kilam
JF-Expert Member
- Aug 5, 2011
- 2,092
- 2,126
Sio kweli, Somalia ni jamii moja na lugha yao moja lakini wanapigana.Kitu chochote kinacholeta matatizo katika jamii au kuwafanya watu watengane, wachukiane na kupigana ni kitu kibaya bila kujali nani amekileta.
Ukabila ni chimbuko letu waafrika, lakini katika nchi nyingi, ukabila umekua ndio chanzo cha mifarakano na mapigano, dini zimeletwa na wageni, lakini kuna baadhi ya nchi dini zimekua chanzo cha mifarakono na mapigano.
Pale ambapo makabila hayana athari mbaya kama Tanzania, sio vibaya kuendekeza na kutanguliza makabila, lakini kwa nchi kama Rwanda na Kenya, ni hatari sana kuachia ukabila kuzagaa mitaani kwasababu ni sawa na kumwaga Petrol katika nyasi kavu, lazima yatalipuka.
Huwezi kumwambia mtu akatae asili yake ili awe mtumwa wa identity bandia ya mzungu.
Lazima tukubali kuwa sisi ni watu tofauti na historia zetu ni tofauti. Huwezi kulazimisha watu tofauti waishi pamoja kwa kupuuza tofauti zao.
Kwa nini hatupambani kuondoa dini za kigeni kwa sababu ni msingi wa matatizo mengi Afrika?