Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,403
- 31,376
Mwaka wa uchaguzi umefika, wakati tuliousubiri kwa miaka 5 kuwatia adabu wale wasiotusikiliza, wale wasiojali maisha yetu na wale wasiojali Tanganyika ya kesho ndio huu. Hiki ni kizazi kinachojinasibu kwa teknolojia na maendeleo, lakini kwa kudhani kuwa maendeleo ni internet/ipod n.k kizazi kimejivua jukumu la ukombozi wa nchi toka lindi la umasikini. Sasa watu hukaa mbele ya kompyuta zao kusubiri kusikia nini Dr Slaa au Selelii watafanya.
Hatuwezi kuikomboa nchi kwa fikra za kukejeliana badala ya kujibu au kuandika hoja zenye mashiko na nguvu. Hatuwezi kuiokomboa nchi kama tumejikita kwenye mawazo ya kuwakosoa wale wanaojitahidi japo kwa uchache wao. Hatuwezi kuiokomboa nchi kama tutawaendekeza wale wanaotutoa kwenye hoja kwa kuchomeka ubinfsi.
Kampeni zimeanza, hatuna sababu ya kusubiri Dr Slaa atafanya nini, sisi tunatakiwa tumwambie afanye nini ili kufikia ukombozi. Sisi ndio injini ya Slaa na sio kinyume chake. Tunatakiwa tujawe na jaziba na chachu ya ukombozi ili kila asubuhi Dr Slaa ajue ana watu wanamdai, ana deni! Sio muda wa kusikiliza Dr kasema nini bali ni wa kumwambia Dr tuelekee huku! Hakuna nchi, jamii au taifa lililokombolewa na mtu mmoja, ni nguvu ya umma, na umma ni sisi.
Kampeni zimeanza, na tunashuhudia wananchi wakiimbishwa na kuchezeshwa nyimbo wasizozijua lakini wanaziimba vizuri. CCM ni nambari moja, fungua njia CCM ipite n.k.
Wakiambiwa ilani imetekelezeka wanapiga makofi ili wasije nyimwa kofia au khanga. Sio kuwa hawajui udanganyifu bali umasikini na kukosa kitu mbadala ndio kikwazo.
Tuanze kampeni ya kuisadia nchi bila magari au helikopta! tuanzie humu JF. Tuanze na wewe unayesoma, chapisha [print] picha hizo na umuonyeshe, Mkeo, Shemejio, Baba, Mama,hata Mama mkwe kisha muulize maswali haya kwa utulivu bila ushabiki!
1. Ilani ya uchaguzi kuhusu elimu imetekelezeka kivipi kwa kuangali hizo shule hapo chini?
2. Vipi ccm inunue magari 200 ishindwe kujenga shule hiyo hapo chini?
3. waulizeni, je hao watoto ni sehemu ya nambari one ya ccm ?
4. Je hao watoto wataweza kununua ma vx au watabaki kucheza ngoma kama wazazi wao?
5. Je, zile kompyuta wanazoahidiwa wananchi zitawekwa wapi kama watoto wamekaa
juu ya mawe?
6. Waulizeni wanapoimba na kucheza ngoma, ni ushindi upi wanaosherehekea, kutojenge wa shule nzuri kama zile za ''academy'' au kuwaona watoto wao wamekaa juu ya mawe kama mama zao wanapokuwa wanawapikia!!!!.
Pelekeni ujumbe bila ghadhabu wala munkari, na mwisho muwaambie je wapo tayari kuendelea na hali hii iliyodumu miaka 50!! au wapo tayari kwa maamuzi magumu dhidi ya mazoea lakini yenye tija kwa vizazi vijavyo?
Ili kujenga uthubutu kwako kwanza kabla ya mwenzako, mwambie Mama Mkwe '' Chagua wabunge chadema, chagua Slaa'' ukifanikiwa au la! nenda kwa jirani naye mpe dozi! usikate tamaa kwasababu mafanikio hayaji katika sahani ya dhahabu! yanaambatana na jasho.
Hatuwezi kuikomboa nchi kwa fikra za kukejeliana badala ya kujibu au kuandika hoja zenye mashiko na nguvu. Hatuwezi kuiokomboa nchi kama tumejikita kwenye mawazo ya kuwakosoa wale wanaojitahidi japo kwa uchache wao. Hatuwezi kuiokomboa nchi kama tutawaendekeza wale wanaotutoa kwenye hoja kwa kuchomeka ubinfsi.
Kampeni zimeanza, hatuna sababu ya kusubiri Dr Slaa atafanya nini, sisi tunatakiwa tumwambie afanye nini ili kufikia ukombozi. Sisi ndio injini ya Slaa na sio kinyume chake. Tunatakiwa tujawe na jaziba na chachu ya ukombozi ili kila asubuhi Dr Slaa ajue ana watu wanamdai, ana deni! Sio muda wa kusikiliza Dr kasema nini bali ni wa kumwambia Dr tuelekee huku! Hakuna nchi, jamii au taifa lililokombolewa na mtu mmoja, ni nguvu ya umma, na umma ni sisi.
Kampeni zimeanza, na tunashuhudia wananchi wakiimbishwa na kuchezeshwa nyimbo wasizozijua lakini wanaziimba vizuri. CCM ni nambari moja, fungua njia CCM ipite n.k.
Wakiambiwa ilani imetekelezeka wanapiga makofi ili wasije nyimwa kofia au khanga. Sio kuwa hawajui udanganyifu bali umasikini na kukosa kitu mbadala ndio kikwazo.
Tuanze kampeni ya kuisadia nchi bila magari au helikopta! tuanzie humu JF. Tuanze na wewe unayesoma, chapisha [print] picha hizo na umuonyeshe, Mkeo, Shemejio, Baba, Mama,hata Mama mkwe kisha muulize maswali haya kwa utulivu bila ushabiki!
1. Ilani ya uchaguzi kuhusu elimu imetekelezeka kivipi kwa kuangali hizo shule hapo chini?
2. Vipi ccm inunue magari 200 ishindwe kujenga shule hiyo hapo chini?
3. waulizeni, je hao watoto ni sehemu ya nambari one ya ccm ?
4. Je hao watoto wataweza kununua ma vx au watabaki kucheza ngoma kama wazazi wao?
5. Je, zile kompyuta wanazoahidiwa wananchi zitawekwa wapi kama watoto wamekaa
juu ya mawe?
6. Waulizeni wanapoimba na kucheza ngoma, ni ushindi upi wanaosherehekea, kutojenge wa shule nzuri kama zile za ''academy'' au kuwaona watoto wao wamekaa juu ya mawe kama mama zao wanapokuwa wanawapikia!!!!.
Pelekeni ujumbe bila ghadhabu wala munkari, na mwisho muwaambie je wapo tayari kuendelea na hali hii iliyodumu miaka 50!! au wapo tayari kwa maamuzi magumu dhidi ya mazoea lakini yenye tija kwa vizazi vijavyo?
Ili kujenga uthubutu kwako kwanza kabla ya mwenzako, mwambie Mama Mkwe '' Chagua wabunge chadema, chagua Slaa'' ukifanikiwa au la! nenda kwa jirani naye mpe dozi! usikate tamaa kwasababu mafanikio hayaji katika sahani ya dhahabu! yanaambatana na jasho.