Nguo ya kuazima haisitiri matako"Vyeti vya kununua, au feki"

PRINCEHOPE

Member
Aug 28, 2013
92
67
Kuna dogo nilisoma naye shule ya msingi, mkoa fulani, yeye maksi hazikutosha akaenda Private School, Mimi nikachaguliwa kuendelea na elimu karibu na bure. Sasa maisha yamesonga, Dogo form four marks zikatosha akaenda kujiunga na shule moja maarufu na kongwe mkoani Tanga. Dogo akasoma term moja tu, ya pili wakati wa kwenda akakunja kuelekea Dar, akakutana na vijana wakamla hela zote, akauza na alivyokuwa navyo. Mama yake akamtumia nauli ya kurudi mkoani, na aliporudi akaulizwa kulikoni kutokwenda shule, jibu alilotoa ni kuwa walimu hawapo, akimaanisha waliopo hawafundishi. Basi mama yake, akasitisha zile jitihada za kumuendeleza kielimu. Dogo akaanza kuishi maisha aliyoyachagua, kamali, pool table n.k. akaja kuuza cheti cha Form Four, ambapo ndiyo kiini cha mada yangu. Aliyemuuzia, akakitumia kwenda kusoma nursing, akapata kazi. Mwajiri wake hiyo mnunuzi wa cheti na wangu akawa mmoja, Kimbembe kwenye jina sasa, lile jina likawa lina click kichwani kwangu, maana namjua mmiliki. Nikashindwa kuvumilia, nikamuuliza ndugu, huyu mwenye jina namfahamu, vipi, akajibu kuwa ni mtoto wa baba mkubwa, ila majina wazazi waliamua kutupa yanayofanana tu. Nikaridhika kwa sehemu, ila nikawa naendelea kufuatilia. Ohoo, si serikali ya awamu ya tano ilipoanza kufukunyua vyeti vya taaluma, yale dada kasepa, na hajulikani alipo. Jamani tusisitizane kila mtu kwa nafasi yake kama kuna ndugu, wasome na wamiliki vyeti vyao, hata kama kaxungusha, si yake Bwana. Ni bora kuwa na kisepe ukajifunga vizuri, maadamu ni chako hakuna mtu atakayekuja kukuvua, kuliko ukaazima nguo ya mtu, akaja kukuvua mbele za watu.
 
Huyo dada alikuwa anatumia cheti cha kijana wa kiume?,au yale majina yetu Bahati,Riziki nk?...yaani unauza cheti?,huyo dogo itabidi afanyiwe brain surgery,atakuwa na uvimbe tu kichwani...
 
Hivi nini haswa hatima ya hawa walio fanyiwa ukaguzi ...na vyeti vyao vibovu na wakaambiwa waendelee kupiga jobu
 
Yeah mkuu,siku hizi humu kumejaa story za kutunga mno.
Muuzaji wa cheti ni mwanaume, mnunuzi ni mwanamke, na ndiyo majina yetu ya kibantu" Bahati, Shukuru, Ahsante, Matatizo " na wala siyo ya kutunga. Ila silazimishi mtu aamini, kwa watu wa Fasihi wanaangalia msisitizo wa mwandishi, na msisitizo wangu siyo jinsia, Bali ni kushawishi watu wasome, wasitegemee kununua vyeti ama kughushi. Ahsante kwa mlioelewa
 
Mi kuna jamaa nmemaliza nae f4 akapata 26 dv 4, hakpata hata chuo walimu, mi nilipata dv 2 point 18, alikua ananifata kabsa kwenye kukaa, aliuza chet 3m akanunua bodaboda! Jamaa kapata gap jwtz maana alikua na Mkubwa huyo aliyenunua chet, kajenga kjjn kwao Nyumba kama 3 hv za maana na gari kama kawaida nayo nzr tu, sasa sijui kama katumbuliwa au bado anakula nchi!

Watu kweli walikua wananunua na wanapga gap ktk maisha, maana Nepotism ilikuwa ndo dhamana!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom