Alexander The Great
JF-Expert Member
- Aug 28, 2018
- 4,502
- 23,581
Edson Arantes Nascimento "Pele" ambae ni "TUNU" kwa taifa la brazil na mchezaji pekee alieshinda "WORLD CUP" kwa mara tatu (1958, 1962, 1970) anatambulika kwa wengi kama ndio mchezaji bora ambae hajawahi kutokea katika historia ya mpira wa miguu.
Anapitia wakati mgumu kutokana na "MSONGO WA MAWAZO (DEPRESSION)", kufikia hatua hawezi "KUTEMBEA WALA KUTOKA NJE YA NYUMBA YAKE". Mwanae wa kiume Edinho amesema katika mahojiano na vyombo vya habari kua Baba yake mwenye umri wa miaka 79 "Amedhoofika sana, kupelekea mawazo yanamfanya ashindwe hata kutembea kawaida, hasa akiwaza (Pele) kuwa yeye ni mfalme wa mpira wa miguu na mfano wa kuigwa, hilo jambo linamfanya kuwa na aibu kuonekana mbele ya hadhara".
Mwezi April mwaka jana Pele alilazwa muda mfupi baada ya kuonekana nchini ufaransa (Paris) na mchezaji chipukizi Kylian Mbappe.
Ikumbukwe Pele ni miongoni mwa wanaadamu wanaoishi na Figo (Kidney) moja tu, baada ya kupoteza figo moja wakati akicheza mpira na kuvunjika mbavu ilioharibu figo yake moja.
-Binaadamu hatujafa, hatujaumbika. Licha ya vyeo na pesa mwanadamu anazokua nazo, pindi muda ukifika hazitamsaidia.
Anapitia wakati mgumu kutokana na "MSONGO WA MAWAZO (DEPRESSION)", kufikia hatua hawezi "KUTEMBEA WALA KUTOKA NJE YA NYUMBA YAKE". Mwanae wa kiume Edinho amesema katika mahojiano na vyombo vya habari kua Baba yake mwenye umri wa miaka 79 "Amedhoofika sana, kupelekea mawazo yanamfanya ashindwe hata kutembea kawaida, hasa akiwaza (Pele) kuwa yeye ni mfalme wa mpira wa miguu na mfano wa kuigwa, hilo jambo linamfanya kuwa na aibu kuonekana mbele ya hadhara".
Mwezi April mwaka jana Pele alilazwa muda mfupi baada ya kuonekana nchini ufaransa (Paris) na mchezaji chipukizi Kylian Mbappe.
Ikumbukwe Pele ni miongoni mwa wanaadamu wanaoishi na Figo (Kidney) moja tu, baada ya kupoteza figo moja wakati akicheza mpira na kuvunjika mbavu ilioharibu figo yake moja.
-Binaadamu hatujafa, hatujaumbika. Licha ya vyeo na pesa mwanadamu anazokua nazo, pindi muda ukifika hazitamsaidia.