Bonson
Senior Member
- Apr 20, 2013
- 183
- 147
Ndugu wa JF,
Msemo wa Kiswahili, MNYONGE MNYONGENI ILA HAKI YAKE MPENI, ni dhahiri na kweli. Kwanza nianze kwa kutoa msimamo wangu binafsi kuhusu kuuwawa kwa Ndugu Mabina; ni kweli raia walikasirishwa na matendo ya Mabina; lakini hata hivyo si haki kwa raia kujichukulia sheria mikononi. Hali hii ikiendelea kwa kweli Nchi haita tawalika. Naomba tuache ushabiki wa kiasiasa katika hili jambo; ni lazima vitendo hivi vikemewe katika jamii.
Kwa upande mwingine; nitoe lawama kwa mfumo wa haki (Mahakama) na vyombo vingine na usalama. Ni hatari pale ambapo raia wataamini kwamba hawawezi pata haki yao katika vyombo hivi. NI HATARI SANA MNYONGE ANAPOCHOKA KUNYONGWA!! Tusipokuwa makini tutajikuta tunaibomoa nchi yetu kwa sababu ya wachache wasiotaka kutenda haki kwa jamii.
Rai yangu kwa walio madarakani na nafasi za maamuzi ni kwamba tukumbuke msimamo wa Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere; "CHEO NI DHAMANA; SITATUMIA CHEO CHANGU KWA MANUFAA YANGU BINAFSI AU KUGANDAMIZA WANYONGE."
Asanteni.
Msemo wa Kiswahili, MNYONGE MNYONGENI ILA HAKI YAKE MPENI, ni dhahiri na kweli. Kwanza nianze kwa kutoa msimamo wangu binafsi kuhusu kuuwawa kwa Ndugu Mabina; ni kweli raia walikasirishwa na matendo ya Mabina; lakini hata hivyo si haki kwa raia kujichukulia sheria mikononi. Hali hii ikiendelea kwa kweli Nchi haita tawalika. Naomba tuache ushabiki wa kiasiasa katika hili jambo; ni lazima vitendo hivi vikemewe katika jamii.
Kwa upande mwingine; nitoe lawama kwa mfumo wa haki (Mahakama) na vyombo vingine na usalama. Ni hatari pale ambapo raia wataamini kwamba hawawezi pata haki yao katika vyombo hivi. NI HATARI SANA MNYONGE ANAPOCHOKA KUNYONGWA!! Tusipokuwa makini tutajikuta tunaibomoa nchi yetu kwa sababu ya wachache wasiotaka kutenda haki kwa jamii.
Rai yangu kwa walio madarakani na nafasi za maamuzi ni kwamba tukumbuke msimamo wa Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere; "CHEO NI DHAMANA; SITATUMIA CHEO CHANGU KWA MANUFAA YANGU BINAFSI AU KUGANDAMIZA WANYONGE."
Asanteni.