Nguvu ya saikolojia

Hata hospital wagonjwa wengi matatizo yao yameanzia vichwani..mwisho wa siku namna unavyowaza inaathiri mpaka mwili..lakini kimsingi hawaumwi kihivyo..japo wapo wagonjwa serious kwahiyo mind na body ndio kila kitu,vina uhusiano mkubwa sana!
 
Nakumbuka wakati wa utoto nilipokuwa sitaki kwenda shule basi usiku najifanya naumwa najilaza na kuvuta hisia za kujihisi naumwa,basi baada ya muda mwili unakuwa wamoto na ukinitizama unaona kabisa naumwa na panadol napewa nameza.

Ukiamini jambo kwa dhati linakuwa nyinyi watu wa dini mnaiita imani
Na hapo ndio utagundua there is no god at all
 
Wachawi na wasiojulikana hawataelewa chochote kabisa.

Hata hii comment yangu hawataielewa kamwe.
 
Na Dr.Christopher Cyrilo

Siku moja, mtu mmoja alitoka nyumbani kuelekea hospitalini kwa sababau ya maumivu makali aliyokuwa nayo mkono wa kulia.

Alipokutana na daktari, alimueleza namna mkono ule unavyouma hadi kushindwa kufanya shughuli zake za kila siku.
Daktari alipougusa, mtu yule alitoa sauti kubwa inayoashiria maumivu makali.

Daktari, akahisi kuwapo kwa tatizo kubwa zaidi ya maumivu yale. Mtu yule hakuwa amepata ajali, hakuwa amepigwa, hakuwa ameanguka. Hakukuwa na jibu la sababu ya maumivu yake kutoka katika maelezo yake. Uchunguzi wa papo kwa papo aliofanya daktari nao haukutoa majibu yoyote. Kwahiyo tegemeo pekee alilobaki nalo daktari ni vipimo.
Hata hivyo vipimo havikuonesha tatizo lolote.

Daktari alibaki na kitendawili kigumu akilini mwake. Aliwaza kama kweli mtu huyo anaugua au anajifanya kuugua. Lakini kwa tahadhari kubwa, aliendelea kuonesha kujali. Ndipo alipouliza zaidi na zaidi na kugundua kuwa yule jamaa alikuwa na matatizo makubwa kwenye ndoa yake. Matatizo ya miaka kadhaa hivi.

Nyumbani kwake hakukuwa na amani hata kidogo, mkewe na watoto wake walikuwa wamemtenga baba yao, kutokana na makosa aliyotenda huko nyuma. Pia, wazazi na baadhi ya ndugu wa huyo jamaa walifariki kwa pamoja kwenye ajali ya gari la familia. Kwa matukio hayo na kutosamehewa na mke na watoto, yule jamaa aliathirika kisaikolojia kiasi cha kuwa na dalili za maradhi ya akili.

Mojawapo ya dalili hizo ni hiyo ya kuhisi maumivu yasiyokuwepo.
Kwa kuwa ubongo ndio unaotafsiri maumivu, bila ubongo mtu hawezi kuhisi maumivu. Na endapo kuna athari katika sehemu ya ubongo inayotafsiri maumivu ya sehemu fulani ya mwili, basi kuna uwezekano mtu kupata maumivu sehemu hiyo ya mwili hata kama hakuna sababu katika sehemu husika, lakini kama kuna tatizo la kiakili/kwenye ubongo.

Dalili za aina hii hutokea kwa nadra. Mara nyingi huanza kwa hisia za kutambaliwa na mdudu mwilini wakati hakuna kitu (Tactile Hallucinations); kisha huweza kuendelea zaidi na kufikia kupata maumivu, kwa sababu za kisaikolojia.

Yule daktari alipogundua uwezekano wa maradhi ya akili kwa mtu yule, aliamua kubadili mbinu za kumsaidia. Alimpa ushauri, na uhakika wa kupona, na dawa za maumivu. Kisha akamualika nyumbani kwake kwa ajili ya chakula cha jioni.

Siku fulani jioni, yule jamaa alifika nyumbani kwa daktari wake. Daktari alimkaribisha na kuanza kupiga naye stori bila kumuuliza hali ya mkono wake. Stori nyingi zilikuwa za kuchekesha au kufurahisha. Baada ya muda, Daktari alimkaribisha yule jamaa ndani kwa ajili ya chakula, huku stori zikiendelea.

Kwa makusudi kabisa, Daktari alimkabidhi yule jamaa birika la chai, upande wake wa kulia wa yule jamaa, naye alipokea kwa mkono wa kulia (uliokuwa na maumivu) na kuanza kumimina chai kwenye kikombe. Wakati jamaa akiendelea kumimina chai, kulikuwa na ukimya, lakini daktari alikuwa akitazama ule mkono kwa mshangao kidogo.

Yule jamaa alipogundua daktari anautazama mkono wake, mara moja mkono ukaanza kuuma, akaliachia lile birika la chai na kuanza kupiga kelele za maumivu.

Tendo hilo liliweza kumpatia majibu ya uhakika daktari, kwamba maumivu yale yalisababishwa na maradhi ya kisaikolojia.

Saikolojia ni elimu pana sana. Ndio daraja linalounganisha imani na sayansi, na ndio ukuta unaotenganisha mambo hayo mawili.
Tazama wagonjwa wa akili wanaozurura barabarani na kula takataka chafu lakini wanaendelea kuishi. Kula wewe unayejua kuwa ni uchafu uone kitakachotokea.

Umewahi kubanwa na tumbo la kuendesha? Fikiria unavyokaribia chooni na hali unayoisikia, kadiri unavyokikaribia choo, hali inakuwa mbaya zaidi. Lakini ukikuta kuna mtu bado unaweza kuvumilia, huyo mtu akitoka hali inaanza kuwa mbaya zaidi wakati unaingia kujisaidia. Ukichelewa tu unachafua nguo.

Wamasai na jamii nyingine wanaishi na kupishana na simba porini, ni saikolojia.
Mtoto mdogo anayetambaa anacheza na nyoka, ni saikolojia.

Saikolojia inaathiri sana maisha yetu, uchumi wetu, afya zetu na mahusiano yetu.
Cha msingi ni kujifunza kwamba; kuna nguvu kubwa katika ubongo wa binadamu. Nguvu hiyo ni kubwa kuliko mbingu na ardhi kwa pamoja.

Ndio nguvu inayobadili mambo madogo kuwa makubwa na makubwa kuwa madogo. Ndio nguvu inayofanya ya muhimu yasiwe muhimu na yasio muhimu yawe na umuhimu mkubwa.
Itaendelea.

Christopher Cyrilo
Aina hii ya maumivu ambayo hayaelezeki kitabibu bali kisaikolojia yanatokana na tatizo lijulikanalo SOMATOFORM DISORDER.
 
Huwa nasikia hata mtu kabla hajapata majibu ya vipimo vya HIV nakuonekana +huwa na furaha na afya tele ila tu akipima nakukutwa + akapewa majibu baaasi ndio mwisho wake na afya huanza kudorola yaani.
 
Asante kwa mada nzuri yenye kufikirisha, nadhani kichwa cha habari hii kilipaswa kuwa 'Nguvu ya Akili'
 
Sawia kabisa, hata mi nishawahi kuwa mhanga wa hili. Kuna kipindi niliugua msongo wa mawazo na ukazidi nikawa mtu wa kuwaza kuwa na huzuni na hofu masaa yote, matokeo yake nlipata physical symptoms- kuna kipindi nilikuwa naugua tumbo na kuharisha juu, kuna kipindi nilikuwa naugua meno.
Kama ni tumbo linauma hasa na kuharisha, nashukuru Mungu nilikuwa mwepesi wa kutambua ni kutokana na msongo ndo maana nimeugua namna hiyo maana tayari nilikuwa nauelewa na matokeo ya stress katika mwili hivyo sikunywa dawa bali nilijaribu kujisahaulisha na kufanya kama ninafuraha basi napona naacha kuharisha ila yakirudi tu kichwani kazi ipo au yakiondoka maswahiba ya tumbo yanakuja meno, meno ndo ilikuwa kiboko nilikuwa naskia maumivu makali haswa nashindwa hata kufanya kazi yoyote nalala tu, akili ikitulia nikawa na furaha meno yanapona ila mawazo yakirudi yanaanza tena. Bahati nzuri nikaja nikapona msongo wa mawazo nikajifunza kuicontrol akili na kuwa na furaha, nikapona sikupata tena hayo maumivu ya mwili
 
Fact sana somo la Saikolojia ni pana sana ukilifatilia kwa undani unatokea kwenye ule unaousikiaga unaitwa ulimwengu wa Roho uko ndo miujiza inakotokaga
 
Na Dr.Christopher Cyrilo

Siku moja, mtu mmoja alitoka nyumbani kuelekea hospitalini kwa sababau ya maumivu makali aliyokuwa nayo mkono wa kulia.

Alipokutana na daktari, alimueleza namna mkono ule unavyouma hadi kushindwa kufanya shughuli zake za kila siku.
Daktari alipougusa, mtu yule alitoa sauti kubwa inayoashiria maumivu makali.

Daktari, akahisi kuwapo kwa tatizo kubwa zaidi ya maumivu yale. Mtu yule hakuwa amepata ajali, hakuwa amepigwa, hakuwa ameanguka. Hakukuwa na jibu la sababu ya maumivu yake kutoka katika maelezo yake. Uchunguzi wa papo kwa papo aliofanya daktari nao haukutoa majibu yoyote. Kwahiyo tegemeo pekee alilobaki nalo daktari ni vipimo.
Hata hivyo vipimo havikuonesha tatizo lolote.

Daktari alibaki na kitendawili kigumu akilini mwake. Aliwaza kama kweli mtu huyo anaugua au anajifanya kuugua. Lakini kwa tahadhari kubwa, aliendelea kuonesha kujali. Ndipo alipouliza zaidi na zaidi na kugundua kuwa yule jamaa alikuwa na matatizo makubwa kwenye ndoa yake. Matatizo ya miaka kadhaa hivi.

Nyumbani kwake hakukuwa na amani hata kidogo, mkewe na watoto wake walikuwa wamemtenga baba yao, kutokana na makosa aliyotenda huko nyuma. Pia, wazazi na baadhi ya ndugu wa huyo jamaa walifariki kwa pamoja kwenye ajali ya gari la familia. Kwa matukio hayo na kutosamehewa na mke na watoto, yule jamaa aliathirika kisaikolojia kiasi cha kuwa na dalili za maradhi ya akili.

Mojawapo ya dalili hizo ni hiyo ya kuhisi maumivu yasiyokuwepo.
Kwa kuwa ubongo ndio unaotafsiri maumivu, bila ubongo mtu hawezi kuhisi maumivu. Na endapo kuna athari katika sehemu ya ubongo inayotafsiri maumivu ya sehemu fulani ya mwili, basi kuna uwezekano mtu kupata maumivu sehemu hiyo ya mwili hata kama hakuna sababu katika sehemu husika, lakini kama kuna tatizo la kiakili/kwenye ubongo.

Dalili za aina hii hutokea kwa nadra. Mara nyingi huanza kwa hisia za kutambaliwa na mdudu mwilini wakati hakuna kitu (Tactile Hallucinations); kisha huweza kuendelea zaidi na kufikia kupata maumivu, kwa sababu za kisaikolojia.

Yule daktari alipogundua uwezekano wa maradhi ya akili kwa mtu yule, aliamua kubadili mbinu za kumsaidia. Alimpa ushauri, na uhakika wa kupona, na dawa za maumivu. Kisha akamualika nyumbani kwake kwa ajili ya chakula cha jioni.

Siku fulani jioni, yule jamaa alifika nyumbani kwa daktari wake. Daktari alimkaribisha na kuanza kupiga naye stori bila kumuuliza hali ya mkono wake. Stori nyingi zilikuwa za kuchekesha au kufurahisha. Baada ya muda, Daktari alimkaribisha yule jamaa ndani kwa ajili ya chakula, huku stori zikiendelea.

Kwa makusudi kabisa, Daktari alimkabidhi yule jamaa birika la chai, upande wake wa kulia wa yule jamaa, naye alipokea kwa mkono wa kulia (uliokuwa na maumivu) na kuanza kumimina chai kwenye kikombe. Wakati jamaa akiendelea kumimina chai, kulikuwa na ukimya, lakini daktari alikuwa akitazama ule mkono kwa mshangao kidogo.

Yule jamaa alipogundua daktari anautazama mkono wake, mara moja mkono ukaanza kuuma, akaliachia lile birika la chai na kuanza kupiga kelele za maumivu.

Tendo hilo liliweza kumpatia majibu ya uhakika daktari, kwamba maumivu yale yalisababishwa na maradhi ya kisaikolojia.

Saikolojia ni elimu pana sana. Ndio daraja linalounganisha imani na sayansi, na ndio ukuta unaotenganisha mambo hayo mawili.
Tazama wagonjwa wa akili wanaozurura barabarani na kula takataka chafu lakini wanaendelea kuishi. Kula wewe unayejua kuwa ni uchafu uone kitakachotokea.

Umewahi kubanwa na tumbo la kuendesha? Fikiria unavyokaribia chooni na hali unayoisikia, kadiri unavyokikaribia choo, hali inakuwa mbaya zaidi. Lakini ukikuta kuna mtu bado unaweza kuvumilia, huyo mtu akitoka hali inaanza kuwa mbaya zaidi wakati unaingia kujisaidia. Ukichelewa tu unachafua nguo.

Wamasai na jamii nyingine wanaishi na kupishana na simba porini, ni saikolojia.
Mtoto mdogo anayetambaa anacheza na nyoka, ni saikolojia.

Saikolojia inaathiri sana maisha yetu, uchumi wetu, afya zetu na mahusiano yetu.
Cha msingi ni kujifunza kwamba; kuna nguvu kubwa katika ubongo wa binadamu. Nguvu hiyo ni kubwa kuliko mbingu na ardhi kwa pamoja.

Ndio nguvu inayobadili mambo madogo kuwa makubwa na makubwa kuwa madogo. Ndio nguvu inayofanya ya muhimu yasiwe muhimu na yasio muhimu yawe na umuhimu mkubwa.
Itaendelea.

Christopher Cyrilo
 
Back
Top Bottom