Elections 2010 Ni aibu kwa Wagombea Urais [NCCR,CUF,TLP] kushindwa na Peter Kuga Mziray

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,269
54,664
Jamani huyu Peter Mziray mimi namuona kama ni mgombea binafsi vile.

Sasa nimeshtuka kwamba kuna majimbo ambayo ameweza kuwashinda wagombea wa vyama established kama NCCR,CUF,na TLP.

I mean haistahili kabisa kwa mgombea anayejaribu kushika madaraka ya dola kushindwa ktk jimbo hata moja na mgombea wa chama cha kwenye briefcase kama Peter Mziray.
 
..jamani huyu Peter Mziray mimi namuona kama ni mgombea binafsi vile.

..sasa nimeshtuka kwamba kuna majimbo ambayo ameweza kuwashinda wagombea wa vyama established kama NCCR,CUF,na TLP.

..i mean haistahili kabisa kwa mgombea anayejaribu kushika madaraka ya dola kushindwa ktk jimbo hata moja na mgombea wa chama cha kwenye briefcase kama Peter Mziray.
KWA USHABIKI NA UNAZI NI KWELI, REALITY KUNA SEHEMU PIA AMEMSHINDA DOKTA, THEN JE YEYE HAKUWA AKIGOMBEA URAIS??? je kule ambako dokta hakupata kura hata moja???:smile-big: au nako Kuga amechakachuwa???:smile-big:
 
.... Inawezekana Peter Mziray akawa ni BOYA la CCM mumuone ni mpinzani kumbe anatumika kupunguza kura za wapinzani. Wakati huo huo CCM wanaendeleza uchakachuaji mwingine kiulaini
 
Mwanamageuko,

..actually so far sijaona mahali ambapo Dr.Slaa ameshindwa na Kuga Mziray.

..kwa kweli kama kuna eneo ambalo atakuwa ameshindwa basi itanipunguzia imani niliyokuwa nayo kwa Dr.Slaa.

..jamani we r talking about losing to Peter Mziray. c'mon now.
 
As of yesterday:

Presidential poll results at 10.30Pm

Candidate Party Votes %

P.Mziray APPT 50,675 1.4

J.Kikwete CCM 2,469,507 68.2

W.SLAA CHADEMA 736,366 20.3

I.LIPUMBA CUF 308,597 8.5

H.RUNGWE NCCR 10,120 0.3

M.MUHUNYWA TLP 6,994 0.2

F.DOVUTWA UPDP 4,321 0.1

SPOILT 74,138 2.0

TOTAL VOTES 3,660,718
 
Naomba kutoa nadharia zifuatazo katika hili
  • Kwa kuwa wapigakura wengi kwa sasa ni vijana, Kuga Mziray amekuwa kwa kiasi fulani kivutio kwao maana ana mwonekano wa ujana ukimlinganisha na mzee mwenye ndevu zake na wengine
  • Kwa kuwa picha ya Mziray ilikuwa ya mwanzo kabisa kwenye karatasi ya kura ilikuwa jaribu tosha kwa mtu mwenye haraka zake kuweka tick kwa mgombea huyu, Mziray alijua mantiki ya kicha kuonekana ya kwanza kwenye karatasi ya kura ndo maana alibadilisha jina la chama kutoka PPT-Maendeleo kuwa APPT-maendeleo ili kiwe cha kwanza kialphabet
  • Kuga Mziray alifanya mikutano mingi ya kampeni zaidi ya baadhi ya wagombea
  • Naye ni mgombea serious, sio underdog, vinginevyo tume isingemteua
 
As of yesterday:

Presidential poll results at 10.30Pm

Candidate Party Votes %
P.Mziray APPT 50,675 1.4
J.Kikwete CCM 2,469,507 68.2
W.SLAA CHADEMA 736,366 20.3
I.LIPUMBA CUF 308,597 8.5
H.RUNGWE NCCR 10,120 0.3
M.MUHUNYWA TLP 6,994 0.2
F.DOVUTWA UPDP 4,321 0.1
SPOILT 74,138 2.0
TOTAL VOTES 3,660,718

asante mkuu kwa data, afu hizo za dk ni baada ya kuchakachulia na sisiem
 
Bado Niponipo,

..sasa mpaka sasa hivi si aibu kubwa kwa chama kama NCCR,TLP,na UDP?

..lakini mimi sijaangalia matokeo ya ujumla.

..kuna matokeo ya majimbo yaliletwa hapa nikakuta kuna maeneo Mziray anashika nafasi ya tatu.

..hicho ndicho kilichonisukuma mimi kuweka bandiko hili.
 
Bado Niponipo,

..sasa mpaka sasa hivi si aibu kubwa kwa chama kama NCCR,TLP,na UDP?

..lakini mimi sijaangalia matokeo ya ujumla.

..kuna matokeo ya majimbo yaliletwa hapa nikakuta kuna maeneo Mziray anashika nafasi ya tatu.

..hicho ndicho kilichonisukuma mimi kuweka bandiko hili.

Mkuu, UDP haikuwa na mgombe urais. Aidha kuna jimbo liltangazwa jana, Mziray hakupata kura hata moja
 
Mwanamageuko,

..actually so far sijaona mahali ambapo Dr.Slaa ameshindwa na Kuga Mziray.

..kwa kweli kama kuna eneo ambalo atakuwa ameshindwa basi itanipunguzia imani niliyokuwa nayo kwa Dr.Slaa.

..jamani we r talking about losing to Peter Mziray. c'mon now.
Joka kuu, embu angalia mahala ambako hakuna vigango utaona kilichotokea:smile-big:
 
Bado Niponipo,

..sasa mpaka sasa hivi si aibu kubwa kwa chama kama NCCR,TLP,na UDP?

..lakini mimi sijaangalia matokeo ya ujumla.

..kuna matokeo ya majimbo yaliletwa hapa nikakuta kuna maeneo Mziray anashika nafasi ya tatu.

..hicho ndicho kilichonisukuma mimi kuweka bandiko hili.

Joka kuu!

Ndiyo demokrasia hiyo kaka, jamaa nimemsikiliza kwenye TV mara moja akiwa anafanyiwa mahojiano naweza eleza machache.
1. He is young and looks young
2. Very composed
3. Exposed, labda ni baada ya kukaa muda mrefu ughaibuni
4. Jamaa ana degree ya Uchumi Kilimo
5. Jamaa alikuwa na sera nzuri na vile vile alifanyiwa mahojiano na vyombo kadhaa, wengine sikuwahi kuwasikia
6. You can tell he's kinda person, who believe what he's preaching.

Jamaa atashika nafasi ya nne, hadi sasa ni number nne akiwa na 1.4% wengine, H.RUNGWE NCCR 0.3%, M.MUHUNYWA 0.2%, F.DOVUTWA UPDP 0.1%
 
Joka kuu!

Ndiyo demokrasia hiyo kaka, jamaa nimemsikiliza kwenye TV mara moja akiwa anafanyiwa mahojiano naweza eleza machache.
1. He is young and looks young
2. Very composed
3. Exposed, labda ni baada ya kukaa muda mrefu ughaibuni
4. Jamaa ana degree ya Uchumi Kilimo
5. Jamaa alikuwa na sera nzuri na vile vile alifanyiwa mahojiano na vyombo kadhaa, wengine sikuwahi kuwasikia
6. You can tell he's kinda person, who believe what he's preaching.

Jamaa atashika nafasi ya nne, hadi sasa ni number nne akiwa na 1.4% wengine, H.RUNGWE NCCR 0.3%, M.MUHUNYWA 0.2%, F.DOVUTWA UPDP 0.1%

Dovutwa hiyo zero yake keshampa mkuu :smile:
 
Mwanamageuko said:
Joka kuu, embu angalia mahala ambako hakuna vigango utaona kilichotokea

Mwanamageuko,

..sidhani kama vigango na ukatoliki ilikuwa a significant factor ktk uchaguzi wa mwaka huu.

..Mbulu ni jimbo ambalo ni ngome ya Kanisa Katoliki. jimbo hilo ndiyo kati ya maeneo ya kwanza kuingia ukatoliki ktk Tanganyika.

..katika uchaguzi wa wabunge wa jimbo la Mbulu, mgombea Muislamu amemshinda mgombea Mkatoliki.

..sidhani kama wa-Tanzania waliangalia dini ya mgombea ktk uchaguzi huu.
 
Mwanamageuko,

..sidhani kama vigango na ukatoliki ilikuwa a significant factor ktk uchaguzi wa mwaka huu.

..Mbulu ni jimbo ambalo ni ngome ya Kanisa Katoliki. jimbo hilo ndiyo kati ya maeneo ya kwanza kuingia ukatoliki ktk Tanganyika.

..katika uchaguzi wa wabunge wa jimbo la Mbulu, mgombea Muislamu amemshinda mgombea Mkatoliki.

..sidhani kama wa-Tanzania waliangalia dini ya mgombea ktk uchaguzi huu.
ni kweli kabisa havikuhusika...
rejea mgombea wa Karatu (aliyeachiwa Jimbo!!):smile-big: je hapakuwapo mtu mwingine pale anaefaa, namaanisha raia wa kawaida apo:smile-big: (nimetaja kule nyuma.. kuna mzozo baina ya dokta na jimbo kule je haiwezi kuwa sababu???)
 
Mtu kama LIPUMBA kushindwa na Mziray wala nisingeona ajabu. Huyu jamaa kila uchaguzi yumo tu. Sijui nani huwa anamshauri agombee tena.

Nina uhakika 100% hata mwenyewe anajua HATOWEZA kupata uRais wa nchi hii. Anagombea tu kutimiza wajibu kwa kuwa huwa kuna imani kwamba CUF wanaweza kushinda Zanzibar.

Sasa nadhani 2015 hawezi kuingiza mguu tena. Maalim Seifpia. Kitendo cha kukubali ''kuibiwa'' ushindi ili japo aambulie uVice President/uWaziri Kiongozi was enough evidence
 
Mwanamageuko said:
ni kweli kabisa havikuhusika...
rejea mgombea wa Karatu (aliyeachiwa Jimbo!!):smile-big: je hapakuwapo mtu mwingine pale anaefaa, namaanisha raia wa kawaida apo:smile-big: (nimetaja kule nyuma.. kuna mzozo baina ya dokta na jimbo kule je haiwezi kuwa sababu???)

Mwanamageuko,

..aliyegombea kwa tiketi ya Chadema Karatu ni Mchungaji wa Kanisa la Lutheran.

..sasa itakuwa ni speculation tu kudai kwamba kuna mkono wa kanisa katoliki na vigango.

..of course kulikuwa na wagombea wengine, lakini hawakupita ktk kura za maoni za Chadema.

..pia hakuna kifungu chochote kile cha Katiba kinachozuia viongozi wa dini kama Mashekhe,Mapadri,Wachungaji etc etc kugombea nafasi za uongozi.

..tumeshawahi kuwa na Mashekhe, Ma-Alhaji, Mapadre, Wachungaji, ktk nafasi za ubunge na uongozi kwa nyakati tofauti na sikuona kama imani zao ziliathiri utendaji wao wa kazi. actually Shekhe Prof.Mikidadi alikuwa ni kati wa wabunge walionivutia sana kutokana na michango yao bungeni. mwingine alikuwa ni Yohana Misigalo mbunge wa Tabora mjini.
 
As of yesterday:

Presidential poll results at 10.30Pm

Candidate Party Votes %

P.Mziray APPT 50,675 1.4

J.Kikwete CCM 2,469,507 68.2

W.SLAA CHADEMA 736,366 20.3

I.LIPUMBA CUF 308,597 8.5

H.RUNGWE NCCR 10,120 0.3

M.MUHUNYWA TLP 6,994 0.2

F.DOVUTWA UPDP 4,321 0.1

SPOILT 74,138 2.0

TOTAL VOTES 3,660,718

Hii inathibitisha kuwa katika tafiti zangu za mwisho sikukosea sana, kwani zilinipa matokeo yafuatayo:


Mh KIKWETE....................62% (error...3 + -)


Mh SLAA.................18% (Error......4 + -)


Mh Lipumba .........15% (Error .....4 + -)




Na hivyo ndivyo ndivyo ilivyo angalau kwa nafasi ya kwanza mpaka ya tatu. Kuhusu asilimia nazo sio mbaya sana kumekuwa na tofauti ya + - 5 mpaka 8. Hata hivyo mchezo bado haujaisha hivyo bado ninamatumaini ya + - 4 % kwa kila mgombea.

Kiknachohitajiwa sasa hivi ni kwa Mh SLAA kuyakubali matokeo na kusaini tu. Hakuna cha zaidi wala cha upungufu.

CHONDE CHONDE MLIO KARBU NAYE MSHAURINI AFANYE HIVYO. SI MMEONA MFANO WA SHEIKH SHARIF, HUO NDIO UUNGWANA.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom