Ni jambo la kushangaza kwa Mkurugenzi aliyeiba mabati kuendelea kuwa ofisini hadi muda huu

Kuwa msimamizi wa uchaguzi hakumfanyi kuwa na mandate ya kufanya ubadhirifu wa mali za umma mkuu. Sheria ichukue mkondo wake
Mbona umekomaa na huyo mkurugenzi wakati Kuna gaidi moja lilikwiba 8.9 bilion michango ya wabunge na hakufukuzwa ofisini?
 
Mkurugenzi wa halmashauri ya gairo, bw Asajile Mwambambala aliyehusika katika wizi wa mabati zaidi ya 1100 mwaka huu mwezi wa saba alipaswa awe nje ya ofisi hadi muda huu. kwani kwa mujibu wa kanuni za maadili ya utumishi wa umma ni kosa kwa mtumishi yeyote wa serikali kujihusisha na wizi au ubadhirifu wa mali yoyote ya kiofisi au mali ya umma

Kwahiyo nilitegemea katika hatua za awali, wizara ya Tamisemi ambao ndio mamlaka yake ya nidhamu wawe wamemwandikia barua ya kumsimamisha kazi mara moja mkurugenzi huyo ili hatua zingine ziweze kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani kwa makosa aliyoyatenda

Badala yake mkurugenzi huyo hadi muda huu bado yupo ofisini na mwezi huu wa tisa anasubiri kulipwa mshahara ambao kimsingi ni kodi ya wavuja jasho aliowaibia mabati.

Je, kitendo hiki cha DED kuendelea kubaki ofsini kinatoa tafsiri gani?

Au labda waziri mwenye dhamana anakubaliana na kitendo hicho kilichofanywa na DED ndio maana anachelewa kuchukua hatua?

Je, mamlaka zake za uteuzi na nidhamu kuchelewa kuchukua hatua ni kutengeneza mwanya wa kuja kumsafisha baadaye ionekane hakuhusika katika kufanya ubadhirifu?
Juzi Kati ameyarudisha na ameyagawa kwenye Shule za sekondari na msingi.
 
Mkurugenzi wa halmashauri ya gairo, bw Asajile Mwambambala aliyehusika katika wizi wa mabati zaidi ya 1100 mwaka huu mwezi wa saba alipaswa awe nje ya ofisi hadi muda huu. kwani kwa mujibu wa kanuni za maadili ya utumishi wa umma ni kosa kwa mtumishi yeyote wa serikali kujihusisha na wizi au ubadhirifu wa mali yoyote ya kiofisi au mali ya umma

Kwahiyo nilitegemea katika hatua za awali, wizara ya Tamisemi ambao ndio mamlaka yake ya nidhamu wawe wamemwandikia barua ya kumsimamisha kazi mara moja mkurugenzi huyo ili hatua zingine ziweze kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani kwa makosa aliyoyatenda

Badala yake mkurugenzi huyo hadi muda huu bado yupo ofisini na mwezi huu wa tisa anasubiri kulipwa mshahara ambao kimsingi ni kodi ya wavuja jasho aliowaibia mabati.

Je, kitendo hiki cha DED kuendelea kubaki ofsini kinatoa tafsiri gani?

Au labda waziri mwenye dhamana anakubaliana na kitendo hicho kilichofanywa na DED ndio maana anachelewa kuchukua hatua?

Je, mamlaka zake za uteuzi na nidhamu kuchelewa kuchukua hatua ni kutengeneza mwanya wa kuja kumsafisha baadaye ionekane hakuhusika katika kufanya ubadhirifu?
Msimamizi na muajiri mkuu wa serikali,Raisi,yupo bize anatembeza tumbo,na mimacho ya kulegeza,
Kama watendaji wa Tasac na hazina walipiga milioni 500!kwa kwa kukaa vikao tu,na wakakalipiwa tu,na mpaka leo wapo wanakula bata,sembuse DED aliyeiba tumabati!
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Asajile Mwambambale na watumishi saba wa halmashauri ya Wilaya ya Kilosa waliodaiwa kuiba mabati 1,172 wameyarejesha wilayani humo.

Hawa ni viongozi ni watumishi wa umma, wamekiri kuiba ni wahujumu uchumi haitoshi tu kuyarudisha bali walitakiwa wafunguliwe mashitaka na wafukuzwe kazi. Kwanini hadi leo DED bado yuko ofisini? Rais anasubiri nini kumfuta kazi mteule wake?

A037CFEF-EBD8-41EF-B3DE-6B459F78AF41.jpeg
 
Hapo ndo nakumbuka enzi Za Magufuli huyu jamaa angekuwa ameshatumbuliwa, ila huyu mama ni dhaifu sijui kama miradi aliyoacha RIP itakamilika kwa ulegevu huu, wizi umetamalaki kila halmashauri sasa hivi,
 
Leo hii bavicha unashauri Rais kumtumbua mtu?

Si juzi tu hapa mlikuwa mnawatetea kwamba wanaonewa wakitumbuliwa na Magu?
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Asajile Mwambambale na watumishi saba wa halmashauri ya Wilaya ya Kilosa waliodaiwa kuiba mabati 1,172 wameyarejesha wilayani humo.

Hawa ni viongozi ni watumishi wa umma, wamekiri kuiba ni wahujumu uchumi haitoshi tu kuyarudisha bali walitakiwa wafunguliwe mashitaka na wafukuzwe kazi. Kwanini hadi leo DED bado yuko ofisini? Rais anasubiri nini kumfuta kazi mteule wake?

View attachment 1928957
Angekuwa mtendaji wa kata sasahivi angekuwa magereza kwa uhujumu uchumi
 
Leo hii bavicha unashauri Rais kumtumbua mtu?

Si juzi tu hapa mlikuwa mnawatetea kwamba wanaonewa wakitumbuliwa na Magu?
Usiwe filimbi, kuna makosa yaliyo wazi kama haya huwezi kuyatetea sio anafukuza mtu kwa tetesi za kutembea na hawala yake.
 
Hivi unajua huo wizi umechunguzwa na kutolewa ripoti na jeshi la polisi?

Kwahiyo unataka kusema jeshi la polisi wameongopa na wanataka kumbambikia DED kesi ya wizi?
Nini msimamo wako kuhusu jeshi la polisi?,unawakubali?
 
Mama kazidiwa na majukumu ya royal tour, apewe muda...
Mama sio lazima afanye kila kitu ndio maana anateua mawaziri ili wamsaidie. Mathalani hili suala la DED lipo chini ya TAMISEMI lakini waziri yupo kimya hata kukemea hajakemea au naye anasubiri maagizo kutoka juu?
 
Back
Top Bottom