Nguvu ya umma yafa kifo cha mende; BAVICHA wasarenda

THINKINGBEING

JF-Expert Member
Aug 9, 2010
2,779
1,304
Hatimaye ile nguvu ambayo umma wa waTanzania umekuwa ukiitegemea pale watawala wanapofanya ndivyo sivyo imekufa rasmi baada ya BAVICHA kubariki hilo litokee.
Falsafa ya nguvu ya umma/people's power ya CHADEMA kwa muda mrefu imetumika kuongoza harakati ambazo matokeo yake hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.

Kwa bahati mbaya kiongozi mpya wa CHADEMA ndugu Lowassa amesema hataki kuona falsafa hiyo pendwa ikiendelea kufanya kazi.
Akitoa muelekeo huo mpya wa chama Lowassa alisema;
"Uanaharakati ni nini, ni ile unagombea jambo, unafanya maandamano, unasukuma hiki, unasukuma hiki, unaregista hiki, kupiga mistari kwenye ukuta, unaweka matangazo, na nini, halafu mnazuia serikali isifanye kazi yake, maandamano kila siku, huo ndiyo uanaharakati".

Baada ya kuuelezea uanaharakati alisema CHADEMA haitaendelea kufanya hayo tena.
Baada ya tamko la Lowassa mwenyekiti wa CHADEMA mh.Mbowe aliibuka na kuwakataza BAVICHA wasiende Dodoma kufanya harakati waliyokusudia.

Leo BAVICHA wamesema rasmi wametii kauli ya Mbowe japo hawakubaliani nayo na kudai ni itifaki imewalazimisha kukubali.Kitendo hiki kinatosha kusema ile falsafa ya PIPOZ POWER kwaheri.
 
Ulivyonza nikama umesikitika lakini ulivyomaliza nikama umefurahi, hujaeleweka subiri teuzi kama Mrema kapata, JPM bado anazo teuzi utapata tu.
 
I have tried to read yout thread.Apparently, I found no "substance".This is rubbish.It is supposed to be in dustibin.
 
Hatimaye ile nguvu ambayo umma wa waTanzania umekuwaku ukiitegemea pale watawala wanapofanya ndivyo sivyo imekufa rasmi baada ya BAVICHA kubariki hilo litokee.
Falsafa ya nguvu ya umma/people's power ya CHADEMA kwa muda mrefu imetumika kuongoza harakati ambazo matokeo yake hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.
Kwa bahati mbaya kiongozi mpya wa CHADEMA ndugu Lowassa amesema hataki kuona falsafa hiyo pendwa ikiendelea kufanya kazi.
Akitoa muelekeo huo mpya wa chama Lowassa alisema;
"Uanaharakati ni nini, ni ile unagombea jambo, unafanya maandamano, unasukuma hiki, unasukuma hiki, unaregista hiki, kupiga mistari kwenye ukuta, unaweka matangazo, na nini, halafu mnazuia serikali isifanye kazi yake, maandamano kila siku, huo ndiyo uanaharakati".
Baada ya kuuelezea uanaharakati alisema CHADEMA haitaendelea kufanya hayo tena.
Baada ya tamko la Lowassa mwenyekiti wa CHADEMA mh.Mbowe aliibuka na kuwakataza BAVICHA wasiende Dodoma kufanya harakati waliyokusudia.
Leo BAVICHA wamesema rasmi wametii kauli ya Mbowe japo hawakubaliani nayo na kudai ni itifaki imewalazimisha kukubali.Kitendo hiki kinatosha kusema ile falsafa ya PIPOZ POWER kwaheri.

Kwa taarifa yako mleta mada hiyo ni mbinu ya kisasa wametumia Bavicha katika kuonyesha jinsi mkuu wa nchi anavyofanya upendeleao, na kufanya mambo fulanifulani kinyume na sheria za nchi. Katika mbinu hiyo kile kilichokuwa kikilalamikiwa na wengi kwamba jeshi la polisi linatumika na wanasiasa wa chama tawala limedhihirika na lile katazo la kuzuia mikutano ya kisiasa limefanyika kwa hila zilezile za viongozi wengi wa kiafrika dhidi ya demokrasia. Jeshi letu limekuwa likitumwa na viongozi wa ccm kuhujumu vyama vya upinzani na demokrasia kwa ujumla kwa visingizio vya kitoto eti intelijensia. Sasa wananchi wote wamegundua kwamba rais anafanya kazi kwa kujali itikadi na sio kama anavyohubiri majukwaani. Kwa mazingira yalivyo hakuna ambaye angeenda kwani polisi wangeumiza watu wengi sana maana sasa hivi vyeo vinatokea kwa kunyanyasa raia ili mkuu afurahi. Ila kiukweli tumegundua rais anafanya kazi kwa kukibeba chama chake dhidi ya vyama vingine na wala sio kwa maslahi ya taifa kama ambavyo anahubiri mdomoni.
 
Hatimaye ile nguvu ambayo umma wa waTanzania umekuwaku ukiitegemea pale watawala wanapofanya ndivyo sivyo imekufa rasmi baada ya BAVICHA kubariki hilo litokee.
Falsafa ya nguvu ya umma/people's power ya CHADEMA kwa muda mrefu imetumika kuongoza harakati ambazo matokeo yake hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.
Kwa bahati mbaya kiongozi mpya wa CHADEMA ndugu Lowassa amesema hataki kuona falsafa hiyo pendwa ikiendelea kufanya kazi.
Akitoa muelekeo huo mpya wa chama Lowassa alisema;
"Uanaharakati ni nini, ni ile unagombea jambo, unafanya maandamano, unasukuma hiki, unasukuma hiki, unaregista hiki, kupiga mistari kwenye ukuta, unaweka matangazo, na nini, halafu mnazuia serikali isifanye kazi yake, maandamano kila siku, huo ndiyo uanaharakati".
Baada ya kuuelezea uanaharakati alisema CHADEMA haitaendelea kufanya hayo tena.
Baada ya tamko la Lowassa mwenyekiti wa CHADEMA mh.Mbowe aliibuka na kuwakataza BAVICHA wasiende Dodoma kufanya harakati waliyokusudia.
Leo BAVICHA wamesema rasmi wametii kauli ya Mbowe japo hawakubaliani nayo na kudai ni itifaki imewalazimisha kukubali.Kitendo hiki kinatosha kusema ile falsafa ya PIPOZ POWER kwaheri.
Sasa kama Wapo na fisadi hiyo pipoz pawa wataipataje?
 
Nimesikitishwa sana na kauli ya mwenyekiti wa BAVICHA kwamba hawajakubaliana na maamuzi ya Mbowe ila wanalazimika kuyaheshimu kwa sababu za kiitifaki.
 
walikuwa wanajifurahisha wawakilishi wao wapate namna ya kurudi nyumbani baada ya kwenda kula ubuyu,zabibu& toilet paper na kurudi jimboni! ilikuwa aibu wasingerudi hivi hivi huo ulikuwa wimbo wakuwarudisha
 
Hiv kweli wanajamvi bavicha hoja yao itakuwa ni demokirasia mpaka pale magufuli atakapomaliza muda wake??

Kwa sababu kila kukicha awaji na hoja mpya kukemea ufisadi??

Hoja za kuitetea jamii hakuna??

Mfano tuliona swala la VAT lilivyo leta mshike mshike hakuna matamko yaliyoletwa hapa kuweza kutafuta suluhu ya kuiondoa hiyo VAT??

Kila siku kupanga mambo yasiyo na masilai Kwa taifa ???

Hivi mwananchi anayeishi mtama ,kondoa,ngala,bujola lunzewe hayo matamko yanamsadia nini??
Lazima tuwa wakweli !!!

Hivi kukalia hoja moja kuandaa press conference kwa pesa za uma tunazowapa kupitia Luzuku mkaja kuongelea swala moja tu la democrasia hivi hao wananchi mnawasaidia nini ??

Kila siku matamko matamko yasiyo na faida kwa taifa yanini??

Lazima Kama nchi tufike sehemu tukubali kwamba uchaguzi umepita tuongelee mambo yenye faida kwa watanzania wote!!!

Kuna kipindi wanafunzi wa chou kikuu walicheleweshwa kupewa pesa lakini sikuwaona bavicha wakija kuwatetea!!!

Kwanini liwe swala moja tu la democrasia??

Hivi kweli bado mna mawazo kwamba Africa inaweza kukombolewa kwa democrasia tu ??

Wananchi watapata maji kwa njia ya democrasia???

Wamama watapata vitanda hospitali kwa njia ya democrasia??

Barabara zitajengwa na democrasia?

Kiukweli bavicha mumepotea sana hakuna haja ya kupewa posho!!!
Mkumbuke posho mnazopewa ni pesa za umma kama hamleti hoja za kuisaidia nchi afadhari mjiuzuru!!

Tokeni mkemee ufisadi!!
Tokeni mtetee watu wapate maji na umeme vijijini
Tokeni mtetee masilai ya wafugaji na wakulima
Tokeni mtetee wanyonge kupitia maswala ya VAT
Tokeni mtuonyeshe vyanzo vipya vya mapato kuliko hivi vinavyowakamua wanyonge
Tokeni mtetee wanafunzi wapate mikopo vyuo vikuu kwa wakati!!
Tokeni na kuamasisha upatikanaji wa madawati kwa 100%
Mbona hatuwaoni tena ???.

Kwanini amjitofautishi na Uvccm?? Mnatakiwa kujitofautiaha na Uvccm!!

Mimi sipendi unafiki lakini matamko yenu yote ambayo mumeyatoa hayatekelezeki!!

Na hamuwaezi kila siku mnatoa matamko ambaye hayana afya kwa taifa taifa likawasikiliza!!!
Bavicha mmepoteza dila Uo ndo ukweli!!!
 
Unaonekana wewe ni mwanachama wa chama cha mapinduzi, sitegemei wewe kuikibali bavicha. Endelea na imani yako kwa chama chako. Acha bavicha nao wafanye majukumu yao.
Haaa mkuu Mimi sina chama ila kwa haya yanayoendelea ni bora hata wangekaa kimya
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom