Antiqua"]Ndugu zangu, tumejadili sana habari za madini. Ni sawa, lakini Je vipi hawa watu wanaoanzisha NGO'S kusingizia watoto yatima? Hatuoni kwamba haya mashirika yametajirisha watu binafsi kuliko malengo yenyewe? Hawa yatima wanapata misaada mingi kupitia haya mashirika lakini matokeo yake wachache wanajinufaisha. Je hii inatofauti na hawa mafisadi. Mimi nawaweka kwenye page moja yenye malengo sawa mabaya ya kuharibu maendeleo yetu. Ukizingatia hizi NGO'S hazilipi kodi. Ebu tulichangie mawazo kidogo kwa wenye utafiti na hili.