kagombe
JF-Expert Member
- Mar 1, 2015
- 3,508
- 1,642
Kwa Wale wazee wa movie.
Hebu tujuzane movie kali uliyoikubali kuanzia scenes arrangements, location, actors, scenes originality, story originality na vingine vingi.
Kwangu mimi Tangu nianze kuangalia movie ya MAD MAX FURY ROAD sijawahi kuona tena movie kali kama ile.
Kiukweli wameitengeneza katika uhalisia wa aina yake.
Mpangilio wa Visa unaeleweka hata bila ya kusikiliza maneno.
Washiriki wameweza kucheza katika nafasi zao kila mmoja akionesha umahiri kwa nafasi yake.
Pia mwanamke amepewa nafasi ya ujasiri mkubwa huku location zikitumika ambazo sio rahisi kuzipata.
Pia ni filamu ambayo imebase kwenye action ( hakuna stori ni kashkash mwanzo mwisho.)
Huwezi kusinzia ukiangalia hii filamu. Huwa naingalia bila kuichoka.
Kiukweli kwa upande wangu MAD MAX nimeikubali.
Sasa vipi kwa upande wenu wadau wa Filam?
shamba kubwa