NHIF matatani, kilio cha wamiliki wa hospitali binafsi kukatwa mabilioni ya fedha chaibuka

Nyanswe Nsame

Senior Member
Jul 9, 2019
158
175
WAMILIKI wa hospitali na zahanati binafsi mkoani Mwanza wameingia katika mvutano mkubwa na mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) kuhusu makato ya fedha wanazokatwa kila mwezi zinazotokana na matibabu wanayotoa kwa wateja wa mfuko huo.

NHIF mkoa wa Mwanza inatuhumiwa kuendesha utaratibu feki wa makato ya fedha kwa hospitali na zahanati binafsi mkoa wa Mwanza na kusababisha hasara na kilio kikubwa kwa wamiliki wa hospitali hizo.

Kilio cha wamiliki wa hospitali hizo kinatokana na NHIF kufanya makato ya fedha zinazotokana na matibabu yaliyofanywa na hospitali hizo ( mfano hospitali A imefanya matibabu ya Tsh. Milioni 70 kwa mwezi lakini NHIF inakata Milioni 20).

Pia NHF inalalamikiwa na wadau hao wa afya mkoani mwanza kufanya makato hayo wanayodai sio halali.

NHF mkoa wa Mwanza imekuwa na utaratibu ambao sio rasmi wa kukata fedha bila utaratibu kwa kisingizio kuwa hospitali hizo zimetoa matibabu kwa wagonjwa waliopo kwenye mfuko huo bila utaratibu (yaani wamefanya vipimo kwa mgonjwa ambavyo havikutakiwa kufanyika).

Mmiliki wa zahanati moja jijini Mwanza (jina limehifadhiwa) amesema NHIF wamekuwa na utaratibu huo ambao unawaumiza wamiliki wa zahanati na hospitali binafsi.

Amesema NHIF chini ya meneja wa mkoa wa Mwanza, JARALTH MUSHASHU kwa kipindi cha miaka miwili yaani 2019 na 2020 wamezidi kuwanyanyasa watoa huduma ya afya wa hospitali binafsi jambo ambalo limekuwa ni kilio kwao.

Amemtaja msimamizi wa kitengo cha malipo DK. JULIETH MUHANIKA ambaye ndiye kikwazo na anayeongoza mchezo huo ambao umesababisha wamiliki hao kushindwa kutoa huduma stahiki kwa wagonjwa.

Amesema.Dk JULIETH anafanya hivyo kwa lengo la kuwatisha wamiliki wa hospitali na zahanati kutengeneza mazingira ya "Rushwa" jambo ambalo wameona hawewezi kutoa fedha kwa kuwa wanachokidai ni haki yao.

Mmiliki huyo ameeleza kuwa, ukipeleka malipo ya milioni 17 NHIF wanakata kiasi cha milioni mbili au zaidi fedha hizo, jambo ambalo amedai limeonesha kuna njia inayotumika isiyo halali kwao.

"Kwa mfano mimi kwa mwezi uliopita kunaa fedha malipo niliandika ili nilipwe na NHIF cha kushangaza kiasi cha fedha ambazo nimeandika nikashangaa nakatwa fedha bila kupewa ufafanuzi kwanini nimekatwa.

"Unaweza kupeleka fomu 1000 za wateja waliotibiwa hapa zikakatwa fomu 200, sasa kwa hali hiyo tayari wamenipa hasara na kila nikijaribu kupeleka malalamiko yangu sipewi majibu.

"Kuna makato ambayo yanafanyika ambayo hayaeleki, mimi kwa miaka hii miwili kwa hesabu za haraka nimekatwa zaidi ya milioni 40 na hiyo ni hesabu ndogo ambayo nimepiga ni zaidi ya hiyo nikikaa nikapiga vizuri.

"Ukipiga hesabu za haraka haraka kwa miaka hii miwili mitatu ambayo makato yamekuwa makubwa, hospitali zote makato yaliofanyika ni mabilioni ya fedha kwa kuwa kuna hospitali moja mwezi ulioisha wamekatwa kama Tsh. milioni 100.

"Zamani kulikuwa na makato ya kawaida sana ambayo tulikuwa tunayavumilia lakini kwa miaka hii tumeona tuanze kuamka na kulalamika kwa sababu imekuwa ni kikwazo kikuwa kwetu licha malalamiko yetu hayafanyiwi kazi.

"Shida iliyopo wanataka tuwafuate tuzungumze nao, wanachokifanya ni ktengeneza mazingira ya rushwa kwetu, sasa hatuwezi kutoa rushwa kwa mtu wakati tunachokipa ni kidogo sana.

"Pia utaratibu huu wa makato unaofanyika ni kwa mkoa wa Mwanza pekee na mikoa mingine nimejaribu kuzungumza nao wamesema huo utaratibu haupo," mmiliki wa zahanati jijini Mwanza.

Mmiliki huyo wa zahanati amesema, msimamizi wa kitengo cha malipo Dk. Julieth ndiye anayefanya mpango huo kwa kushirikiana na meneja wa mkoa huo ili waweze kupewa kitu kidogo.

Mmiliki huyo anasikitika na kueleza kwamba, wanakata fedha zao bila utaratibu kwa kisingizio kwamba hospitali au kituo cha afya kimefanya matibabu kwa mgonjwa kwa kufanya vipimo ambavyo sio sahihi.

"Mfano wamekuwa wakisema kwamba tumefanya vipimo kwa mgonjwa isivyo halali wakati mimi ndiye daktari ambaye nimekutana na mgonjwa na kumuangalia na kuona ni vipimo vipi anatakiwa kufanyiwa na dawa ipi nimpe lakini wao wanasema tumefanya makosa.

"Kama wana mashaka na sisi wanachotakiwa kufanya wao ni kuchukua taarifa za kila mgonjwa anayefika katika kila hospitali na kuzungumza nae kuona tulichofanya ni uongo au ni ukweli sio watu wanakaa na kukata fedha zetu bila sababu.

"Imefika mahala tunataka hata kujitoa NHIF lakini tukijitoa hatuwezi kupata wagonjwa kwa kuwa watu wengi sasa hivi wapo NHIF maanake.

Amesema wamekuwa wajipa matumaini kuwa suala hilo litapatiwa ufumbuzi lakini mpaka sasa tatizo limeendelea kukuwa na kuzidi kuumiza wamiliki wa hospitali na zahanati binafsi.

Kwa upande wake, Mmiliki mmoja wa hospitali kubwa binafsi jijini Mwanza ambaye aligoma kutajwa jina lake, amesema NHIF mkoa wa Mwanza imekuwa ni kikwazo kwa wamiliki wa hospitali mkoani humo.

Amesema suala hilo wameisha kutana na NHIF kuzungumza nao kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita lakini mpaka sasa hakuna mabadiliko yoyote yanayoonekana.

Amesema bima zote zina matatizo lakini NHIF imekuwa "sugu" kwa kuwa wameshindwa kuonesha mwanga wa namna ambavyo wataweza kutatua tatizo hilo.

Amesema pamoja na kukata fedha zao, lakini NHIF imekuwa ikikaa miezi miwili hadi mitatu bila kuwalipa hali zao wamiliki wa hospitali na zahanati binafsi.

Ameendelea kueleza kwamba asilimia 80 au 90 ya wagonjwa wanaoenda katika hospitali hiyo ni wateja wa NHIF na kwamba kibaya zaidi wanapolipa fedha hizo lazima wanazikata.

"Unakuta unapeleka milioni 70 kwa mwezi ili ulipwe wanachokifany wanakata milioni 10 au zaidi sasa imefika mahala tumeamua kuacha kuzungumza nao.

"Hata tukipiga kelele hakuna wanachokifanya maana hawatusikilizi, yaani wao wamekaa kwa kutuvizia ukifanya kakosa kidogo tu wanakukata.

"Hili suala tulishalipeleka kwenye chama chetu cha APHFTA (Chama cha watoa huduma za afya binafsi nchini) wakatukutanisha na NHIF lakini hakuna mabadiliko ambayo yalishafanyika sasa tumeona hii imekuwa kero,"amesema mmiliki huyo wa hospitali.

Amesema kwa uhalisia makato yanayofanyika sio sahihi, na sababu za kukata kwao fedha hizo hazina mashiko kutokana na daktari ndiye aliyemuona mgonjwa na kumpa matibabu baada ya kumfanyia vipimo.

"Jamani hospitali binafsi tunateseka sana hatuna pakukimbilia, tunapojaribu kulalamika tunapewa vitisho na hii inafanyika kwa mwanza pekee kwa nini inakuwa kwetu tu, ingekuwa ni nchi nzima hapo tungesema ni ajenda ya taifa.

"Hospitali hizi binafsi lengo kubwa ni kutoa huduma bora kwa mgonjwa na sio biashara lakini tukisema tuanze kufanya biashara hatutatoa huduma kwa wagonjwa lakini wao hawalioni hilo.

Kutokana na tatizo hilo ambalo limekuwa kero kwa hospitali hizo mkoani humo, wamiliki hao wameiomba serikali kuunda tume huru kuchunguza suala hilo ili kuangalia kama makato yanayofanywa na NHIF kama ni halali na kwamba endapo ikibainika sio halali walipwe fedha zao zilizokatwa kwa kipindi chote.

Pamoja na kulipwa makato ya fedha zao, wanashinikiza watumishi hao wa umma wachukuliwe hatua kali za kisheria ili kumaliza tatizo hilo.
 
"Imefika mahala tunataka hata kujitoa NHIF lakini tukijitoa hatuwezi kupata wagonjwa kwa kuwa watu wengi sasa hivi wapo NHIF"

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

"Mitano tena!"

"Hii sio awamu ya kupata raha"
 
"Imefika mahala tunataka hata kujitoa NHIF lakini tukijitoa hatuwezi kupata wagonjwa kwa kuwa watu wengi sasa hivi wapo NHIF"

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

"Mitano tena!"

"Hii sio awamu ya kupata raha"
Watu wanaumizwa wanadhulumiwa haki yao, wewe unacheka. Matibabu kwani yanatolewa bure?
 
Wahusika washikamane kuondoa udhalimu huo.
Wamiliki wa hospital binafsi wapambanie haki yao ya msingi
 
NHIF imekua ikilalamikiwa muda sana. Sishangai sana. Na watetezi wa serikali si kila kitu mnakua mnapinga shenzi zenu. Kuna mambo hata sisi tusiokua waungaji mkono wa serikali tunaelewa vikwazo vinasababishwa na watu waliopewa dhaman kwenye hizo taasisi na sio maagizo ya serikali kuu.

Wewe Magu2016 ni kilaza sana. Hampendi kusoma habari nzima. Soma utaona malalamiko yapo Mwanza tu na si mikoa mingine. Hivyo ni dhahiri tatizo ni uongozi wa NHIF Mwanza. Lakini, wewe Magu2016 kwa namna ulivyo kilaza namba 1 umeona hapo ni Jiwe kasemwa. Vingine tumieni common sense. Jiwe atapita ila mengine lazima yaendelee.
 
Tusikimbilie kuwahukumu Nhif sababu wamiliki wa hospital wameulizia mikoa mingine wameambiwa hakuna kitu kama hicho hivyo inawezekana ni tatizo binafsi la wafanyakazi wa nhif Mwanza.
 
Kwa nini uhangaike nao NHIF,,wewe kama tabibu fuata miongozo ya tiba, wanaita STG, kutegemea hadhi ya kituo chako. Kama kuna huduma iliyo nje ya Tanzania STG,mteja/mgonjwa achangie kama anataka kupona.

Mie nilikumbana na hali hiyo kwa ndugu yangu mgonjwa,nikaambiwa hii huduma haipo NHIF,nikapiga simu kwa NHIF(maana mimi ndiye ninayechangia kila mwezi).

Nilichojibiwa nikaomba nihamie kwa Mugabe, customer care ya NHIF ni mbovu, kuna dada anaongea kunya, eti hatujakuomba uwe mwanachama. Ikabidi nilipie hivo vipimo, na mgonjwa alipata matibabu stahiki. AMEPONA.

Ni sisi wanachama tuandamane ofisi za NHIF, tujue haki yetu,waache urasimu. Madaktari bingwa wapo hadi vituo vya afya,wapanue wigo wa huduma
 
Huwa nawaangalia hospitali binafsi ninapoenda kutibiwa kwa bima. Unajaziwa fomu ila hawakupi nakala yako kama mwanachama...ukitoka wanaongeza huduma zaidi ya ulizopewa (nina ushahidi)

Kumbe na nyie mkiwakilisha madai yenu yanapigwa panga!

Pia kuna mchezo mwingine mchafu wa hospitali za umma ila ngoja niishie hapa maana "Mtanzania kila ana gene za upigaji kwenye DNA yake!
 
Jiwe baada ya kuifilisi mifuko ya jamii akaamua kuiua na kuinganisha, pia akaamua kuwanyima watu pesa zao akiwalaghai atawapa wakitimiza miaka 55 bila pesa ya usumbufu.

Sasa amekomba pesa NHIF
 
Unawakumbuka watu waliofirisika baada ya kulisha majeshi bila kulipwa kwa miaka nenda rudi? Huko ndiko NHIF inataka kuwapeleka watoa huduma hawa
 
Back
Top Bottom