Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Ndani ya miezi 12 tumeona mifumuko ya bei kuanzia bei ya mkate, unga, nyama hata nauli ya basi. Wengine wameamua kurudi kijijini kwa ugumu wa maisha na wengine wamehamia kwa ndugu kupunguza makali ya kodi ya nyumba.
Ukweli halisi matabaka yote ya watu yanahitajika mjini ili maisha yaende leo. Sisi wapika maandazi tuna umuhimu katika kundi la watu wa kipato fulani, wakila maandazi mawili na maji wanamshukuru Mungu na siku inapita kesho wanakwenda kwa matajiri kutafuta kibarua.
Mfumuko wa bei umebadilishaje maisha yako?
Ukweli halisi matabaka yote ya watu yanahitajika mjini ili maisha yaende leo. Sisi wapika maandazi tuna umuhimu katika kundi la watu wa kipato fulani, wakila maandazi mawili na maji wanamshukuru Mungu na siku inapita kesho wanakwenda kwa matajiri kutafuta kibarua.
Mfumuko wa bei umebadilishaje maisha yako?