Ni huduma gani uliyopata kutoka Taasisi ya Umma/Binafsi kinyume na matarajio ikakustajabisha?

Zegota

JF-Expert Member
Jun 5, 2020
274
584
Nakumbuka ilikuwa mwaka jana, Ndugu yangu mmoja alikuwa amemaliza kidato cha sita na alikuwa huko sitimbi.

Akanipigia simu ili nimsaidie upatikanaji wa cheti chake cha kuzaliwa ili aombe mkopo baada ya matokeo kutoka kama vigezo vilivyokuwa vimeainishwa.

Nikawazamia RITA, nikajaza fomu zao kwa majina sahihi ya ndugu yangu then nikalipia gharama zilizohitajika nikairudisha ile fomu na nikapewa muda wa kwenda kuchukua cheti.. baada ya kupata cheti, dogo akaniambia nimsaidie wakihakiki ili majina yatumwe bodi ya mkopo.

Nikauliza wale staff walionipa kile cheti lengo la kuhakiki vile vyeti vya kuzaliwa kwa wanaoenda kuendelea na masomo ya chuo, wakaniambia ni kuweza kutambua vyeti visivyo halali. Nikawapa kile cheti nikidhani watakiingiza kwenye mfumo moja kwa moja maana wamekitoa wao muda si mrefu na kunipa, wakaniambia. Mr Zegota hapa unatakiwa ulipie Tsh 3000/= ili tuhakiki hiki cheti kujua kama sio feki.

Hili jibu lilifanya nibaki nimeduwaa yaani wamenipa cheti mda huohuo halafu wananiambia kwamba natakiwa nilipie kuhakikiwa kama ni halali, Nikaona kama haileti mantiki vile. Baada ya kuendelea kuwabana na maswali kutaka kujua kiundani jamaa wakaonesha kukasirika na kupanick.

Nikaona isiwe kesi, nikalipa kwa Tigo pesa kwa malipo ya serikali nikaendelea na process zingine walizonielekeza za kuhakiki, Mpaka leo bado nashangaa ina maana RITA wana mitambo fake mle ndani ya kutengeneza vyeti vya kuzaliwa?

By the way, hii ndio Bongoland.

Leta kisa chako cha huduma uliyopata na ukabaki kushangaa kutoka kwa hizi ofisi za hapa nchini za umma au binafsi.
 
Mimi nataka kujua wapi pa kuripoti usiporidhishwa na huduma (hasa ofisi za umma). Bado Kuna ile Hali ya kufanya kwa kujisikia wakikuacha hujui utareport wapi.
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka jana, Ndugu yangu mmoja alikuwa amemaliza kidato cha sita na alikuwa huko sitimbi.

Akanipigia simu ili nimsaidie upatikanaji wa cheti chake cha kuzaliwa ili aombe mkopo baada ya matokeo kutoka kama vigezo vilivyokuwa vimeainishwa.

Nikawazamia RITA, nikajaza fomu zao kwa majina sahihi ya ndugu yangu then nikalipia gharama zilizohitajika nikairudisha ile fomu na nikapewa mda wa kwenda kuchukua cheti.. baada ya kupata cheti, dogo akaniambia nimsaidie wakihakiki ili majina yatumwe bodi ya mkopo.

Nikauliza wale staff walionipa kile cheti lengo la kuhakiki vile vyeti vya kuzaliwa kwa wanaoenda kuendelea na masomo ya chuo, wakaniambia ni kuweza kutambua vyeti visivyo halali. Nikawapa kile cheti nikidhani watakiingiza kwenye mfumo moja kwa moja maana wamekitoa wao mda si mrefu na kunipa, wakaniambia... Mr Zegota hapa unatakiwa ulipie Tsh 3000/= ili tuhakiki hiki cheti kujua kama sio feki.

Hili jibu lilifanya nibaki nimeduwaa yaani wamenipa cheti mda huohuo halafu wananiambia kwamba natakiwa nilipie kuhakikiwa kama ni halali, Nikaona kama haileti mantiki vile. Baada ya kuendelea kuwabana na maswali kutaka kujua kiundani jamaa wakaonesha kukasirika na kupanick.

Nikaona isiwe kesi, nikalipa kwa Tigo pesa kwa malipo ya serikali nikaendelea na process zingine walizonielekeza za kuhakiki, Mpaka leo bado nashangaa ina maana RITA wana mitambo fake mle ndani ya kutengeneza vyeti vya kuzaliwa?

By the way, hii ndio Bongoland.

Leta kisa chako cha huduma uliyopata na ukabaki kushangaa kutoka kwa hizi ofisi za hapa nchini za umma au binafsi.
nimecheka sana.
 
Taasisi nyingi bado zinaendeshwa hovyo hovyo sana mpaka unatamani kuwazaba vibao!

Ubabaishaji na uswahili swahili tu mijitu inajivuta kama kobe! VERY LAZY LAZY LAZY LAZY!

Jamani mliojiriwa kwenye mataasisi hayo badilikeni. Changamkeni mfanye kazi kama watu wenye akili timamu.

Unafika unakuta jitu linaongea na simu, mara linatafuna sijui karanga. Jitu linababaika tu hakuna kitu linachofanya mradi siku zimeenda kalipwa mshahara aende kula mishkaki.
 
Taasisi nyingi bado zinaendeshwa hovyo hovyo sana mpaka unatamani kuwazaba vibao!

Ubabaishaji na uswahili swahili tu mijitu inajivuta kama kobe! VERY LAZY LAZY LAZY LAZY!

Jamani mliojiriwa kwenye mataasisi hayo badilikeni. Changamkeni mfanye kazi kama watu wenye akili timamu.

Unafika unakuta jitu linaongea na simu, mara linatafuna sijui karanga. Jitu linababaika tu hakuna kitu linachofanya mradi siku zimeenda kalipwa mshahara aende kula mishkaki.
Hii kweli kaka
 
Tanesco walinishangaza kidogo.

Inafahamika ukilipa ili ufungiwe umeme (line mpya) inachukua mpaka miezi mitatu na kuendelea, ila ilinishangaza mara baada ya kulipia benki ndani ya wiki napigiwa simu wapo njiani.

Nadhani kama wanawatendea wengine hivi basi wamebadirika na kongore kwao.
 
Tanesco walinishangaza kidogo.

Inafahamika ukilipa ili ufungiwe umeme (line mpya) inachukua mpaka miezi mitatu na kuendelea, ila ilinishangaza mara baada ya kulipia benki ndani ya wiki napigiwa simu wapo njiani.

Nadhani kama wanawatendea wengine hivi basi wamebadirika na kongore kwao.
Hawa jamaa wameaadvance sana siku hizi, tatizo ni metre zao zikiharibika baada wakupe bure wanakuuzia tena kwa 380k...
 
Baada ya kulipa Hyo pesa umepewa na risiti. kama hapana basi itakuwa imeveshwa suti
Hapana mkuu ilikuwa halali kabisa, na risiti wanatoa..

wanaibaje pesa inayolipwa kwa control namba? Ule ulikuwa utaratibu uliowekwa na serikali nadhani hata mwaka huu ni hivohivo
 
Mleta mada wanaohakiki sio wanaotoa vyeti kuna segregation of duties naona wewe ndie hujielewi kabisa

UNADHANI HUYO MTOAJI KAZI YAKE NYINGINE KUHAKIKI!!!!
 
Back
Top Bottom