Uchaguzi 2020 Ni hatua zipi za kisheria ambazo Tume (NEC) ina mamlaka dhidi ya mgombea anayetaka kusababisha uvunjifu wa amani?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,952
4,326
Kuna kanuni zilizowekwa kwa mjibu wa sheria ya uchaguzi wa namna ambavyo wagombea wanatakiwa kuzifuata wanapofanya kampeni kushawishi kura za wananchi. Kabla ya kuteuliwa na NEC wagombea hawa waliapa mbele ya mahakimu au majaji kuwa watazingatia kanuni na maadili hayo yaliyowekwa kwa mjibu wa sheria.

Kuna mgombea fulani ambaye ni wazi kabisa katika kampeni zake hazingatii kabisa hizo kanuni, taratibu na maadili aliyoapa kufuata. Lugha na maneno anayotumia dhidi ya mgombea mwenzake hayakubaliki hayakubaliki hata kidogo na ni kinyume na maadili yaliyowekwa na sheria hiyo. Ni maneno makali yenye kuuzi, kufedhehesha na kumudhalilisha (defarmatory) mgombea mwenzake.

Anatumia lugha ya kibabe yenye kuchochea uvunjifu wa amani. Amekuwa akirudia rudia kuwa ana watu wengi nyuma yake (wafuasi wake) na kwamba wasijaribu kumugusa maana moto watakaouwasha hakuna atakaye weza kuuzima. Bahati nzuri wale wa upande mwingine wamejitahidi sana kuwa wavumilivu na wastaarabu.

Sasa ni nani mwenye mamlaka ya kutiepusha tusifike pabaya? Jee Tume yetu ya uchaguzi inayo mamlaka ya kumchukulia hatua zipi za kisheria mtu kama huyu? Je, ina mamlaka ya kumpa onyo kali, karipio au kufuta uteuzi wake wa kuwa mgombea kabla hajawasha huo moto anaousema?
 
Sidhani kama NEC ina uwezo wa kumchukulia hatua Rais Magufuli kwa kuibua hisia za ukabila na ukanda kwenye kampeni, jambo ambalo ni kosa kubwa kwa sheria zetu.

Mtu anayeegemea kwenye ukabila na ukanda, ni hatari sana kwa amani ya nchi yetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajifanya hujaelewa ni nani anayetaka kuwasha moto? Of course vyombo vya habari vyenye uzalendo haviwezi kuandika au kurusha maneno yake ya kutaka kuvuruga amani yetu. Ila NEC tunadhani inatakiwa kumuadabisha mtu huyu mapema iwezekanavyo kabla hajatuvurugia amani yetu. Kwanza anajua fika kwamba hatashinda uchaguzi; ije mvua au lije jua. Katumwa na mabeberu kuja kutuvuruga ili mabeberu warudi kupora natural resources zetu.
 
Hah hah hah. Mnaanza kujuta kwa nini hamkumuengua. Ngoja mpate moto!
Bado anaweza kuenguliwa kwa kukiuka kiapo alichoapa mbele ya mahakama kuu kwamba atazingatia maadili ya kampeni kama zilivyowekwa kwa mjibu wa sheria. NEC ndiyo ilimteuwa na ina mamlaka ya kutengua uteuzi wake wakati wo wote. Uamuzi wake hauwezi kupingwa mahakamani.

Na huyo mgombea analijua hilo. Na anataka iwe hivyo ili akawaeleze waliomtuma kwani anajuwa hawezi kupata kura zaidi ya laki moja. Hawezi kuzunguka nchi nzima na hako kamtumba ka helikopta kenye pilot mwenye umri wa miaka 80. Nchi yetu ni kubwa kuliko ukizijumulisha nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kwa pamoja. Hawezi.
 
Dk Akili bwana;

Bams ametoa hoja ya kwanini unagikiri kwanini Magufuli awezi kuwajibishwa na NEC kwa kutaka kutugawa makusudi kabisa kwa kutenda kosa la kuwatisha wapiga kura na kuhutubia kwa kilugha na kusema yeye achanguliwe kwasababu ni wa nyumbani msukuma...ja ajabu umerukia tena kwingine.
 
..
Kuna mgombea fulani ambaye ni wazi kabisa katika kampeni zake hazingatii kabisa hizo kanuni, taratibu na maadili aliyoapa kufuata....

Anatumia lugha ya kibabe yenye kuchochea uvunjifu wa amani....

Sasa ni nani mwenye mamlaka ya kutiepusha tusifike pabaya? Jee Tume yetu ya uchaguzi inayo mamlaka ya kumchukulia hatua zipi za kisheria mtu kama huyu? Jee ina mamlaka ya kumpa onyo kali, karipio au kufuta uteuzi wake wa kuwa mgombea kabla hajawasha huo moto anaousema?

Huyo mgombea anajua sheria na kanuni za uchaguzi ila anafanya makusudi. Kwa kuwa kwenye sanduku la kura hana nafasi kabisa, anasubiri achukuliwe hatua akiamini vurugu zitatokea. Anachosahau ni kwamba anawaharibia wagombea wa chama chake wa Ubunge na Udiwani. Tume ya uchaguzi imemwacha aadhibiwe na wapiga kura
 
Huyo mgombea anajua sheria na kanuni za uchaguzi ila anafanya makusudi. Kwa kuwa kwenye sanduku la kura hana nafasi kabisa, anasubiri achukuliwe hatua akiamini vurugu zitatokea. Anachosahau ni kwamba anawaharibia wagombea wa chama chake wa Ubunge na Udiwani. Tume ya uchaguzi imemwacha aadhibiwe na wapiga kura
Ni sawa kabisa ila tume ya uchaguzi ikiendelea kumuacha hivyo hivyo, uvumilivu wa upande wa pili unaweza kushindikana. Na utakaposhindikana na wakaanza kujibu mapigo huo moto anaotaka uwake unaweza kweli ukawaka. Watakaoumia moto huo utakapowaka hasa watakuwa watoto, akina mama, walemavu na wazee. Tume angalao limpe onyo sasa hivi. Afanye kampeni za kiustaarabu kama ambavyo wenzake wanafanya. Wanamuogopa kitu gani? Wao ni tume huru. Na nchi yetu ni nchi huru. Hatupaswi kuogopa cho chote.
 
Ni sawa kabisa ila tume ya uchaguzi ikiendelea kumuacha hivyo hivyo, uvumilivu wa upande wa pili unaweza kushindikana. Na utakaposhindikana na wakaanza kujibu mapigo huo moto anaotaka uwake unaweza kweli ukawaka. Watakaoumia moto huo utakapowaka hasa watakuwa watoto, akina mama, walemavu na wazee. Tume angalao limpe onyo sasa hivi. Afanye kampeni za kiustaarabu kama ambavyo wenzake wanafanya. Wanamuogopa kitu gani?
Naamini hotuba zake na mapokeo ya jamii vinafuatiliwa kwa ukaribu sana. Pia naimini upande unaokebehiwa umejifunza na utamudu kuvumilia.
 
Na mimi nimemsikia huyo mgombea. Anachochea ukabila kwa kuzungumza lugha za kikabila katika mikutano yake huku kanuni za uchaguzi zinakataza. Huyu anataka kutugawa na kuleta vita ya makabila.

Pia anatishia wananchi kuwa wasipomchagua yeye au wabunge na madiwani wa chama chake atawakomesha.
 
Naamini hotuba zake na mapokeo ya jamii vinafuatiliwa kwa ukaribu sana. Pia naimini upande unaokebehiwa umejifunza na utamudu kuvumilia.
Upande wa pili unaweza kushindwa kumudu kuendelea kumvumilia. Mwenezi leo kadokeza.
 
Upande wa pili unaweza kushindwa kumudu kuendelea kumvumilia. Mwenezi leo kadokeza.
Yawezekana ikawa hivyo lakini tukumbuke kuna maisha baada ya uchaguzi. Anayekebehi na anayefanyiwa kitendo hicho wote wataendelea kuishi nchi hii, mmoja akiwa na madaraka.

Tuombe tu kuwa busara inatawala wakati huu, wa kupiga kura na baada ya kura, kukubali matokeo.

Kilicho wazi, kutokana na mada iliyorushwa na ITV muda mfupi uliopita, mgombea anayetoa matusi na/au kumkejeli mgombea mwingine asitegemee kura. Na ndiyo maana kwenye hizo kampeni watu wanashangilia kwa kebehi bila kufanya vurugu. Tume ikingilia italipua vurugu, ambacho mgombea anayetumia lugha ya matusi anataka iwe.
 
Unajifanya hujaelewa ni nani anayetaka kuwasha moto? Of course vyombo vya habari vyenye uzalendo haviwezi kuandika au kurusha maneno yake ya kutaka kuvuruga amani yetu. Ila NEC tunadhani inatakiwa kumuadabisha mtu huyu mapema iwezekanavyo kabla hajatuvurugia amani yetu. Kwanza anajua fika kwamba hatashinda uchaguzi; ije mvua au lije jua. Katumwa na mabeberu kuja kutuvuruga ili mabeberu warudi kupora natural resources zetu.
Neno mabeberu limewakaa sana midomoni mwenu kama mlivyo karirishwa. Lakini mkiulizwa hao mabeberu ni akina nani hasa hamtoi majibu. Hamna tofauti na kasuku kuimba kitu usichokijua.
 
Unajifanya hujaelewa ni nani anayetaka kuwasha moto? Of course vyombo vya habari vyenye uzalendo haviwezi kuandika au kurusha maneno yake ya kutaka kuvuruga amani yetu. Ila NEC tunadhani inatakiwa kumuadabisha mtu huyu mapema iwezekanavyo kabla hajatuvurugia amani yetu. Kwanza anajua fika kwamba hatashinda uchaguzi; ije mvua au lije jua. Katumwa na mabeberu kuja kutuvuruga ili mabeberu warudi kupora natural resources zetu.
Lazima uwe mjinga hasa kuamini kwamba siasa za ukabila na ukanda, siyo hatari kwa amani ya nchi yetu.

Mwalimu alifanya jitihada kubwa, na hakuwa na huruma na yeyote anayeendekeza siasa za kikabila, ukanda hata dini lakini leo inaonekana ni sifa kuegemea kwenye ukabila na ukanda. Na kuna wayu waendawazimu hawaoni hiyo kama ni hatari.

Unadhani kutatokea nini kwa mfano, Lisu naye akaenda mikoa ya kati, Kaskazini, Kusini, Nyanda za juu Kusini na Pwani, akawaambia kuwa Magufuli ameomba wasukuma wamchague kwa kuwa ni msukuma mwenzao, ninyi mtamchagua kwani ninyi ni wasilukuma wenzake? Nichagueni mimi kwa sababu mimi silitegemei kabila langu bali nategemea kura za ninyi Watanzania wote. Unadhani reaction ya wasio wasukuma itakuwaje?

Na je, baadaye hakutatokea kuchukiana au kupendana kwa misingi ya kikabila?

Kauli ya Rais Magufuli ya kusema, wasukuma nichagueni mimi msukuma mwenzenu na ni wa huku huku ilikuwa mbaya kabisa, na isiyostahili kutetewa na mtu yeyote mwenye upendo na Taifa letu.

Rais Magufuli atuambie, baada ya kuwaomba wasukuma wamchague kwa vile ni msukuma mwenzao, hahitaji kura za sisi wote tusio wasukuma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom