Uchaguzi 2020 Ni haki tena ni vema Rais Magufuli akapita bila kupingwa uchaguzi mkuu 2020

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,752
139,556
Simuoni mtu mwingine kati ya watia nia ya urais kutoka vyama vyote mwenye uwezo wa kutupa uongozi katika level ya uchumi wa kati zaidi ya Rais Magufuli.

Nitazungumza na viongozi wa vyama vyote vya siasa ili tuweze kumpa heshima ya kipekee Rais Magufuli aweze kupita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu ujao.

Nitaanza mazungumzo na rafiki zangu Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Hashimu Rungwe......ninaamini watakuwa wazalendo na kuwashawishi wafuasi wao.

Maendeleo hayana vyama

cc: Mzee Mgaya, Mchungaji Erasto, Pascal Mayalla, Daudi Mchambuzi!
 
Wazee wenzako sio matahira km wewe mataga Jpm kafanya jambo gani la maana huyu msanii baba kailuki
 
Nilikuambia huyo jamaa hawezi siasa za ushindani, ndio maana kila mwanaccm anajitahidi kutaka asiingie kwenye ushindani maana atachemsha. Ni hivi lazima ashindane.

Huyo toka akiwa mbunge alikuwa anapita kwa fugisu. Yeye atumie tu madaraka yake kunajisi uchaguzi kama kawaida yake.
 
Naona kila mkikumbuka kilichomkuta JK vs Slaa uchaguzi wa 2010, kila mwanaccm akimuangalia Magufuli anajua lazima afungishe.

Inafahamika akisimamishwa mpinzani atakayeweka data za ukweli, nje ya hizi wananchi wanazolishwa, Magufuli hana uwezo wa kupangua hoja.

Mambo ya ajira yakiwekwa wazi na mishahara lazima mzee apanick. Ikizingumziwa Demokrasia na kundi la watu wasiojulikana, udhaifu wote wa mzee utakuwa wazi, na huenda hali hiyo ikamuacha na msongo wa mawazo ndani ya maisha yake yote hapa duniani.

Hivyo wanaccm wanaomba usiku na mchana jamaa asifanye mtihani, maana wanajua fedheha itakayowakuta.
 
Simuoni mtu mwingine kati ya watia nia ya urais kutoka vyama vyote mwenye uwezo wa kutupa uongozi katika level ya uchumi wa kati zaidi ya Rais Magufuli.

Nitazungumza na viongozi wa vyama vyote vya siasa ili tuweze kumpa heshima ya kipekee Rais Magufuli aweze kupita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu ujao.

Nitaanza mazungumzo na rafiki zangu Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Hashimu Rungwe......ninaamini watakuwa wazalendo na kuwashawishi wafuasi wao.

Maendeleo hayana vyama

cc: Mzee Mgaya, Mchungaji Erasto, Pascal Mayalla, Daudi Mchambuzi!
Mkuu umenifanya nicheke tu na kuisikitia nchi yangu.Yaani Kama Magufuri ndo genius wa Tanzania sioni ni kwa sababu gani hatuingizwi kwenye maajabu ya dunia,Magufuli huyu huyu anayetekekeza budget zake kwa below average ndo afanye nini eti? Labda Kama tunafika huko kwa propoganda
 
Mkuu umenifanya nicheke tu na kuisikitia nchi yangu.Yaani Kama Magufuri ndo genius wa Tanzania sioni ni kwa sababu gani hatuingizwi kwenye maajabu ya dunia,Magufuli huyu huyu anayetekekeza budget zake kwa below average ndo afanye nini eti? Labda Kama tunafika huko kwa propoganda

Wamepiga propaganda za kutosha kwa muda wa miaka mitano, wanajua sasa ni muda wa rekodi kuwekwa sawa, hawataki jamaa yao aingie kwenye kikaango ili anyooshe maelezo! Na sababu ni kuwa wanajua mzee baba ni mtu wa kupanick akisikia ukweli ukimwagwa hadharani.
 
Naona kila mkikumbuka kilichomkuta JK vs Slaa uchaguzi wa 2010, kila mwanaccm akimuangalia Magufuli anajua lazima afungishe. Inafahamika akisimamishwa mpinzani atakayeweka data za ukweli, nje ya hizi wananchi wanazolishwa, Magufuli hana uwezo wa kupangua hoja. Mambo ya ajira yakiwekwa wazi na mishahara lazima mzee apanick. Ikizingumziwa Demokrasia na kundi la watu wasiojulikana, udhaifu wote wa mzee utakuwa wazi, na huenda hali hiyo ikamuacha na msongo wa mawazo ndani ya maisha yake yote hapa duniani. Hivyo wanaccm wanaomba usiku na mchana jamaa asifanye mtihani, maana wanajua fedheha itakayowakuta.
Napenda thinking yako brother.
 
Lijuakali ana maelezo tofauti ya nani anafanya figisu kwenye uchaguzi
Nilikuambia huyo jamaa hawezi siasa za ushindani, ndio maana kila mwanaccm anajitahidi kutaka asiingie kwenye ushindani maana atachemsha. Ni hivi lazima ashindane. Huyo toka akiwa mbunge alikuwa anapita kwa fugisu. Yeye atumie tu madaraka yake kunajisi uchaguzi kama kawaida yake.
 
Ccm nawaambia ujumbe huu...."Acheni propaganda mfu hizo, Magu anapita mtarudi kuanza kusifia chama muda umewaacha, Magu anapita Tanzania inabaki. Simamieni kweli.
 
Simuoni mtu mwingine kati ya watia nia ya urais kutoka vyama vyote mwenye uwezo wa kutupa uongozi katika level ya uchumi wa kati zaidi ya Rais Magufuli.

Nitazungumza na viongozi wa vyama vyote vya siasa ili tuweze kumpa heshima ya kipekee Rais Magufuli aweze kupita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu ujao.

Nitaanza mazungumzo na rafiki zangu Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Hashimu Rungwe......ninaamini watakuwa wazalendo na kuwashawishi wafuasi wao.

Maendeleo hayana vyama

cc: Mzee Mgaya, Mchungaji Erasto, Pascal Mayalla, Daudi Mchambuzi!
Maelezo yako yote hujataja chama chako hata Mara moja...Mfichieni madhaifu lkn kumbukeni ataondoka na aibu juu.
 
Lijuakali ana maelezo tofauti ya nani anafanya figisu kwenye uchaguzi

Acha Lijualikali, hata akisimama Mbowe na Mnyika sasa hivi waseme kuwa cdm huwa wanashinda kwa wizi, na ccm huwa inashinda kihalali, bado ukweli utabaki kama ulivyo. Ukweli kama ukweli hauhitaji nguvu kubwa kuutetea, maana ukweli unajisimamia.
 
Lijuakali ana maelezo tofauti ya nani anafanya figisu kwenye uchaguzi
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Sawa ila fananisha kati ya ushahidi ulioelezwa na mwizi mwenyewe s ushahidi wa hisia.
Acha Lijualikali, hata akisimama Mbowe na Mnyika sasa hivi waseme kuwa cdm huwa wanashinda kwa wizi, na ccm huwa inashinda kihalali, bado ukweli utabaki kama ulivyo. Ukweli kama ukweli hauhitaji nguvu kubwa kuutetea, maana ukweli unajisimamia.
 
Sawa ila fananisha kati ya ushahidi ulioelezwa na mwizi mwenyewe s ushahidi wa hisia.

Yaani mtu aseme ukweli kuwa yuko bungeni kwa wizi wa kura, na wala bunge lisichukue hatua kwa kuwa na mbunge aliye ndani ya bunge kwa wizi! Hapo inahitaji elimu ya chuo kikuu kweli kujua ni siasa maji taka ndani ya bunge kigoyo?

Ni sawa na mke wako kusema huyo mtoto unayemlea sio wakwako, na ww unakenua eti mke wako katoa ukweli na sio hisia, bila kufanyia kazi kauli yake!
 
Simuoni mtu mwingine kati ya watia nia ya urais kutoka vyama vyote mwenye uwezo wa kutupa uongozi katika level ya uchumi wa kati zaidi ya Rais Magufuli.
Sasa kama huoni unataka tukuvalishe miwani? Hayo si ni matatizo yako mwenyewe?
 
Wakati wa kuachana huwa wanatoa siri boss
Yaani mtu aseme ukweli kuwa yuko bungeni kwa wizi wa kura, na wala bunge lisichukue hatua kwa kuwa na mbunge aliye ndani ya bunge kwa wizi! Hapo inahitaji elimu ya chuo kikuu kweli kujua ni siasa maji taka ndani ya bunge kigoyo? Ni sawa na mke wako kusema huyo mtoto unayemlea sio wakwako, na ww unakenua eti mke wako katoa ukweli na sio hisia, bila kufanyia kazi kauli yake!
 
Kupita bila kupingwa si kipimo kizuri, kipimo kizuri ni kupingwa halafu upite. Jeshi ambalo halijapigana vita utajiaminishaje kuwa ni jeshi imara? Acha JPM apite (na atapita) kwenye kikaango cha uchaguzi na hapo atakuwa imara zaidi kwani ambayo yawezekana hayazungumzwi, sasa yatasemwa hadharani kwenye kampeni; atayasikia na akirudi anayafanyia kazi. Si unajua hata haya anayofanyia kazi yalisemwa hadharani na upinzani!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom