Ni Haki Rais Na Waziri Kiongozi Kuikimbia Nchi Ikiwa Gizani??

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Mafundi warejea kushughulikia umeme Z`bar

2008-06-02 09:32:07
Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema wataalam wa umeme kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wamerejea tena Zanzibar kuanza kazi ya matengenezo ya njia ya umeme iliyoharibika katika eneo la Fumba wilaya ya Magharibi Unguja.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Bw. Mausosur Yusuf Himid alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia kukosekana kwa umeme visiwani hapa kwa wiki mbili.

Alisema matengenezo hayo yanashirikisha jopo la mafundi kutoka Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) na wataalam wengine kutoka nje.

``Kazi ya matengenezo inaendelea huku tukiendelea kusubiri wataalam walioshughulikia mradi huu na wakati wo wote watawasili toka Norway na Ufaransa,`` alisema.

Alisema hadi sasa serikali imefanikiwa kudhibiti tatizo la uhaba wa maji baada ya kuweka majenereta katika vyanzo vya maji, lakini serikali imeagiza jenereta nne kutoka Tanzania Bara ili maeneo yaliyosalia yawe yanapata huduma hiyo.

Awali wataalam kutoka TANESCO waliondoka Zanzibar baada ya kushauriwa na SMZ wasifanye matengenezo hadi watalaam kutoka nje watakapowasili.

Wakati huo huo, Rais Aman Abeid Karume anaondoka kwenda Italia kuhudhuria mkutaano wa wakuu wa nchi unaohusiana na Usalama wa Chakula Duniani na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi na matumizi ya nishati inayotokana na kilimo.

Taarifa ya serikali imesema kuwa Rais Karume anamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano huo unaotarajiwa kuanza Juni 3 hadi Juni 5.

Rais Karume ameandamana na mkewe, Mama Shadya, Waziri wa Kilimo wa Jamhuri ya Muungano, Stephen Wassira na Waziri wa Kilimo na Mifugo Zanzibar, Burhan Saadat Haji.


Taarifa ilisema kwamba mkutano huo una lengo la kutafuta hatua za pamoja katika kushughulikia upungufu wa chakula duniani uliosababisha mfumuko wa bei na kuathiri nchi mbalimbali duniani, hususan Afrika.

Wakati huo huo, Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha, anaondoka kesho kuelekea Afrika Kusini kwa ziara ya wiki moja.

Taarifa ya serikali imesema kwamba akiwa nchini humo Waziri Kiongozi atakutana na viongozi mbalimbali wa serikali nchini humo
.

SOURCE: Nipashe
 
na kwa nini asikae nchini kusaidiana na watendaji wengine kutafuta suluhu la tatizo?


wananchi wamuhisije au wamfahamu vipi ikiwa rais na waziri kiongozi wote wanaondoka wakati nchi iko katika hali ya janga la umeme ?
 
na kwa nini asikae nchini kusaidiana na watendaji wengine kutafuta suluhu la tatizo?


wananchi wamuhisije au wamfahamu vipi ikiwa rais na waziri kiongozi wote wanaondoka wakati nchi iko katika hali ya janga la umeme ?

Kwani wana wasiwasi gani? Wao wanajua waharibu, wananchi wawapende au wawachukie wataendelea tu kutawala, mapinduzi daima!
 
wananchi wa zanzibar si wajinga wanajua kila kinachoendelea na hesabu yake itawashinda baadae wakiwafanyia zihaka
 
na kwa nini asikae nchini kusaidiana na watendaji wengine kutafuta suluhu la tatizo?


wananchi wamuhisije au wamfahamu vipi ikiwa rais na waziri kiongozi wote wanaondoka wakati nchi iko katika hali ya janga la umeme ?

Mtu wa Pwani -wacha nikupinge kwa hili. Kwani Waziri wa Maji Uenzi na Nishati si yupo., Kama BLM limekutana likajadili suala hilo, likakubaliana kipi cha kufanya na kumpa kazi Waziri mhusika kuna haja gani ya Rais na Waziri Kiongozi kusitisha majukumu yao mengine na kumsimamia Waziri kutekeleza majukumu yake. Fahamu Nchi haijatangaza hali ya hatari (jambo pekee linalomlazimisha Kiongozi Mkuu kuwepo). Hebu soma kutokana na kadhia ya Richmond jinsi Wakubwa walivyolitia mkono kwa undani suala lile na matokeo yake.
 
Mtu wa Pwani -wacha nikupinge kwa hili. Kwani Waziri wa Maji Uenzi na Nishati si yupo., Kama BLM limekutana likajadili suala hilo, likakubaliana kipi cha kufanya na kumpa kazi Waziri mhusika kuna haja gani ya Rais na Waziri Kiongozi kusitisha majukumu yao mengine na kumsimamia Waziri kutekeleza majukumu yake. Fahamu Nchi haijatangaza hali ya hatari (jambo pekee linalomlazimisha Kiongozi Mkuu kuwepo). Hebu soma kutokana na kadhia ya Richmond jinsi Wakubwa walivyolitia mkono kwa undani suala lile na matokeo yake.

Ndivyo tulivyo kama jina lako linavyosema hubadili msimamo wewe kazi yako ni kutetea CCM Znz na viongozi wake - kama mpopoa embe aso na shebaha atalopata ndio hilo hilo - na wewe leo umepata na uko sahihi, nakuuna mkono kwa hilo kwani maana ya Rais kuteuwa mawaziri ndio maana yake wamsaidie na hata wangebaki hapo Zanzibar wakati chanzo cha ukosefu wa umme kimeshajulikana wangesaidia nin?

Jengine ni kuwa safari aloenda nayo ni muhimu kwani ukosefu wa chakula duniani ni janga jengine ambalo linatishia dunia sasa hivi - kwa hivyo ana haki ya kuhudhuria. Tatizo langu ni kuwa kama atafahamu nini kinaongelewa na umuhimu wake kwa nchi kwani hadi sasa katika bajeti ya serikali ya SMZ umuhimu anaupa katika bajeti ya Vikosi vya SMZ badala ya Kilimo.(Kilimo inapata chini ya asilmia 6 ya bajeti wakati vikosi ni mara mbili na nusu ya hiyo ya Kilimo)
 
Wakiwepo au wakiondoka yote sawa ,lazima wafuate matakwa ya waliowaweka madarakani ,sasa hivi ndio kama alivyosema huyo waziri wanasubiri mafundi wote wakati huu kwa pamoja yule wa Norway na mpya wa Ufaransa wamewaita "mafundi wa mradi huu" ila wamebadilisha kutoka kuwasili ndani ya siku mbili sasa watawasili wakati wowote inaelekea wamishapanda ndege kuelekea Zanzibar au wakati wowote inawezekana mwisho wa mwaka au wakati wowote kama kitakavyotokea kiyama wakati wowote.
 
wananchi wa zanzibar si wajinga wanajua kila kinachoendelea na hesabu yake itawashinda baadae wakiwafanyia zihaka

Hii ni kweli kabisa... mambo ya kuchukulia vitu for granted karibu yatapitwa na wakati na itakuwa vigumu kutawala hata kama una historia nzuri kwenye ukkombozi wa nchi kama ilivyo kwa Mugabe kule Zim
 
Mtu wa Pwani -wacha nikupinge kwa hili. Kwani Waziri wa Maji Uenzi na Nishati si yupo., Kama BLM limekutana likajadili suala hilo, likakubaliana kipi cha kufanya na kumpa kazi Waziri mhusika kuna haja gani ya Rais na Waziri Kiongozi kusitisha majukumu yao mengine na kumsimamia Waziri kutekeleza majukumu yake. Fahamu Nchi haijatangaza hali ya hatari (jambo pekee linalomlazimisha Kiongozi Mkuu kuwepo). Hebu soma kutokana na kadhia ya Richmond jinsi Wakubwa walivyolitia mkono kwa undani suala lile na matokeo yake.


ingawa kweli mie ni mpofu lakini sitoki madenda swahiba wangu.

hivi baraza la mapinduzi lilikaa lini na limetoa maagizo gani?

waungwana kuna mambo ukiyakosea kidogo kisiasa umeliwa, nchi inawahitaji viongozi wake ktk kipindi hiki zaidi kuwa nao pamoja na kuhangaika ktk kutatua matatizo yao kunawapa faraja kuwa viongozi wetu ni kweli wetu.

ila huu mchezo wa kufanya kama hakuna kitu na kusonga mbele madhara yake yatakuja kuonekana. halafu micuf wasiseme na tumewapa mwanya wenyewe.


sasa mtizame mwiba atavyotaka kutukaa kooni kama ngoma ya mdumange
 
Ndivyo tulivyo kama jina lako linavyosema hubadili msimamo wewe kazi yako ni kutetea CCM Znz na viongozi wake - kama mpopoa embe aso na shebaha atalopata ndio hilo hilo - na wewe leo umepata na uko sahihi, nakuuna mkono kwa hilo kwani maana ya Rais kuteuwa mawaziri ndio maana yake wamsaidie na hata wangebaki hapo Zanzibar wakati chanzo cha ukosefu wa umme kimeshajulikana wangesaidia

Sawa. Najua kuwa mimi sina shabaha. Lakini labda na wewe leo umepata, kwa vile nikueleze ukweli kuwa mimi si mtetezi wa CCM tu. Bali mimi natetea wananchi halisi wa Zanzibar (Wazanzibari-Kindakindaki (Hawa wanajumuisha Wahadimu/Washirazi-wale Washamba-., Watumbatu, ma Wapemba fyoko) wawe popote pale. Tafadhali karibu. Jumuika nami.
 
Soma yafuatayo kwa lafudhi ya Kizenji:
Rais karume na Waziri wake Shamsi Vuai wakizungumzia matayarisho yao ya kusafiri wiki hii:
AK: Yakhe!! Vuai, miye nshajiandaa kuelekea huko kwa wenzetu wenye umeme!! Weye wasemaje na safari yako?
SV: Mkubwa akinena mdogo hufuata. hiyo ya kusini mwetu ndio naelekea mara tu ukiondoka. sina neno kabisa roho jepesi kabisa
AK: Sasa wananchi wako waambiweje kutokana na suala hili?
SV: wahenga wetu walisema Subira yavuta heri mkuu
AK: Alaaah! weye wayaelewa mno haya mambo (huku akicheka) ila wahenga nao walisema mfagizi ngazi huanzia juu wala si chini, yasije yale mambo ya bara yakatujia na sisi. wamuona hamadi macho yanavyomtoka?
SV: Walaahi! Hapati kiti chako! Weye ndiyo wastahili tokea mwanzo yale yalikuwa marasharasha ya kipemba ati!
AK: Tena wanikumbusha, miye tangu nazaliwa naona vibatari kwetu hawa watu wataka umeme wa nini hali wanautumia kutafuta vya uvunguni???
SV: Walaahi! Miye nawashangaa!! wazungu wanaipenda zanzibar ikiwa kama ilivyo na haina maendeleo wapate kuipiga picha vyema watutangaze huko makwao, haya umeme wa nini??
AK: Miye ngoja nikatende kazi za kiraisi huko nje watanijuaje wakati nimejichimbia huku shimoni??
SV: Sawa kabisa mkuu! Miye nitafanya kazi ya kuutangaza ufalme wako kule kwa mandela.
AK: Tukirudi tutawapa taarifa za wenzetu huko wala hawatakumbuka ya umeme. Sijui Jakaya ana mpango gani ila nisimsumbue maana naye kabanwa kweli.
SV: Sawa mkuu, miye natoka hivyo nasikia swala linakaribia kuanza.
AK: haya safiri salama
 
Soma yafuatayo kwa lafudhi ya Kizenji:
Rais karume na Waziri wake Shamsi Vuai wakizungumzia matayarisho yao ya kusafiri wiki hii:
AK: Yakhe!! Vuai, miye nshajiandaa kuelekea huko kwa wenzetu wenye umeme!! Weye wasemaje na safari yako?
SV: Mkubwa akinena mdogo hufuata. hiyo ya kusini mwetu ndio naelekea mara tu ukiondoka. sina neno kabisa roho jepesi kabisa
AK: Sasa wananchi wako waambiweje kutokana na suala hili?
SV: wahenga wetu walisema Subira yavuta heri mkuu
AK: Alaaah! weye wayaelewa mno haya mambo (huku akicheka) ila wahenga nao walisema mfagizi ngazi huanzia juu wala si chini, yasije yale mambo ya bara yakatujia na sisi. wamuona hamadi macho yanavyomtoka?
SV: Walaahi! Hapati kiti chako! Weye ndiyo wastahili tokea mwanzo yale yalikuwa marasharasha ya kipemba ati!
AK: Tena wanikumbusha, miye tangu nazaliwa naona vibatari kwetu hawa watu wataka umeme wa nini hali wanautumia kutafuta vya uvunguni???
SV: Walaahi! Miye nawashangaa!! wazungu wanaipenda zanzibar ikiwa kama ilivyo na haina maendeleo wapate kuipiga picha vyema watutangaze huko makwao, haya umeme wa nini??
AK: Miye ngoja nikatende kazi za kiraisi huko nje watanijuaje wakati nimejichimbia huku shimoni??
SV: Sawa kabisa mkuu! Miye nitafanya kazi ya kuutangaza ufalme wako kule kwa mandela.
AK: Tukirudi tutawapa taarifa za wenzetu huko wala hawatakumbuka ya umeme. Sijui Jakaya ana mpango gani ila nisimsumbue maana naye kabanwa kweli.
SV: Sawa mkuu, miye natoka hivyo nasikia swala linakaribia kuanza.
AK: haya safiri salama
Nkhaa!!!!!!!Haya ya Kikwajuni Juu.
 
..unguja itaacha lini kutegemea umeme wa tanganyika?

..si walishasema kuwa watazalisha wao.
 
Back
Top Bottom