Ni aibu kubwa kwa CCM kuogopa Katiba Mpya wakati mchakato ulianzishwa na mwenyekiti wa CCM

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Feb 19, 2021
3,086
4,879
Hakika haiingi akilini kuona viongozi wa CCM ndio wako na vipaza sauti wakipinga Upatikanaji Wa Katiba Mpya kwa kisingizio cha tunajenga uchumi na eti Wananchi wanataka Elimu Maji na MaDawa
ujenzi wa uchumi ni Mchakato endelevu toka awamu ya 1 mpaka mwisho wa dunia Ujenzi wa UCHUMI hautakoma.

Pili huduma za Elimu,Maji na Madawa ni endelevu toka mkoloni alikuwa Anazitoa na Zitaendelewa kutolewa mpaka mwisho wa dunua kwa hiyo hakuna wakati zitakoma kwa hiyo viongozi kujikita kwenye hoja hizi ni hoja dhaifu sana.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete ambaye alikuwa mwenyekiti wa CCCM ndiye aliyesema kuna haja ya kuwa na katiba mpya kwani miaka 50 ya Katiba iliyopo imepitwa na WAKATI kutokana na mabadiliko mengi yaliyotokea Tanzania na duniani na pia katiba iliyopo haikuwashirikisha wananchi pamoja na kuanzisha huo mchakato aliendelea kujenga uchumi na kuwapatia Wananchi huduma za Elimu Maji na Madawa kwa sababu ni huduma endelevu

Viongozi Acheni kutoa hoja nyepesi nyepesi kwenye jambo zito

Kumbukeni wabunge wa Bunge la Katiba Wamelipwa posho lakini kazi hawajakamilisha wana deni la katiba mpya

Katiba ni ya wananchi tunaihitaji
 
Tunahitaji usimamizi bora wa hivyo vinavyojengwa kwakutumia katiba iliyo bora hiyo katiba haitahitaji force account ambayo kazi zinafanyika kwa viwango vilivyo chini na kuua biashara za ujenzi
 
Katiba Mpya siyo kipaumbele kwa sasa kwa kuwa wanasiasa wanataka kutumia kigezo cha siasa kwa manufaa yao kurudi kwenye siasa baada ya kustaafishwa 2020.. Katiba Mpya itapatikana na wananchi na wale waliokwamisha BMK na UKAWA hawawezikuwa sehemu ya mchakato
 
Katiba Mpya siyo kipaumbele kwa sasa kwa kuwa wanasiasa wanataka kutumia kigezo cha siasa kwa manufaa yao kurudi kwenye siasa baada ya kustaafishwa 2020..

Katiba Mpya itapatikana na wananchi na wale waliokwamisha BMK na UKAWA hawawezikuwa sehemu ya mchakato


MAENDELEO KWANZA
 
UKAWA si ilisaini makubaliano haya baada ya kususia bunge la katiba na wale wanaharakati? walipofika nje wakatibuana na CUF wakajiondoa kwa uroho wa watu wakaingia kwenye uchaguzi na wakapata wabunge 60-lini hawa wabunge 60 waliwahi kuongelea UKAWA tena na madai ya katiba?



Image


Image


Image

UKAWA ilivunjika? Ilitimiza haya makubaliano? Lini waliwahi kusema ukawa imevunjika na haya siyo makubaliano tena? Kwa hiyo baada ya kukosa ubunge na wengine kukimbilia nje ya Tanzania ndiyo wanaanza kudai katiba? Kwa mtindo huu KATIBA isubiri tulete MAENDELEO tusichoshane

 
Acheni unafiki, waliokimbia bunge la katiba hadi mchakato ukaparaganyika si hao bwana zenu wa UKAWA baada ya kuvimbiwa hela za posho za waTZ maskini!! Mungu akawalaani kwa tamaa zenu za fedha na madaraka mkaparaganyana na kutukanana August, 2015!! Wanafiki wakubwa
 
Katiba Mpya siyo kipaumbele kwa sasa kwa kuwa wanasiasa wanataka kutumia kigezo cha siasa kwa manufaa yao kurudi kwenye siasa baada ya kustaafishwa 2020..

Katiba Mpya itapatikana na wananchi na wale waliokwamisha BMK na UKAWA hawawezikuwa sehemu ya mchakato


MAENDELEO KWANZA
Kama imeshindwa kupata Maendeleo kwa Miaka 60 Kwa KATIBA ILIYOPO ulitarajia KUYAPATA KWA KATIBA HIYO HIYO ni KICHAA TU ndio Atayapata kwa Katiba hiyo iliyopo
 
Katiba Mpya siyo kipaumbele kwa sasa kwa kuwa wanasiasa wanataka kutumia kigezo cha siasa kwa manufaa yao kurudi kwenye siasa baada ya kustaafishwa 2020..

Katiba Mpya itapatikana na wananchi na wale waliokwamisha BMK na UKAWA hawawezikuwa sehemu ya mchakato


MAENDELEO KWANZA
MAENDELEO KWANZA,Swadaktaaaa lakini hatujaleta maendeleo kama aliyoleta Hitler kwa watu wake.Kipi kilitokea??
 
UKAWA si ilisaini makubaliano haya baada ya kususia bunge la katiba na wale wanaharakati? walipofika nje wakatibuana na CUF wakajiondoa kwa uroho wa watu wakaingia kwenye uchaguzi na wakapata wabunge 60-lini hawa wabunge 60 waliwahi kuongelea UKAWA tena na madai ya katiba?



Image


Image


Image

UKAWA ilivunjika? Ilitimiza haya makubaliano? Lini waliwahi kusema ukawa imevunjika na haya siyo makubaliano tena? Kwa hiyo baada ya kukosa ubunge na wengine kukimbilia nje ya Tanzania ndiyo wanaanza kudai katiba? Kwa mtindo huu KATIBA isubiri tulete MAENDELEO tusichoshane

Kukubali kutokukubaliana ni sehemu ya democracy. Kushindwana ktk hoja hasa upande moja unapotumia hila kupitisha matakwa yao ni sawa tu.

Hila hizo ndiyo zinaiogofya Ccm kuendelea na mchakato. Na huku wakijua wananchi walio wengi hawapo pamoja nao.
 
Ubinafsi tu unawasumbua kama kawaida ya sisi ngozi nyeusi. Ila kiuhalisia hata wao wanajua umuhimu wa katiba mpya. Mama Samia mwenyewe alikiri kwamba anatambua umuhimu wa katiba mpya
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom