Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Ni aibu kubwa kwa Mheshimiwa Rais Kikwete kusema kuwa hawajui wamiliki wa Dowans
Maelezo yaliyotolewa na Mh Kikwete kujibu tuhuma zinazoelekezwa kwake binafsi na ama wajumbe wa kamati nyeti za chama chake kuwa yeye hawajui na wala hajawahi kukutana na wamiliki wa Dowans ni kujivunjia heshima yeye na wasaidizi wake.
Kama kweli Mh Kikwete angetaka kuwafahamu wamiliki halisi isingechukua hata wiki mbili {ana miundombinu na rasilimali za kuweza kufanya hivyo}, manung'uniko juu ya Dowans/Richmond yana zaidi ya miaka minne sasa na imemchukua zaidi ya wiki nne kulizungumzia suala hili baada ya mahakama ya ICC kuiamuru serikali kulipa. Katika hali ya kawaida tungetarajia basi Rais awe muungwana atusaidie wananchi wake kupata ukweli baada ya watu kumtuhumu yeye binafsi na kama kweli yey hapendi kuona Dowans ikilipwa kama alivyosema (kitu ambacho kinatia shaka kama kweli huu ndio msimamo wake).
Dowans/Richmond ni bomu linaloweza kusambaratisha mshikamana na utengamano wa nchi hii... kama tulivyoona wanafunzi wakidai kuongezewa posho yao na wakihusisha madai yao na serikali kuwalipa Dowans.. TUCTA wana madai ambayo hayajalipwa na serikali kwa kisingizio kuwa haina hela, wanaweza sasa kukaza uzi kwani wanajua serikali ina pesa: walimu, madaktari, n.k. nao wamekuwa wakilalamika kuwa mishahara yao ni duni... itakuwa nao wakisisitiza kuwa waongezewe mishahara kwa kuwa mwajiri wao ambaye mara zote amekuwa akilalamika kuwa hana pesa kumbe anazo za kuchezea?
Inawezakana tu kwa Mh Rais kusema hawajui wamiliki wa Dowans kama hasemi ukweli ama hayuko makini, kwa mtu yeyeto aliye makini na mwenye mamlaka aliyonayo Kikwete na kwa kuwa alikuwa amaeamua kuvunja ukimya na kuamua kulisemea hili alitakiwa atoe maelezo yanayojitoshereza, siyo porojo alizotoa pale Dodoma siku ya maadhimisho ya miaka 34 ya CCM.
Ni aibu kwa watu wenye uelewa kuridhika na kusifia maelezo yale ya Rais, ni aibu kwa wote waliokuwa wakimsikiliza na kumshangilia kwa maelezo yale ya rejareja...
Kama ni kweli Rais hatuambii ukweli basi ni aibu nyingine kubwa!
Maelezo yaliyotolewa na Mh Kikwete kujibu tuhuma zinazoelekezwa kwake binafsi na ama wajumbe wa kamati nyeti za chama chake kuwa yeye hawajui na wala hajawahi kukutana na wamiliki wa Dowans ni kujivunjia heshima yeye na wasaidizi wake.
Kama kweli Mh Kikwete angetaka kuwafahamu wamiliki halisi isingechukua hata wiki mbili {ana miundombinu na rasilimali za kuweza kufanya hivyo}, manung'uniko juu ya Dowans/Richmond yana zaidi ya miaka minne sasa na imemchukua zaidi ya wiki nne kulizungumzia suala hili baada ya mahakama ya ICC kuiamuru serikali kulipa. Katika hali ya kawaida tungetarajia basi Rais awe muungwana atusaidie wananchi wake kupata ukweli baada ya watu kumtuhumu yeye binafsi na kama kweli yey hapendi kuona Dowans ikilipwa kama alivyosema (kitu ambacho kinatia shaka kama kweli huu ndio msimamo wake).
Dowans/Richmond ni bomu linaloweza kusambaratisha mshikamana na utengamano wa nchi hii... kama tulivyoona wanafunzi wakidai kuongezewa posho yao na wakihusisha madai yao na serikali kuwalipa Dowans.. TUCTA wana madai ambayo hayajalipwa na serikali kwa kisingizio kuwa haina hela, wanaweza sasa kukaza uzi kwani wanajua serikali ina pesa: walimu, madaktari, n.k. nao wamekuwa wakilalamika kuwa mishahara yao ni duni... itakuwa nao wakisisitiza kuwa waongezewe mishahara kwa kuwa mwajiri wao ambaye mara zote amekuwa akilalamika kuwa hana pesa kumbe anazo za kuchezea?
Inawezakana tu kwa Mh Rais kusema hawajui wamiliki wa Dowans kama hasemi ukweli ama hayuko makini, kwa mtu yeyeto aliye makini na mwenye mamlaka aliyonayo Kikwete na kwa kuwa alikuwa amaeamua kuvunja ukimya na kuamua kulisemea hili alitakiwa atoe maelezo yanayojitoshereza, siyo porojo alizotoa pale Dodoma siku ya maadhimisho ya miaka 34 ya CCM.
Ni aibu kwa watu wenye uelewa kuridhika na kusifia maelezo yale ya Rais, ni aibu kwa wote waliokuwa wakimsikiliza na kumshangilia kwa maelezo yale ya rejareja...
Kama ni kweli Rais hatuambii ukweli basi ni aibu nyingine kubwa!