Wana JF!
Nimekuwa nikifuatilia mijadala inayoendelea kuhusu Katibu Mkuu wa CHADEMA kuwa na kadi ya CCM. Kwa mujibu wa katiba ya CCM, mwanachama atakoma uanachama wa CCM kama atajiunga na chama kingine na sii kurudisha kadi.
Pia kwa siku za hivi karibuni, tumesikia kuwa shehana kubwa ya meno ya tembo imekamatwa huko mashariki mwa Asia. Tumesikia kuwa meli iliyosafirisha shehena hiyo inamilikiwa na Katibu mkuu wa CCM. Sheria zetu zinaitaka serikali kuvitaifisha vyombo vitakavyojihusisha kusafirisha maliasili zilizopatikana kwa njia haramu (Ujangili). Mpaka leo hatujapata taarifa yoyote kuhusu kutaifishwa kwa meli hiyo.
Je, kati ya makatibu wakuu hawa ni nani ana kashfa ya kujadili? Ni nani atakuwa anajihusisha na uhalifu?
Nimekuwa nikifuatilia mijadala inayoendelea kuhusu Katibu Mkuu wa CHADEMA kuwa na kadi ya CCM. Kwa mujibu wa katiba ya CCM, mwanachama atakoma uanachama wa CCM kama atajiunga na chama kingine na sii kurudisha kadi.
Pia kwa siku za hivi karibuni, tumesikia kuwa shehana kubwa ya meno ya tembo imekamatwa huko mashariki mwa Asia. Tumesikia kuwa meli iliyosafirisha shehena hiyo inamilikiwa na Katibu mkuu wa CCM. Sheria zetu zinaitaka serikali kuvitaifisha vyombo vitakavyojihusisha kusafirisha maliasili zilizopatikana kwa njia haramu (Ujangili). Mpaka leo hatujapata taarifa yoyote kuhusu kutaifishwa kwa meli hiyo.
Je, kati ya makatibu wakuu hawa ni nani ana kashfa ya kujadili? Ni nani atakuwa anajihusisha na uhalifu?