Cantalisia
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,222
- 2,925
Habari zenu wadau,mwenzenu hili limenipa utata kidogo,kuna kaka fulan amepanga nyumba ya jiran na ninapoishi huyu jamaa ni mtoto pekee kwa baba na mama yake ila baba alishafariki,mama yake nae anaishi mtaa wa jirani na anapoishi mwanae, huyu mama siku zote alishapanga mwanae akitaka kuoa basi aone binti wa kitanga ila kwa bahati mbaya yule kaka hakuwahi kubahatika kuwa na mpnz wa kutoka tanga,ikawa mama yake anamfatilia kwa kila mpnz anayekuwa nae na akigundua sio wa tanga anaanzisha visa vya ajabu mpaka msichana anaamua kutosa jamaa,visa vyake ni pamoja na kuibuka kwa mwanae alifajiri na akikuta jamaa kalala na binti panachimbika amtukana huyo binti na kumfukuza na kumkanya kumona na mwanae, sasa tabia hiyo ikamkera sana jamaa akaamua kuwashirikisha ndugu wengine wa mkanye mama yake tabia hiyo, ila huyo mama hakuacha na akaendelea na upuuzi wake,sasa jamaa akapata binti wa kichaga na kabla hajaanza kwenda nae kwake alimpa story nzima kuhuhsu tabia ya mama yake, yule dada akubali na kumwomba jamaa amruhusu kukomesha tabia mbaya ya mama yake, jamaa kutokana na kero za mama na amempenda yule dada na ana mapango wakumuoa akaubali.
Sasa juzi kati mama akagundua mwanae ana mpnz na huwa anakuja kulala mara kwa mara, kama kawa siku hiyo kaibuka kwa mwanae saa kumi na moja alfajiri akagonga yule dada ndio akaenda kumfungulia, alipoingia tu akaanza kumhoji yule binti anafanya nn pale na maswali kibao mpaka kabila binti akamwambia ni mchaga, mama akaanza kubwata katukana sana mda wote jamaa yuko chumban anasikilizia,yule binti akafunga malango wa kutoke nje na akamuuliza yule mama sababu za kutukanwa na kutakiwa aondoke pale mda ule ni nn,yule mama hakujibu akamkata kibao yule binti, wandugu dada alitembeza kibano cha ukweli kwa bi mkubwa mpaka akawa naomba msaada jamaa hakutoka chumbani,binti akamwambia bi mkubwa apige magoti na amwombe msamaha na aahidi kuacha tabia yake chafu, ili kuepuka kipigo zaidi bi mkubwa akakubali na wakayamaliza na mama akaondoka kimya kimya bila hata kuuliza aliko mwanae,je hata kama mama mkwe ni mcharuko ni haki kwa binti kumtia adabu?wadau mnalionaje hili nawakilisha.
Sasa juzi kati mama akagundua mwanae ana mpnz na huwa anakuja kulala mara kwa mara, kama kawa siku hiyo kaibuka kwa mwanae saa kumi na moja alfajiri akagonga yule dada ndio akaenda kumfungulia, alipoingia tu akaanza kumhoji yule binti anafanya nn pale na maswali kibao mpaka kabila binti akamwambia ni mchaga, mama akaanza kubwata katukana sana mda wote jamaa yuko chumban anasikilizia,yule binti akafunga malango wa kutoke nje na akamuuliza yule mama sababu za kutukanwa na kutakiwa aondoke pale mda ule ni nn,yule mama hakujibu akamkata kibao yule binti, wandugu dada alitembeza kibano cha ukweli kwa bi mkubwa mpaka akawa naomba msaada jamaa hakutoka chumbani,binti akamwambia bi mkubwa apige magoti na amwombe msamaha na aahidi kuacha tabia yake chafu, ili kuepuka kipigo zaidi bi mkubwa akakubali na wakayamaliza na mama akaondoka kimya kimya bila hata kuuliza aliko mwanae,je hata kama mama mkwe ni mcharuko ni haki kwa binti kumtia adabu?wadau mnalionaje hili nawakilisha.