Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Leonard Mubali, Kigoma
KAMATI Maalum ya Ushauri ya mkoa wa Kigoma imevunja ngome ya kisiasa ya mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe baada ya kupitisha mgawanyo wa majimbo katika wilaya za Kigoma na Kasulu.
Endapo mapendekezo ya kamati hiyo yataridhiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (RCC), ngome kuu ya mbunge huyo machachari wa Chadema na mahala alipozaliwa patamegwa na kuingizwa katika jimbo Kigoma Mjini linaloshikiliwa na mbunge wa CCM, Peter Selukamba.
Kutokana na mgawanyo huo Zitto ataathirika kwa kukosa kura 20,688 za wakazi wa kata ya Mwandiga ambao sasa wameondolewa kutoka Jimbo la Kigoma Kaskazini na kupelekwa katika jimbo jipya la Kigoma ambayo ni sehemu ya manispaa ya Kigoma Ujiji.
Mwaka 2005 Zitto alishinda ubunge katika jimbo la Kigoma Kaskazini baada ya kupata 28,198 akimbwaga kwa mbali mpinzani mkuu Halimeshi Mayonga wa CCM ambaye alipata kura 21,822. Sehemu kubwa ya ushindi wa Zitto ulipatikana katika kata ya Mwandiga
Wagombea wengine walioshiriki uchaguzi huo na kura zao kwenye mabano ni Matete Kaseba wa CUF (3,73 na Kassim Wamala wa DP (49).
Kutokana na mabadiliko hayo, kuna uwezekano mkubwa Zitto kwenda kugombea Kigoma Mjini na hivyo kuweka nafasi ya Selukamba katika hali tete.
Wachambuzi wengine wa mambo wanadai kwamba hatua ya RCC inaweza kumfanya Zitto kugombea jimbo mojawapo jijini Dar es Salaam ambako ana ushawishi mkubwa kutokana na kufanya kazi nyingi za kitaifa.
Akisoma maazimio ya kikao hicho ambacho hakikuhudhuriwa na mbunge mmoja yeyote wa mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Mkoa huo Joseph Simbakalia alisema, mkoa wa Kigoma sasa umependekezwa kuwa na majimbo 10 ya uchaguzi badala ya majimbo saba yaliyopo.
Katika manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa Jimbo la awali la Kigoma Mjini limegawanywa na kupatikana majimbo mawili ya Kigoma na Ujiji ambapo wapiga kura 54,701 kutoka jimbo la Kigoma Kusini litakalojulikana kama Jimbo la Malagarasi watahamia katika Jimbo la Ujiji.
Simbakalia alisema kuwa baada ya mapendekezo hayo kupitishwa na NEC, Halmashauri ya Wilaya Kigoma itakuwa na majimbo matatu ambayo ni Buhingu na Malagarasi (yaliyokuwa Jimbo la Kigoma Kusini) na Kalinzi (lililokuwa jimbo la Kigoma Kaskazini).
Kwa hali hiyo kupitishwa kwa mapendekezo hayo kunaifanya wilaya ya Kigoma kuwa na jumla ya majimbo matano ya uchaguzi kutoka majimbo matatu yaliyopo sasa.
Aidha, mapendekezo hayo yaliyopitishwa na kamati ya ushauri ya mkoa yameifanya wilaya Kasulu kuwa na majimbo matatu ambayo ni Kasulu Mjini, Kasulu Vijijini baada ya Jimbo la Kasulu Mashariki kugawanywa huku jimbo la Kasulu Magharibi likibaki kama lilivyo.
Hakuna mapendekezo yoyote yaliyotolewa na wilaya Kibondo katika mchakato huo wa kuongeza majimbo mkoani Kigoma na kwamba majimbo hayo kwa sasa yatabaki kama yalivyo.
Kama utetezi wao kuhusu kugawanywa kwa majimbo hayo Wakuu wa wilaya za Kasulu na Kigoma, wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri walisema kuwa mapendekezo yao yamelenga kupeleka uwakilishi karibu na wananchi na kufanya huduma muhimu na maendeleo kuwafikia kwa haraka.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kigoma John Mongela alisema kuwa kutekelezwa kwa mpango maalum wa kiuchumi kutaifanya manispaa ya Kigoma Ujiji kuwa na ongezeko kubwa la watu na shughuli ambazo zinahitaji usimamizi wa karibu wa kiutawala.
Sambamba na hilo alisema kuwa wakati Manispaa ya Kigoma Ujiji ikiwa hivyo sehemu ya Lugufu ya Halamshauri ya Wilaya Kigoma itakuwa na shughuli nyingi za kilimo ikiwa ni kituo muhimu cha kilimo mkoani Kigoma ambacho kitachangia ongezeko kubwa la watu katika wilaya hiyo.
KAMATI Maalum ya Ushauri ya mkoa wa Kigoma imevunja ngome ya kisiasa ya mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe baada ya kupitisha mgawanyo wa majimbo katika wilaya za Kigoma na Kasulu.
Endapo mapendekezo ya kamati hiyo yataridhiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (RCC), ngome kuu ya mbunge huyo machachari wa Chadema na mahala alipozaliwa patamegwa na kuingizwa katika jimbo Kigoma Mjini linaloshikiliwa na mbunge wa CCM, Peter Selukamba.
Kutokana na mgawanyo huo Zitto ataathirika kwa kukosa kura 20,688 za wakazi wa kata ya Mwandiga ambao sasa wameondolewa kutoka Jimbo la Kigoma Kaskazini na kupelekwa katika jimbo jipya la Kigoma ambayo ni sehemu ya manispaa ya Kigoma Ujiji.
Mwaka 2005 Zitto alishinda ubunge katika jimbo la Kigoma Kaskazini baada ya kupata 28,198 akimbwaga kwa mbali mpinzani mkuu Halimeshi Mayonga wa CCM ambaye alipata kura 21,822. Sehemu kubwa ya ushindi wa Zitto ulipatikana katika kata ya Mwandiga
Wagombea wengine walioshiriki uchaguzi huo na kura zao kwenye mabano ni Matete Kaseba wa CUF (3,73 na Kassim Wamala wa DP (49).
Kutokana na mabadiliko hayo, kuna uwezekano mkubwa Zitto kwenda kugombea Kigoma Mjini na hivyo kuweka nafasi ya Selukamba katika hali tete.
Wachambuzi wengine wa mambo wanadai kwamba hatua ya RCC inaweza kumfanya Zitto kugombea jimbo mojawapo jijini Dar es Salaam ambako ana ushawishi mkubwa kutokana na kufanya kazi nyingi za kitaifa.
Akisoma maazimio ya kikao hicho ambacho hakikuhudhuriwa na mbunge mmoja yeyote wa mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Mkoa huo Joseph Simbakalia alisema, mkoa wa Kigoma sasa umependekezwa kuwa na majimbo 10 ya uchaguzi badala ya majimbo saba yaliyopo.
Katika manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa Jimbo la awali la Kigoma Mjini limegawanywa na kupatikana majimbo mawili ya Kigoma na Ujiji ambapo wapiga kura 54,701 kutoka jimbo la Kigoma Kusini litakalojulikana kama Jimbo la Malagarasi watahamia katika Jimbo la Ujiji.
Simbakalia alisema kuwa baada ya mapendekezo hayo kupitishwa na NEC, Halmashauri ya Wilaya Kigoma itakuwa na majimbo matatu ambayo ni Buhingu na Malagarasi (yaliyokuwa Jimbo la Kigoma Kusini) na Kalinzi (lililokuwa jimbo la Kigoma Kaskazini).
Kwa hali hiyo kupitishwa kwa mapendekezo hayo kunaifanya wilaya ya Kigoma kuwa na jumla ya majimbo matano ya uchaguzi kutoka majimbo matatu yaliyopo sasa.
Aidha, mapendekezo hayo yaliyopitishwa na kamati ya ushauri ya mkoa yameifanya wilaya Kasulu kuwa na majimbo matatu ambayo ni Kasulu Mjini, Kasulu Vijijini baada ya Jimbo la Kasulu Mashariki kugawanywa huku jimbo la Kasulu Magharibi likibaki kama lilivyo.
Hakuna mapendekezo yoyote yaliyotolewa na wilaya Kibondo katika mchakato huo wa kuongeza majimbo mkoani Kigoma na kwamba majimbo hayo kwa sasa yatabaki kama yalivyo.
Kama utetezi wao kuhusu kugawanywa kwa majimbo hayo Wakuu wa wilaya za Kasulu na Kigoma, wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri walisema kuwa mapendekezo yao yamelenga kupeleka uwakilishi karibu na wananchi na kufanya huduma muhimu na maendeleo kuwafikia kwa haraka.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kigoma John Mongela alisema kuwa kutekelezwa kwa mpango maalum wa kiuchumi kutaifanya manispaa ya Kigoma Ujiji kuwa na ongezeko kubwa la watu na shughuli ambazo zinahitaji usimamizi wa karibu wa kiutawala.
Sambamba na hilo alisema kuwa wakati Manispaa ya Kigoma Ujiji ikiwa hivyo sehemu ya Lugufu ya Halamshauri ya Wilaya Kigoma itakuwa na shughuli nyingi za kilimo ikiwa ni kituo muhimu cha kilimo mkoani Kigoma ambacho kitachangia ongezeko kubwa la watu katika wilaya hiyo.