Ni aibu kuona Wabunge wa CCM na wengineo wakibisha bila kujua maana ya uraia pacha au mtu anakuwaje raia pacha!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kwa mara nyingine tena nimeshuhudia jinsi Wabunge wa CCM wanavyobishia mambo huku wakiwa mbumbumbu katika suala linalojadiliwa. Yaani inafedhehesha sana kuona jinsi mbunge anasimama kubishia kitu ambacho hana hata uelewa nacho!

Mbunge wa Mbeya, Sugu, alipendekeza kwamba serikali itafakari tena juu ya kuruhusu suala la uraia pacha.

Wakasimama wabunge wa CCM, na bila aibu wanabisha kwamba serikali isiruhusu uraia pacha kwa kuwa hao wanaotaka uraia pacha waliukana uraia wa Tanzania!

Halafu wengine wanasema diaspora ni raia kama Sugu alivyo raia kule Mbeya!

Hivi mbunge anaweza kuwa poyoyo kiasi hicho katika kuelewa maana ya uraia pacha? Unawezaje kusema diaspora hawahitaji uraia pacha kwa kuwa tayari ni raia kama una akili sawasawa? Nikakumbuka hata humu Jamii Forum kulitokea ubishi sana juu ya kuruhusu uraia pacha, na nilishuhudia watu wakibisha bila hata kuelwa utaratibu wa kuwa raia pacha.

Kwa faida ya hawa wabunge vihiyo na wengineo, ningependa kuainisha mambo ya msingi matano katika suala la uraia pacha. Ni wazi kwamba hawa waheshimiwa wabunge na watu wengi humu JF hawayaelewi na wamekuwa wakibisha kuhusu uraia pacha bila kujua uraia pacha unatolewa katika misingi gani.
  1. Uraia pacha si kwa ajili ya raia wa Tanzania ambaye aliukana uraia wa Tanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania kama raia wa nchi nyingine. Ikiwa Mtanzania alishaukana uraia wa Tanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania, ili aweze kuwa raia pacha inabidi kwanza arudi Tanzania, na labda aishi kwa kibali (residence/permanent permit) nchini kwa muda usiopungua miaka mitano, na ndio ataomba tena kuwa raia wa Tanzania na kumfanya awe raia pacha - ikiwa nchi ambayo ni raia wake kwa sasa inamruhusu kuwa raia pacha, na Tanzania itakubali kumpa tena uraia. Kwa hiyo ni vigumu kwa mtu aliyeukana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine kuwa raia pacha
  2. Uraia pacha unakuja kwa raia wa Tanzania ambaye anaomba uraia wa nchi nyingine kwa kuwa ameishi katika nchi hiyo kwa muda mrefu kwa residence/permanent permit, bila kuwa ameukana uraia wake wa Tanzania. Kwa hiyo uraia pacha kwa Mtazania hautolewi na serikali ya Tanzania kwa kuwa huyo mtu tayari ni Mtanzania, bali anakuwa nao mtu aliekubaliwa kuwa raia wa nchi anayokaa baada ya hiyo nchi kumruhusu awe raia wa nchi hiyo huku akiendelea kuwa raia wa Tanzania
  3. Uraia pacha hauji kwa raia wa nchi nyingine akiwa anaishi nje ya Tanzania. Mtu asiye raia wa Tanzania anakuwa raia pacha pale ambapo serikali ya Tanzania inamruhusu kuwa raia wa Tanzania kwa kuwa amekuwa akiishi Tanzania kwa residence/perment permit kwa muda mrefu kutokana na sababu kama kuoa/kuolewa, kuwa mwekezaji nk., na anaendelea kuwa raia wa nchi yake ya kuzaliwa
  4. Sio rahisi kuwa raia pacha, hata pale Tanzania ikiruhusu, kwa kuwa ili uwe raia pacha lazima uwe umeishi kihalali katika nchi nyingine kwa muda uisiopungua miaka mitano na nchi hiyo ikubali ombia lako la kuwa raia wake.Kwa hiyo hata Tanzania ikiruhusi uraia pacha ni watu wachache sana watakuwa raia pacha. Huwezi kuwa raia pacha kama ni raia wa Tanzania hujawahi kuishi nchi nyingine zaidi ya Tanzania au kama ni raia wa nchi nyingine hujawahi kuishi Tanzania kwa muda mrefu
  5. Hakuna kibali kinachotolewa na Tanzania au serikali nyingine kinaitwa "Raia Pacha". Uraia pacha ni hali inayokutokea kwa kuwa serikali mbili zinakutambua kuwa raia halali wa nchi hizo.
Kwa kifupi, si rahisi kwa Mtanzania aliyeukana Utanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania kuwa raia pacha, kwa kuwa ili aupate itambidi arudi tena Tanzania na kuishi kwa kibali kwa muda usiopungua miaka mitano ndio aombe uraia wa Tanzania upya na kuwa raia pacha. Sio jambo automatic kwamba tukiruhusu uraia pacha wale wote walioukana uraia wa Tanzania huko nyuma watarudishiwa uraia wa Tanzania na kuwafanya wawe raia pacha.

Pili uraia pacha hautolewi kwa mtu asiye Mtanzania ambaye hajawahi kuishi Tanzania, na akiwa nje ya Tanzania. Raia wa nje kuwa raia pacha na Tanzania lazima awe ameishi kihalali Tanzania kwa muda usiopungua miaka mitano, kama nchi nyingi zinavyofanya.

Tatu, uraia pacha kwa Mtanzania hautolewi na serikali ya Tanzania bali na serikali ambako raia wa Tanzania anaishi kwa muda mrefu akiwa bado ni mTanzania na hajaukana Utanzania. Kinachotokea kwa huyo siyo Tanzania kumpa uraia pacha bali ni Tanzania kuruhusu yeye kuomba uraia wa nchi anakoishi sasa bila kuwa ameukana uraia wa Tanzania.

Hivyo natoa wito kwa Wabunge na wengineo kuacha kubisha juu ya uraia pacha kwa mihemuko bila kujua undani wa uraia pacha, au kwa kisingizio cha uzalendo wakati kilichowakaa akilini wengi wenu ni wivu tu usio na maana. Hili ndilo watu wanaita joka la mndimu - unakuwa joka kwenye mdimu unawazuia watu kuchuma ndimu wakati wewe huli ndimu na hutegemei kula ndimu katika maisha yako, na mbaya zaidi unawaambia watu kula ndimu ni kitu kibaya na hujawahi kuonja ndimu na wala hutegemei kula ndimu. Swali limeulizwa, ni nchi ngapi zilizoruhusu uraia pacha zimeathirka na kuruhusu uraia pacha na hata zikaamua kusimamisha uraia pacha?

Ni kiongozi asiyetumia akili peke yake ndiye atafikiri kwamba Mtanzania mwenye uraia pacha ni hatari zaidi kwa usalama wa Tanzania kuliko mtu aliyekua raia wa Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya, India, Pakistan, Oman, Somalia, DRC, Russia, Marekani nk ambaye amepewa uraia wa Tanzania kwa kuwa amesema ameukana uraia wa nchi yake.

Acheni kupotosha watu kwa hizi cheap propaganda dhidi ya uraia pacha.
 
1125250

Huyu Mbunge anahitaji kuelimishwa, hajui anachokiongea. Anapaswa kuelewa mambo kabla ya kuyaongelea. Mtu aliyeukana uraia wa Tanzania na kuwa raia wa nchi nyingine hawezi kuwa raia pacha wa Tanzania kirahisi.

Huyu jamaa si ana PhD huyu sijui sheria? Really?
 
1125259

Kangi Lugola anaweka drama za kisiasa hapa. Kwanza aniambie ni vipi raia wa Tanzania ambaye ameruhusiwa kuwa Raia wa Afrika kusini anakuwa hatari kwa usalama wa Tanzania huko Afrika Kusini, tofauti na alivyokuwa akiishi Afrika Kusini akiwa permanent resident bila kuwa raia.

Au Kangi atuambie ni vipi raia wa Afrika Kusini aliyeishi Tanzania zaidi ya miaka mitano na kuruhusiwa kuwa raia wa Tanzania ghafla anakuwa issue ya kiusalama kwa Tanzania, kwa kuwa sasa anaishi Tanzania kama raia.

Jamani, acheni propaganda sizizo na msingi.
 
Kwa mara nyingine tena nimeshuhudia jinsi Wabunge wa CCM wanavyobishia mambo huku wakiwa mbumbumbu katika suala linalojadiliwa. Yaani inafedhehesha sana kuona jinsi mbunge anasimama kubishia kitu ambacho hana hata uelewa nacho!

Mbunge wa Mbeya, Sugu, alipendekeza kwamba serikali itafakari tena juu ya kuruhusu suala la uraia pacha.

Wakasimama wabunge wa CCM, na bila aibu wanabisha kwamba serikali isiruhusu uraia pacha kwa kuwa hao wanaotaka uraia pacha waliukana uraia wa Tanzania!

Halafu wengine wanasema diaspora ni raia kama Sugu alivyo raia kule Mbeya!

Hivi mbunge anaweza kuwa poyoyo kiasi hicho katika kuelewa maana ya uraia pacha? Unawezaje kusema diaspora hawahitaji uraia pacha kwa kuwa tayari ni raia kama una akili sawasawa? Nikakumbuka hata humu Jamii Forum kulitokea ubishi sana juu ya kuruhusu uraia pacha, na nilishuhudia watu wakibisha bila hata kuelwa utaratibu wa kuwa raia pacha.

Kwa faida ya hawa wabunge vihiyo na wengineo, ningependa kuainisha mambo ya msingi matano katika suala la uraia pacha. Ni wazi kwamba hawa waheshimiwa wabunge na watu wengi humu JF hawayaelewi na wamekuwa wakibisha kuhusu uraia pacha bila kujua uraia pacha unatolewa katika misingi gani.
  1. Uraia pacha si kwa ajili ya raia wa Tanzania ambaye aliukana uraia wa Tanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania kama raia wa nchi nyingine. Ikiwa Mtanzania alishaukana uraia wa Tanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania, ili aombe kuwa raia pacha inabidi kwanza arudi Tanzania, na labda aishi kwa kibali (residence/permanent permit) nchini kwa muda usiozidi miaka mitano, na ndio ataomba kuwa raia pacha - ikiwa nchi ambayo ni raia wake kwa sasa inamruhusu kuwa raia pacha. Kwa hiyo ni vigumu kwa mtu aliyeukana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine kuwa raia pacha
  2. Uraia pacha unakuja kwa raia wa Tanzania ambaye anaomba uraia wa nchi nyingine kwa kuwa ameishi katika nchi hiyo kwa muda mrefu kwa residence/permanent permit, bila kuwa ameukana uraia wake wa Tanzania. Kwa hiyo uraia pacha kwa Mtazania hautolewi na serikali ya Tanzania kwa kuwa huyo mtu tayari ni Mtanzania, bali anakuwa nao mtu aliekubaliwa kuwa raia wa nchi anayokaa baada ya hiyo nchi kumruhusu awe raia wa nchi hiyo huku akiendelea kuwa raia wa Tanzania
  3. Uraia pacha hauji kwa raia wa nchi nyingine akiwa anaishi nje ya Tanzania. Mtu asiye raia wa Tanzania anakuwa raia pacha pale ambapo serikali ya Tanzania inamruhusu kuwa raia wa Tanzania kwa kuwa amekuwa akiishi Tanzania kwa residence/perment permit kwa muda mrefu kutokana na sababu kama kuoa/kuolewa, kuwa mwekezaji nk., na anaendelea kuwa raia wa nchi yake ya kuzaliwa
  4. Sio rahisi kuwa raia pacha, hata pale Tanzania ikiruhusu, kwa kuwa ili uwe raia pacha lazima uwe umeishi kihalali katika nchi nyingine kwa miaka isiyopungua miaka mitano na nchi hiyo ikubali ombia lako la kuwa raia wake.Kwa hiyo hata Tanzania ikiruhusi uraia pacha ni watu wachache sana watakuwa raia pacha. Huwezi kuwa raia pacha kama ni raia wa Tanzania hujawahi kuishi nchi nyingine zaidi ya Tanzania au kama ni raia wa nchi nyingine hujawahi kuishi Tanzania kwa muda mrefu
  5. Hakuna kibali kinachotolewa na Tanzania au serikali nyingine kinaitwa "Raia Pacha". Uraia pacha ni hali inayokutokea kwa kuwa serikali mbili zinakutambua kuwa raia halali wa nchi hizo.
Kwa kifupi, si rahisi kwa Mtanzania aliyeukana Utanzania na sasa anaishi nje ya Tanzania kuwa raia pacha, kwa kuwa ili aupate itambidi arudi tena Tanzania na kuishi kwa kibali kwa muda usiopungua miaka mitano ndio aombe uraia wa Tanzania upya na kuwa raia pacha.

Pili uraia pacha hautolewi kwa mtu asiye Mtanzania ambaye hajawahi kuishi Tanzania, na akiwa nje ya Tanzania. Raia wa nje kuwa raia pacha na Tanzania lazima awe ameishi kihalali Tanzania kwa muda usiopungua miaka mitano, kama nchi nyingi zinavyofanya.

Tatu, uraia pacha kwa Mtanzania hautolewi na serikali ya Tanzania bali na serikali ambako raia wa Tanzania anaishi kwa muda mrefu akiwa bado ni mTanzania na hajaukana Utanzania. Kinachotokea kwa huyi siyo Tanzania kumpa uraia pacha bali ni Tanzania kuruhusu yeye kuomba uraia wa nchi anakoishi sasa bila kuwa ameukana uraia wa Tanzania.

Hivyo natoa wito kwa Wabunge na wengineo kuacha kubisha juu ya uraia [pacha kwa mihemuko bila kujua undani wa uraia pacha, au kwa kisingizio cha uzalendo wakati kilichowakaa akilini wengi wenu ni wivu tu usio na maana. Hili ndilo watu wanaita joka la mndimu - unakuwa joka kwenye mdimu unawazuia watu kuchuma ndimu wakati wewe huli ndimu na hutegemei kula ndimu katika maisha yako, na mbaya zaidi unawaambia watu kula ndimu ni kitu kibaya na hujawahi kuonja ndimu na wala hutegemei kula ndimu. Swali limeulizwa, ni nchi ngapi zilizoruhusu uraia pacha zimeathirka na kuruhusu uraia pacha na hata zikaamua kusimamisha uraia pacha?


Asante kwa kujitahidi kufafanua hili suala kwa ndugu zetu, ambao wengi bado hawaelewi au wengine wanapotosha kwa makusudi. Binafsi, napingana na hii dhana ya kusema kwamba mtu "ameukana uraia wa Tanzania", kitu ambacho si kweli. Watanzania wengi niwajuao mimi, nikiwemo na mimi mwenyewe tunaipenda sana nchi yetu na popote pale tulipo hujisikia fahari kuwa na uraia na asili ya nchi inayoitwa Tanzania. Hivyo basi, kinacho tokea ni kwamba sheria za Tanzania kama zilivyo sasa haziruhusu raia wake kuwa na uraia mwengine zaidi ya Tanzania.

Matokeo yake ni kwamba Mtanzania anayeishi nje akichukua uraia wa nchi anayoishi, anakuwa moja kwa moja (automatically) amepoteza uraia wa Tanzania. Takwa hilo la kisheria lina tofauti na kusema kwamba mtu "ameukana" uraia wa Tanzania, kwani ukweli ni kwamba kungekuwa na chaguo la kisheria la kubaki na uraia wa Tanzania pindi uchukuapo uraia wa nchi nyingine (nchi nyingi zina ruhusu hili na ndio huita "uraia pacha"), basi wengi wangefanya hivyo. Kwa maana hiyo, si kweli kwamba watu "wamekana" uraia wa Tanzania, basi sheria imewalazimisha kufanya hivyo. Ni rahisi kuhoji kwa kusema "kama mtu anajua sheria ya Tanzania hairuhusu kwanini anachukua uraia mwingine?" Ili kutoa jibu la ufasaha, mtu anatakiwa ajue tofauti ya uraia na utaifa. Uraia unatambulishwa na karatasi (passport), ambalo utasema ndio mtu ana "likana", lakini utaifa unatambulishwa na asili, lugha, tabia, mazoea, na hata rangi, nk, ambavyo sio rahisi mtu "kuvikana" hata kama angependa kufanya hivyo. Kwa maneno mengine, kila mtu anaweza akawa raia wa nchi yeyote duniani, lakini sio kila mtu anaweza akawa na utaifa wa nchi yeyote duniani. Utaifa ni zawadi ya pekee inayotoka kwa Mwenyezimungu, ndio maana hamna anayeweza kuchagua azaliwe wapi au awe na wazazi wa aina gani.

Tuacheni chuki ndugu zangu kwa kutaka kuwapora Watanzania wenzetu utaifa wao. Pia, ni muda sasa kuacha kutishana kwamba uraia pacha ni "hatari kwa usalama" wa nchi yetu, na badala yake tuungane na nchi nyingine duniani kuruhusu suala hili na kupata faida zake (Mada ya siku nyingine).
 
Asante kwa kujitahidi kufafanua hili suala kwa ndugu zetu, ambao wengi bado hawaelewi au wengine wanapotosha kwa makusudi. Binafsi, napingana na hii dhana ya kusema kwamba mtu "ameukana uraia wa Tanzania", kitu ambacho si kweli. Watanzania wengi niwajuao mimi, nikiwemo na mimi mwenyewe tunaipenda sana nchi yetu na popote pale tulipo hujisikia fahari kuwa na uraia na asili ya nchi inayoitwa Tanzania. Hivyo basi, kinacho tokea ni kwamba sheria za Tanzania kama zilivyo sasa haziruhusu raia wake kuwa na uraia mwengine zaidi ya Tanzania.

Mkuu nimekuelewa sana. Ni kweli "kuukana" uraia wa Tanzania ni semantics za lugha. Lakini aibu pale inapotokea kwamba mtu level ya mbunge au waziri anasema "walioukana" uraia wa anzania, eidha kwa literally kuukana au kupoteza ni wasaliti wa Tanzania. Dhana nzima ya watu hao kukataa uraia pacha ipo katika kudhani uraia pacha ni kwa ajili ya watu "walioukana" uraia na ni kama wanalipiza kisasi kwa watu hao "kuukana" hata kwa namna ya "kuupoteza".

Ila ukweli unabaki pale pale, kwamba kwa mtu ambae alipoteza au "kuukana" uraia wa Tanzania, ili awe tena raia wa Tanzania ni process ndefu inahusika. Sidhani ni suala la kusema mimi sasa nataka kurudia uraia wa Tanzania.

Kwa hiyo ni akili finyu sana kubishia suala la uraia pacha kwa kuwa na mentality kwamba uraia pacha ni kwa ajili ya wale "walioukana" uraia wa Tanzania.
 
Bila shaka uraia pacha utamuwesesha raia wa nchi ingine aje aombe uraia hapa kwetu, hilo pia linakwenda kubadilisha sheria ya ardhi namba 4 inayosema kwamba mgeni ataruhusiwa kumiliki ardhi kama muwekezaji hivyo labda wasiwasi wa hao mambumbumbu ni kuweka rehani ardhi ya Tanzania kwa wageni watakao kua na raia pacha...
 
Asante kwa kujitahidi kufafanua hili suala kwa ndugu zetu, ambao wengi bado hawaelewi au wengine wanapotosha kwa makusudi. Binafsi, napingana na hii dhana ya kusema kwamba mtu "ameukana uraia wa Tanzania", kitu ambacho si kweli. Watanzania wengi niwajuao mimi, nikiwemo na mimi mwenyewe tunaipenda sana nchi yetu na popote pale tulipo hujisikia fahari kuwa na uraia na asili ya nchi inayoitwa Tanzania. Hivyo basi, kinacho tokea ni kwamba sheria za Tanzania kama zilivyo sasa haziruhusu raia wake kuwa na uraia mwengine zaidi ya Tanzania.

Matokeo yake ni kwamba Mtanzania anayeishi nje akichukua uraia wa nchi anayoishi, anakuwa moja kwa moja (automatically) amepoteza uraia wa Tanzania. Takwa hilo la kisheria lina tofauti na kusema kwamba mtu "ameukana" uraia wa Tanzania, kwani ukweli ni kwamba kungekuwa na chaguo la kisheria la kubaki na uraia wa Tanzania pindi uchukuapo uraia wa nchi nyingine (nchi nyingi zina ruhusu hili na ndio huita "uraia pacha"), basi wengi wangefanya hivyo. Kwa maana hiyo, si kweli kwamba watu "wamekana" uraia wa Tanzania, basi sheria imewalazimisha kufanya hivyo. Ni rahisi kuhoji kwa kusema "kama mtu anajua sheria ya Tanzania hairuhusu kwanini anachukua uraia mwingine?" Ili kutoa jibu la ufasaha, mtu anatakiwa ajue tofauti ya uraia na utaifa. Uraia unatambulishwa na karatasi (passport), ambalo utasema ndio mtu ana "likana", lakini utaifa unatambulishwa na asili, lugha, tabia, mazoea, na hata rangi, nk, ambavyo sio rahisi mtu "kuvikana" hata kama angependa kufanya hivyo. Kwa maneno mengine, kila mtu anaweza akawa raia wa nchi yeyote duniani, lakini sio kila mtu anaweza akawa na utaifa wa nchi yeyote duniani. Utaifa ni zawadi ya pekee inayotoka kwa Mwenyezimungu, ndio maana hamna anayeweza kuchagua azaliwe wapi au awe na wazazi wa aina gani.

Tuacheni chuki ndugu zangu kwa kutaka kuwapora Watanzania wenzetu utaifa wao. Pia, ni muda sasa kuacha kutishana kwamba uraia pacha ni "hatari kwa usalama" wa nchi yetu, na badala yake tuungane na nchi nyingine duniani kuruhusu suala hili na kupata faida zake (Mada ya siku nyingine).
Naunga mkono hoja.

Hizi hoja kuu mbili(walioukana utanzania na sababu za kiusalama) zinazotumiwa kuzimisha hili swala binafsi siziafiki.

Watanzania wengi nje ya nchi wamebaki na uraia wao licha ya kuwa na uwezo/nafasi ya kuuana.Baadhi wamelazika kuchukua uraia wa nchi nyingine kutokana na sababu za kikazi au za kijamii ambapo hawakua na namna nyingine ya kufanya ukizingatia kuwa katiba yetu inakataa kuwa na uraia wa nchi mbili.

Swala la sababu za kiusalama.Kwa waTZ walionje ya nchi huwa wanafanya application ya kuomba uraia na wanakaguliwa maisha yao kabla ya kupewa uraia mwingine.Vivyo hivyo nchini Tanzania, mtu yeyote asiye raia wa Tanzania akitaka kuwa raia wa Tanzania, anachunguzwa maisha yake na ofisi husika zikijiridhisha kuwa hana hatari wanampa uraia.Nchi hailazimishwi kumpa mtu uraia wa Tanzania eti kwa sababu tuu tumeruhusu uraia pacha.

Kwa dunia ya leo, uraia pacha ni wa muhimu sana.
 
Kwa kweli nikiwa kama victim hii mada imenigusa Sana, nikiwa na permanent resident miaka 8 Sasa nikiwa na non citizen ID miaka 5 Sasa ndani ya S. Africa nikamua kuenda SA home affair kuomba passport ya south kutokana na vitambilisho nilivyonavyo ni haki yangu kupewa passport lkn kufika home affair nikambia huwezi kupewa kwa sababu nchi yako tz wametuambia watanzania tusiwape passport nikawauliza kwa nn wakaniambia cc tumeambiwa na balozi yenu tusiwape coz mtakua na raia pacha na nchi yenu imezuia mtu kuwa na raia pacha, kwa kweli ckuamini nikaona maybe nimekutana na mtu mbaya pale home affair ikabidi niende nyengine na nyengine lakn majibu ni Yale Yale, sasa najiuliza je cc watz tuna tatizo gani ivi cc watz tuna akili kweli inaonekana hao viongozi tulowachagua hawapendi kuona waliowachagua wanaendelea, kwa kweli roho mbaya na ujinga umetushika cc watz,hiyo ilitokea miaka 2 iliopita Sasa wiki ilopita nikalenga tena ili kuona may be mambo yamebadilika lkn nililolikuta ni baya Zaid wameniambia itabidi niende ubalozini nikafute uraia wangu kabisa, Sasa mm ctaki kufuta uraia wa tz, yaani nimeshakula ng'ombe mzima na mkia wake bado kipande kidgo cha mkia lkn tz imenikwamisha, je mtu kama mm Nina haki ya kupenda au kuchukia uongozi wa tz
 
Bila shaka uraia pacha utamuwesesha raia wa nchi ingine aje aombe uraia hapa kwetu, hilo pia linakwenda kubadilisha sheria ya ardhi namba 4 inayosema kwamba mgeni ataruhusiwa kumiliki ardhi kama muwekezaji hivyo labda wasiwasi wa hao mambumbumbu ni kuweka rehani ardhi ya Tanzania kwa wageni watakao kua na raia pacha...
Mkuu, ukishasema uraia pacha utamwezesha raia wa kigeni aje kuomba uraia tayari una mentality ya Wabunge na Kangi.

Raia wa kigeni hawezi kuwa raia pacha kwa kuja kuomba uraia wa Tanzania. ILi kuomba uraia unatakiwa uwe tayari unaishi Tanzania kwa muda mrefu na una shughuli maalum kama kazi au uwekezaji, au umeolewa/kuoa na Mtanzania. Na mara nyingi kuwa raia ni baada ya kuwa mkazi wa kudumu. Kwa hiyo huwezi "kuja" Tanzania ili uombe uraia na kuwa raia pacha.
 
Kwa kweli nikiwa kama victim hii mada imenigusa Sana, nikiwa na permanent resident miaka 8 Sasa nikiwa na non citizen ID miaka 5 Sasa ndani ya S. Africa nikamua kuenda SA home affair kuomba passport ya south kutokana na vitambilisho nilivyonavyo ni haki yangu kupewa passport lkn kufika home affair nikambia huwezi kupewa kwa sababu nchi yako tz wametuambia watanzania tusiwape passport nikawauliza kwa nn wakaniambia cc tumeambiwa na balozi yenu tusiwape coz mtakua na raia pacha na nchi yenu imezuia mtu kuwa na raia pacha, kwa kweli ckuamini nikaona maybe nimekutana na mtu mbaya pale home affair ikabidi niende nyengine na nyengine lakn majibu ni Yale Yale, sasa najiuliza je cc watz tuna tatizo gani ivi cc watz tuna akili kweli inaonekana hao viongozi tulowachagua hawapendi kuona waliowachagua wanaendelea, kwa kweli roho mbaya na ujinga umetushika cc watz,hiyo ilitokea miaka 2 iliopita Sasa wiki ilopita nikalenga tena ili kuona may be mambo yamebadilika lkn nililolikuta ni baya Zaid wameniambia itabidi niende ubalozini nikafute uraia wangu kabisa, Sasa mm ctaki kufuta uraia wa tz, yaani nimeshakula ng'ombe mzima na mkia wake bado kipande kidgo cha mkia lkn tz imenikwamisha, je mtu kama mm Nina haki ya kupenda au kuchukia uongozi wa tz
Pole Mkuu. Tanzania iliwaambia South Africa Mtanzania yeyote anaeomba uraia wa South Africa lazima ombi lake lipelekwe Ubalozi wa Tanzania pale Pretoria ili likapitishwe na Tanzania. Lengo ni kukufuta uraia wa Tanzania na kukuita ili urudishe passport ya Tanzania. Kisha wanatuma taarifa kwa Wizara ya Mambo ya Ndani Tanzania kwamba wewe sio raia tena wa Tanzania, na wakurekodi kuwa umeukana uraia wa Tanzania.
 
Bila shaka uraia pacha utamuwesesha raia wa nchi ingine aje aombe uraia hapa kwetu, hilo pia linakwenda kubadilisha sheria ya ardhi namba 4 inayosema kwamba mgeni ataruhusiwa kumiliki ardhi kama muwekezaji hivyo labda wasiwasi wa hao mambumbumbu ni kuweka rehani ardhi ya Tanzania kwa wageni watakao kua na raia pacha...
Mkuu hao mambumbumbu unaosema ww hawajali kuhusu ardhi coz wanauhakika muombaji uraia hawezi kupata ardhi kirahisi wanachogopa wao kuja kuondolewa madarakani coz wtz wengi wanaoishi nje wamesoma na Wana mali kwa hyo wanajaribu kuwabana ili wasipate nafasi ya kuekeza
 
Mkuu hao mambumbumbu unaosema ww hawajali kuhusu ardhi coz wanauhakika muombaji uraia hawezi kupata ardhi kirahisi wanachogopa wao kuja kuondolewa madarakani coz wtz wengi wanaoishi nje wamesoma na Wana mali kwa hyo wanajaribu kuwabana ili wasipate nafasi ya kuekeza
Ni uoga usio na maana Mkuu. Kama ni kura ambazo CCM wanashinda watu watakaokuwa na uraia pacha si wengi kiasi cha kubadilisha matokeo ya uchaguzi tuliyozoea Tanzania. Hata hivyo huo ndio ufinyu wa kufikiri wa hao wanaoitwa viongozi wa Tanzania.
 
Pole Mkuu. Tanzania iliwaambia South Africa Mtanzania yeyote anaeomba uraia wa South Africa lazima ombi lake walipekele Ubalazi wa Tanzania pale Pretoria ili likapitishwe na Tanzania. Lengo ni kukufuta uraia wa Tanzania na kukuita ili urudishe passport ya Tanzania. Kisha wanatuma taarifa kwa Wizara ya Mambo ya Ndani Tanzania kwamba wewe sio raia tena wa Tanzania, na wakurekodi kuwa umeukana uraia wa Tanzania.
Kuhusu hilo nimestuka mapema mkuu, ila kwa Sasa acha nile nao sahani moja mpaka kieleweke acha nitumie passport ya tz na huku niko na I'd ya south
 
Ni uoga usio na maana Mkuu. Kama ni kura ambazo CCM wanashinda watu watakaokuwa na uraia pacha si wengi kiasi cha kubadilisha matokeo ya uchaguzi tuliyozoea Tanzania. Hata hivyo huo ndio ufinyu wa kufikiri wa hao wanaoitwa viongozi wa Tanzania.


Tatizo la CCM kwenye hii issue ya uraia pacha ni kuogopa tu ushindani utakaoletwa na Watanzania wa diaspora, ambao wengi wameelimika au kutokana na kuishi kwao kwenye nchi za kigeni zilizoendelea, wamekuwa na uelewa wa mambo ambao utaleta shida kwa viongozi wa CCM waliozoea kuabudiwa na wajinga. CCM wamegeuza ujinga au uelewa mdogo wa mambo wa Watanzania walio wengi (haswa wanaoishi Tanzania) kama mtaji wa kisiasa. Hivyo basi, wanaogopa kwamba wenzao wa diaspora watakuja ku challenge nafasi zao za kisiasa au hata wakiamua kubaki kuwa raia wa kawaida, watahoji kwa hoja nzito zaidi madudu yao ndani ya uongozi. Ndio maana, kama mnakumbuka ile "katiba ya Warioba" ilivyokuwa inajadiliwa, baadae CCM wali compromise kwenye kipengele cha uraia pacha kwa kusema kwamba wanadiaspora watapewa "hadhi maalum" lakini ni marufuku kujihusisha na siasa.

Ni shida sana! Yaani wana angalia maslahi yao tu na nafasi zao za kisiasa, huku wakisahau faida ambazo nchi itapata, ikiwemo kuturudishia wataalamu wetu waliotapakaa duniani kote wakinufaisha nchi nyingine kupitia taaluma zao kama udaktari, uhandisi, IT, nk. Sio tu kwamba uraia pacha utaleta nguvu kazi bora Tanzania, bali pia utaleta wananchi wenye kujitambua zaidi na kuhoji mambo kwa maslahi ya nchi yao, na hivyo kuongeza chachu kwenye gurudumu la maendeleo.
 
Tatizo la CCM kwenye hii issue ya uraia pacha ni kuogopa tu ushindani utakaoletwa na Watanzania wa diaspora, ambao wengi wameelimika au kutokana na kuishi kwao kwenye nchi za kigeni zilizoendelea, wamekuwa na uelewa wa mambo ambao utaleta shida kwa viongozi wa CCM waliozoea kuabudiwa na wajinga. CCM wamegeuza ujinga au uelewa mdogo wa mambo wa Watanzania walio wengi (haswa wanaoishi Tanzania) kama mtaji wa kisiasa. Hivyo basi, wanaogopa kwamba wenzao wa diaspora watakuja ku challenge nafasi zao za kisiasa au hata wakiamua kubaki kuwa raia wa kawaida, watahoji kwa hoja nzito zaidi madudu yao ndani ya uongozi. Ndio maana, kama mnakumbuka ile "katiba ya Warioba" ilivyokuwa inajadiliwa, baadae CCM wali compromise kwenye kipengele cha uraia pacha kwa kusema kwamba wanadiaspora watapewa "hadhi maalum" lakini ni marufuku kujihusisha na siasa.

Ni shida sana! Yaani wana angalia maslahi yao tu na nafasi zao za kisiasa, huku wakisahau faida ambazo nchi itapata, ikiwemo kuturudishia wataalamu wetu waliotapakaa duniani kote wakinufaisha nchi nyingine kupitia taaluma zao kama udaktari, uhandisi, IT, nk. Sio tu kwamba uraia pacha utaleta nguvu kazi bora Tanzania, bali pia utaleta wananchi wenye kujitambua zaidi na kuhoji mambo kwa maslahi ya nchi yao, na hivyo kuongeza chachu kwenye gurudumu la maendeleo.
Kweli Mkuu. Ndio maana inasemwa kuwa wanaopinga uraia pacha ni sawa na joka la mndimu- Hawana sababu za maana au zenye mshiko. Kwa mtu wa kawaida wa mtaani inajulikana ni wivu tu, na kwa viongozi aidha nao ni sababu za wivu, umbumbumbu au kwa kuwa tu wanaona kama suala la uraia pacha ni ajenda ya vyama vya upinzani.
 
Kuhusu hilo nimestuka mapema mkuu, ila kwa Sasa acha nile nao sahani moja mpaka kieleweke acha nitumie passport ya tz na huku niko na I'd ya south
Utakua umefanya jambo jema sana, usikubali kurudisha passport, nchi yetu inasikitisha maana hata kwa nchi zingine tunaonekana kituko, nchi maskini kama Tz eti inajifaraghua kumfuta mtu uraia, ndio maana raia wanajifungia sana, wanakosa confidence ya kutoka nje ya nchi.
 
Bila shaka uraia pacha utamuwesesha raia wa nchi ingine aje aombe uraia hapa kwetu, hilo pia linakwenda kubadilisha sheria ya ardhi namba 4 inayosema kwamba mgeni ataruhusiwa kumiliki ardhi kama muwekezaji hivyo labda wasiwasi wa hao mambumbumbu ni kuweka rehani ardhi ya Tanzania kwa wageni watakao kua na raia pacha...
Hili nalo neno
lakini sidhani kama mtu mwenye asili ya nje ya Tanzania, ambae amepewa Uraia wa Tanzania pasipo kuukana Uraia wa nchi yake ya asili (Uraia pacha), Kwamba atakuwa na haki zoote anazopata Mtanzania halisi, binafsi nadhani lazima patakua na mipaka katika maswala ya msingi, Vinginevyo unaweza ukauza Nchi
 
Hili nalo neno
lakini sidhani kama mtu mwenye asili ya nje ya Tanzania, ambae amepewa Uraia wa Tanzania pasipo kuukana Uraia wa nchi yake ya asili (Uraia pacha), Kwamba atakuwa na haki zoote anazopata Mtanzania halisi, binafsi nadhani lazima patakua na mipaka katika maswala ya msingi, Vinginevyo unaweza ukauza Nchi
Nadhani mkuu hujaelewa concept ya uraia pacha ukiwa ba uraia pacha hakuna swala la kuukana uraia wa awali yani unakua Mkenya - Mtanzania kama vile yule jamaa Kevin Prince Boateng ni mjerumani na mghana pia kama sijakosea kwaio habari za kuukana uraia wa awali hazipo kabisa
 
Hili nalo neno
lakini sidhani kama mtu mwenye asili ya nje ya Tanzania, ambae amepewa Uraia wa Tanzania pasipo kuukana Uraia wa nchi yake ya asili (Uraia pacha), Kwamba atakuwa na haki zoote anazopata Mtanzania halisi, binafsi nadhani lazima patakua na mipaka katika maswala ya msingi, Vinginevyo unaweza ukauza Nchi
Ningependa sana mtu anieleweshe ni kitu gani kitamuwezesha mtu kuuza nchi kwa kuwa tu sasa amekuwa raia wa Tanzania baada ya kuishi hapa nchini kwa zaidi ya miaka mitano. Na hiyo nchi ataiuzaje?

Na pili nihakikishieni kwamba watu mnaoogopa kuuza nchi ni hao tu ambao wana sababu za msingi za kutaka uraia pacha uruhusiwe, na sio watanzania wengine ambao ni raia tayari.

Hivi hao Magufuli anaposema wameipiga sana hii nchi ni raia pacha? Hao waliokuwa wakitorosha Tanzanite na dhahabu, wakilipa mishahara hewa, wakifanya tenda hewa, wakikwepa kodi, waliotuingiza mikataba mibovu, wasijulikana kuteka watu, ni raia pacha? Kwa nini muone mtu akiwa raia pacha ni mbaya kwa Tanzania kuliko hao wote?
 
Nadhani mkuu hujaelewa concept ya uraia pacha ukiwa ba uraia pacha hakuna swala la kuukana uraia wa awali yani unakua Mkenya - Mtanzania kama vile yule jamaa Kevin Prince Boateng ni mjerumani na mghana pia kama sijakosea kwaio habari za kuukana uraia wa awali hazipo kabisa
Wengi hawaelewi Mkuu, lakini watabisha hadi asubuhi uraia pacha haufai! Eti raia pacha watauza nchi, jamani!

Mtu anaishi kama mkazi wa Tanzania kwa miaka kumi, anaomba uraia ili awe raia pacha anaambiwa atakuwa hatari kwa usalama wa Tanzania! Sasa nimeishi kama permanent resident miaka kumi hiyo hatari haipo, inakuja pale tu ninapokuwa raia wa Tanzania nikawa raia pacha.
 
Back
Top Bottom