Nigrastratatract nerve
JF-Expert Member
- Sep 4, 2019
- 1,395
- 3,899
World Bank wameikopesha Tanzania mabillioni ya shilingi na wao furaha yao ni kuona wanalipwa hela zao kama zilivyo Taasisi zingine za fedha ambazo zingependa wateja walipaji wazuri, imeelezwa kuwa tangu Rais Magufuli aingie ameonyesha nidhamu ya hali ya juu sana kwenye ulipaji wa madeni ya Tanzania kwenye Taasisi za kifedha.
Wazungu pia pamoja na mambo mengine wameona Magufuli ni mkweli na mwenye misimamo isiyoyumba kitendo cha kuitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati kimevuruga Sera za upinzani zilizobainisha kuwa JPM anaharibu uchumi.
Wapinzani wanaweza wakafikiri kuwa kuisimanga Tanzania kwa mambo mazuri inayoyafanya kwa ajili ya watu wake ndio kutawafanya waingie Ikulu, hapana wajitafakari sana Mzungu ana urafiki wa masilahi na si vinginevyo hii ya Bank ya Dunia imewavua nguo wapinzani na wazodoaji wa JPM wanaoshinda kutwa mitandaoni kubeza juhudi za Serikali.
Wazungu pia pamoja na mambo mengine wameona Magufuli ni mkweli na mwenye misimamo isiyoyumba kitendo cha kuitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati kimevuruga Sera za upinzani zilizobainisha kuwa JPM anaharibu uchumi.
Wapinzani wanaweza wakafikiri kuwa kuisimanga Tanzania kwa mambo mazuri inayoyafanya kwa ajili ya watu wake ndio kutawafanya waingie Ikulu, hapana wajitafakari sana Mzungu ana urafiki wa masilahi na si vinginevyo hii ya Bank ya Dunia imewavua nguo wapinzani na wazodoaji wa JPM wanaoshinda kutwa mitandaoni kubeza juhudi za Serikali.