Ni ajabu! Account za FB, Instagram na Twitter za Rais Donald Trump wa U.S.A zafungwa kwa muda usiojulikana

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Screenshot_20210107-201915.png

Screenshot_20210108-091618.png

Sasa ni wazi kabisa Urais wa Donald Trump unaisha kwa aibu na fedheha kubwa.

Kitendo cha kuhamasisha wafuasi wake jana kuvamia jengo la Bunge la Congress (Capitol Hill) ili kuzuia bunge lisifanye kazi yake kumwidhinisha Rais Mteule Joe Biden (D) na makamu wake Kamala Harris ilikuwa ni ishara ya mwisho kuwa huyu mzee ni "mentally unfit" na hafai kukalia kiti cha Urais hata kwa siku 14 zilizobaki.

Sasa kwa sababu ya "uropokaji" wake bila ya kupima madhara ya kauli zake hizo, amefungiwa kutumia mitandao yote mikubwa ya kupashana habari duniani ikiwemo Facebook, Instagram na Twitter.

Inasemekana kwa sasa, yumo kifungoni cha kutopiga wala kupokea simu yoyote kwa yeyote.

Aidha, tayari utaratibu wa kumng'oa White House kabla hata ya tarehe 20/1/2021 siku ya kuapishwa Rais Joe Biden maarufu kama "impeachment" unaandaliwa kwa mujibu wa sheria za Marekani. Na hii ni dharura na itafanyika kwa udharura pia.

Tayari pia mawaziri wengi na maafisa wa taasisi nyeti za serikali kama FBI, CIA nk baadhi wameachia ngazi na wengine wanajiandaa kwa kuwa wamechukizwa na tabia ya Rais Trump isiyojali sheria na katiba ya nchi na hata kuhatarisha usalama wa RAIA na NCHI kwa ujumla.

Naye Makamu wa Rais, Bw. Mike Pence, amechukizwa sana na tabia ya Rais na katika hali ya kushangaza, akasema wazi kuwa, hakubaliani naye.

Na Republicans wenzake wamemtaka kuitisha baraza la mawaziri haraka iwezekanavyo ili kuweka njia ya kumwondoa Donald Trump madarakani kwa kutumia Article 25 ya katiba ya Marekani inayoweka utaratibu wa VP kuchukua madaraka ya Rais iwapo ameshindwa ku - discharge majukumu yake ya Urais kwa sababu zozote zile kabla ya mambo kuharibika zaidi.

Kwa kifupi Wamerekani wamechukizwa sana na kilichotokea jana tendo lililochagizwa na kauli za Rais. Hawatamani hata awe Rais kwa kwa siku mbili zijazo.

For sure kabisa, ni wazi sasa, kuwa Donald Trump hamalizi wiki moja ijayo akiwa Rais wa Marekani.
 
Dunia inapaswa kujifunza kutokana na tabia mbaya ilofanywa na Trump. Ni aibu kwa Taifa kubwa kama Marekani kuharibiwa taswira yake ya heshima ambayo imetengeneza kwa muda mrefu sana ije kuharibiwa na mtu mmoja kwa muda mfipi sana. Naamini sheria za Marekani zitafanyakazi juu ya uchokozi ulooneshwa na ndugu Trump
 
Huu Uzi WA Kiswahili lakini ngumu kuchangia hatari. Wajuzi njooni sie wengine weupe na issue za USA.
 
Si ni nyinyi mliokuwa mnaisifia kuwa Marekani ni baba wa demokrasia?
Wewe mada imekuzidi uwezo,subiri za level yako ndio ujadili!

Unadhani tatizo ni Marekani au tatizo ni Trump?Unadhani ingekuwa Tanzania,Rais aliyeko madarakani afanye kama anayofanya Trump,nani angeweza kumtoa?Hapo nchi za Africa ndipo zinapaswa kujifunza umuhimu wa kuwa na taasis imara!

Angalia tu hapo Museven anavyobadili katiba kama anavyojisikia ili aendelee kutawala! Hata akishindwa uchaguzi,akagoma kuachia madaraka,nani atamgusa?Vyombo vyote vitamnyenyekea!
 
Na Secret Service wamempunguzia huduma.
Taasisi 'zinamuondoa' kimtindo siku chache kabla ya matarajio yake
 
CIA wanasikitika maana huyu boya hakuandaliwa na systems ameibuka nguvu yake kuwa white na tajiri .....walimchukia Obama hawa Rep ndio kusa kumpa mwema hovyo ! Aibu kubwa sanaaa
 
Si ni nyinyi mliokuwa mnaisifia kuwa Marekani ni baba wa demokrasia?
Ndiyo demokrasia yenyewe hiyo, kwamba, kama watu wataamua kutumia uhuru wao wa kidemokrasia kuchagua mwehu, wanafanya hivyo na gharama yake ndiyo hiyo na wamejifunza...

Hiyo ndiyo demokrasia haswa siyo hizi za kwetu mtu mmoja tu kwa chuki zake binafsi anaamua kutopingwa na Bernard Membe na kumkata mapema huku watu wakitamani kumchagua aliyekatwa...!
 
Back
Top Bottom