gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,330
- 3,388
Ndugu zangu vita inayoendelea Irani imesababisha upandaji wa bei ya nishati kitu ambacho kimesababisha mfumuko wa bei kwenye bidhaa karibu zote,kwenye uchumi gharama za nishati/mafuta/gas zikipanda lazima bei ya bidhaa ipande.
Kwasasa hali ya maisha kwa upande wa wafanyakazi imekua mbaya zaidi kwani kipato cha mtumishi kwa mwezi ni fixed.
Inapotokea upandaji wa gharama za maisha kwa kiwango kikubwa kama ilivyo sasa wahanga wa kwanza ni wafanya kazi.
Nauli za usafiri makazini zimepanda kiasi ambacho watumishi inawalazimu wakati fulani kutembea waendapo makazini,
Bidhaa kama gas yakupikia nayo tayari imepanda mara dufu,hivi kukaa kimya ni sawa?
Upo utitiri wa vyama vya wafanyakazi lakini haieleweki vina msaada gani kwa hao wanaowatumikia.
Kama walikua wamelala basi sasa waamke wajue wajibu wao,
Kama viongozi wa vyama vya wafanyakazi waliopo wamewekwa na dola basi ni vizuri wajitafakari kama bado wanapaswa kuendelea kuwepo kwenye nafasi zao.
Kwasasa hali ya maisha kwa upande wa wafanyakazi imekua mbaya zaidi kwani kipato cha mtumishi kwa mwezi ni fixed.
Inapotokea upandaji wa gharama za maisha kwa kiwango kikubwa kama ilivyo sasa wahanga wa kwanza ni wafanya kazi.
Nauli za usafiri makazini zimepanda kiasi ambacho watumishi inawalazimu wakati fulani kutembea waendapo makazini,
Bidhaa kama gas yakupikia nayo tayari imepanda mara dufu,hivi kukaa kimya ni sawa?
Upo utitiri wa vyama vya wafanyakazi lakini haieleweki vina msaada gani kwa hao wanaowatumikia.
Kama walikua wamelala basi sasa waamke wajue wajibu wao,
Kama viongozi wa vyama vya wafanyakazi waliopo wamewekwa na dola basi ni vizuri wajitafakari kama bado wanapaswa kuendelea kuwepo kwenye nafasi zao.