Ni aibu kusema Mwanza ni jiji la pili, limechoka, linachekesha, halmashauri hazina hela

Hali siyo nzuri Mwanza. (1) machinga wamejazana mbele ya maduka hasa Barabara ya Nyerere na hakuna cha kuwafanya. Katika nchi iliyo na maendeleo lazima kuwe na mpangilio wa kila kitu ndiyo maana kuna Idara katika Halmashauri zetu inayoitwa Idara ya Mipango Miji. Machinga wanatakiwa wapewe sehemu yao maalum lakini hawaguswi na viongozi wa Jiji ukiwaeleza kuhusu machinga hawana la kufanya.

(2) Soko Kuu lilivunjwa kwa nia nzuri kabisa ya kujenga soko la kisasa lakini sasa yapata kama miezi mitano hakuna kinachoendelea. Labda kuna sababu ya maana lakini hata hivyo basi wananchi tungeelezwa juu ya ucheleweshaji huo.

(3) Serikali ione uwezekano wa kuwapa Halmashauri fedha za kutekeleza shida ndogo ndogo zinazojitokeza ili zirekebishwe mara moja.

(4) Soko ambalo wafanyabiashara wamehamia kutoka soko kuu linasikitisha. Kwa kweli ni pachafu na hasa Jumapili wafanyabiashara wanapanga bidhaa zao mpaka barabarani. Hapa Mwanza kuna tatizo. Mwanza kunihitajika Idara ya Mipango Miji ambayo haingiliwi vinginevyo kila mtu atakuwa ndiye Afisa Mipango Miji.
Chinga wanapewa viburi na waomba kura wao
Hapa Tanzania na Afrika viongozi hufanya vitu ili wasinyimmwe kura.
Nakuunga mkono. mji wote umejaa chinga
 
Siyo Mwanza, siyo Dar, Dom, Ar na kila mji mkubwa, ukitaka usafi na ustaarabu kwenye miji basi ondoa machinga. Ila ukitaka Vita na Serikali hasa kipindi hiki cha uchaguzi waambie kuhusu kuwafukuza machinga.
 
Mwanza pana hali sio nzuri...Hali mbaya ssna watu wanajaa milimani kule mvua zikija vinyesi vyoote ziwani..Kuna mitaa michafu squatter kali sana ila ndio hivyo utafanya nn??
 
NAWATAFUNA,
aiseee wacha bwana,hujajibu hata suala la taa barabarani na ni muda gani zipo gizani,vipi kuhusu halmashauri kufulia,nimeshangaa jana hata lile billboard kubwa pale karibu na passion hotel limepata tangazo la sayona...hahahahaha
eti 2 years,mi naongeza na mingine mitatu hakuna kitakachofanyika,tunza hii comment.


Majiji mazuri ya kuishi ndani ya Tanzania bara

1 Mwanza
2 Arusha
3 Dar/Mbeya
 
mara nyingi nikitoka dar kwenda kwetu tarime nilikuwa napita mwanza usiku, mwaka fulani gari lilisumbua nikapita mwanza saa 6 mchana nikaiona mwanza kwamara ya kwanza kwenye mwanga,.,aisee ni aibu tupu, watu wamejenga milimani hovyo, mimaji michafu sijui ya mavi inamiminika kutoka angani, kifupi mwanza ni jalalani nisiongee sana
 
mara nyingi nikitoka dar kwenda kwetu tarime nilikuwa napita mwanza usiku, mwaka fulani gari lilisumbua nikapita mwanza saa 6 mchana nikaiona mwanza kwamara ya kwanza kwenye mwanga,.,aisee ni aibu tupu, watu wamejenga milimani hovyo, mimaji michafu sijui ya mavi inamiminika kutoka angani, kifupi mwanza ni jalalani nisiongee sana


Wewe utakuwa mtu wa kaskazini ama dar,,,ndio kazi yenu kukashifu lake zone. Niseme tu, Tanzania nzima kuchafu,,,atleast Mwanza Arusha na Moshi.
 
mara nyingi nikitoka dar kwenda kwetu tarime nilikuwa napita mwanza usiku, mwaka fulani gari lilisumbua nikapita mwanza saa 6 mchana nikaiona mwanza kwamara ya kwanza kwenye mwanga,.,aisee ni aibu tupu, watu wamejenga milimani hovyo, mimaji michafu sijui ya mavi inamiminika kutoka angani, kifupi mwanza ni jalalani nisiongee sana
Mwaka gani huo ulipita jombaa ?
Alafu kila mkoa una mitaa ya skwata,hakuna mkoa wa kishua tupu hakunaga,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mti wenye matunda daima hupigwa mawe
Kama anakuja mgeni mwanza unamuambia eti mwanza ndilo jiji la pili Tanzania atakushangaa sana,last time nilikuwepo huko 6 years ago kulikuwa na ahueni,nipo huku sasa kwa miezi kadhaa tangu mwaka jana

Ndugu zangu ambao hamjaja mwanza muda mrefu hali ya huku ni kichekesho,ngoja niseme machache tu:

-Ukiingia mwanza ile stend ya zamani imevunjwa kwa mbwembwe ikasogezwa kwa mbele yako tu kichekesho sasas,ile stendi ya zamani hakuna kinachoendelea hata tofali moja halijawekwa ingawa ni takribani miezi minne,wanadai kuna kesi utajiuliza haraka ya kuvunja ilikuwa ni nini?hapo walipohamia sasa nakuhakikishia hata stendi ya Nanjilinji ni kali kuliko huo upuuzi hapo kwanza imekuwa ni maficho ya vibaka,ni pachafu kama li mwanza lilivyo sasa hivi

_Ukifika mjini kati sasa utacheka,soko kuu lilifungwa wale wauzaji wamesambaa pale mjini hakufai narudia tena HAKUFAI,na soko lenyewe haijulikani ni kinaendelea ni kama vile hela hakuna sijui?

-Barabara ni chafu hazisafishwi ipasavyo hapo nazungumzia za lami,taa za barabarani zile za security zipo lakini haziwashwi,uende nyasaka,igoma,nyegezi umeme ukikatika usiku inasikitisha sana ni giza tororo

-Barabara za mitaani kama kwa mbunge mabula anayejifanya mzalendo ni kituko kama siyo wale vijana wanaotupiaga vi gunia vya mchanga kuziba mashimo na baadaye kuomba hela basi hata bwana mabula ile barabara ya majengo kufika kwake angeshindwa,nimeambiwa halmashauri hazina hata hela ndogondogo maana zote zinapelekwa hazina kwa matumizi ya maana kama vile kununua mandege kwa cash

MWANZA IMEDODAQUOTE]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unapita tu.... Unajua asilimia 5% tu
mara nyingi nikitoka dar kwenda kwetu tarime nilikuwa napita mwanza usiku, mwaka fulani gari lilisumbua nikapita mwanza saa 6 mchana nikaiona mwanza kwamara ya kwanza kwenye mwanga,.,aisee ni aibu tupu, watu wamejenga milimani hovyo, mimaji michafu sijui ya mavi inamiminika kutoka angani, kifupi mwanza ni jalalani nisiongee sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mwanza inajengwa na itazidi kujengwa,
Soko jipya linajengwa na routes za daladala zimebadilishwa ili kupisha ujenzi wa soko,karibu na soko daladala hazitopita tena,

Stendi mpya ya kisasa inajengwa,
Vurugu zoote za jamu ya machinga zitakoma soko likikamilika,machinga woote watawekwa kwa mpangilio mzuri ndani ya soko jipya litakapo isha,

utanuzi wa barabara ya shinyanga road kuwa 4ways utaanza mapema mwaka huu,

After 2 years Mwanza itakua levo nyingine kwa hapa bongo,
kuna miradi mikubwa ya kuboresha jiji la mwanza mingi na ya kuvutia,


Sent using Jamii Forums mobile app
Sorry unaweza kushare na mimi hiyo miradi mipya Mwanza...
 
jiji la mwanza linatia huruma,
barabara za mtaa hovyoo sana,
maeneo kama mahina hamna umeme hlf ni ktkt ya jiji,
 
Nikianza kuifananinisha makoroboi na kariakoo sioni nailinganishaje. Makoroboi haijapangwa kama kariakoo. Kariakoo iko juu zaidi. Najikita kuzungumzia mgeni anapokuja kutafuta kitu au kununua kitu. Mfano ukienda kariakoo unaweza kuta maduka hata ishirini yanejipanga mstari mmoja yanauza simu, au matairi ya magari au vipuri, au electronics au vyombo vya majumbani au furniture. Lakini makoroboi haieleweki hapa mmoja anauza nguo hapa simu, hapa mwingine viatu hapa mtu anauza vyombo yaan mwanza haiwezi ifikia dar
 
Kwanza inashangaza hoja nyepesi zinazozungumzwa kuelezea ubaya wa jiji na kuacha hoja kuu ya makazi holela.Hata vyote hivyo unavyosema vikifanyiwa kazi lakini ujenzi holela,kykosekana maeneo yalitotengwa kwa ajili ya bustani na fukwe za umma na Kudhibiti taka ,jiji litabakia kuwa uswazi na uswahili kila kona.
Cha kushangaza sijasikia chama chochote kikiongelea kutiwa mkazo kwenye matumizi bora ya ardhi ikiwamo kufuta makazi ya uswazi na ujenzi kufuata mipango miji.Seems watanzania kuishi hovyo hovyo na mauchafu Kama nzi na wanyama ndio ustaarabu wetu labda.
Mapesa yanayowekwa kujenga hayo mastendi ushenzi zinatosha Sana kuipanga hiyo miji ,mnaisafiri nchi za jirani hamuoni aibu? Bora kuwa na specific uswazi kuliko uswazi kila sehemu
 
Back
Top Bottom