Ni jinsi gani Hezbollah iliweza kushinda vita dhidi ya Israel? (2006)

Hezbolla hawaja wahi kushinda vita dhidi ya Israel.


Hakuna taifa la Kiarabu limewahi kushinda vita dhidi ya israel.

Waarabu ni watu wa ajabu sana.. hadi leo wanasema vita ya siku 6 eti walishinda.

Na mtapata tabu sana.

Israel anamkana Mungu wako/Yesu
Hautambui ukristo wako
Anakuona wewe ni taka taka tu usie na thamani yoyote,

Na bado unamkingia kifua,,
 
Sasa ndugu yangu hao ndugu zao waarabu mna connection gani na we mwenye ngozi nyeusi.

Kama kuna ukweli usemwe.

Waarabu hawaja wahi shinda vita hata moja dhidi ya wayahudi.

Maneno mengi, kazi hakuna
Na mtapata tabu sana.

Israel anamkana Mungu wako/Yesu
Hautambui ukristo wako
Anakuona wewe ni taka taka tu usie na thamani yoyote,

Na bado unamkingia kifua,,
 
Na Waziri wao mkuu kujiuzulu daadeki, hawaamini ile vita mpaka leo.
story ya uongo hii, miaka yote israel anatawala anga la Lebanon na hakuna anayemgusa sa anashindwaje na kajikikundi? yaani waarabu washinde si dunia ingesimama kwa shangwe?
 
Sasa ndugu yangu hao ndugu zao waarabu mna connection gani na we mwenye ngozi nyeusi.

Kama kuna ukweli usemwe.

Waarabu hawaja wahi shinda vita hata moja dhidi ya wayahudi.

Maneno mengi, kazi hakuna


Kwenye hiyo vita, nyuma ya israel kulikuwa na wakina nani waliomsaidia? Njoo na fact with evidence
 
Samahani hivi Yesu alipokiita kile kizazi "kilicholaaniwa... joka wana wa majoka..." hivi kilicholaaniwa huwa kimebarikiwa? Hivi aliposema "...hakuna hata jiwe moja litakalobaki bila kubomoshwa!!" Alimaanisha mashujaa hao "waliotawaliwa na wamisri, waajemi, waroma kisha waarabu ushujaa na ubarikiwa wao ulikuwa wapi dahari ya miaka hiyo hata wakakimbilia mataifa ya ulaya ambako nako walikutana na Hitler wateule hao?
Una ahakika gani km hawa jamaa ndio wale waliotajwa kwe ye baibo
 
Umenipa mwanga mzuri sana, akhsante sante leta na mwendelezo... Kongole Kongole kwa sauti ya juuuuuuuuuuuuuu
Hii ni vita iliyojulikana kama July War au 2006 Lebanon war unakuwa hujakosea kabisa, vita hii ilichukua takribani siku 34 tu, ni muda mchache tu, lakini kuna mengi ya kufahamu juu ya hii vita, naomba uketi usome kwa makini mwanzo mwisho.

CHANZO CHA VITA
Israel ilikuwa na wafungwa(Lebanese Prisoners) akiwemo Samir Al-Quntar na ndugu zake, Hezbollhah walikuwa wanahitaji wafungwa hao waachiliwe ki diplomasia na wapelekwe Lebanon, Israel ilikataa kata kata.

Lebanon ilishavunja sheria mara 100 katika kuvuka blue line kati ya mwaka 2000-2006 ni katika wakati huo huo Israel alivunja sheria mara 11,782 katika anga,maji na ardhini kwa kuvuka blue line.

Blue Line
ni alama ya mpaka kati ya Lebanon na Israeli iliyowekwa na Umoja wa Mataifa mnamo 7 Juni 2000 kwa madhumuni ya kuamua ikiwa Israeli imejiondoa kabisa kutoka Lebanon.

Ni jinsi gani sasa Hezbollah watafanikisha kuwapata wafungwa wao? Njia ilikuwa ni moja tu, kuwakamata askari wa Israel(IDF), ndipo ikaandaliwa operation iliyojulikana kwa jina la Operation truthful promise, nia ikiwa ni kukamata askari wa IDF ili waje wabadilishane na wafungwa wa Lebanese waliokuwa wanashikiliwa na Israel hapo baadae.

Operation Truthful promise au Hezbollah cross border raid kwa jina lingine, ndipo ilipofanyika mnamo tarehe 12 July 2006.

Shambulizi hili ni pale Hezbollah waliporusha maroketi katika sehemu mbali mbali ndani ya Israel wakitumia rockets zijulikanazo kama Kayusha, walivuka Blue Line na kuingia Israel wakipiga ambush Humvee za IDF mbili zilizokuwa mpakani kabisa mwa Israel karibu na uzio na kuzilipua kwa Anti Tank Guided Missile(ATGM), hii ilipelekea askari wawili(2) wa IDF kutekwa nyara, watatu(3) waliuawa pale pale, Pia katika jaribio lililofeli la askari wa Israel kwenda kuwaokoa wenzao, askari watano(5) waliuawa katika jaribio hilo la uokoaji nchini Lebanon.

Hezbollah ilidai wafungwa wake waachiliwe kwa kubadilishana na wafungwa wa IDF ambao walikuwa ni mateka nchini Lebanon, Israel wakajibu hapana haiwezekani kwa wakati huo prime minister wa Israel alikuwa Ehud Olmert.

Baada ya Israel kukataa ilikuwa wazi vita inakwenda kutokea.

Ndipo waziri mkuu wa Israel akasema "Lebanon italipa kwa kitu walichofanya" na pia bwa Ehud Olmert alisisitiza "Lebanon itegemee maumiu makali sana na tutafika mbali zaidi"

View attachment 1469714

Naam yalikuwa ni maneno ya bwana Ehud Olmert waziri mkuu wa Israel, hakika Hezbollah alikuwa amegusa pabaya, sasa kinachokwenda kutokea unakijua, unajua Israel ilishapigana vita ya siku 6 na na kuwa mshindi dhidi ya Egypt,Syria na Jordan? Na sasa wanakwenda kukabiliana na Hezbollah kikundi kidogo cha wanamgambo? keti hapo hapo uendelee kusoma.

Ni katika siku hio hio (12 Julai 2006), Baraza la Mawaziri liliamua kumpa mamlaka Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na manaibu wao kutekeleza mpango mzima waliokuwa wamepanga dhidi ya kuishambulia vibaya Lebanon, Waziri mkuu akasema katika shambulio hilo inabidi wasishambulie makazi ya watu, Kamanda wa jeshi la anga Israel Dan Halutz alisema "Ikiwa askari wa Israel hawatorudishwa, tutarudisha saa ya Lebanon miaka 20 nyuma"

Pia mkuu wa jeshi la Israel upande wa kaskazini alisema "Hii ni vita kati ya Israel na Lebanon, sasa tushambulie wapi? kama wapo Lebanon, tutapiga Lebanon haijalishi wapo sehemu gani, iwe kusini au Hezbollah walipo."

Pia Serikali za AMerika, Uingereza, Ujerumani, Australia, na Canada zilidai ni haki ya Israeli kujilinda. Serikali ya Amerika ilijibu zaidi kwa kuidhinisha ombi la Israeli la kupatiwa Guided Missiles zenye accuracy ya hali ya juu.

Upande wa Hezbollah sasa kiongozi wao bwana Hassan Nasrallah alisema "Israeli wamevunja mpango wa zamani wa kuwaachilia wafungwa hawa, na kwa kuwa diplomasia imeshindwa, vurugu ndio chaguo pekee lililobaki". Nasrallah alitangaza kwamba "hakuna operesheni ya kijeshi itakayoweza kuwaokoa wafungwa hawa ... Njia pekee, kama nilivyoonyesha, ni ile ya mazungumzo yasiyokuwa ya moja kwa moja na kubadilishana wafungwa".

View attachment 1469718

VITA INAANZA
Na vita ikatangazwa rasmi, ni tarehe 12 julai 2006, Wakati wa siku ya kwanza ya Vita, Jeshi la Anga la Israeli, jeshi la maji walifanya mashambulio zaidi ya 100 dhidi ya kambi za Hezbollah kusini mwa Lebanon, kati yao makao makuu ya mkoa huko Ya'tar. Madaraja matano ya kupita kwenye mito ya Litani na Zahrani pia yakaharibiwa, iliripotiwa kumzuia Hezbollah kuhamisha askari waliotekwa nyara.

Naam hakika Israel ilishambulia kwa nguvu haswa toka angani na ardhini, ilikuwa si mchezo.

Mashambulio kutoka ardhini, baharini na angani yaliendelea katika siku inayofuatia. Miongoni mwa sehemu zilizopigwa yalikuwa makao makuu ya Hezbollah katika vitongoji vya kusini vya Beirut na vile vile ofisi na nyumba za uongozi, kituo cha Televisheni cha al-Manar na kituo cha redio cha al-Nour, runways na depo za mafuta za Uwanja wa ndege wa kimataifa Rafic Hariri Beirut. Vile vile vilivyolengwa ni kambi za Hezbollah, depo na madaraja, barabara na vituo vya petroli kusini mwa Lebanon. Raia 44 waliuawa kwa siku hio. sio mchezo.

Israel hakuishia hapo, Jeshi la Anga la Israeli katika usiku wa manane, 13 Julai, lilishambulia na kuharibu roketi launchers 59 ambazo zilikuwa ni medium range ziitwazo Fajr zilizowekwa kusini mwa Lebanon. Operesheni inadaiwa ilichukua tu dakika 34 kutekeleza lakini ilikuwa matokeo ya miaka sita ya kukusanya akili na kupanga. Kati ya nusu na theluthi mbili ya uwezo wa roketi wa Hezbollah wa wastani IDF ilidai kuwa umefutwa. Kulingana na waandishi wa habari wa Israel Amos Harel na Avi Issacharoff operesheni hiyo ilikuwa "hatua ya kijeshi ya kuvutia zaidi ya Israeli" na "pigo kubwa kwa Hezbollah". Katika siku iliyofuatia IAF ilishambulia na kuharibu sehemu kubwa ya makombora marefu ya Hezbollah Zelzal-2.

"Makombora yote ya masafa marefu yameharibiwa,"Kamanda Halutz alisema na pia aliiambia serikali ya Israeli, "tumeshinda vita."

Ni katika siku za mwanzoni kabisa jeshi la Israel walisema wamemaliza kambi zote za Hezbollah kwa mashambulizi na wamepiga launchers za Kayusha rockets, walisema Hezbollah sio kitu na vita inaisha mapema kabisa.

Kufikia siku ya nne ya vita IDF ilikuwa haioni pa kupiga kwani targets zote 83 kwenye orodha zilikuwa zimeshapigwa.
Sehemu kubwa za miundombinu ya raia ya Lebanon ziliharibiwa, pamoja na barabara urefu wa kilomita 640, madaraja 73, na sehemu nyingine kama vile uwanja wa ndege wa kimataifa wa Beirut Rafic Hariri, bandari, vyanzo na vituo vya matibabu ya maji taka, vyanzo vya umeme, vituo vya mafuta 25, sehemu 900 za kibiashara, shule 350 na hospitali mbili, nyumba 15,000 ziliharibiwa vibaya na Nyumba zaidi ya 130,000 ziliharibiwa kiasi.

Hezbollah inajibu.
Kituo cha Televisheni cha Hezbollah al-Manar kilionya jamii za Kiarabu na Kiebrania juu ya shambulio la roketi baadaye. Vile vile Hezbollah ilituma ujumbe wa maandishi kuonya wakaazi wa Israeli waondoke katika nyumba zao ili wasipatwe na shambulio roketi.

Hakika vita imesimama sasa, sasa ni kupiga nikupige.
Tofauti na Israel ilipodhani kuimaliza Hezbollah, kumbe ndio kwanza kama ni movie ya Titanic bado watu walikuwa hawajaingia hata melini kuanza safari.

Tuendelee...

Kikosi cha roketi cha Hezbollah kilirusha kati ya makombora 3,970 na 4,228 kwa kiwango cha zaidi ya makombora 100 kwa siku, kiasi ambacho hakijawahi kutokea tangu Vita vya Iran na Iraqi. Karibu 95% ya hayo yalikuwa ni makombora ya 122mm( Katyusha) kombora hizo zilikuwa zina vichwa vya kilo 30, na zilikuwa zinasafiri hadi km 30 . Takriban 23% ya makombora haya yaligonga miji na maeneo yaliyojengwa kaskazini mwa Israeli, wakati mabaki yaligonga maeneo ya wazi.

Miji iliyopigwa ilikuwa Haifa, Hadera, Nazareti, Tiberia, Nahariya, Safi, Shaghur, Afula, Kiryat Shmona, Beit She'an, Karmiel, Acre, na Ma'alot-Tarshiha, na miji kadhaa, kibbutzim, moshavim, na Vijiji vya Druze na Benki ya kaskazini magharibi pia ilipigwa.

Labda niweke mambo sawa hizi rockets za Katyusha katika mapigano ya nyuma zilitumika sana, hivyo hata kipindi IDF inakwenda kumtandika Hezbollah waliona hizo kombora sio kitu na walijua ndio kitu Hezbollah ndicho walichokuwa wakitegemea zaidi, kumbe haikuwa hivyo.

Hezbollah toka mara ya kwanza kwenye ile mission yao Operation truthful promise walianza kurusha hizo Katyusha ambapo hazikuua raia yeyote yule Israel, roketi hizi zilikuwa ni za ki zamani hivyo Hezbollah walizitumia kuwa pumbaza Israel na Israel wakapumbazika kweli.

Japo Mashambulio ya roketi ya Hezbollah pia yalilenga na kufanikiwa kupiga kambi za jeshi nchini Israeli.hata hivyo uongozi wa jeshi la Israel ulikuwa mkali sana na marufuku kabisa kwa vyombo vya habari vya Israeli kuripoti matukio kama haya. Agizo la wakati wa vita kwa vyombo vya habari lilisema kwamba "Uongozi wa Jeshi hatakubali ripoti za Hezbollah kupiga makombora katika kambi za IDF na au vifaa vya jeshi."

Naam kwa kutumia mbinu mpya na mikakati, silaha mpya na advanced kabisa, Hezbollah ndipo ilipogeuza mchezo mzima juu chini na chini juu. Ni vita ambayo Hezbollah waliita "surprises".
Ndipo Hassan Nasrallah akasema "ile surprise ambayo tumeahidi ndio inaanza"

Surprise ya kwanza kutoka Hezbollah
Kuna meli (Warship) moja ya ya Israel ambayo ni very powerful according to IDF, ilijulikana kama Hanit, nadhani unaelewa unaposikia warship, ni meli ya kivita na ina uwezo mkubwa wa kuzuia missiles na kushambulia.Ni moja ya meli iliyotumika pia kushambulia, kumbuka Israel ilishambulia toka angani, majini na ardhini, na silaha ilikuwa ikiogopeka majini ilikuwa ni hii Hanit warship.

Hanit ilipigwa kombora linalofahamika kwa jina la C-802 lililo tengenezwa China na kuwa modified na Iran, range yake ni km 120, mpaka hapo Israel ilifahamu fika kwamba sasa meli zake hazina maana tena mbele ya Hezbollah pia Israel ilifahamu fika sasa ndio imeanza kuona vita halisi.

Katika shambulio hilo askari wanne waliuawa waliokuwa katika meli hio Staff Sergeant Tal Amgar, Corporal Shai Atas, Sergeant Yaniv Hershkovitz, na First Sergeant Dov Steinshuss.

2_wa.jpg

1_wa.jpg

3_wa.jpg

Surprise ya pili
Wakati huu Hezbolla walipanga mashambulizi dhidi ya mji wa Haifa, Israel ikiwa inategemea Hezbolla bado atakuwa anatumia Katyusha misssiles, kumbe haikuwa hivyo, na hapo ndipo surprise ya pili ikatokea, ulikuwa ni wakati Israel kukutana na surprise ya pili.

Ndipo kombora aina Zelzal-2 na aina ntingine za kombora toka Iran zikaanza kumiminika kwa wingi ndani ya Israel, kombora hizi zilikuwa zinafika sehemu yeyote Israel na pia zilikuwa zinabeba warhead yenye mlipuko wa hali ya juu takribani kilo 600. Ndivyo vita ilivyoendelea

Haifa ni mji muhimu sana katika uchumi wa taifa la Israel, na sasa Israel ilibidi iseme kwa kitu walichofanya Hezbollah juu ya kushambulia haifa hakika ni strategy ya hatari sana waliotumia tokana na makazi ya watu, lakini Israel pia ilipiga makazi ya watu.

Hezbollah ikiwa inalenga sehemu muhimu na za kiuchumi vita iliendelea, Israel alikuwa akipiga kofi Hezbollah anarudisha vile vile na vita ikaendelea

Haifa hakika ilishambuliwa, power plant,barabara, majengo, hata magari yalikuwa yanawaka moto tu , raia walikufa wengi, kambi za jeshi zilipigwa.

Haifa ikawa target ya Hezbollah, Israel ikaona hali ni mbaya, kwa sababu walichokuwa wakifanya Hezbollah ilikuwa ni kulipiza kama Israel inavyopiga makazi ya Lebanon na wao wanapiga Haifa city.

Ni wakati huo Israel ikaona Hezbollah hataki mchezo na hapo Israel akaogopa kuipiga Beirut kwa kujua kwamba Tel-Aviv ingepata mvua ya makombora, na utakuwa mwanzo wa kuipoteza Tel-Aviv.

Hakuna asiyejua kwamba USA na Israel hawawezi kabisa kuwa na diplomasia na kundi kama Hezbollah pia wanajulikana kwa uvunjifu wa amani na kukiuka haki za binadamu hasa kwa nchi zetu tusiojiweza.

Kwa maana diplomasia ilifeli mwanzoni hivyo njia pekee ili uweze kusikilizana nao ni kutumia nguvu, naam Haifa iliendelea kumiminiwa missiles.

Mnamo Julai 16, wafanyakazi wanane wa Reli ya Israeli waliuawa kwa kupigwa na roketi kwenye kituo cha treni. Kiongozi wa Hezbollah Hassan Nasrallah alisema hapo awali Hezbollah ilikuwa inalenga makombora yake kwenye "vituo vya kijeshi tu". Lakini kwa kuwa Israeli, alisema, amepiga raia basi Hezbollah hakuwa na chaguo ila kujibu kwa kulenga miji ya Israeli.

F060813ff02-640x400.jpg

Haifa

13assess600.jpg

Haifa Israel
Hezbollah ikawa inajikadiria tu irushe missile ngapi kama Israel akiwashambulia. Umoja wa mataifa ukaanza kufanya mazungumo juu ya kukatishwa vita hivyo, wakati mwanzoni wali support, so Israel ana hali mbaya, lakini UN haikufanikisha hilo jambo mara moja,

Surprise ya tatu
Kuna Tanks zilikuwa zinajulikana kama merkava tanks za 4th generation, hakika zilisifiwa kwa nguvu, uwezo wa kupambana, maneuvers, pia timu za waliokuwa waki operate hizi tanks walijulikana kama the best ones katika mafunzo duniani.

Pia zilisifika kuwa ni hatari zaidi duniani na very powerful, kwa uwezo wake mkubwa wa hizi tanks katika mapambano au aina yeyote ya battle field IDF waliikubali sana Merkava.

Licha ya sifa zote hizo ilizonazo Hezbollah iliweza kujua weakness zake na kuweza kuwashangaza IDF, yeah ni surprise nyingine, pia walikuwa wana silaha kwa ajili ya kuhakikisha Merkava ina baki chuma chakavu.

Ilikuwa ni Anti Tank Missile toka Russia na hapo kulikuwa na Milan pamoja na Kornet, vitu ambavyo IDF waliona sasa maji yamezidi unga, katika shambulio baya kutokea ni baada ya Hezbollah kuipiga tank huko Hujeir, hakika hakuna aliyepona, crew nzima waliisha pale pale.

Pia Abram Tank ya USA ilipigwa pia. Kama tanks za kawaida kama Merkava za mwanzoni almost zaidi ya 50 ziliharibiwa.
Pia katika missiles hizo walikuta missile za Iranian Made.

Kama kawaida vita ya ana kwa ana ilikuwepo(ardhini)/(ground war).

Kwa kutumia jeshi dogo lililoiva kisawa sawa, Hezbollah hakika hawa askari wake wa ardhini walikuwa highly trained(mafunzo ya hali ya juu), pia walikuwa na vifaa vyote vya kisasa kama jeshi la Israel kama vile night goggles,vifaa vya mawasiliano na pia wakati mwingine walionekana wakiwa na uniforms kama za IDF, na vifaa vya kivita vya kisasa kabisa.

Askari mmoja wa Israeli ambaye alishiriki katika vita hio alisema kuwa "wapiganaji wa Hezbollah huwezi kuwafananisha na Hamas au Wapalestina, wameiva na wana mafunzo ya hali ya juu. Hakika sote tulishangazwa".

Harakati za kusimamisha vita
Wakati jeshi la IDF likiwa linakumbana na mbinu mpya za kijeshi pia kichapo kikali, UN wakaona ni wakati wa kusimamisha vita kwani Israel wapo vibaya mpaka hapo, na jeshi la Hezbillah morali ya vita ndio kwanza kama wanaanza, hakika ipo wazi ni katika wakati huu, IDF mashambulizi yao ni ya kusua sua kwa sababu zifuatazo.

1-Wanaogopa kuendelea kupiga miji kama Beirut kwa sababu Hezbollah tayari wana missiles za kufika Tel-Aviv hivyo wangejibu , hivyo vita inge changamka.

2-Israel walishambulia targets zaidi ya 100 za Hezbollah, lakini kinyume na walivyotegemea hakika jeshi la Hezbollah lilikuwa na nguvu bado na mirindimo iliendelea, ipo wazi niliandika ilifikia kipindi Israel wakaanza kukuna vichwa ni wapi wapige tena.

3-Israel walikuwa wameshambulia kwa nguvu sana mwanzoni, hivyo ni katika wakati huu silaha zao zilitumika nyingi sana na nyingine ziliharibiwa,hivyo kulikuwa na upungufu wa silaha tofauti na mwanzoni,ukizingatia kuna kambi zilipigwa na wanajaeshi wa IDF kuuliwa, vifaa vya vita kama ile meli ya Hanit iliyopigwa, kwani tokea baharini walirusha shells 2500 kuelekea Lebanon.

Mazungumzo ya kusimamisha vita hayakufanyika kwa mara moja, yaliendelea kwa wiki kadhaa kwa pande mbili kushindwa kuelewana,UN ikiwa mpatanishi , kutokuelewana huko ni pamoja na Lebanon kusema vita isimame pasipo masharti yeyote wakati huo Israel iliomba kuwe na masharti kuhusu kuachiliwa kwa IDF soldiers wawili.

Hata hivyo harakati za kusimamisha vita zikiongozwa na UK na US zilicheleweshwa makusudi wakijua labda Hezbollah inaweza kuwa defeated, lakini haikuwa hivyo, na ipo wazi vita ilisimamishwa kwa kuwa walijua Hezbollah kuwa defeated ni ngumu sasa na matokeo yatakuwa mabaya.

Ni julai 25 bibi Condoleeza Rice alikutana na waziri mkuu wa Israel Ehud Olmert katika harakati za kuzuia vita alisikika akisema "Tunaposhughulika na hali za sasa, tunahitaji kila wakati kujitambua na kuangalia ni aina gani ya Mashariki ya Kati tunajaribu kujenga. Ni wakati wa Mashariki ya Kati mpya"

english_mediacenter_events_publishingimages_7de0dc36e168457796a28ac4d0acce26condbig2.jpg
Yalikuwa ni maneno ya busara toka kwa Secretary of state of US bi Condoleeza Rice baada ya kichapo heavy toka kwa Hezbollah pia waziri Olmert aliongelea wakati mgumu wanaokutana nao alisikika akizungumzia jinsi vita ilivyo waweka wanachi wa Israel zaidi ya 1.5 million katika hali mbaya, kazi zikiwa zimesimama hivyo ni jukumu lao kuwasaidia.

Katika hotuba hio waziri Olmert alizungumza wazi kwamba walikuwa wanahitaji suluhisho kusimamisha vita, Hakika kipigo heavy kiliwafanya Israel wafuate matakwa ya Hezbollah bila wao kupenda.



Baada ya pande mbili zote kuridhiana na Israel kuomba wanajeshi wake waachiliwe, Israel na Hezbiollah walisimamisha vita kwa usimamizi wa UN(US), ilikuwa ni saa 2 asubuhi ya 14 august 2006 vita ilisimama rasmi huku Hezbollah ikiwa imefanikiwa pakubwa kwa jambo walilokuwa wanahitaji, wafungwa wa Hezbollah akiwemo bwana Samir Al-Quntar kuachiwa na ndugu zake, vile vile Israel walikabidhiwa askari wao na vita ikawa imesimama.

Hakika hakuna aliyeamini kama Hezbollah angefanya jambo hilo, inasemekana kwamba licha ya Israel kupiga kituo cha television cha Lebanon kwa jina la Al-Manar ilichukua dakika mbili tu wakarudi hewani.

Wakati wa vita Jeshi la Anga la Israeli ilifanya combat missions 11,897, ambapo ilikuwa zaidi ya idadi ya ya Vita vya Oktoba 1973 (11,223) na mara mbili katika Vita vya Kwanza vya Lebanon (6,052).

Wanajeshi wa Israeli walirusha makombora 170,000, zaidi ya mara mbili ya idadi katika Vita vya Oktoba 1973. Afisa mwandamizi katika IDF Armored Corps aliiambia gazeti la Haaretz kwamba atashangaa ikiwa ikitokea kwamba hata wapiganaji watano wa Hezbollah wameuawa na mikombora 170,000.

Kulingana na matokeo ya upelelezi wa kijeshi wa baada ya vita uchunguzi wa kambi ya IDF ulifanikiwa kuharibu Katyusha rockets 100 kati ya 12,000. Tofauti na jeshi la Israel walivyodhani.

Maafisa wa Amerika walidai kwamba Waisraeli hawakufanikiwa katika ufanisi wa vita vya anga dhidi ya Hezbollah na walionyesha kutofaulu kupiga kwa kiongozi yeyote wa Hezbollah licha ya kuteremsha tani 23 za mabomu kwenye makao yake makuu.

Kulingana na mchambuzi wa kijeshi William Arkin alisema kuna ushahidi mdogo kwamba Jeshi la Anga la Israeli lilifanikikwa kidogo sana katika madai ya kuangamiza roketi za masafa marefu na mafupi katika siku za kwanza za vita. Alitupilia mbali madai yote kama "upuuzi" na "hadithi".

Katika kumbukumbu ya miaka sita ya vita vya Lebanon Hezbollah mwenyekiti Hassan Nasrallah alidai kuwa Hezbollah alijua kuwa Waisraeli walikuwa wakikusanya taarifa za kiintelejensia dhidi ya makombora yao yalipo na walifanikiwa kuyahamisha bila kugunduliwa. Maeneo mengi yaliyoshambuliwa na jeshi la anga la Israeli kwa hivyo yalikuwa tupu.

Hata hivyo Israel walidai katika vita hivyo Iran ilihusika kutoa msaada wa vifaa mbali mbali pia Gazeti la Israel la Haaretz lilielezea Hezbollah kuwa ilifundishwa, pia walikuwa na ujuzi,walijipanga vizuri, na pia silaha za kisasa kutoka majeshi ya Syria, Iran, Russia, na China.

Hassan Nasrallah alishawahi kusikika akisema kuwa wana makombora ya kuirudisha Israel nyuma kwenye zama za mawe.

Naama na hapo ndio mwisho wa vita hii ambayo askari 121 wa IDF waliuawa, helicopters ziliharibiwa, meli, vifaru nauharibifu mkubwa wa miundo mbinu.

Pia jeshi la Hezbollah walipoteza askari wao 250.

Hakika kikundi kidogo kabisa cha jeshi la Hezbollah kiliweza kuihangaisha nchi ya Israel na kuishinda katika vita Israel, mpaka Israel kuona vita imekuwa chungu licha ya kutumia uwezo wake,intelejensia, pia kutumia jeshi la anga, ardhi na maji kuipiga Hezbollah, je swali langu.

Israel itaweza ku defeat Iran ambapo ndio walioipatia Hezbollah mafunzo ya kijeshi,silaha na mbinu? kila siku naona watu wana linganisha Iran na Israel.



khamsrallamani-e1569711056798.jpg

Khamenei, Nasrallah kiongozi wa Hezbollah na Qasim Suleimani (enzi za uhai wake).


MWISHO
 
Hii ni vita iliyojulikana kama July War au 2006 Lebanon war unakuwa hujakosea kabisa, vita hii ilichukua takribani siku 34 tu, ni muda mchache tu, lakini kuna mengi ya kufahamu juu ya hii vita, naomba uketi usome kwa makini mwanzo mwisho.

CHANZO CHA VITA
Israel ilikuwa na wafungwa(Lebanese Prisoners) akiwemo Samir Al-Quntar na ndugu zake, Hezbollhah walikuwa wanahitaji wafungwa hao waachiliwe ki diplomasia na wapelekwe Lebanon, Israel ilikataa kata kata.

Lebanon ilishavunja sheria mara 100 katika kuvuka blue line kati ya mwaka 2000-2006 ni katika wakati huo huo Israel alivunja sheria mara 11,782 katika anga,maji na ardhini kwa kuvuka blue line.

Blue Line
ni alama ya mpaka kati ya Lebanon na Israeli iliyowekwa na Umoja wa Mataifa mnamo 7 Juni 2000 kwa madhumuni ya kuamua ikiwa Israeli imejiondoa kabisa kutoka Lebanon.

Ni jinsi gani sasa Hezbollah watafanikisha kuwapata wafungwa wao? Njia ilikuwa ni moja tu, kuwakamata askari wa Israel(IDF), ndipo ikaandaliwa operation iliyojulikana kwa jina la Operation truthful promise, nia ikiwa ni kukamata askari wa IDF ili waje wabadilishane na wafungwa wa Lebanese waliokuwa wanashikiliwa na Israel hapo baadae.

Operation Truthful promise au Hezbollah cross border raid kwa jina lingine, ndipo ilipofanyika mnamo tarehe 12 July 2006.

Shambulizi hili ni pale Hezbollah waliporusha maroketi katika sehemu mbali mbali ndani ya Israel wakitumia rockets zijulikanazo kama Kayusha, walivuka Blue Line na kuingia Israel wakipiga ambush Humvee za IDF mbili zilizokuwa mpakani kabisa mwa Israel karibu na uzio na kuzilipua kwa Anti Tank Guided Missile(ATGM), hii ilipelekea askari wawili(2) wa IDF kutekwa nyara, watatu(3) waliuawa pale pale, Pia katika jaribio lililofeli la askari wa Israel kwenda kuwaokoa wenzao, askari watano(5) waliuawa katika jaribio hilo la uokoaji nchini Lebanon.

Hezbollah ilidai wafungwa wake waachiliwe kwa kubadilishana na wafungwa wa IDF ambao walikuwa ni mateka nchini Lebanon, Israel wakajibu hapana haiwezekani kwa wakati huo prime minister wa Israel alikuwa Ehud Olmert.

Baada ya Israel kukataa ilikuwa wazi vita inakwenda kutokea.

Ndipo waziri mkuu wa Israel akasema "Lebanon italipa kwa kitu walichofanya" na pia bwa Ehud Olmert alisisitiza "Lebanon itegemee maumiu makali sana na tutafika mbali zaidi"

View attachment 1469714

Naam yalikuwa ni maneno ya bwana Ehud Olmert waziri mkuu wa Israel, hakika Hezbollah alikuwa amegusa pabaya, sasa kinachokwenda kutokea unakijua, unajua Israel ilishapigana vita ya siku 6 na na kuwa mshindi dhidi ya Egypt,Syria na Jordan? Na sasa wanakwenda kukabiliana na Hezbollah kikundi kidogo cha wanamgambo? keti hapo hapo uendelee kusoma.

Ni katika siku hio hio (12 Julai 2006), Baraza la Mawaziri liliamua kumpa mamlaka Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na manaibu wao kutekeleza mpango mzima waliokuwa wamepanga dhidi ya kuishambulia vibaya Lebanon, Waziri mkuu akasema katika shambulio hilo inabidi wasishambulie makazi ya watu, Kamanda wa jeshi la anga Israel Dan Halutz alisema "Ikiwa askari wa Israel hawatorudishwa, tutarudisha saa ya Lebanon miaka 20 nyuma"

Pia mkuu wa jeshi la Israel upande wa kaskazini alisema "Hii ni vita kati ya Israel na Lebanon, sasa tushambulie wapi? kama wapo Lebanon, tutapiga Lebanon haijalishi wapo sehemu gani, iwe kusini au Hezbollah walipo."

Pia Serikali za AMerika, Uingereza, Ujerumani, Australia, na Canada zilidai ni haki ya Israeli kujilinda. Serikali ya Amerika ilijibu zaidi kwa kuidhinisha ombi la Israeli la kupatiwa Guided Missiles zenye accuracy ya hali ya juu.

Upande wa Hezbollah sasa kiongozi wao bwana Hassan Nasrallah alisema "Israeli wamevunja mpango wa zamani wa kuwaachilia wafungwa hawa, na kwa kuwa diplomasia imeshindwa, vurugu ndio chaguo pekee lililobaki". Nasrallah alitangaza kwamba "hakuna operesheni ya kijeshi itakayoweza kuwaokoa wafungwa hawa ... Njia pekee, kama nilivyoonyesha, ni ile ya mazungumzo yasiyokuwa ya moja kwa moja na kubadilishana wafungwa".

View attachment 1469718

VITA INAANZA
Na vita ikatangazwa rasmi, ni tarehe 12 julai 2006, Wakati wa siku ya kwanza ya Vita, Jeshi la Anga la Israeli, jeshi la maji walifanya mashambulio zaidi ya 100 dhidi ya kambi za Hezbollah kusini mwa Lebanon, kati yao makao makuu ya mkoa huko Ya'tar. Madaraja matano ya kupita kwenye mito ya Litani na Zahrani pia yakaharibiwa, iliripotiwa kumzuia Hezbollah kuhamisha askari waliotekwa nyara.

Naam hakika Israel ilishambulia kwa nguvu haswa toka angani na ardhini, ilikuwa si mchezo.

Mashambulio kutoka ardhini, baharini na angani yaliendelea katika siku inayofuatia. Miongoni mwa sehemu zilizopigwa yalikuwa makao makuu ya Hezbollah katika vitongoji vya kusini vya Beirut na vile vile ofisi na nyumba za uongozi, kituo cha Televisheni cha al-Manar na kituo cha redio cha al-Nour, runways na depo za mafuta za Uwanja wa ndege wa kimataifa Rafic Hariri Beirut. Vile vile vilivyolengwa ni kambi za Hezbollah, depo na madaraja, barabara na vituo vya petroli kusini mwa Lebanon. Raia 44 waliuawa kwa siku hio. sio mchezo.

Israel hakuishia hapo, Jeshi la Anga la Israeli katika usiku wa manane, 13 Julai, lilishambulia na kuharibu roketi launchers 59 ambazo zilikuwa ni medium range ziitwazo Fajr zilizowekwa kusini mwa Lebanon. Operesheni inadaiwa ilichukua tu dakika 34 kutekeleza lakini ilikuwa matokeo ya miaka sita ya kukusanya akili na kupanga. Kati ya nusu na theluthi mbili ya uwezo wa roketi wa Hezbollah wa wastani IDF ilidai kuwa umefutwa. Kulingana na waandishi wa habari wa Israel Amos Harel na Avi Issacharoff operesheni hiyo ilikuwa "hatua ya kijeshi ya kuvutia zaidi ya Israeli" na "pigo kubwa kwa Hezbollah". Katika siku iliyofuatia IAF ilishambulia na kuharibu sehemu kubwa ya makombora marefu ya Hezbollah Zelzal-2.

"Makombora yote ya masafa marefu yameharibiwa,"Kamanda Halutz alisema na pia aliiambia serikali ya Israeli, "tumeshinda vita."

Ni katika siku za mwanzoni kabisa jeshi la Israel walisema wamemaliza kambi zote za Hezbollah kwa mashambulizi na wamepiga launchers za Kayusha rockets, walisema Hezbollah sio kitu na vita inaisha mapema kabisa.

Kufikia siku ya nne ya vita IDF ilikuwa haioni pa kupiga kwani targets zote 83 kwenye orodha zilikuwa zimeshapigwa.
Sehemu kubwa za miundombinu ya raia ya Lebanon ziliharibiwa, pamoja na barabara urefu wa kilomita 640, madaraja 73, na sehemu nyingine kama vile uwanja wa ndege wa kimataifa wa Beirut Rafic Hariri, bandari, vyanzo na vituo vya matibabu ya maji taka, vyanzo vya umeme, vituo vya mafuta 25, sehemu 900 za kibiashara, shule 350 na hospitali mbili, nyumba 15,000 ziliharibiwa vibaya na Nyumba zaidi ya 130,000 ziliharibiwa kiasi.

Hezbollah inajibu.
Kituo cha Televisheni cha Hezbollah al-Manar kilionya jamii za Kiarabu na Kiebrania juu ya shambulio la roketi baadaye. Vile vile Hezbollah ilituma ujumbe wa maandishi kuonya wakaazi wa Israeli waondoke katika nyumba zao ili wasipatwe na shambulio roketi.

Hakika vita imesimama sasa, sasa ni kupiga nikupige.
Tofauti na Israel ilipodhani kuimaliza Hezbollah, kumbe ndio kwanza kama ni movie ya Titanic bado watu walikuwa hawajaingia hata melini kuanza safari.

Tuendelee...

Kikosi cha roketi cha Hezbollah kilirusha kati ya makombora 3,970 na 4,228 kwa kiwango cha zaidi ya makombora 100 kwa siku, kiasi ambacho hakijawahi kutokea tangu Vita vya Iran na Iraqi. Karibu 95% ya hayo yalikuwa ni makombora ya 122mm( Katyusha) kombora hizo zilikuwa zina vichwa vya kilo 30, na zilikuwa zinasafiri hadi km 30 . Takriban 23% ya makombora haya yaligonga miji na maeneo yaliyojengwa kaskazini mwa Israeli, wakati mabaki yaligonga maeneo ya wazi.

Miji iliyopigwa ilikuwa Haifa, Hadera, Nazareti, Tiberia, Nahariya, Safi, Shaghur, Afula, Kiryat Shmona, Beit She'an, Karmiel, Acre, na Ma'alot-Tarshiha, na miji kadhaa, kibbutzim, moshavim, na Vijiji vya Druze na Benki ya kaskazini magharibi pia ilipigwa.

Labda niweke mambo sawa hizi rockets za Katyusha katika mapigano ya nyuma zilitumika sana, hivyo hata kipindi IDF inakwenda kumtandika Hezbollah waliona hizo kombora sio kitu na walijua ndio kitu Hezbollah ndicho walichokuwa wakitegemea zaidi, kumbe haikuwa hivyo.

Hezbollah toka mara ya kwanza kwenye ile mission yao Operation truthful promise walianza kurusha hizo Katyusha ambapo hazikuua raia yeyote yule Israel, roketi hizi zilikuwa ni za ki zamani hivyo Hezbollah walizitumia kuwa pumbaza Israel na Israel wakapumbazika kweli.

Japo Mashambulio ya roketi ya Hezbollah pia yalilenga na kufanikiwa kupiga kambi za jeshi nchini Israeli.hata hivyo uongozi wa jeshi la Israel ulikuwa mkali sana na marufuku kabisa kwa vyombo vya habari vya Israeli kuripoti matukio kama haya. Agizo la wakati wa vita kwa vyombo vya habari lilisema kwamba "Uongozi wa Jeshi hatakubali ripoti za Hezbollah kupiga makombora katika kambi za IDF na au vifaa vya jeshi."

Naam kwa kutumia mbinu mpya na mikakati, silaha mpya na advanced kabisa, Hezbollah ndipo ilipogeuza mchezo mzima juu chini na chini juu. Ni vita ambayo Hezbollah waliita "surprises".
Ndipo Hassan Nasrallah akasema "ile surprise ambayo tumeahidi ndio inaanza"

Surprise ya kwanza kutoka Hezbollah
Kuna meli (Warship) moja ya ya Israel ambayo ni very powerful according to IDF, ilijulikana kama Hanit, nadhani unaelewa unaposikia warship, ni meli ya kivita na ina uwezo mkubwa wa kuzuia missiles na kushambulia.Ni moja ya meli iliyotumika pia kushambulia, kumbuka Israel ilishambulia toka angani, majini na ardhini, na silaha ilikuwa ikiogopeka majini ilikuwa ni hii Hanit warship.

Hanit ilipigwa kombora linalofahamika kwa jina la C-802 lililo tengenezwa China na kuwa modified na Iran, range yake ni km 120, mpaka hapo Israel ilifahamu fika kwamba sasa meli zake hazina maana tena mbele ya Hezbollah pia Israel ilifahamu fika sasa ndio imeanza kuona vita halisi.

Katika shambulio hilo askari wanne waliuawa waliokuwa katika meli hio Staff Sergeant Tal Amgar, Corporal Shai Atas, Sergeant Yaniv Hershkovitz, na First Sergeant Dov Steinshuss.

2_wa.jpg

1_wa.jpg

3_wa.jpg

Surprise ya pili
Wakati huu Hezbolla walipanga mashambulizi dhidi ya mji wa Haifa, Israel ikiwa inategemea Hezbolla bado atakuwa anatumia Katyusha misssiles, kumbe haikuwa hivyo, na hapo ndipo surprise ya pili ikatokea, ulikuwa ni wakati Israel kukutana na surprise ya pili.

Ndipo kombora aina Zelzal-2 na aina ntingine za kombora toka Iran zikaanza kumiminika kwa wingi ndani ya Israel, kombora hizi zilikuwa zinafika sehemu yeyote Israel na pia zilikuwa zinabeba warhead yenye mlipuko wa hali ya juu takribani kilo 600. Ndivyo vita ilivyoendelea

Haifa ni mji muhimu sana katika uchumi wa taifa la Israel, na sasa Israel ilibidi iseme kwa kitu walichofanya Hezbollah juu ya kushambulia haifa hakika ni strategy ya hatari sana waliotumia tokana na makazi ya watu, lakini Israel pia ilipiga makazi ya watu.

Hezbollah ikiwa inalenga sehemu muhimu na za kiuchumi vita iliendelea, Israel alikuwa akipiga kofi Hezbollah anarudisha vile vile na vita ikaendelea

Haifa hakika ilishambuliwa, power plant,barabara, majengo, hata magari yalikuwa yanawaka moto tu , raia walikufa wengi, kambi za jeshi zilipigwa.

Haifa ikawa target ya Hezbollah, Israel ikaona hali ni mbaya, kwa sababu walichokuwa wakifanya Hezbollah ilikuwa ni kulipiza kama Israel inavyopiga makazi ya Lebanon na wao wanapiga Haifa city.

Ni wakati huo Israel ikaona Hezbollah hataki mchezo na hapo Israel akaogopa kuipiga Beirut kwa kujua kwamba Tel-Aviv ingepata mvua ya makombora, na utakuwa mwanzo wa kuipoteza Tel-Aviv.

Hakuna asiyejua kwamba USA na Israel hawawezi kabisa kuwa na diplomasia na kundi kama Hezbollah pia wanajulikana kwa uvunjifu wa amani na kukiuka haki za binadamu hasa kwa nchi zetu tusiojiweza.

Kwa maana diplomasia ilifeli mwanzoni hivyo njia pekee ili uweze kusikilizana nao ni kutumia nguvu, naam Haifa iliendelea kumiminiwa missiles.

Mnamo Julai 16, wafanyakazi wanane wa Reli ya Israeli waliuawa kwa kupigwa na roketi kwenye kituo cha treni. Kiongozi wa Hezbollah Hassan Nasrallah alisema hapo awali Hezbollah ilikuwa inalenga makombora yake kwenye "vituo vya kijeshi tu". Lakini kwa kuwa Israeli, alisema, amepiga raia basi Hezbollah hakuwa na chaguo ila kujibu kwa kulenga miji ya Israeli.

F060813ff02-640x400.jpg

Haifa

13assess600.jpg

Haifa Israel
Hezbollah ikawa inajikadiria tu irushe missile ngapi kama Israel akiwashambulia. Umoja wa mataifa ukaanza kufanya mazungumo juu ya kukatishwa vita hivyo, wakati mwanzoni wali support, so Israel ana hali mbaya, lakini UN haikufanikisha hilo jambo mara moja,

Surprise ya tatu
Kuna Tanks zilikuwa zinajulikana kama merkava tanks za 4th generation, hakika zilisifiwa kwa nguvu, uwezo wa kupambana, maneuvers, pia timu za waliokuwa waki operate hizi tanks walijulikana kama the best ones katika mafunzo duniani.

Pia zilisifika kuwa ni hatari zaidi duniani na very powerful, kwa uwezo wake mkubwa wa hizi tanks katika mapambano au aina yeyote ya battle field IDF waliikubali sana Merkava.

Licha ya sifa zote hizo ilizonazo Hezbollah iliweza kujua weakness zake na kuweza kuwashangaza IDF, yeah ni surprise nyingine, pia walikuwa wana silaha kwa ajili ya kuhakikisha Merkava ina baki chuma chakavu.

Ilikuwa ni Anti Tank Missile toka Russia na hapo kulikuwa na Milan pamoja na Kornet, vitu ambavyo IDF waliona sasa maji yamezidi unga, katika shambulio baya kutokea ni baada ya Hezbollah kuipiga tank huko Hujeir, hakika hakuna aliyepona, crew nzima waliisha pale pale.

Pia Abram Tank ya USA ilipigwa pia. Kama tanks za kawaida kama Merkava za mwanzoni almost zaidi ya 50 ziliharibiwa.
Pia katika missiles hizo walikuta missile za Iranian Made.

Kama kawaida vita ya ana kwa ana ilikuwepo(ardhini)/(ground war).

Kwa kutumia jeshi dogo lililoiva kisawa sawa, Hezbollah hakika hawa askari wake wa ardhini walikuwa highly trained(mafunzo ya hali ya juu), pia walikuwa na vifaa vyote vya kisasa kama jeshi la Israel kama vile night goggles,vifaa vya mawasiliano na pia wakati mwingine walionekana wakiwa na uniforms kama za IDF, na vifaa vya kivita vya kisasa kabisa.

Askari mmoja wa Israeli ambaye alishiriki katika vita hio alisema kuwa "wapiganaji wa Hezbollah huwezi kuwafananisha na Hamas au Wapalestina, wameiva na wana mafunzo ya hali ya juu. Hakika sote tulishangazwa".

Harakati za kusimamisha vita
Wakati jeshi la IDF likiwa linakumbana na mbinu mpya za kijeshi pia kichapo kikali, UN wakaona ni wakati wa kusimamisha vita kwani Israel wapo vibaya mpaka hapo, na jeshi la Hezbillah morali ya vita ndio kwanza kama wanaanza, hakika ipo wazi ni katika wakati huu, IDF mashambulizi yao ni ya kusua sua kwa sababu zifuatazo.

1-Wanaogopa kuendelea kupiga miji kama Beirut kwa sababu Hezbollah tayari wana missiles za kufika Tel-Aviv hivyo wangejibu , hivyo vita inge changamka.

2-Israel walishambulia targets zaidi ya 100 za Hezbollah, lakini kinyume na walivyotegemea hakika jeshi la Hezbollah lilikuwa na nguvu bado na mirindimo iliendelea, ipo wazi niliandika ilifikia kipindi Israel wakaanza kukuna vichwa ni wapi wapige tena.

3-Israel walikuwa wameshambulia kwa nguvu sana mwanzoni, hivyo ni katika wakati huu silaha zao zilitumika nyingi sana na nyingine ziliharibiwa,hivyo kulikuwa na upungufu wa silaha tofauti na mwanzoni,ukizingatia kuna kambi zilipigwa na wanajaeshi wa IDF kuuliwa, vifaa vya vita kama ile meli ya Hanit iliyopigwa, kwani tokea baharini walirusha shells 2500 kuelekea Lebanon.

Mazungumzo ya kusimamisha vita hayakufanyika kwa mara moja, yaliendelea kwa wiki kadhaa kwa pande mbili kushindwa kuelewana,UN ikiwa mpatanishi , kutokuelewana huko ni pamoja na Lebanon kusema vita isimame pasipo masharti yeyote wakati huo Israel iliomba kuwe na masharti kuhusu kuachiliwa kwa IDF soldiers wawili.

Hata hivyo harakati za kusimamisha vita zikiongozwa na UK na US zilicheleweshwa makusudi wakijua labda Hezbollah inaweza kuwa defeated, lakini haikuwa hivyo, na ipo wazi vita ilisimamishwa kwa kuwa walijua Hezbollah kuwa defeated ni ngumu sasa na matokeo yatakuwa mabaya.

Ni julai 25 bibi Condoleeza Rice alikutana na waziri mkuu wa Israel Ehud Olmert katika harakati za kuzuia vita alisikika akisema "Tunaposhughulika na hali za sasa, tunahitaji kila wakati kujitambua na kuangalia ni aina gani ya Mashariki ya Kati tunajaribu kujenga. Ni wakati wa Mashariki ya Kati mpya"

english_mediacenter_events_publishingimages_7de0dc36e168457796a28ac4d0acce26condbig2.jpg
Yalikuwa ni maneno ya busara toka kwa Secretary of state of US bi Condoleeza Rice baada ya kichapo heavy toka kwa Hezbollah pia waziri Olmert aliongelea wakati mgumu wanaokutana nao alisikika akizungumzia jinsi vita ilivyo waweka wanachi wa Israel zaidi ya 1.5 million katika hali mbaya, kazi zikiwa zimesimama hivyo ni jukumu lao kuwasaidia.

Katika hotuba hio waziri Olmert alizungumza wazi kwamba walikuwa wanahitaji suluhisho kusimamisha vita, Hakika kipigo heavy kiliwafanya Israel wafuate matakwa ya Hezbollah bila wao kupenda.



Baada ya pande mbili zote kuridhiana na Israel kuomba wanajeshi wake waachiliwe, Israel na Hezbiollah walisimamisha vita kwa usimamizi wa UN(US), ilikuwa ni saa 2 asubuhi ya 14 august 2006 vita ilisimama rasmi huku Hezbollah ikiwa imefanikiwa pakubwa kwa jambo walilokuwa wanahitaji, wafungwa wa Hezbollah akiwemo bwana Samir Al-Quntar kuachiwa na ndugu zake, vile vile Israel walikabidhiwa askari wao na vita ikawa imesimama.

Hakika hakuna aliyeamini kama Hezbollah angefanya jambo hilo, inasemekana kwamba licha ya Israel kupiga kituo cha television cha Lebanon kwa jina la Al-Manar ilichukua dakika mbili tu wakarudi hewani.

Wakati wa vita Jeshi la Anga la Israeli ilifanya combat missions 11,897, ambapo ilikuwa zaidi ya idadi ya ya Vita vya Oktoba 1973 (11,223) na mara mbili katika Vita vya Kwanza vya Lebanon (6,052).

Wanajeshi wa Israeli walirusha makombora 170,000, zaidi ya mara mbili ya idadi katika Vita vya Oktoba 1973. Afisa mwandamizi katika IDF Armored Corps aliiambia gazeti la Haaretz kwamba atashangaa ikiwa ikitokea kwamba hata wapiganaji watano wa Hezbollah wameuawa na mikombora 170,000.

Kulingana na matokeo ya upelelezi wa kijeshi wa baada ya vita uchunguzi wa kambi ya IDF ulifanikiwa kuharibu Katyusha rockets 100 kati ya 12,000. Tofauti na jeshi la Israel walivyodhani.

Maafisa wa Amerika walidai kwamba Waisraeli hawakufanikiwa katika ufanisi wa vita vya anga dhidi ya Hezbollah na walionyesha kutofaulu kupiga kwa kiongozi yeyote wa Hezbollah licha ya kuteremsha tani 23 za mabomu kwenye makao yake makuu.

Kulingana na mchambuzi wa kijeshi William Arkin alisema kuna ushahidi mdogo kwamba Jeshi la Anga la Israeli lilifanikikwa kidogo sana katika madai ya kuangamiza roketi za masafa marefu na mafupi katika siku za kwanza za vita. Alitupilia mbali madai yote kama "upuuzi" na "hadithi".

Katika kumbukumbu ya miaka sita ya vita vya Lebanon Hezbollah mwenyekiti Hassan Nasrallah alidai kuwa Hezbollah alijua kuwa Waisraeli walikuwa wakikusanya taarifa za kiintelejensia dhidi ya makombora yao yalipo na walifanikiwa kuyahamisha bila kugunduliwa. Maeneo mengi yaliyoshambuliwa na jeshi la anga la Israeli kwa hivyo yalikuwa tupu.

Hata hivyo Israel walidai katika vita hivyo Iran ilihusika kutoa msaada wa vifaa mbali mbali pia Gazeti la Israel la Haaretz lilielezea Hezbollah kuwa ilifundishwa, pia walikuwa na ujuzi,walijipanga vizuri, na pia silaha za kisasa kutoka majeshi ya Syria, Iran, Russia, na China.

Hassan Nasrallah alishawahi kusikika akisema kuwa wana makombora ya kuirudisha Israel nyuma kwenye zama za mawe.

Naama na hapo ndio mwisho wa vita hii ambayo askari 121 wa IDF waliuawa, helicopters ziliharibiwa, meli, vifaru nauharibifu mkubwa wa miundo mbinu.

Pia jeshi la Hezbollah walipoteza askari wao 250.

Hakika kikundi kidogo kabisa cha jeshi la Hezbollah kiliweza kuihangaisha nchi ya Israel na kuishinda katika vita Israel, mpaka Israel kuona vita imekuwa chungu licha ya kutumia uwezo wake,intelejensia, pia kutumia jeshi la anga, ardhi na maji kuipiga Hezbollah, je swali langu.

Israel itaweza ku defeat Iran ambapo ndio walioipatia Hezbollah mafunzo ya kijeshi,silaha na mbinu? kila siku naona watu wana linganisha Iran na Israel.



khamsrallamani-e1569711056798.jpg

Khamenei, Nasrallah kiongozi wa Hezbollah na Qasim Suleimani (enzi za uhai wake).


MWISHO

hata kwenye global millitary rank ya mwaka 2020 inaonesha iran iko juu ya israel kijeshi.
Iran iko namba 14 na Israel iko namba 18, lakini sasa kinachompa kiburi muyahudi ni marekani kumlinda sana, unaweza kuona sasahivi ashampa na ndege za F-35 fighter jet tiari
 
Usipuuze Iran

Iran siyo ya kupuuzwa mkuu, hakuna nchi ambayo inamnyima muyahudi usingizi kwa eneo la mashariki ya kati kama Iran.

Iran ndiyo inayonyima usingizi Netanyahu kila kukicha.

fuatilia mikutano yote ya UN na ya Baraza la usalama la umoja wa mataifa ambayo israel inakuwa imealikwa then fuatilia israel inachangia nini, asilimia zaidi 80 za hoja za UN ni kuisema Iran kuwa ni tishio kwa usalama wa wayahudi mashariki ya kati

Sasa wewe sema tu ina nini zaidi ya pesa ya mafuta ndo utakupajua hata israel haina kitu zaidi ya jangwa
 
Japo umeandika kiushabiki lakini Nimependa sana hili chapisho lako.

Nimecheka sana hapa
Sijui, imeshwaelezwa hapa yule Samir Kuntar alifungwa kwa sababu gani na Israeli? Kwa sababu alichinja watoto wawili (bila shaka akiamini anatekeleza kazi ya mshujaa kwa ukombozi wa Palestina..). Soma hapa:

"On 22 April 1979, at the age of 16, Kuntar participated in the killing of an Israeli policeman and the attempted kidnapping of an Israeli family in Nahariya that resulted in the deaths of four Israelis and two of his fellow kidnappers.

Kuntar and his team broke into an apartment building and kidnapped a father, 31-year-old Danny Haran, and his 4-year-old daughter, Einat, taking them to a nearby beach. According to eyewitnesses and forensic reports, Kuntar shot Danny to death at close range, and then killed the girl Einat by smashing her skull against the rocks with the butt of his rifle. During the attack, Smadar Haran accidentally suffocated her two-year-old daughter Yael to death while attempting to quiet her whimpering, which would have revealed their hiding place.[11] Newsweek states that the details of Kuntar's attack are "so sickening they give pause even to some of Israel's enemies."

Je ni ajabu Israeli hawakutaka kumwacha (hata hivyo, hawakumnyonga, bali walimpa nafasi ya kusoma gerezani na kufikia digrii ya kwanza)?
Hatimaye walimwacha, ila si mwaka unaotaja 2006, bali 2008. Vita ilikwisha bila kurudishwa kwa Kuntar.

Sioni ni namna gani Hezbollah ilishinda? Tangu vita ile wamekaa kimyakimya. Yaani wanapiga makelele kwa sauti, lakini hawa shambulii tena mpakani. Walirusha roketi elfu nyingi ila waliua watu kama 40 tu.

Israeli nayo haikushinda. Walionyesha kwamba si watu wa kuchezwa na walifaulu Hezbollah ilipaswa kupunguza askari zake mpakani. Lakini hawakuweza kuvunja Hezbollah.

Wahanga walikuwa Lebanoni na raia zake.

NB: Kuntar aliuawa hatimaye 2015 pale Dameski,Syria. Hizbollak walidai kwamba aliuawa na roketi za Israeli, lakini Jeshi Huru la Syria (wapinzani wa Assad) walisema ni hao wenyewe waliomwua.
 
Japan na Ujerumani walishindwa kwenye vita zao na impact yake inaonekana.

Japan alikuwa mjeuri sana dhidi ya America hivi sasa hawezi hata kumkoholea, Germany pia alivyoshindwa vita akapoteza u-super power wake.

Issue ya Israel ni tofauti haihusishi uchumi wala chochote zaidi ya CHUKI za waislamu dhidi ya Israel.

Iran kama ndiye alitoa hayo makombora na yakafanya hayo maajabu mbona hajatimiza adhima yake hadi leo mbona kaiacha inapeta?

na kama kweli walipigwa na kakikundi mbona waislamu waarabu wamekalia midomo tu ooooh tunaonewa ooooh wanatulipua oooh twende UN oooh muamala wa karne kwanini wasitumie hizohizo njia wawafumue waondoke?
Iran ni taifa la kiislam Hezbollah ni jeshi la kiroho kwa mujibu wa vitabu vya kiroho ktk uislam wayahudi wataangamizwa ktk siku za mwisho mwisho kwetu sisi wayahudi ni watu waliolaaniwa na mungu kwa sababu mungu aliwatea mitume kadhaa hawakuamini na mwisho walimslubu issa bin mariam . Kufikia hapo mungu aliwalaani.ila tukumbuke pamoja na lana hio mungu hatowanyang'anya neema yao aliyowaahidi na kuwapa ya hekima na busara ambayo ndio inayowapa jeuri na kiburi hiki mpk leo ila ahadi ya mungu muumba ipo palepale wataangamia na kudhalilika siku za mwisho mungu alimlaani shetani kwa kutomsujudia adam lkn hakumnyang'Anya uwezo wake mpk leo hii kwa hivo tofauti yetu waislam na waikristo ipo hapo sisi tunaamini waisrae wamelaaniwa lkn wenzetu mnasema ni taifa teule.
 
Hiyo Google ni ya waarabu au ya mashariki?

Kama haina jeshi zuri mbona waarabu (waislamu) wameshindwa kuwaondoa waebrania kabisa na wasiwahi kurudi tena?
Palestina wanaramani yao inayoonyesha kuanzia mwaka 47 hadi sasa "eti" territory zao zilivyochukuliwa, nchi zote za kiislamu haziwataki waebrania na zinatamani sio tu waondoke waangamie kabisa.

Swali kama Hezbollah walishinda kwa hizo missiles mbona hawakutumia mbinu hizohizo waongeze na zingine wawamalize kabisa kama wanavyootaga?
Kilichopo pale si Israel ile UK,US, Ndani ya middle east lkn muisrael kama muisrael haipo na nguvu kama wengi wanavyodhani 'iran anauwezo wa kuifuta israel ndani muda mfupi sana lkn kitakacho fuata UK na us nao wataiangamiza iran na kuhakikishia israel kama Israel si lolote si chochote
 
Hiyo Google ni ya waarabu au ya mashariki?

Kama haina jeshi zuri mbona waarabu (waislamu) wameshindwa kuwaondoa waebrania kabisa na wasiwahi kurudi tena?
Palestina wanaramani yao inayoonyesha kuanzia mwaka 47 hadi sasa "eti" territory zao zilivyochukuliwa, nchi zote za kiislamu haziwataki waebrania na zinatamani sio tu waondoke waangamie kabisa.

Swali kama Hezbollah walishinda kwa hizo missiles mbona hawakutumia mbinu hizohizo waongeze na zingine wawamalize kabisa kama wanavyootaga?
Jikwamue kutoka utumwa wa fikra
 
Kuna kinanitatiza sana sisi waislamu tunawachukia waisrael kwa sbb wamelaaniwa na mungu tunaamini hivyo kwa mujibu maandiko ya kitabu chetu lkn upande wa wakristo wanawatukuza waisrael na kuwaweka ktk daraja la taifa teule la mungu swali langu ni je waikristo wanampenda yesu au wa awapenda waliomsulubu ambao ni waisraeli? Na ktk maandiko ya waikristo mtawala wa kirumi aliwapa chaguo waisrael wachague aachiwe baraba ambaye alikua jambazi ili yesu auwawe au amuachie yesu ili baraba auwawe waisrael walichagua aachiwe baraba jambazi na muuaji yesu asulubiwe swali je wakristo mnapenda yesu au waliomuua?
 
Sir Issue ni Mkuu wa Majeshi hakutaka kuendelea na vita, ila Olmert alitaka iendelee.
ndio maana sisi tunasimamia msimamo wetu kuwa Israel haikushindwa hatubahatishi.
.
Israel angelishindwa angepata tabu sanaaa na hata wangeshakuwa hawapo tena kwenye kale kaeneo. Ila bado wapo na wanawachekecha waarabu vilivyo.
Chanzo cha vita ni wafungwa na mwisho ni wafungwa Hezbollah mdai israel ni mdaiwa mwisho wa siku wafungwa walibadilishana hivyo mdai alishinda kama israel alishinda kwa nn aliwaachia wafungwa? Kuhusu hasara kila upande ulidai kumtia hasara mwenzie lkn ukweli utabaki ukweli kwa sbb hezbollah waliwapata wafungwa wao na kama israel alimtia hasara kubwa Hezbollah kwa nn alikubali kuwaachia wafungwa? ni dhahiri walipata hasara ndio maana walikubali madai ya awali ya Hezbollah kabla vita kuanza
 
Back
Top Bottom