Alex Fredrick
JF-Expert Member
- Jun 21, 2016
- 680
- 1,338
Pamoja na dhamira njema ya Mh Rais Magufuli kuwekeza Bajeti kubwa kwenye Sekta ya Afya lakini bado kuna baadhi ya watendaji wanamuangusha Rais
Kwenye vifurushi vya Bima ya afya walivyonavyo NHIF kipo kifurushi cha mtoto afya ambacho watoto chini ya miaka 18 wanalipia 50.400 tu kwa mwaka
Ilikuwa ukilipia inachukua mwezi mmoja kuweza kupata Kadi ya Matibabu,
Sasa tunaona utaratibu umebadilika kutoka mwezi mmoja mpaka miezi mitatu kitu ambacho kimeleta usumbufu kwa Wananchi
Yaani mtoto amezaliwa leo inachukua miezi mitatu ndo aje apate Kadi ya Matibabu kwahiyo ikitokea ameugua kabla ya muda huo inakuwa shida na hasa kama familia haina pesa
Rai yangu kwa Waziri wa afya na Bodi nzima ya NHIF kushughulikia hili haraka na sio lazima kila kitu mpaka aje Mh Rais kutengua
Watoto ni Taifa la kesho na lazima tuonyeshe UTU kwa kuwalinda hasa wanapougua
Ni matumaini yangu NHIF watarudisha ule utaratibu wa zamani wa mwezi mmoja tu na sio huu wa miezi mitatu
Alex Fredrick
Kwenye vifurushi vya Bima ya afya walivyonavyo NHIF kipo kifurushi cha mtoto afya ambacho watoto chini ya miaka 18 wanalipia 50.400 tu kwa mwaka
Ilikuwa ukilipia inachukua mwezi mmoja kuweza kupata Kadi ya Matibabu,
Sasa tunaona utaratibu umebadilika kutoka mwezi mmoja mpaka miezi mitatu kitu ambacho kimeleta usumbufu kwa Wananchi
Yaani mtoto amezaliwa leo inachukua miezi mitatu ndo aje apate Kadi ya Matibabu kwahiyo ikitokea ameugua kabla ya muda huo inakuwa shida na hasa kama familia haina pesa
Rai yangu kwa Waziri wa afya na Bodi nzima ya NHIF kushughulikia hili haraka na sio lazima kila kitu mpaka aje Mh Rais kutengua
Watoto ni Taifa la kesho na lazima tuonyeshe UTU kwa kuwalinda hasa wanapougua
Ni matumaini yangu NHIF watarudisha ule utaratibu wa zamani wa mwezi mmoja tu na sio huu wa miezi mitatu
Alex Fredrick