UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,715
Nimetoka zangu Tarime nikapata safari kidogo ya wilaya ya Mugumu huko ujombani kwao na mama.
Pale kwa Mjomba wao walikuwa wakiabudu siku ya jumamosi(Wasabato),sasa mwanaume kwakuwa na mimi nilikuwa mwanafamilia,nikajiandaa kuanzia siku ya ijumaa ili jumamosi na mimi nizame chachi kama kawaida,nakumbuka nilikuwaga na shati langu ambalo nililipenda sana lilikuwa jekundu na pia nilikuwa nina suruali nyeusi,kwa miaka ile ukipiga Suruali nyeusi na shati jekundu ulikuwa ukitoka chicha!.
Sasa siku ya ibada kama kawaida nikawa nimeamka nikachukua pasi ya mkaa nikanyoosha pamba zangu kisha nikawa nimevaa.Niliondoka kuelekea kanisani nikiwa nimewaka hatari,sasa nilipofika chachi nikakaa viti vya katikati,kumbe kuna kunguni kadhaa walikuwa wakinitembelea kwenye ile shati,nilishindwa kuelewa wale kunguni nilitoka nao kwa anko au niliwavagaa hapo hapo chachi!.
Kuna bwana mdogo mmoja alikuwa nyuma yangu si akaanza kumwambia maza ake aliyekuwa amekaa nae nyuma yangu tena kwa sauti kubwa ambayo ilifanya kila mtu kuniangalia.
Bwana mdogo "Mama ona kunguni"
Aliendelea "Mama kunguni hawa hapa"
Mwanaume nikageuka nyuma kuangalia nikadhani kuna mtu aliyekuwa nao,ile nageuka kutazama nyuma nakuta macho ya watu kibao waliokuwa nyuma yangu wakiwemo warembo wakiwa wananitazama,kujitazama mabegani na kwenye kola ya shati nakuta wadudu kadhaa wanatembea kwa madaha kama mimi ndiye ninaye wafuga!.
Aisee niliona aibu na dogo nae akawa anazidi kunizodoa kwamba nina kunguni.Nilipoondoka Mugumu sikuwahi kurudi hadi leo hii.
Niliamua kunyanyuka wakati ibada inaendelea nikatoka nje lakini nilikuwa naona watu wanacheka kinafiki,kiukweli ile hali ilinichukiza sana hadi kulichukia kanisa.
wale kunguni waliniaibisha sana siku hiyo.
Pale kwa Mjomba wao walikuwa wakiabudu siku ya jumamosi(Wasabato),sasa mwanaume kwakuwa na mimi nilikuwa mwanafamilia,nikajiandaa kuanzia siku ya ijumaa ili jumamosi na mimi nizame chachi kama kawaida,nakumbuka nilikuwaga na shati langu ambalo nililipenda sana lilikuwa jekundu na pia nilikuwa nina suruali nyeusi,kwa miaka ile ukipiga Suruali nyeusi na shati jekundu ulikuwa ukitoka chicha!.
Sasa siku ya ibada kama kawaida nikawa nimeamka nikachukua pasi ya mkaa nikanyoosha pamba zangu kisha nikawa nimevaa.Niliondoka kuelekea kanisani nikiwa nimewaka hatari,sasa nilipofika chachi nikakaa viti vya katikati,kumbe kuna kunguni kadhaa walikuwa wakinitembelea kwenye ile shati,nilishindwa kuelewa wale kunguni nilitoka nao kwa anko au niliwavagaa hapo hapo chachi!.
Kuna bwana mdogo mmoja alikuwa nyuma yangu si akaanza kumwambia maza ake aliyekuwa amekaa nae nyuma yangu tena kwa sauti kubwa ambayo ilifanya kila mtu kuniangalia.
Bwana mdogo "Mama ona kunguni"
Aliendelea "Mama kunguni hawa hapa"
Mwanaume nikageuka nyuma kuangalia nikadhani kuna mtu aliyekuwa nao,ile nageuka kutazama nyuma nakuta macho ya watu kibao waliokuwa nyuma yangu wakiwemo warembo wakiwa wananitazama,kujitazama mabegani na kwenye kola ya shati nakuta wadudu kadhaa wanatembea kwa madaha kama mimi ndiye ninaye wafuga!.
Aisee niliona aibu na dogo nae akawa anazidi kunizodoa kwamba nina kunguni.Nilipoondoka Mugumu sikuwahi kurudi hadi leo hii.
Niliamua kunyanyuka wakati ibada inaendelea nikatoka nje lakini nilikuwa naona watu wanacheka kinafiki,kiukweli ile hali ilinichukiza sana hadi kulichukia kanisa.
wale kunguni waliniaibisha sana siku hiyo.