Siyo siri tena kwamba bunge sasa limekandamizwa na nguvu toka juu.
Ukiniuliza sababu za kujiuzulu kwa mwenyekiti (Hawa Ghasia) na makamu wake ktk kamati ya bajeti jawabu litakuwa ni rahisi tu...
"Sakata la Korosho".
Kama mtakumbuka sakata hili lilipelekea nguvu toka juu kutishia kuwatwanga mashangazi wa kusini.
Sasa nguvu kutoka juu imeamua kumsukuma nje kinara wa sakata hili Hawa Ghasia. Na bado haitaishia hapo. Nimetonywa kwamba kila aliye lishadadia sakata hili nguvu kutoka juu itamshughulikia 2020.
Siyo mara ya kwanza kwa nguvu toka juu kuwafyeka wenyeviti wa kamati za bunge. Bado tunawakumbuka Dr Kafumu (mwenyekiti) na makamu wake Vicky Kamata amabao wallikwaza nguvu toka juu kwa kupanga mpango wa kumtembelea mbunge mwenzao G. Lema akiwa gerezani Kisongo.
Nguvu kutoka juu imelikamata bunge kweli kweli .
Hivi Nape Moses hana kamati yoyote huko?