Ni jinsi gani unavyoweza kujikinga na dawa(sumu) wanazotumia wezi usiku ili ulale fofofo wakuibie?

nacho1

Member
Aug 31, 2014
80
65
kuna wizi umezuka maeneo nayoishi ambapo wezi hao wanatumia dawa inayowafanya waliomo ndani ya nyumba wanayotaka kuiba kulala fofofo kisha kuwaibia.

Mimi natafuta namna yakukabiliana na hili tatizo binafsi na pia kuisaidia jamii inayonizunguka waweze kujikinga na huu uhuni wa wezi.

Wanakemia, waamini wa dini mbalimbali na wajuvi wa mambo kama mshana jr. Naomba ushirikiano kutatua hili tatizo
 
Lala na beseni la maji ndio dawa pekee wakipuliza asubuhi utakuta beseni lina povu ujue usiku kulikuwa na shughuli kwako isipokuwa haikufanya kazi, ning'iniza kikombe cha bati mlangoni wakishika mlango tu kinaanguka kelele zake hata wenyewe watakimbia maana huwa kina kelele sana mkuu
 
Umenikumbusha miaka kadhaa iliyopita walitufanyia mchezo huo!
Yaani walitoa nguo zote hata zilizotundikwa nyuma ya mlango hakuna hata aliyeshtuka!
Hiyo kitu mbaya sana aiseee!

Suluhisho ni kulock mlango kwa ndani na kufuli unapoenda kulala ili hata kama watapulizia kupitia durishani basi wasiweze kuingia!!Sisi tulifanikiwa kwa njia hiyo......
Nasikia huwa wanatumia chloroform
 
Lala na beseni la maji ndio dawa pekee wakipuliza asubuhi utakuta beseni lina povu ujue usiku kulikuwa na shughuli kwako isipokuwa haikufanya kazi, ning'iniza kikombe cha bati mlangoni wakishika mlango tu kinaanguka kelele zake hata wenyewe watakimbia maana huwa kina kelele sana mkuu
hiyo kitu ni Kali sana mkuu!
Wanapulizia kupitia nafasi zilizopo kwenye dirisha kabla ya kuingia kwa hiyo hata kikombe kidondoke huwezi kusikia kabisa!
Mara ya pili nilishuhudia wakati nipo chuo second year washkaji zangu kwenye zile hostel za mtaani waliibiwa kila kitu nyumbani nzima!

We fikiria mpaka wanaburuza masabufa na majiko ya gesi ila hakuna aliyeshtuka.....
.
 
Dawa ni hiyo ya kulala na maji ndaji ya beseni na ndoo kama tahadhari ila kama dawa ikipulizwa nyingi na ikakufikia direct inaweza ikakudhuru na wakaingia usisikie.cha kusaidia ni kufunga taa za ulinzi ili wapate hofu
 
Fanya ivi kabla ya kulala uwe unasali iyo ndo dawa yao,kama ni mwisilamu uwe unasali rakaa mbili kabla ya kulala, ama ukishindwa kusali rakaa mbili uwe unatoa sadaka kwa kunuia kutoibiwa,nina uhakika hao wezi hawataisogelea nyumba yako biithinallah
 
Njia ya kwanza ni hiyo kama imetumika nusu kaputi lakini kama huko mtaani kwenu munaibiwa halafu waloibiwa wanagundua usiku huohuo basi tambua sio nusu kaputi kinachofanywa ni hiki(nakupa elimu ya darasani) epuka kulala haraka ukiingia chumbani jaribu maana kwa kufanya ivyo itakuchukua dk 15 tu kukuchukua usingizi mzito utakaodumu kwa nusu saa kabla ya kuja usingizi wa kawaida, kipindi cha usingizi mzito hata ipigwe kelele ya namna gani auwezi kusikia na hapa kwa wezi wenye kufahamu kitu hiki basi hapo wanatumia muda huu kukuibia utaweza kusikia kelele kama zitajirudia kwa muda mrefu lakini sio kwa muda mfupi na wanaweza kukuhamisha kitandani na usijue nafikiri nitakua nimekusaidia.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom