Ni aibu kubwa kuwa ombaomba huku tukigawa mali kama njugu!!

awamu3imetulimaza

New Member
Jul 2, 2006
1
1
Mkono awashushua wenyeviti halmashauri

na Charles Mullinda

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, amewashushia tuhuma nzito wenyeviti wa halmashauri za wilaya ilimo migodi ya dhahabu inayoendeshwa na Kampuni ya Barrick Gold Tanzania kwa kukubali kupokea kodi ya sh milioni 240 kwa mwaka.

Amesema kitendo walichokifanya kimewadhalilisha na kuonyesha jinsi walivyo waroho na wasivyofikiria juu ya athari zinazosababishwa na wawekezaji hao wanapochimba madini.

“Ni ujinga mtupu uliofanyika; yaani walipoona pesa, bila kufikiri wakakubali kuzichukua,” alisema.

Mkono aliyasema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima kwa simu kuhusu hatua ya Kampuni ya Barrick Gold Tanzania kuanza kulipa kodi ya dola za Kimarekani 200,000 sawa na sh milioni 240 kila mwaka kwa halmashauri hizo za wilaya.

Alisema kabla ya kuamua kuzichukua fedha hizo, kulikuwa na ulazima wa kukaa chini na kuangalia uharibifu wa mazingira unaosababishwa na kampuni hiyo, sambamba na kuangalia faida wanayoipata wawekezaji hao kama inalingana na kodi wanayotoa.

“Kulikuwa na ulazima wa kukaa chini na kuangalia jinsi mazingira yanavyoharibiwa, mashimo yanayoachwa baada ya kuchimba, pale kwangu katika mgodi wa Buhemba kuna vifusi vinalingana na mlima. Je, hiyo pesa wanayotoa kwa halmashauri itatosha kufukia kifusi hicho?

“Katika kazi zao, wanatumia vijana wetu ambao wamesoma, hakuna mtu ambaye hana elimu pale. Je, wanachangia nini katika elimu? Hizo fedha wanazotoa zitasaidia katika elimu? Na si elimu tu, barabara, maji na mambo mengi ya maendeleo,” alisema Mkono.

Mbunge huyo alisema kampuni hiyo inatumia vijana wa Kitanzania ambao wamesomeshwa na Watanzania bila kuchangia chochote katika elimu; wanatumia barabara na huduma nyingine za muhimu zilizotokana na jasho la wananchi wa kawaida, huku wakivuna faida kubwa.

Alisisitiza kwamba sh milioni 240 kwa mwaka zilizoanza kutolewa na Kampuni ya Barrick hazitoshi kwa sababu kazi ya kufukia mashimo yaliyotokana na uchimbaji wa dhahabu itahitaji mabilioni ya fedha.

“Nasisitiza ni lazima tuelewe ni kiasi gani cha madini wanachimba na kuchukua kuondoka nayo ili tupime na sisi kiasi kinachostahili watupatie.

“Kuweka wastani wa sh milioni 240 kwa migodi yote, ni upuuzi kwa sababu kuna sehemu ipo dhahabu nyingi kuliko kwingine, sasa kwanini iwe kiasi hicho hicho?” alihoji Mkono.

Alisema kama hoja hizo zingezingatiwa, hata Rais Jakaya Kikwete asingekuwa na sababu ya kwenda kuomba ufadhili kwa ajili ya kujenga chuo kikuu hapa nchini.

“Dhahabu ilikuwepo siku nyingi, lakini ilitunzwa na kuwekewa ulinzi kwa makusudi ili ije isaidie ujenzi wa nchi yetu na maendeleo kwa ujumla, hivi hata wewe unaona ni jambo zuri kwa rais wetu kwenda kuomba ufadhili wa kujengewa chuo kikuu wakati kuna dhahabu lukuki hapa nchini?” alihoji Mkono.

Alitahadharisha viongozi kuwa makini katika kutetea maslahi ya wananchi ili kujiepusha na migogoro ambayo inazikumba nchi nyingine zenye utajiri wa asili kama uliopo Tanzania.

Alitoa mfano wa nchi za Nigeria na Afrika Kusini, ambako kuna machafuko ya kila mara katika maeneo yenye migodi, kwamba yanasababishwa na uonevu wa wawekezaji kwa wananchi ambao ndio wenye mali.

Aidha, Mkono alisema Kampuni ya Barrick inapaswa kushitakiwa kwa kukiuka mkabata wake wa uchimbaji madini ilioingia na serikali.

Alisema Barrick haipaswi kusamehewa kwa kuwadhulumu Watanzania iliotakiwa kuwalipa mrahaba kupitia halmashauri zao za wilaya kwa mujibu wa mkataba, na pia inapaswa ieleze waziwazi imekuwa ikikiuka mkataba wake kwa miaka mingapi.

Mkono alisema mtu yeyote anayevunja sheria ni budi afikishwe mbele ya sheria, jambo ambalo linapaswa kufanyika kwa Kampuni ya Barrick ambayo imedhihirisha kuwa ilikuwa ikivunja mkataba wake kwa kutolipa kodi ambayo iko kwenye mkataba wake tangu ilipoanza shughuli za kuchimba madini hapa nchini.

Kulingana na mikataba ya wawekezaji hao, kodi ya dola 200,000 ilitakiwa kulipwa kwa halmashauri za wilaya husika baada ya kutunga sheria ndogo kuhusu suala hilo, lakini kutokana na usiri uliokuwapo katika mikataba hiyo, hazikuweza kutambua suala hilo.

Hivi karibuni, Kampuni ya Barrick Gold Tanzania ilitoa sh milioni 240 kwa kila halmashauri, ambako imewekeza migodi yake. Fedha hizo zilikabidhiwa kwa wenyeviti wa halmashuri husika katika hafla iliyofanyika mjini Dodoma Juni 14.

Mkono alionyesha kutokubaliana waziwazi na hatua hiyo baada ya kususia hafla ya kukabidhiwa fedha hizo na kuwaeleza waandishi wa habari kuwa hili lilikuwa tukio chafu ambalo hakuwa tayari kulishuhudia likifanyika mbele ya macho yake.

Mkono alikaririwa na waandishi wa habari akieleza kwamba kiwango hicho ni kidogo na kukubali kukipokea, ni kujitia kitanzi kwa sababu kisheria ukipokea hicho kidogo unakuwa umekikubali moja kwa moja.



Swali ni kwanini tumeamua kukaa kimya huku mali yetu ikiedelea kuibwa bila huruma na sisi kugeuzwa kuwa omba omba> Je hizo halmashauri ni nani aliezipa huo uwezo wa kufanya maamuzi ya utumbo kama haya???

kwa madiwani wengi ni darasa la saba huko mara! huo ni ukweli mtupu!
 
Ndg Mkono,

Pongezi, umeongea vema sana, however, ulikuwa wapi siku Bi Maua Daftari aliposema mikataba ni SIRI?, tulitegemea watu Wanasheria kama ninyi (Mliobobea + Mbunge) kupiga sana kelele kuhusu kauli ya Daftari,............. wanasheria mna usemi wenu "silence means YES" sasa naona UNAPIGIA KELELE END RESULT baada ya kukubali kilichosemwa bungeni!!!. mimi nikiwa mmoja wa wanachi wako tuliokupa kura nachelea kuona unachosema ni honest!

Kama unasoma hii forum, tafadhali panga mikakati ya kupeleka hoja Bungeni ili wabunge kama ninyi muwa na nafasi ya kui-review mikataba kw amanufaa ya sisi wananchi
 
Huyo Mbunge ambaye ni mwizi mkubwa wa mali ya serikali anapaswa kuwa mtu wa mwisho duniani kuongelea mambo ya wizi, huyu ambaye kila siku anafanya mipango ya ujanja kupewa tenda za serikali za sheria na kui-over charge serikali kwa kugawana na mawaziri leo anaweza kuthubutu kuwatukana viongozi wa manispaa? Ama kweli nyani haoni his behind?

Hela za kuilipia ile ndege aliyomkodishia mgombea mmoja wa urais wa CCM kuzunguka bongo nzima kutafuta signatures, alizipata wapi? Kama kawaida wananchi wa bongo wataendelea kudanganywa tu na waizi kama huyu!
 
Mzee Es,
Samahani mkuu lakini, kuna kuna wakati nashindwa kuelewa kama kweli wewe ndiye Mzee Es aama kuna mtu anatumia jina lako. Nakuona umepooza sana kwa hoja mzee vipi umeishiwa?

Swala hapa ni hili la Barricks Gold na uhalali wa viongozi wetu kukubali kupokea hizo dola laki 2 kama ruzuku kwa halmashauri hali fedha hizi hazikupigiwa hesabu ya kimapato kama inavyotakiwa.
Huyu mbunge hata kama anayo mabaya yake hii ni kesi nyingine kabisa na unaweza kuiweka hapa tukaijadili kwa mapana lakini kuchukua hoja kwa kutazama nani kasema sidhani kama ni mwendo mzuri.
Labda mwenzetu unakubaliana na mikataba ya madini na vizuri utuambie hayo mazuri yake nasi tupate kuona ukichaa wa huyu mbunge.
 
Mzee ES, Mkono ni tajiri toka siku nyingi ana kesi ntinyi za kimataifa ana hela siyo kwa kuibia nchi. Ni kweli kama alivyosema Mkandara wakati mwingine unamchesha siyo kwa kutojua ila tu kwa chuki zako binfasi na kundi la mwalimu!

sijui mwl na kundi lake walikukosena nini??


Hivi kweli mambo anayaofanya mkono jaribu kwenda uone katika jimbo lake ! ni mkono huhyu huyu alieyatamka wazi bungeni waktai wa awamu ya Mkapa na kukemea kuhusu uuzwaji wa nyumba za serkali lakini wabunge wengine wote wlaikaa kimya! ninamnukuu" alisema mimi siyo mjamaa lakinini kwa hili la uuzinaji wa nyumba za serkali kana kwamba baadaya ya hii serkali hakutakuwa na serkali nyingine au tunaenda mbinguni ni ajabu kubwa na inatia shaka kama kweli nyie ni wajamaa!!

Mzee ES tunaheshimu michango yako lakini jaribu tu kidogo kupunguza upenze na chuki zisiso za maana utakuwa kiongozi mzuri hapa kazi yetu ni kufundishana na kukosoana! Mimi Mkwa sasa nimeongia kwa nguvu mpya katika hii Formu ninaipenda kwa sasabu nimeona kuna watu wenye tofauti katika mitizamo na michango yao wote ni mizuri.
 
Mwakapungi unasema kweli? au na wewe ni mmoja wao!

http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2006/07/03/69547.html



Huyo Mkono tumeskia kazi zake, sasa hilo la deal za kupata kesi mimi silijui ila tu kama alivyosema Mkwawa insemekana jamaa anapta international case.

Hilo la kutoa la kutoa hela wakati wa Kampeni tukianza kuulizana hapa itakuwa kazi wenye katika CC ya CCM liliwashinda! Kikwete alitumia Kiasi gani alipta wapi? Malecela alikodi ndge alipoulizwa alisema rafikia yake alimlipia! hilo ninadhani tuliache kampeni zimeisha na makundi yaishe taratibu japo walioshindwa itawachukua miaka 20 kukubali!
 
Hebu nijaribu kuwaelewa wazee,

Mwizi mmoja kwa sababu akiiba anawasaidia wananchi, na kwamba anapewa njia za kuiba mpaka nje ya nchi kwa kuwatumia viongozi wetu wa nchi na kugawana nao, na kwamba ameanza kuiba siku nyingi, basi it is ok kwake kuwatukana wezi wengine wa serikali wadogo wadogo!

Mkandara ni kweli bro kuwa sasa wewe ndiye bingwa wa issues na maneno yako humu kwenye hii forum ndio ukweli wenyewe,

lakini samahani, ninamjua Mkono tena na deal zake zote, Mkono ni another bongo Mafiya kama Mtandao nilishamzungumza toka BCS, na sikukusikia ukisema kitu, two wrongs haziwezi ku-make right, Mkono ni mwizi kama hao anaowapigia kelele na anapaswa kuwa mtu wa mwisho kuwauliza wezi wenziwe nuless kama hakupata mgawo kwenye hayto madini! Hayo maneno mengine nimeyazoea that is why I am ES!
 
Mzee ES,
Be that it may that Mkono is a thief. Does that take away anything in his message? Should he just keep quiet and watch these foreigners continue to plunder our wealth. Like Mkandara says we can debate Mkono's thievery in another forum. Let us focus on his message for now.
 
Mzee Es,
Siku zote wewe bingwa ktk kuendesha hoja ndani ya mada. Na mara kadhaa nimeona watu wakitaka kutafsiri hoja zako nje ya mada kwa sababu umehusisha mtu wasiomtegemea ndani ya mada husika. Kwa mtazamo huo nimekuwa nikikubaliana nawe kwa sababu walitaka kukutoa nje ya mada. Kwa hiyo binafsi huangalia mada yenyewe, hoja inayohusika kisha huitazama shilingi yangu kwa malengo ya kutafuta reality ama correct way ya ku-deal na swala hilo. Mara nyingi nimejikuta nakubaliana na wewe kwa sababu hizo hizo na sio swala la Right or Wrong! kwani hatupo kanisani wala msikitini hapa.

Lakini hapa Mzee Es kidogo umetoka nje. Wana mtandao umewasema sana kwa mabaya na mazuri yanayotokea ndani ya hoja ama mada yenyewe. Wengine tumeshindwa kuamini hadi yalipotokea kweli.
Kwa mfano hapo zamani ungesema mambo kibao ya MKONO yanayohusu yeye na madini na jinsi alivyotaka kuwafanyizia watu wa Mara. Ama uhusiano wa Mkono na Jambazi fulani la madini.
 
WanaTEF,

Nionavyo afadhali ya huyu Mkono anayeiba kisha kurudisha baadhi kwa wananchi kuliko hao manyang'au mengine kama Mahalu. Alichokemea ni sahihi na hili alilianzia toka siku ya kukabidhiwa hizo hela.

ES kutofautiana ni jambo la kawaida miongoni mwa watu, Unaweza kuwa upo sahihi lakini sio kwenye hii mada. Nami naungana na wengine kusema umeteleza kidogo na kutoka nje ya mada.

FD
 
Mkono amegenga ofisi mpya kabisa ya CCM Musoma mjini. Mkono amejenga shule za sekondari si chini ya kumi tena kwa kutumia hela yake Wilaya ya Musoma vijini ilikuwa nyuma sana kishule sasa nenga Butiama kajenga shule mpya kubwa ya kisasa kila darasa na ofisi lina Computer, Nenda Busegwe hivyo hivyo nenda kinubwa hivyoi hivyo nenda Kisamwene hivyo hivyo nenda majita hukuo nenda Kiagata huko angalai mabarabara!!!

We achaa kumechezea Mkono bwana usijaribu uajimaliza mwenyewe!!!

Jaribu kwenda tu Musoma upate kazi zake alizozifanya!

Hili la wizi kama una ushahidi weka hadharani!!

Kama alivyosema FD kuna wangapia ni matajiri wa kutuppwa tena wameiba kwelie kwlei kama Former PM ila wanachofanya wafischa hela zao maana waito misaada wana hofiu wizi wao utajulikana!

kama mtu una chuki binafsi usdhani utaweza kuwadanganya wachangiaji humu ndani.
 
Ninadhani ni wakti muafaka sasa tuendelea na maada yenyewe kuhusu Mrahaba na ni kwa nini hawa Makaburu hawakuwa wanalipa huo mrahaba wakti wa serikali ya awamu ya tatu!!

Huu ujinga iko siku tutafikisha mahakamani tu!
 
Ndiyo wazee na wewe bwana Es naona umepotea kwa kiasi kikubwa mno.Mimi nadhani mnakosea sana habari za kusifu ilipashwa mmpe John Malecela Mgogo ndipo bwana Es angaliona ni jambo la maana .Wewe Es sina hakika kama kweli wewe ni Mbunge maana huonekani hata kuwajua watu wa CCM wa maana na wenye kupenda maendeleo .

Una habari kwamba huyu Mbunge wa Musoma vijijini hata kampeni hakupiga kama wengine ?Huyu ukifika Musoma anajulikana kwa jina Mukono kwa Mukono kwamba onyesha bidii yeye anakuja kumalizia .Ni Mbunge wa Mkoa huyu mpenda maendeleo hana mchezo .

Kabla hujasema sana kuhusu wizi wa huyu jamaa basi fika angalau hapa Musoma ujionee baadaye twende kwenye Jimbo la Mzee wako Malecela utakuta watu hata shule hawana kazi yake kubwa ni kutafuta namna ya kuiyumbisha Tanzania kwa kukaa an kukataa wagombea binafsi na kuhubiri ugomvi dhidi ya wapinzani utadhani si watanzania .

Wewe kijana Es tema mate chini na uwe na aibu kwanza mpe Mukono hongera kwa kuwa basi ni mwizi ambaye anajali yaani haibi kama hao wenzio kwamba wanakimbizia pesa nje yeye anaiba na kuwapa watu wenye mahitaji .Kaiba hana nyumba SA wala Lushoto.Kaiba lakini anasimama na kukekemea uozo wa Bunge la CCM.

Tuache na Mukono wetu naona sasa wewe umeishiwa huna la kusema zaidi .
 
Mzee Es hajakosea hata kidogo hapo juu kuwa huyu Big shot lawyer (wa Bongo) "anapaswa kuwa mtu wa mwisho duniani kuongelea mambo ya wizi, huyu ambaye kila siku anafanya mipango ya ujanja kupewa tenda za serikali za sheria na kui-over charge serikali kwa kugawana na mawaziri leo anaweza kuthubutu kuwatukana viongozi wa manispaa". Nyie mnaomtetea mtu huyu ambaye alishirikiana na baadhi ya watu katika serikali iliyopita kushauri na kupitia baadhi ya mikataba mibovu kama uuzaji/ubinafsishaji wa makampuni kama NBC na TTCL (kutaja michache tu) mna kila haki ya kufanya hivyo- lakini msitake kuwashawishi watu wote waamini leo hii kuwa 'Mheshimiwa' huyu ni mtu safi asie na dosari ama kuwa sisi sote ni watu tusio fikiri mambo kwa kina.

Binafsi sikusoma 'post' ya Mzee Es kusema kuwa alichosema 'Mheshimiwa' mbunge si sahihi. Sote tunakubali kuwa nchi yetu inapunjwa sana na makampuni haya ya madini toka nje na tungependa kuona kuwa tunapata faidi kubwa zaidi toka katika rasilimali zetu.

Lakini, anapotokea mtu ambaye binafsi ameshiriki katika kuliingiza taifa katika mikataba mibovu na 'wazungu' wasio na huruma halafu tena mtu huyo huyo anadai wazungu hawa "wanacheza rafu"- wakati yeye kama mwanasheria 'mahiri' na mwandamizi anayepaswa/ama aliyepaswa kujua kujua mchezo wa watu hao- watu lazima tujiulize kama kweli yuko 'sincere'!

Mtazamo wangu ni kuwa kucharuka huku kwa sasa ni kuwa:katika zama hizi za nchi kuendeshwa kwa kasi pamoja na mabadilko ya nyadhifa yaliyofanya na yanayoendelea kufanya, vyanzo vya fedha kwa baadhi ya waheshimiwa (na baadhi ya makampuni binafsi yakiwemo ya wanasheria) vyaelekea kunyatiwa.
 
Nchi hii ina wanafiki jamani!!

mmoja wao ni kama wewe zaidi!!

wezi akina kigoda, Marry Ndosi, Rubambe na wengine wengi ambao ni wameiba wakiwa serkalini mbona hamupigii kelele!!

Waliosaini mikataba wanajulikana waliouza nchi wanajulikana Mkono unamuingizaje humo!! ama KWELI SASA MMEISHIWA!!!

MKUBALI YAISHE AU WEKENI DATA!

Acheni ushabiki wa kisiasa na kimajimbo hapa!!!

Wekeni data na siyo tu kusema NBC TTCL!!!!!!!!!!!
 
Haya haya ktk kipindi cha lala salama!

Nd. Zaidi anayo point kubwa sana ikiwa maneno haya yana ukweli ndani yake.
Amesema:- Nyie mnaomtetea mtu huyu ambaye alishirikiana na baadhi ya watu katika serikali iliyopita kushauri na kupitia baadhi ya mikataba mibovu kama uuzaji/ubinafsishaji wa makampuni kama NBC na TTCL (kutaja michache tu) mna kila haki ya kufanya hivyo- lakini msitake kuwashawishi watu wote waamini leo hii kuwa 'Mheshimiwa' huyu ni mtu safi asie na dosari ama kuwa sisi sote ni watu tusio fikiri mambo kwa kina.
Hapa sasa tunazungumza!... na itakuwa bora tufahamu nafasi ya huyu Mkono ktk kupitisha mikataba. ...Hivi huyu mkono alishiriki vipi Nd. Zaidi itakuwa bora maanake wengine hapa bado tupo kizani! Uwanja kama huu ndio huwa wa Mzee ES.
 
http://www.mkono.com/

Pitieni hiyo website Mkono amewahi kupata award nyingi tu!

Na amesimamia kesi na kama angesimamia mtu wa nje angelipwa kisai Gani! hao wanaopitia mikataba ni juzi tu tumesikia wameisha lipwa hela nyingi tu na bado hawajatoa taarifa toka 2003. Ila kwa mbali mkakuguzi amedokeza serikali inadanganywa kuhusu kiasi cha madini yanayochimbwa!

Hatusemi kuwa Mkono ni MALAIKA ILA MADA YENYEWE ILIKUWA WZI HAPA NA WATU WANAJRIBU KUIPOTOSHA!!

TUNASEMA ANZISHENI TOPI YA KUMJADILI MKONO. ILA HII YA HAWA WEZI BARRICKS IENDELEE NI KWA NINI WATU WANTATAKA KUIKWAMISHA?


MZEE ZAIDI! WEKA MAMBO WAZI KWENYE TOPIC MPYA KAMA UNAYO!

KAZI ZA KIMATAIFA ZOTE MNATAKA WAPEWE WAZUNGU TU! KAMA IMLIVYOFANYA TANESCO!

TUNATAKA KUJUA NI WAPI MKONO ALIFANYA BLUNDER YA KUSIMAMIA KESI SERIKALI IKASHINDWA NA AKALIPWA HELA!!!!!
 
Zaidi
Ubongo wako umeganda kama maziwa. Unaposema Chenge OUT unamaanisha nini? na huyo mwanasheria wako mpya ametokea wapi? Hivi msaidizi wa Chenge alikuwa nani? Kwa hiyo yeye alikuwa malaika miongoni mwa mashetani? Give me a break!
Sipendi kuiingilia sana hii issue lakini naona watu wana protect interest zao zaidi. It is all good ila msizidishe mipaka mpaka mkawa punguani.
Naona watu mnataka kuua issue ya madini kwa kuingiza issue ya NBC na TTCL. Issue ya NBC ni closed case labda kama kuna rushwa ilitembea. Ile benk ilikuwa kwenye -ve kubwa sana pamoja na kupata ruzuku toka serikalini sasa na tulikuwa tumeishiwa mbinu za kuiokoa, na tuliibinafsisha kwa faidi kwani iliuzwa kwa +ve value. Nawaakishieni kama ile benki ingekuwa bado chini ya serikali sasa hivi tungekuwa tumeisahau kama VIATU BORA.
Madini is very sensitive issue kama hatuna uwezo wa kuyachimba leo tutayachimbi baadaye lakini sasa hivi yanachimbwa kama njugu. Kwa sasa hivi mimi bado niko upande wa mkono mpaka mtu akanihakikishia kama kazi za Mkono zinaathiri uchumi wa nchi, na hata kama kuna mtu atatoa maelezo ya uhakika hiyo itakuwa topic nyingine kabisa ila hapa tunaongelea ukweli wa maneno aliyosema.
 
Mwanakijiji ni vema uvute subira kwanza ili Zaidi na ES waweke Data na hapo utakuwa na kitu cha kuuliza Mkono. Ila unaweza kupta namba yake katiba Bunge ...

Tunasubiri kwa hamu kusikia umewahoji akina mama ana Mkapa kwa ununuzi wa nyumba huko Ilala, akina Rubambe kwa kuuza mashirika at a give away price , Akina Mary Ndosi nk si wamejadiliwa sana! au hao huwezi kuwahoji!

Ninadhani watu wengi wangelifurahi zaidi anza na hao kwa sababu data zipo nyingi za IPTL nk!
 
Back
Top Bottom