Ni aibu wabunge kutetea Mafisadi.

LAZIMA NISEME

JF-Expert Member
Apr 5, 2015
232
260
NI AIBU WABUNGE WA UPINZANI KUTUMIKA KUTETEA MAFISADI.

• Sasa mafisadi watumia wabunge wa upinzani kujisafisha.
• Waahidiwa donge nono kufanikisha kuichafua kazi nzuri inayofanywa na serikali
• Mabilioni yaliyoibwa na kufichwa na mafisadi hao, yatumika kulipa upinzani
• Waandishi nao wamehongwa mamilioni ili kuichafua serikali

Kwa mujibu wa taarifa zinazopatikana NIDA ni kwamba Gharama za mradi wote wa kuzalisha vitambulisho vya uraia (Kitambulisho cha Taifa) ni zile zile ziliokuwa katika mkataba hata pamoja na kufanyiwa maboresho muhimu katika kitambulisho cha uraia.

“Utengenezaji, usambazaji na ukandarasi wa miundo mbinu ya vitambulisho vya taifa unagharimu kiasi cha Dola za kimarekani $3.45 kwa kila kitambulisho mpaka kinapokabidhiwa kwa Mtanzania. Bei hii ya kitambulisho ndiyo bei iliyopo katika mkataba wa awali hata pamoja na maboresho ya msingi yaliyofanyika” Afisa Habari Mkuu wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa NIDA Rose Mdami amekiambia chanzo chetu.

Ikumbukwe kwamba kiwango kiasi hicho cha dola ya Marekani ni sawa na shilingi ya TANZANIA 7,693.5 tu na si shilingi 17,000 kama inavyodaiwa na wabunge wanaotumika na mafisadi.

Kwa mujibu wa maelezo sahihi ya Bi Mdami, maboresho yaliyofanyika ni kuweka saini ya mmiliki wa kitambulisho, kuweka tarehe ya kuzaliwa na kuweka saini ya mtoaji wa kitambulisho na vyote baada ya kuongezea, hakukuathiri bei ya kitambulisho.

Kuwepo kwa saini ya mmiliki, saini ya mtoaji wa kitambulisho na tarehe ya kuzaliwa kumepandisha hadhi ya kitambulisho cha uraia cha Tanzania na kukifanya sasa kuaminika katika taasisi za kifedha, benki, kupigia kura, kuingilia nchi jirani kama Kenya na nyinginezo pamoja na kupata Pasiporti mpya ya kielekroniki na faida nyingine nyingi ambazo HAZIKUWEPO katika kitambulisho kilichokuwa kikitengenezwa awali kabla ya Mheshimiwa Rais Magufuli hajawatumbua watendaji wakuu wa wakati huo.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kwamba wabunge wa upinzani ambao hawana tena pesa kutokana na serikali kuziba mianya yote ya kujipatia fedha kijanjajanja bila kufanyakazi; sasa wamebuni mbinu ya kujikimu na bila aibu wanapokea maelekezo kutoka kwa vibaraka wa tuhumiwa wa ufisadi kwa ahadi ya kulipwa donge nono kwa kila elekezo ili kuwasafisha mafisadi hao kwa kuwafanya wananchi waamini kwamba maboresho yaliyofanyika yaliongeza gharama za kitambulisho cha taifa jambo ambalo sio la kweli.

Taarifa za kiuchunguzi pia zilibaini kuwa mafisadi hao wamejipanga kujisafisha kwa gharama yoyote kama maandalizi yao ya kuharibu uchaguzi mkuu mwaka 2020 kisha mafisadi hao kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu wa 2025.

Baadhi mafisadi na vibaraka wao ambao mawasiliano yao na wabunge wa upinzani pamoja na waandishi yamenaswa wakioongea; Ni wale vigogo walioondolewa NIDA kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na matumizi makubwa ya pesa ambayo hayakuendana na kazi iliyofanyika. Vigogo hao ambao majina yao yapo, wamewaahidi wabunge na waandishi hao kuwapa mgao wa pesa walizochuma katika dili zao za kifisadi kama malipo kwa kuichafua kazi nzuri inayofanywa na serikali ya awamu ya tano.
Mbunge mmoja wa upinzani mwishoni mwa wili iliyopita aliibuka na kudai kwamba gharama ya mradi wa vitambulisho vya uraia zimeongezeka baada ya kufanyika kwa maboresho jambo ambalo sio la kweli huku akitoa takwimu na madai ya kizushi kwa lengo la kuigombanisha Serikali na wananchi wake.

Uchunguzi pia umebaini, wabunge wa upinzani watajitokeza kwa nyakati tofauti tofauti kuongea uwongo kwa nia ya kupotosha umma. Hali kadhalika waandishi na vyombo vya habari vilivyopangwa kuuaminisha Umma na jamii ya kimataifa taarifa hizo za kuzusha, uchunguzi umebaini vimeamrishwa kuanza kutoa habari hizo mwezi huu mfurulizo hadi mwezi Julai 2020 ili kukamilisha awamu ya kwanza ya kuvuruga juhudi za serikali na kuwasafisha mafisadi.

Vigogo wengine walionaswa wakitoa ahadi za malipo kwa wabunge hao ni wale walioondolewa Uhamiaji kwa makosa ya kutaka kuiingiza serikali katika hasara ya zaidi ya dola za marekani milioni 226, Ambapo sasa kwa ujumla wake mradi wa mfumo wa uhamiaji mtandao (e-immigration) umefanyika kwa dola za Marekani milioni 57 tu!

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini, Dkt. Anna Makakala alipozungumza wakati wa uzinduzi wa ePassport amesema kwamba mradi e- immigration utafanyika kwa awamu nne;-
(i). e-Passport ilianza Septemba 2017 hadi Januari 2018 Imeshazinduliwa tarehe Mosi mwezi Februari, 2018 na Mhe. Rais Magufuli.

(ii). e-VISA Februari hadi Juni 2018.

(iii). e-Border utaanza Juni hadi Septemba 2018 na

(iv). e-Immigration kwenye Balozi zote nje ya Tanzania utaanza Septemba hadi Disemba 2018.

Miradi yote mnne itatekelezwa kwa thamani ya dola za kimarekani Milioni 57 tu pamoja na kodi kwa awamu zote na hakuna malipo mengine yatakayoongezeka.

Kufanikiwa kwa mradi huu e-Immigration kwa gharama ya dola za Marekani milioni 57 tu, limewaumbua vigogo walioondolewa Uhamiaji na sasa wanahaha kwa aibu wakidai kwamba gharama iliyotajwa ni kwa ajili ya mradi mradi mmoja tu wa e-Passport tu jambo ambolo sio la kweli.

Ni haki ya watanzania kufahamu juu ya matumizi ya pesa ya kodi zao kwani wanapopata ukweli kuhusu matumizi ya kodi wanayolipa inawapa hamasa kuendelea kufanya kazi kwa ari, kizalendo, kiadilifu na kulipa kodi zaidi kwa mafufaa ya jamii nzima.

Ni wajibu wa kila mtanzania kuwa macho na wale wote wanaotumiwa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali ya awamu ya tano kwa nia ya kuzuia juhudi za kupambana na ufusadi zinazofanywa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli na watendaji wake.
 
Kwanza mimi binafsi bado sijaelewa kitambulisho cha utaifa kilikuwa na kazi gani wakati kuna kitambulisho cha mpiga kura..maana kitambulisho cha taifa ,benki hakitakiwi,kwenye kampuni za mikopo hakitakiwi pia,yaani kila sehemu hakina kazi..sasa sijui kilikuwa na kazi gani??
Hata kusajili line na kurenew line za simu hakihitajiki
 
Ni aibu wabunge kutetea Mafisadi.
- Sasa mafisadi watumia Wabunge wa upinzani kujisafisha.

Kwa mujibu wa taarifa zinazopatika NIDA ni kwamba Gharama za mradi wa wote wa kuzalisha vitambulisho vya uraia zimebaki ni zile zile zilizokuwa katika mkataba wa awali, hata pamoja na kufanyiwa maboresho muhimu katika kitambulisho cha uraia.

Utengenezaji, usambazaji na ukandarasi wa miundo mbinu ya vitambulisho vya uraia unagharimu kiasi cha Dola za kimarekani $3.45 kwa kila kitambulisho mpaka kinapokabidhiwa kwa Mtanzania. Bei hii ya kitambulisho Ndiyo bei iliyo katika mkataba wa awali hata kabla ya maboresho ya msingi yaliyofanyika.

Maboresho yaliyofanyika ni kuweka saini ya Mmiliki wa kitambulisho, kuweka tarehe ya kuzaliwa na kuweka saini ya mtoaji wa kitambulisho.

Kuwepo kwa saini ya mmiliki, saini ya mtoaji wa kitambulisho na tarehe ya kuzaliwa kumepandisha hadhi ya kitambulisho cha uraia.

Ni haki ya watanzania kufahamu juu ya matumizi ya pesa ya kodi zao na ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata ukweli kuhusu matumizi ya kodi wanayolipa kwani inawapa hamasa kuendelea kulipa zaidi kwa manufaa ya jamii nzima.

Ni Wajibu wa kila mtanzania kumulika na kuwa macho na wale wote wanaotumiwa sasa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali ya awamu hii kwa maneno ya uzushi.




PAC Ni Wabunge wa Upinzani sio? Hii nchi imejaa WAPU.MBAVU wengi kiasi kwamba ningekuwa Mungu (bahati mbaya sio na anisamehe kama nakufuru) ningewafutilia mbali nchi ianze 0! Yote yaliyosemwa na Heche yalionekana na kamati ya PAC! Sasa Labda utuambie kuwa PAC Ni ya Wapinzani peke yao, hapo utarleweka, otherwise you must be a s.k.u.n.k!

CCM NI KIWANDA CHA MAFISADI, HAKITAKAA KIPATE MBADALA KATIKA HILO!
 
PAC Ni Wabunge wa Upinzani sio? Hii nchi imejaa WAPU.MBAVU wengi kiasi kwamba ningekuwa Mungu (bahati mbaya sio na anisamehe kama nakufuru) ningewafutilia mbali nchi ianze 0! Yote yaliyosemwa na Heche yalionekana na kamati ya PAC! Sasa Labda utuambie kuwa PAC Ni ya Wapinzani peke yao, hapo utarleweka, otherwise you must be a s.k.u.n.k!

CCM NI KIWANDA CHA MAFISADI, HAKITAKAA KIPATE MBADALA KATIKA HILO!
CCM ni mazwazwa haswa
 
Kwanza mimi binafsi bado sijaelewa kitambulisho cha utaifa kilikuwa na kazi gani wakati kuna kitambulisho cha mpiga kura..maana kitambulisho cha taifa ,benki hakitakiwi,kwenye kampuni za mikopo hakitakiwi pia,yaani kila sehemu hakina kazi..sasa sijui kilikuwa na kazi gani??
Hata kusajili line na kurenew line za simu hakihitajiki
Acha uongo mara kadhaa nimetumia kitambulisho cha taifa benk zote na taasisi nyingine za kifedha na zisizo za kifedha zinazonihudumia mpaka jana.Hakuna mahali kitambulisho changu kimetiliwa mashaka.
Twambie ni benk gani ilikataa kitambulisho chako! Nina wasi wasi huna kitambulisho cha uraia wa Tanzania.
 
WW utakuwa yule mbunge wa mtera UOTE="LAZIMA NISEME, post: 25627122, member: 282912"]Ni aibu wabunge kutetea Mafisadi.
- Sasa mafisadi watumia Wabunge wa upinzani kujisafisha.

Kwa mujibu wa taarifa zinazopatika NIDA ni kwamba Gharama za mradi wa wote wa kuzalisha vitambulisho vya uraia zimebaki ni zile zile zilizokuwa katika mkataba wa awali, hata pamoja na kufanyiwa maboresho muhimu katika kitambulisho cha uraia.

Utengenezaji, usambazaji na ukandarasi wa miundo mbinu ya vitambulisho vya uraia unagharimu kiasi cha Dola za kimarekani $3.45 kwa kila kitambulisho mpaka kinapokabidhiwa kwa Mtanzania. Bei hii ya kitambulisho Ndiyo bei iliyo katika mkataba wa awali hata kabla ya maboresho ya msingi yaliyofanyika.

Maboresho yaliyofanyika ni kuweka saini ya Mmiliki wa kitambulisho, kuweka tarehe ya kuzaliwa na kuweka saini ya mtoaji wa kitambulisho.

Kuwepo kwa saini ya mmiliki, saini ya mtoaji wa kitambulisho na tarehe ya kuzaliwa kumepandisha hadhi ya kitambulisho cha uraia.

Ni haki ya watanzania kufahamu juu ya matumizi ya pesa ya kodi zao na ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata ukweli kuhusu matumizi ya kodi wanayolipa kwani inawapa hamasa kuendelea kulipa zaidi kwa manufaa ya jamii nzima.

Ni Wajibu wa kila mtanzania kumulika na kuwa macho na wale wote wanaotumiwa sasa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali ya awamu hii kwa maneno ya uzushi.




[/QUOTE]
Ww
 
WW utakuwa yule mbunge wa mtera UOTE="LAZIMA NISEME, post: 25627122, member: 282912"]Ni aibu wabunge kutetea Mafisadi.
- Sasa mafisadi watumia Wabunge wa upinzani kujisafisha.

Kwa mujibu wa taarifa zinazopatika NIDA ni kwamba Gharama za mradi wa wote wa kuzalisha vitambulisho vya uraia zimebaki ni zile zile zilizokuwa katika mkataba wa awali, hata pamoja na kufanyiwa maboresho muhimu katika kitambulisho cha uraia.

Utengenezaji, usambazaji na ukandarasi wa miundo mbinu ya vitambulisho vya uraia unagharimu kiasi cha Dola za kimarekani $3.45 kwa kila kitambulisho mpaka kinapokabidhiwa kwa Mtanzania. Bei hii ya kitambulisho Ndiyo bei iliyo katika mkataba wa awali hata kabla ya maboresho ya msingi yaliyofanyika.

Maboresho yaliyofanyika ni kuweka saini ya Mmiliki wa kitambulisho, kuweka tarehe ya kuzaliwa na kuweka saini ya mtoaji wa kitambulisho.

Kuwepo kwa saini ya mmiliki, saini ya mtoaji wa kitambulisho na tarehe ya kuzaliwa kumepandisha hadhi ya kitambulisho cha uraia.

Ni haki ya watanzania kufahamu juu ya matumizi ya pesa ya kodi zao na ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata ukweli kuhusu matumizi ya kodi wanayolipa kwani inawapa hamasa kuendelea kulipa zaidi kwa manufaa ya jamii nzima.

Ni Wajibu wa kila mtanzania kumulika na kuwa macho na wale wote wanaotumiwa sasa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali ya awamu hii kwa maneno ya uzushi.



Ww[/QUOTE]
Neno mafisadi imekua ni kichaka cha kujificha pale mnapoambiwa ukweli.Ni kama vile wanadamu tunapomsingizia shetani hata kwenye mambo ya uwazi.Mke wa mtu/mume anapofumaniwa kwa jambo la hiar utasikia "utasikia shetani mke/mume wangu!!!!!Hakuna awamu yenye ufisadi kama hii.Muda utasema tu nyie pigeni ngonjera as if we're all fools
 
Acha uongo mara kadhaa nimetumia kitambulisho cha taifa benk zote na taasisi nyingine za kifedha na zisizo za kifedha zinazonihudumia mpaka jana.Hakuna mahali kitambulisho changu kimetiliwa mashaka.
Twambie ni benk gani ilikataa kitambulisho chako! Nina wasi wasi huna kitambulisho cha uraia wa Tanzania.
Watu wa jf ni kawaida yenu ubishi..kila kitu mnajua nyie
 
mkuu usiwaamini wanasiasa. hata huko serikalini unakokuamini bado ufisadi upo na mafisadi yanaendelea kutamba. hivi kununua watu toka upande mwingine sio ufisadi? namsikitia sana mwananchi wa kawaida anayemwamini mwanasiasa kwa 100% awe wa upinzani au chama tawala
 
WW utakuwa yule mbunge wa mtera UOTE="LAZIMA NISEME, post: 25627122, member: 282912"]Ni aibu wabunge kutetea Mafisadi.
- Sasa mafisadi watumia Wabunge wa upinzani kujisafisha.

Kwa mujibu wa taarifa zinazopatika NIDA ni kwamba Gharama za mradi wa wote wa kuzalisha vitambulisho vya uraia zimebaki ni zile zile zilizokuwa katika mkataba wa awali, hata pamoja na kufanyiwa maboresho muhimu katika kitambulisho cha uraia.

Utengenezaji, usambazaji na ukandarasi wa miundo mbinu ya vitambulisho vya uraia unagharimu kiasi cha Dola za kimarekani $3.45 kwa kila kitambulisho mpaka kinapokabidhiwa kwa Mtanzania. Bei hii ya kitambulisho Ndiyo bei iliyo katika mkataba wa awali hata kabla ya maboresho ya msingi yaliyofanyika.

Maboresho yaliyofanyika ni kuweka saini ya Mmiliki wa kitambulisho, kuweka tarehe ya kuzaliwa na kuweka saini ya mtoaji wa kitambulisho.

Kuwepo kwa saini ya mmiliki, saini ya mtoaji wa kitambulisho na tarehe ya kuzaliwa kumepandisha hadhi ya kitambulisho cha uraia.

Ni haki ya watanzania kufahamu juu ya matumizi ya pesa ya kodi zao na ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata ukweli kuhusu matumizi ya kodi wanayolipa kwani inawapa hamasa kuendelea kulipa zaidi kwa manufaa ya jamii nzima.

Ni Wajibu wa kila mtanzania kumulika na kuwa macho na wale wote wanaotumiwa sasa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali ya awamu hii kwa maneno ya uzushi.



Ww[/QUOTE]
mkuu mwenzetu umelipwa ngapi? wanasiasa hawaaminiki awe ikulu au lumumba.awe ufipa au buguruni. mkuu changanya na zako...
 
Back
Top Bottom