Ni Afrika kwa sababu ya Uvivu hata namna yetu ya Kukaguana ni ya hovyo pia. Ziara za kushtukiza ni Usanii

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,508
23,710
Huwa najiuliza hizi ziara za kushtukiza lengo lake huwa ni kugundua nini? Unaweza shtukiza shambani kujua kama uliowapa kazi ya kulima wanalima au wamelala chini ya vivuli.

Kinyume na hapo dunia ya leo haina wavivu wa namna hiyo au wafujaji wa namna hiyo, ina watu ambao wapo kazini lakini si efficient au ni wezi. Hawa huwezi wagundua kwa kushtukiza kuwa ukienda kwa kunyata utamkuta amebeba container analificha nyuma ya ofisi.

Au ukienda Hosp utakuta Dr. Amelala ofisini wagonjwa wapo kwenye mstari. Hapo unamshtukiza. Kwa level ya Rais mi huwa sioni wanachoshtukiza katika ziara zao. Msafara wa Rais ni mkubwa sana.

Lakini pia Rais ana mikono mirefu anaweza fanya uchunguzi wake bila kwenda kwa kunyata sehemu. Kwenda sehemu na kuuliza maswali kwa ukali, kufoka na kutoa macho haioneshi kuwa hapo Rais umefanya kazi kubwa sana.

Tuacheni usanii wanasiasa hasa wa Afrika. Tufikie hatua mtuheshimu na sisi Wananchi wenu. Kwa nini kila wakati mnatuona kama ni watoto wadogo sana? Please tuheshimiane. Usanii hautusaidii katika maendeleo.
 
Hakuna ziara za kustukiza kwa kiongozi mkubwa...

Sababu taarifa lazima zifike eneo husika kwa sababu za ki-usalama...




Cc: mahondaw
 
Hakuna ziara za kustukiza kwa kiongozi mkubwa...

Sababu taarifa lazima zifike eneo husika kwa sababu za ki-usalama...




Cc: mahondaw
Zipo na zimefanyika awamu hii hii ya5!
Watu wameduwazwa na 'ujio' kisha wakakutwa na mapungufu 'live' ambayo wangelitonywa wangeliweza kufukia mashimo chap kwa haraka.

Mambo ya kiusalama unayoyasema, 'vanguard' huwa ishanusanusa tayari na kujiridhisha kisha kuruhusu mheshimiwa 'kuvamia' kiulaini kabisa.

Zamani ziara zilikuwa ni za 'kuku' kuvunja mifupa na vicheko tele maofisini kwa wakaguliwa.

Lakini siku hizi staff na wakurugenzi wao wakisikia ziara iliyowalenga, basi huanza kuingia makanisani na misikitini kuswali kumuomba Mungu ili aidha ziara tajwa iahirishwe ama ikifanyika basi Mola awaepushilie mbali mabalaa ya kuwajibishwa.
 
Hv kwa msafara wa Rais kuna mtu atashindwa kuutambua? Kwanza hata ulinzi wa siku ya tukio ni tofauti kabis na siku zingine
 
Hv kwa msafara wa Rais kuna mtu atashindwa kuutambua? Kwanza hata ulinzi wa siku ya tukio ni tofauti kabis na siku zingine
Sasa mkuu ukiuona huo msafara unaingia ghafla kwenye 'compound' yako halafu unafanyaje?

Rejea ziara za kushitukiza za Nyerere international airport kukutwa mashine za kuditect mizigo hazifanyi kazi, haya, ziara ya magereza Ukonga na kufukua madudu ya sare na hatimaye jenerali wa magereza kufukuzika, unakumbuka?

Hizo ni kwa uchache, lakini zipo nyingi sana kafanya na zimekuwa na impact chanya.

Unaposhitukizwa hata kwa ugeni wa kawaida, hukutwa na sura halisi ila ukipewa taarifa, utajibaraguza kujiweka sawa.
 
Sasa mkuu ukiuona huo msafara unaingia ghafla kwenye 'compound' yako halafu unafanyaje?

Rejea ziara za kushitukiza za Nyerere international airport kukutwa mashine za kuditect mizigo hazifanyi kazi, haya, ziara ya magereza Ukonga na kufukua madudu ya sare na hatimaye jenerali wa magereza kufukuzika, unakumbuka?

Hizo ni kwa uchache, lakini zipo nyingi sana kafanya na zimekuwa na impact chanya.

Unaposhitukizwa hata kwa ugeni wa kawaida, hukutwa na sura halisi ila ukipewa taarifa, utajibaraguza kujiweka sawa.
Sawa
 
Wengi Walio kuwa Wezi na majambazi siku hizi wame jiajiri kwenye boda boda na bajaji pamoja na kubet. Walio kuwa Vibaka mitaani ndo usiseme sikuhiz wana bet balaa.
 
Back
Top Bottom