, maana wao si watu wenye kuhoji na kutafakari, wanachoambiwa na wakubwa zao wao wanakibeba na kukinadi. Siku nikijiunga na CHADEMA hii (MUNGU wangu aepushie mbali) mtaona maajabu, maana Thread ya Kwanza hapa JF italetwa na John Heche yenye kichwa cha habari "JULIANA, MWAMBA USIOYUMBA" na wale waliokuwa wakikesha kuandika matusi hapa watakuwa wakwanza kuandika kwa mbwembwe za kunisifia...kama wamelogwa hivi.
TUACHE UNAFIKI WA NAMNA HII.