maramia
JF-Expert Member
- Jul 17, 2015
- 2,030
- 1,344
Kwa namna mambo yanavyokwenda, taratibu nimeanza kuamini kwamba hivi sasa ni suala la wakati na majira tu watanzania tutajua siri yote ya mhusika mkuu wa Richmond.
Ili mradi kiongozi mkuu wa nchi kaingia ulingoni kama mlalamikaji kupambana na Lowassa tuliyedhani ndiye mtuhumiwa namba moja wa kashfa ile mambo yanaonekana yatakaa vizuri muda si mrefu.
Ingawa ngumi za jeb za mlalamikaji zinarushwa ovyo hewani wakati zikielekezwa kwa mtuhumiwa huku zikimpalaza msindikizaji wake (Lissu), haijulikani ni kwa nini anampiga jeb msindikizaji badala ya kumdunda moja kwa moja opponent wake.
Lakini lililo dhahiri ni kwamba ilimradi sasa mabondia wamekubali kuingia ulingoni kuzichapa anayesubiriwa ni refa wa kati na majaji washike nafasi zao, tumpate mshindi aliyehusika na kashfa ile ya Richmond.
Ni suala la kusubiri wakati na majira tutamjua mshindi wa Richmond.
Ili mradi kiongozi mkuu wa nchi kaingia ulingoni kama mlalamikaji kupambana na Lowassa tuliyedhani ndiye mtuhumiwa namba moja wa kashfa ile mambo yanaonekana yatakaa vizuri muda si mrefu.
Ingawa ngumi za jeb za mlalamikaji zinarushwa ovyo hewani wakati zikielekezwa kwa mtuhumiwa huku zikimpalaza msindikizaji wake (Lissu), haijulikani ni kwa nini anampiga jeb msindikizaji badala ya kumdunda moja kwa moja opponent wake.
Lakini lililo dhahiri ni kwamba ilimradi sasa mabondia wamekubali kuingia ulingoni kuzichapa anayesubiriwa ni refa wa kati na majaji washike nafasi zao, tumpate mshindi aliyehusika na kashfa ile ya Richmond.
Ni suala la kusubiri wakati na majira tutamjua mshindi wa Richmond.