Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Absalom Kibanda
HEKAHEKA za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu zimepamba moto, na tayari vituko kadha wa kadha vya kisiasa vimeshaanza kuonekana kadiri miezi na siku za kuelekea Oktoba 31 zinavyozidi kujongea.
Matendo na kauli kutoka kwa wanasiasa wa makundi mbalimbali yanayoshereheshwa na matukio ya kutia hamasa na wakati mwingine kukera kama si kushangaza, ni mambo yanayoonekana kuwa ya kawaida kusikika wakati huu taifa linapojiandaa kuwachagua Rais wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, wabunge, wawakilishi na madiwani.
Katika kipindi cha wiki moja au mbili tu zilizopita, taifa limeshuhudia matukio kadha wa kadha mazito kuhusu mustakabali wa nchi hii, ambayo ukiyaangalia utaona moja kwa moja mwelekeo wake unatuongoza kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi huo mkuu.
Ni katika kipindi hiki cha wiki moja, tumemsikia Rais Jakaya Kikwete kwa nyakati mbili tofauti, kwanza akiwa Mwanza na baadaye akizungumza kwa utaratibu aliojiwekea wa kulihutubia taifa kila mwishoni mwa mwezi, akionyesha kukerwa na kukemea tatizo la rushwa na lile la matumizi mabaya ya fedha wakati huu tunapoelekea katika mshikemshike wa uchaguzi mkuu.
Ni wazi kwamba akiwa kiongozi mkuu mwenye dhamana kubwa pengine kuliko mwanasiasa au mtu mwingine yeyote hapa nchini kwa wakati huu, Kikwete anawajibika kiuongozi, kivisheni na kimaadili kutoa matamshi ya namna hiyo yenye kutoa mwongozo na kuonyesha njia sahihi ambayo taifa linapaswa kupita wakati huu tunapojiandaa kwa ajili ya tukio kubwa la kihistoria.
Hata hivyo, kauli hiyo ya Kikwete imepokewa kwa hisia tofauti na wadadisi mbalimbali wa mambo, ambao baadhi yao wameonyesha kuiunga mkono na kummwagia sifa, huku wengine wakiitilia shaka na kuibuka na maswali mengi moja kati yao likiwa ni lile linalohoji, iwapo rais ameitoa kwa moyo wa dhati au kwa sababu tu ya kutaka kuonekana akitimiza wajibu wa kimamlaka unaomtaka aseme lolote jema hata kama atafanya hivyo pasipo kumaanisha kile asemacho.
Ni kwa sababu hiyo ndiyo maana wako waliotafsiri kauli hii ya Kikwete kuwa inayotoa mwelekeo sahihi wa huko tuendako, huku wengine wakiichukulia kuwa ni vitisho visivyo na maana ambavyo kiongozi huyo amekuwa na utamaduni wa kuvitoa kila mara, akijua kwa kufanya hivyo anatimiza wajibu wake wa msingi wa kiuongozi wa kuonyesha njia.
Pasipo kujali ni kundi gani kati ya haya mawili limetoa tafsiri sahihi kwa kile alichokisema JK, binafsi naiona kauli yake hiyo na nyingine nyingi zinazotolewa na makundi mbalimbali ya kijamii, kisiasa na kiserikali yanayomuunga mkono kuwa ni zenye lengo la kumfungulia njia pana zaidi ya ushindi wa kishindo wakati wa uchaguzi huo mkuu wa Oktoba.
Ukiacha kauli hiyo ya Kikwete, kipindi cha wiki hiyo hiyo moja, taifa limeshuhudia kuibuka kwa kikundi kingine cha msimu kilichojipa jina la Amani Forum, kikiongozwa na Mbunge wa Afrika Mashariki, Amaan Walid Kabourou na kujumuisha wanasiasa wengine kadhaa akiwamo, Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Shida Salum ambaye ni mama mzazi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Kwa mara ya kwanza, nilisikia taarifa za kuundwa kwa kikundi hiki kupitia katika kipindi maarufu cha asubuhi cha ‘Jambo Tanzania' kinachorushwa na kituo cha televisheni ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambako wajumbe wake wawili walijitokeza na kueleza kuhusu kuanzishwa na malengo yake.
Nilipowasikiliza wajumbe hao wawili ambao mmoja wao alikuwa Mrema, mara moja kumbukumbu zangu zilinirejesha mwaka 2005 na kabla ya hapo mwaka 2000 wakati wa kipindi kama hiki cha maandalizi ya uchaguzi mkuu, yalipoibuka makundi ya watu tofauti na zikajengwa hoja tofauti ambazo zote zilionekana kubeba ajenda moja kubwa ya kuilinda amani ya taifa hili kwa njia moja tu ya kuwahamasisha wananchi kuendelea kukichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) na aghalab kumpigia debe mgombea wake wa urais.
Kama ilivyokuwa mwaka 2000, walipoibuka watu kumpigia debe aliyekuwa rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa ndivyo inavyotokea leo hii kupitia Amani Forum ambayo viongozi wake wote kwa kauli moja wamesikika wakimpamba Kikwete kwa kila aina ya sifa na kuwaasa Watanzania waendelee kumuamini na kumchagua katika uchaguzi huo wa Oktoba.
Kwa namna ya kustaajabisha, kwanza kupitia TBC na baadaye katika mkutano wa hadhara huko Temeke Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam, viongozi wa Amani Forum wamejitokeza na kuanza kummwagia sifa Kikwete hata kufikia hatua ya kumtangaza kuwa mtu mwenye sifa za kipekee za kuachiwa kuendelea kutawala.
Kimsingi sina sababu hata moja ya kuwaona kuwa ni watu wa ajabu, wa hovyo au wasiofaa katika jamii, watu ambao kwa moyo wao wote na kwa nia njema, wameamua kumuunga mkono Kikwete, CCM au mgombea mwingine yeyote kugombea urais, ubunge, uwakilishi, udiwani au nafasi nyingine kwani wanao uhuru wao wa kikatiba kufanya hivyo.
Pamoja na ukweli huo, katika hili tatizo langu ni hii tabia ya kikachero ambayo imekuwa ikitumiwa na mawakala wa CCM walio serikalini, ndani ya chama hicho tawala na nje, kutumia ushawishi wenye hila, tena wakati usio wa kampeni kujenga hoja za kudumaza demokrasia ya vyama vingi na kuanza kumpigia debe rais aliye madarakani akipachikwa sifa hata asizostahili ili mradi tu kumhakikishia ushindi.
Ni wazi kwamba uamuzi huu wa kikachero wa kumjumuisha Mrema wa TLP na mama mzazi wa Zitto ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA katika kundi la kumpigia debe Kikwete wakati huu, kabla hata uteuzi wa wagombea haujaanza wakitumia staili za kimafia, unaweza kusababisha ufa mwingine wa kutoaminiana miongoni mwa viongozi na wanachama wa vyama hivyo viwili vya upinzani.
Lakini pengine kinachotia shaka zaidi katika hili ni uamuzi wa makachero wanaoitumia Amani Forum kuamua kutumia silaha ya amani kuwa turufu ya kumhakikishia Kikwete na CCM ushindi na kujenga taswira potofu vichwani mwa wananchi ambao ni wapiga kura, kwamba ushindi wa mgombea urais kutoka kambi ya upinzani ni kielelezo cha kuhatarisha umoja na mshikamano wa kitaifa.
Watu wenye kumbukumbu nzuri ni mashahidi wazuri kwamba, katika chaguzi za mwaka 1995, 2000 na 2005, silaha kubwa ambayo imekuwa ikitumiwa na CCM na makachero wanaofanya kazi ya uwakala wa chama hicho, ni kuwatisha wananchi kwamba, uamuzi wowote wa kuwachagua wapinzani katika nafasi za madaraka ya juu, ukiwamo urais ni sawa na kuchagua kutoweka kwa amani katika taifa.
Baadhi yetu bado tunakumbuka vyema namna katika uchaguzi mkuu mmoja, kituo kimoja cha televisheni nchini kwa kujua au kutokujua, kilitumia picha za vita vya wenyewe kwa wenyewe vya nchini Rwanda kama njia ya kuwaasa Watanzania kutoruhusu vyama vya upinzani ambavyo vilidaiwa kujijenga katika misingi ya udini, ukabila na ubinafsi.
Kama hiyo haitoshi, kipindi kingine kama hiki hiki ambacho Amani Forum imeanza kutumika kuwatisha wananchi, makachero wakilitumia Jeshi la Polisi walipenyeza nchini visu ambavyo vilikuwa na mipini inayofanana na rangi ya bendera ya chama kimoja cha siasa na kuvionyesha mbele ya wanahabari vikidaiwa kuingizwa nchini na chama hicho kama silaha za kujihami wakati wa kampeni na hatimaye kwenye uchaguzi.
Historia inaonyesha kuwa matumizi ya propaganda za namna hii, ambazo kwa bahati mbaya zimekuwa zikipuuzwa na kutopewa mikakati imara na ya kudumu ya kukabiliana nayo na makada na viongozi wa vyama vya upinzani, yamekuwa turufu kubwa ya ushindi kwa wagombea urais wa CCM.
Ni kwa njia na mbinu hizo basi, makachero wa CCM huku wakijua fika namna wanavyoweza kuwakoroga wananchi na kuwapiku wapinzani, leo hii wameamua kuja na mkakati huu wa Amani Forum kumhalalishia Kikwete ushindi wa kimbunga kwa namna ile walivyofanikisha ushindi wake mwaka 2005 na kabla ya hapo wa Mkapa mwaka 1995 na 2000.
Akili za kawaida zinathibitisha pasipo shaka kwamba, mkakati wa kumhalalisha Kikwete ulioanzishwa na Sheikh Yahya Hussein na kukwama baada ya kuonekana ukijengwa katika misingi ya imani potofu za kishirikina, sasa umejibadili sura na kujipambanua kwa njia ya Amani Forum ambayo naamini wajumbe wake wanampigia chapuo Kikwete huku wao wenyewe mioyoni mwao wakijua fika kwamba, hastahili kupewa sifa anazobebeshwa.
Hivi ni nani kati ya Kabourou, Mrema, na mama yangu Shida hajui kwa dhati ya moyo wake kwamba miaka mitano ya urais wa Kikwete imethibitisha pasipo shaka kuwa, kiongozi wetu huyo mkuu ametowesha matumaini makubwa aliyoingia nayo madarakani mwaka 2005?
Nitakuwa mkosefu wa hekima iwapo nitaandika kwamba katika kipindi chote cha miaka mitano Kikwete na serikali yake hawajafanya lolote katika medani za siasa, uchumi na jamii ingawa ukweli unabakia pale pale kwamba kama si kwa nguvu za kimtandao na kimfumo ambazo CCM inazo, anaweza akawa rais aliyefanya vibaya kuliko mwingine yeyote tangu taifa hili lianze mfumo wa kuwapa vipindi visivyozidi viwili marais wake.
Watu wenye nia njema na nchi hii wanaweza wakakubaliana nami iwapo nitaandika kwamba, turufu pekee kubwa aliyonayo Kikwete leo na ambayo inaonekana kumpa mwanga wa kushinda kipindi cha pili, ni ukweli kwamba chama kilichompa dhamana ya kutawala si chama cha kisiasa bali ni chama dola ambacho ustawi binafsi wa watu wanaokitumikia ni kuuendeleza urithi wa enzi wa marais kumaliza vipindi vyao viwili pasipo kuangalia na kuwapima katika mizani ya wazi kidemokrasia. Kama hiyo haitoshi, ni wazi kwamba udikteta wa kimfumo uliojengwa ndani ya CCM na madaraka makubwa ya kikatiba aliyonayo rais katika nchi hii, ni miongoni mwa mambo ambayo leo hii yanawatia hofu watu wenye uwezo mkubwa kuliko alionao Kikwete ndani ya CCM wa kariba ya akina Samuel Sitta, Edward Lowassa, Dk. Salim Ahmed Salim, Iddi Simba na wengine kuthubutu kuchukua fomu kumpinga ndani ya chama hicho na nje wakihofu kwamba kwa kufanya hivyo mwisho wao unaweza ukawa mbaya.
Ni wazi kwamba katika mazingira ya vitisho na udikteta wa kimfumo wa namna hii uliojengwa katika misingi ya kikomunisti ambayo ilirithiwa na CCM na serikali zake tangu zama za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kutoka China, Cuba, Korea Kaskazini na lililokuwa Shirikisho la Kisoshalisti la Kisovieti (USSR) ndiyo ambayo leo hii inatoa fursa kwa viongozi wa aina ya Kikwete kupewa sifa nyingi wanazomwagiwa na makundi ya aina ya Amani Forum ambazo aghalab hawastahili.
Hawa wanastahili kuitwa JK Forum badala ya Amani Forum.
HEKAHEKA za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu zimepamba moto, na tayari vituko kadha wa kadha vya kisiasa vimeshaanza kuonekana kadiri miezi na siku za kuelekea Oktoba 31 zinavyozidi kujongea.
Matendo na kauli kutoka kwa wanasiasa wa makundi mbalimbali yanayoshereheshwa na matukio ya kutia hamasa na wakati mwingine kukera kama si kushangaza, ni mambo yanayoonekana kuwa ya kawaida kusikika wakati huu taifa linapojiandaa kuwachagua Rais wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, wabunge, wawakilishi na madiwani.
Katika kipindi cha wiki moja au mbili tu zilizopita, taifa limeshuhudia matukio kadha wa kadha mazito kuhusu mustakabali wa nchi hii, ambayo ukiyaangalia utaona moja kwa moja mwelekeo wake unatuongoza kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi huo mkuu.
Ni katika kipindi hiki cha wiki moja, tumemsikia Rais Jakaya Kikwete kwa nyakati mbili tofauti, kwanza akiwa Mwanza na baadaye akizungumza kwa utaratibu aliojiwekea wa kulihutubia taifa kila mwishoni mwa mwezi, akionyesha kukerwa na kukemea tatizo la rushwa na lile la matumizi mabaya ya fedha wakati huu tunapoelekea katika mshikemshike wa uchaguzi mkuu.
Ni wazi kwamba akiwa kiongozi mkuu mwenye dhamana kubwa pengine kuliko mwanasiasa au mtu mwingine yeyote hapa nchini kwa wakati huu, Kikwete anawajibika kiuongozi, kivisheni na kimaadili kutoa matamshi ya namna hiyo yenye kutoa mwongozo na kuonyesha njia sahihi ambayo taifa linapaswa kupita wakati huu tunapojiandaa kwa ajili ya tukio kubwa la kihistoria.
Hata hivyo, kauli hiyo ya Kikwete imepokewa kwa hisia tofauti na wadadisi mbalimbali wa mambo, ambao baadhi yao wameonyesha kuiunga mkono na kummwagia sifa, huku wengine wakiitilia shaka na kuibuka na maswali mengi moja kati yao likiwa ni lile linalohoji, iwapo rais ameitoa kwa moyo wa dhati au kwa sababu tu ya kutaka kuonekana akitimiza wajibu wa kimamlaka unaomtaka aseme lolote jema hata kama atafanya hivyo pasipo kumaanisha kile asemacho.
Ni kwa sababu hiyo ndiyo maana wako waliotafsiri kauli hii ya Kikwete kuwa inayotoa mwelekeo sahihi wa huko tuendako, huku wengine wakiichukulia kuwa ni vitisho visivyo na maana ambavyo kiongozi huyo amekuwa na utamaduni wa kuvitoa kila mara, akijua kwa kufanya hivyo anatimiza wajibu wake wa msingi wa kiuongozi wa kuonyesha njia.
Pasipo kujali ni kundi gani kati ya haya mawili limetoa tafsiri sahihi kwa kile alichokisema JK, binafsi naiona kauli yake hiyo na nyingine nyingi zinazotolewa na makundi mbalimbali ya kijamii, kisiasa na kiserikali yanayomuunga mkono kuwa ni zenye lengo la kumfungulia njia pana zaidi ya ushindi wa kishindo wakati wa uchaguzi huo mkuu wa Oktoba.
Ukiacha kauli hiyo ya Kikwete, kipindi cha wiki hiyo hiyo moja, taifa limeshuhudia kuibuka kwa kikundi kingine cha msimu kilichojipa jina la Amani Forum, kikiongozwa na Mbunge wa Afrika Mashariki, Amaan Walid Kabourou na kujumuisha wanasiasa wengine kadhaa akiwamo, Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Shida Salum ambaye ni mama mzazi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Kwa mara ya kwanza, nilisikia taarifa za kuundwa kwa kikundi hiki kupitia katika kipindi maarufu cha asubuhi cha ‘Jambo Tanzania' kinachorushwa na kituo cha televisheni ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambako wajumbe wake wawili walijitokeza na kueleza kuhusu kuanzishwa na malengo yake.
Nilipowasikiliza wajumbe hao wawili ambao mmoja wao alikuwa Mrema, mara moja kumbukumbu zangu zilinirejesha mwaka 2005 na kabla ya hapo mwaka 2000 wakati wa kipindi kama hiki cha maandalizi ya uchaguzi mkuu, yalipoibuka makundi ya watu tofauti na zikajengwa hoja tofauti ambazo zote zilionekana kubeba ajenda moja kubwa ya kuilinda amani ya taifa hili kwa njia moja tu ya kuwahamasisha wananchi kuendelea kukichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) na aghalab kumpigia debe mgombea wake wa urais.
Kama ilivyokuwa mwaka 2000, walipoibuka watu kumpigia debe aliyekuwa rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa ndivyo inavyotokea leo hii kupitia Amani Forum ambayo viongozi wake wote kwa kauli moja wamesikika wakimpamba Kikwete kwa kila aina ya sifa na kuwaasa Watanzania waendelee kumuamini na kumchagua katika uchaguzi huo wa Oktoba.
Kwa namna ya kustaajabisha, kwanza kupitia TBC na baadaye katika mkutano wa hadhara huko Temeke Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam, viongozi wa Amani Forum wamejitokeza na kuanza kummwagia sifa Kikwete hata kufikia hatua ya kumtangaza kuwa mtu mwenye sifa za kipekee za kuachiwa kuendelea kutawala.
Kimsingi sina sababu hata moja ya kuwaona kuwa ni watu wa ajabu, wa hovyo au wasiofaa katika jamii, watu ambao kwa moyo wao wote na kwa nia njema, wameamua kumuunga mkono Kikwete, CCM au mgombea mwingine yeyote kugombea urais, ubunge, uwakilishi, udiwani au nafasi nyingine kwani wanao uhuru wao wa kikatiba kufanya hivyo.
Pamoja na ukweli huo, katika hili tatizo langu ni hii tabia ya kikachero ambayo imekuwa ikitumiwa na mawakala wa CCM walio serikalini, ndani ya chama hicho tawala na nje, kutumia ushawishi wenye hila, tena wakati usio wa kampeni kujenga hoja za kudumaza demokrasia ya vyama vingi na kuanza kumpigia debe rais aliye madarakani akipachikwa sifa hata asizostahili ili mradi tu kumhakikishia ushindi.
Ni wazi kwamba uamuzi huu wa kikachero wa kumjumuisha Mrema wa TLP na mama mzazi wa Zitto ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA katika kundi la kumpigia debe Kikwete wakati huu, kabla hata uteuzi wa wagombea haujaanza wakitumia staili za kimafia, unaweza kusababisha ufa mwingine wa kutoaminiana miongoni mwa viongozi na wanachama wa vyama hivyo viwili vya upinzani.
Lakini pengine kinachotia shaka zaidi katika hili ni uamuzi wa makachero wanaoitumia Amani Forum kuamua kutumia silaha ya amani kuwa turufu ya kumhakikishia Kikwete na CCM ushindi na kujenga taswira potofu vichwani mwa wananchi ambao ni wapiga kura, kwamba ushindi wa mgombea urais kutoka kambi ya upinzani ni kielelezo cha kuhatarisha umoja na mshikamano wa kitaifa.
Watu wenye kumbukumbu nzuri ni mashahidi wazuri kwamba, katika chaguzi za mwaka 1995, 2000 na 2005, silaha kubwa ambayo imekuwa ikitumiwa na CCM na makachero wanaofanya kazi ya uwakala wa chama hicho, ni kuwatisha wananchi kwamba, uamuzi wowote wa kuwachagua wapinzani katika nafasi za madaraka ya juu, ukiwamo urais ni sawa na kuchagua kutoweka kwa amani katika taifa.
Baadhi yetu bado tunakumbuka vyema namna katika uchaguzi mkuu mmoja, kituo kimoja cha televisheni nchini kwa kujua au kutokujua, kilitumia picha za vita vya wenyewe kwa wenyewe vya nchini Rwanda kama njia ya kuwaasa Watanzania kutoruhusu vyama vya upinzani ambavyo vilidaiwa kujijenga katika misingi ya udini, ukabila na ubinafsi.
Kama hiyo haitoshi, kipindi kingine kama hiki hiki ambacho Amani Forum imeanza kutumika kuwatisha wananchi, makachero wakilitumia Jeshi la Polisi walipenyeza nchini visu ambavyo vilikuwa na mipini inayofanana na rangi ya bendera ya chama kimoja cha siasa na kuvionyesha mbele ya wanahabari vikidaiwa kuingizwa nchini na chama hicho kama silaha za kujihami wakati wa kampeni na hatimaye kwenye uchaguzi.
Historia inaonyesha kuwa matumizi ya propaganda za namna hii, ambazo kwa bahati mbaya zimekuwa zikipuuzwa na kutopewa mikakati imara na ya kudumu ya kukabiliana nayo na makada na viongozi wa vyama vya upinzani, yamekuwa turufu kubwa ya ushindi kwa wagombea urais wa CCM.
Ni kwa njia na mbinu hizo basi, makachero wa CCM huku wakijua fika namna wanavyoweza kuwakoroga wananchi na kuwapiku wapinzani, leo hii wameamua kuja na mkakati huu wa Amani Forum kumhalalishia Kikwete ushindi wa kimbunga kwa namna ile walivyofanikisha ushindi wake mwaka 2005 na kabla ya hapo wa Mkapa mwaka 1995 na 2000.
Akili za kawaida zinathibitisha pasipo shaka kwamba, mkakati wa kumhalalisha Kikwete ulioanzishwa na Sheikh Yahya Hussein na kukwama baada ya kuonekana ukijengwa katika misingi ya imani potofu za kishirikina, sasa umejibadili sura na kujipambanua kwa njia ya Amani Forum ambayo naamini wajumbe wake wanampigia chapuo Kikwete huku wao wenyewe mioyoni mwao wakijua fika kwamba, hastahili kupewa sifa anazobebeshwa.
Hivi ni nani kati ya Kabourou, Mrema, na mama yangu Shida hajui kwa dhati ya moyo wake kwamba miaka mitano ya urais wa Kikwete imethibitisha pasipo shaka kuwa, kiongozi wetu huyo mkuu ametowesha matumaini makubwa aliyoingia nayo madarakani mwaka 2005?
Nitakuwa mkosefu wa hekima iwapo nitaandika kwamba katika kipindi chote cha miaka mitano Kikwete na serikali yake hawajafanya lolote katika medani za siasa, uchumi na jamii ingawa ukweli unabakia pale pale kwamba kama si kwa nguvu za kimtandao na kimfumo ambazo CCM inazo, anaweza akawa rais aliyefanya vibaya kuliko mwingine yeyote tangu taifa hili lianze mfumo wa kuwapa vipindi visivyozidi viwili marais wake.
Watu wenye nia njema na nchi hii wanaweza wakakubaliana nami iwapo nitaandika kwamba, turufu pekee kubwa aliyonayo Kikwete leo na ambayo inaonekana kumpa mwanga wa kushinda kipindi cha pili, ni ukweli kwamba chama kilichompa dhamana ya kutawala si chama cha kisiasa bali ni chama dola ambacho ustawi binafsi wa watu wanaokitumikia ni kuuendeleza urithi wa enzi wa marais kumaliza vipindi vyao viwili pasipo kuangalia na kuwapima katika mizani ya wazi kidemokrasia. Kama hiyo haitoshi, ni wazi kwamba udikteta wa kimfumo uliojengwa ndani ya CCM na madaraka makubwa ya kikatiba aliyonayo rais katika nchi hii, ni miongoni mwa mambo ambayo leo hii yanawatia hofu watu wenye uwezo mkubwa kuliko alionao Kikwete ndani ya CCM wa kariba ya akina Samuel Sitta, Edward Lowassa, Dk. Salim Ahmed Salim, Iddi Simba na wengine kuthubutu kuchukua fomu kumpinga ndani ya chama hicho na nje wakihofu kwamba kwa kufanya hivyo mwisho wao unaweza ukawa mbaya.
Ni wazi kwamba katika mazingira ya vitisho na udikteta wa kimfumo wa namna hii uliojengwa katika misingi ya kikomunisti ambayo ilirithiwa na CCM na serikali zake tangu zama za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kutoka China, Cuba, Korea Kaskazini na lililokuwa Shirikisho la Kisoshalisti la Kisovieti (USSR) ndiyo ambayo leo hii inatoa fursa kwa viongozi wa aina ya Kikwete kupewa sifa nyingi wanazomwagiwa na makundi ya aina ya Amani Forum ambazo aghalab hawastahili.
Hawa wanastahili kuitwa JK Forum badala ya Amani Forum.