Nguvu ya Umma ilivyookoa majimbo, naomba busara itumike Nchi ibaki salama

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
9,042
32,673
Mwaka 2010 Kama sikosei Wapinzani hasa CHADEMA walidhulumiwa majimbo mengi Sana ya ubunge na pengine udiwani.

Lakini sehemu zote ambazo nguvu ya Umma ilitumika majimbo yaliokolewa
Nitayataja ninayoyakumbuka:

Nyamagana - bila nguvu ya Umma Ezekia Wenje asingekua mbunge

Arusha Mjini- bila nguvu ya Umma God bless Lema asingetangazwa Mshindi.

Ubungo - bila nguvu ya Umma Myika asingetangazwa Mshindi.

Mbeya - bila nguvu ya Umma Sugu asingetangazwa Mshindi.

Iringa Mjini - bila nguvu ya Umma Msigwa asingetangazwa Mshindi.

Kwa uchache na ninayoyakumbuka Ni hayo, Kama Kuna mtu anakumbuka zaidi atuwekee hapa.

Mfano mdogo tu Nyamagana, watu walishaanza kuharibu Mali za serikali ikabidi kwa Busara za RPC wa Mwanza amuamuru mkurugenzi wa Uchaguzi Mwanza kwa kumpa saa moja awe ametangaza matokeo saa moja ikipita ataondoa Polisi wake.

Mkurugenzi kwa kuona hivyo akamtangaza Mshindi halali Bwana Ezekia Wenje wa CHADEMA.
Sehemu nyingine vijana walishaingia mitaani na happy ikawa tete.

Wito wangu kwa watawala na Watu wa Tume,
Tunakwenda kuingia kwenye Uchaguzi Mkuu wenye tensheni kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea hapa nchini,
Wagombea wakubwa wawili Wana tabia za kufanana,
Mmoja Ana nguvu ya dola na hakubali kushidwa,na mwingine Ana nguvu ya Umma na hakubali kushindwa,

Hivyo nawaomba watu wa Tume tumieni busara kumtangaza Mshindi alieshinda kihali kwani mtalindwa na Dunia,kuliko kushinikizwa kumtangaza alieshindwa kihalali na nguvu ya Umma ikachukua nafasi yake na dola ikaingilia matokeo yake Ni kuharibu.Na mkishaharibu dunia itawaadhibu.

Enyi watu wa Tume wekeni Haki na mazingira mazuri ya Uchaguzi
Na kutenda Hali,kinyume na hivyo Ni nyinyi wenyewe mtalazimisha matumizi ya nguvu ya Umma,

Msilazimishe matumizi ya nguvu ya Umma kwa kuonea upande mmoja
Ninavyoona safari hi nguvu ya Umma inaenda kuwa nchi nzima
na sio majimbo machache.

Napenda
Amani na ninaipenda Tanzania,Sina mahali pengine pa kuishi zaidi ya Tanzania.
 
Just asserting the records straight that-indeed the deceased was in fact a one term president.
Does that supposed to mean that, during all those previous months right after the end of his first term our country had no president until recent? Ujinga ni mzigo.
 
Does that supposed to mean that, during all those previous months right after the end of his first term our country had no president until recent? Ujinga ni mzigo.
Kama lugha tu changamoto ndio uite wengine wajinga?

CCM bhana
 
Kwa space ya siku 120? It's below 3% ya full presidential term ya siku 1,825 sasa unasema ni two terms???

Msitafute justification the guy passed away having served one term only....
Are you a mathematician? I presume wewe ni ngwini tu!
 
Kama lugha tu changamoto ndio uite wengine wajinga?

CCM bhana
That's a very tiny error affiliated with typing, have you got the message anyway? Don't shoot the messenger with such creepy little thing. Get straight to the point , to make it clear, I'm simply Tanzanian and not politician of any kind.

However, it seems like CCM did you something you just can't get over it, so don't put that blame on me, got nothing to do with it.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom