Ngome ya vijana ACT Wazalendo tumeiandikia barua Wizara ya Elimu kuhusu makato katika marekebisho ya mikopo elimu ya juu

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Ngome ya vijana Act-Wazalendo tumeendelea kuchukua hatua kadhaa wa kadhaa juu ya changamoto iliyopo katika marejesho ya mikopo elimu ya juu pamoja na sheria yake kuhusu viwango na masharti ya marejesho ya mikopo ya elimu ya juu.

Kama ambavyo mwenyekiti wa Vijana taifa Ndg Abdul Nondo alizungumza na vyombo vya habari kuhusu hili tarehe 14 /Januari/2021, akisema Ngome tumeazimia kuandika barua kwenda katika mamlaka za serikali ili serikali kuchukua hatua stahili.

Mnamo tarehe 20 Januari 202. Katibu wa Ngome ya vijana act wazalendo Ndg Mwanaisha Mndeme aliandika barua kwenda wizara ya Elimu-Dodoma yenye kichwa cha barua,

Serikali kufanya marejeo na tathimini mpya juu ya viwango na masharti ya marejesho ya mikopo elimu ya juu kupitia bodi ya mikopo na sheria yake

Nakala za barua hii zilipelekwa pia Ofisi ya Rais-Ikulu(kupitia Katibu mkuu kiongozi),Ofisi ya Waziri mkuu na Bodi ya mikopo elimu ya juu.Barua hizo zilipelekwa na viongozi wa Ngome ya vijana Petro Ndolezi Amir Khamis na Julius Massabo.

Mbali na barua hizo kupelekwa ofisini ,Ngome ya vijana ilizituma pia barua hizo kupitia email yake actwazalendovijana@gmail.com kwenda katika ofisi zote na kupokelewa.

Hizi ni hatua za awali tuu Ngome ya vijana tunafanya.Ikiwa hakuna hatua zozote zitakazo chukuliwa na serikali bado kuna njia ya ziada tutaifanya ya kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya sheria ya bodi ya mikopo kuvunja mkataba wa msingi (Student's Loan Agreement) kati ya muombaji (Mwanafunzi) na Bodi ya mikopo kwa kushirikiana na wadau ,Azaki na wahanga wa sheria hii.

Tunaendelea kupongeza Azaki mbalimbali ikiwemo kituo cha sheria na haki za binadamu, Wanaharakiti ,wahanga na wanafunzi kwa pamoja wanavyoendelea kupaza sauti kwa pamoja dhidi ya sheria hii .

Ngome ya vijana Act wazalendo tutaendelea kupigania,maslahi ya msingi ya vijana na jamii kwa ujumla dhidi ya uonevu na hata kupokonywa haki.

Imetolewa Na
Idara Ya Habari Uenezi na Mawasiliano kwa Umma
Ngome ya Vijana Taifa.
22/01/2021.

IMG-20210122-WA0063.jpg
IMG-20210122-WA0064.jpg
IMG-20210122-WA0065.jpg
 
Kwani Maalim hajamwambia Magufuli alipoenda Chato?
 
Mwenyekiti wenu ACT Wazalendo taifa anafanyakazi na CCM huko visiwani.

Wapinzani wengine mko Kama popo hamueleweki.

Chadema. Nyumbu

ACT- Wazalendo......Popo
 
Ni Jambo jema kiongozi.

Yaani makubaliano ni 8% mara paaaap 15%. Inauma sana kwa kila mwenye akili timamu zenye hofu ya Mungu.
 
Nyie vijana wa ACT mna akili?
Mnadhani sheria itabadilishwa kwa kuandika barua wizarani au bodi, viongozi wa Africa huwa hawaelewi huo upuuzi.

Kama mpo serious hamasisheni mapooza yote yaliyopo nchini ambayo mnayaita vijana ili yadai haki yao kwa nguvu na kupaza sauti. Siyo hivyo vikaratasi.

ACHENI MAIGIZO
 
Dictator huwa haogopi mahakama bali huogopa nguvu ya umma tu. Anyway fuatilieni tuone kama kuna lolote la maana litapatikana, lakini ccm hawana hofu yoyote na ACT.
 
Mwenyekiti Maalim anafahamu hilo!?
Wenzako wako kwenye kuliponya taifa.
Wewe upo mitandaoni?
By the way wakutafutie hata ukatibu tarafa huko ujiji nawe uende kwenye juhudi za kuliponya taifa.
 
Ngome ya vijana Act-Wazalendo tumeendelea kuchukua hatua kadhaa wa kadhaa juu ya changamoto iliyopo katika marejesho ya mikopo elimu ya juu pamoja na sheria yake kuhusu viwango na masharti ya marejesho ya mikopo ya elimu ya juu.

Kama ambavyo mwenyekiti wa Vijana taifa Ndg Abdul Nondo alizungumza na vyombo vya habari kuhusu hili tarehe 14 /Januari/2021, akisema Ngome tumeazimia kuandika barua kwenda katika mamlaka za serikali ili serikali kuchukua hatua stahili.

Mnamo tarehe 20 Januari 202. Katibu wa Ngome ya vijana act wazalendo Ndg Mwanaisha Mndeme aliandika barua kwenda wizara ya Elimu-Dodoma yenye kichwa cha barua,

Serikali kufanya marejeo na tathimini mpya juu ya viwango na masharti ya marejesho ya mikopo elimu ya juu kupitia bodi ya mikopo na sheria yake

Nakala za barua hii zilipelekwa pia Ofisi ya Rais-Ikulu(kupitia Katibu mkuu kiongozi),Ofisi ya Waziri mkuu na Bodi ya mikopo elimu ya juu.Barua hizo zilipelekwa na viongozi wa Ngome ya vijana Petro Ndolezi Amir Khamis na Julius Massabo.

Mbali na barua hizo kupelekwa ofisini ,Ngome ya vijana ilizituma pia barua hizo kupitia email yake actwazalendovijana@gmail.com kwenda katika ofisi zote na kupokelewa.

Hizi ni hatua za awali tuu Ngome ya vijana tunafanya.Ikiwa hakuna hatua zozote zitakazo chukuliwa na serikali bado kuna njia ya ziada tutaifanya ya kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya sheria ya bodi ya mikopo kuvunja mkataba wa msingi (Student's Loan Agreement) kati ya muombaji (Mwanafunzi) na Bodi ya mikopo kwa kushirikiana na wadau ,Azaki na wahanga wa sheria hii.

Tunaendelea kupongeza Azaki mbalimbali ikiwemo kituo cha sheria na haki za binadamu, Wanaharakiti ,wahanga na wanafunzi kwa pamoja wanavyoendelea kupaza sauti kwa pamoja dhidi ya sheria hii .

Ngome ya vijana Act wazalendo tutaendelea kupigania,maslahi ya msingi ya vijana na jamii kwa ujumla dhidi ya uonevu na hata kupokonywa haki.

Imetolewa Na
Idara Ya Habari Uenezi na Mawasiliano kwa Umma
Ngome ya Vijana Taifa.
22/01/2021.

Mwanaharakati Abdul Nondo,

Nakupongeza kwa ngome ya vijana wa chama chako cha kisiasa kubeba malalamiko ya baadhi ya wanufaika wa mkopo wa elimu ya juu na waathirika wa marejesho ya mkopo huo kutoka serikalini ambao chanzo chake ni kodi za wananchi.

Hata hivyo, pamoja jitihada hizo za kuwapigania kundi nufaika na athirika nimeona kuna mapungufu mengi sana ya kiuandishi,kiweledi na kushindwa kujenga hoja yenye ushahidi dhahiri.

Uwasilishaji wa barua hiyo kwenda kwenye bodi ya mikopo, na durusu kuelekezwa kwenye ofisi ya ya Rais na Waziri mkuu haina nguvu ya kisheria ila imeshamiri maneno ya kiuanaharati tupu ambao unaharibu taswira ya suala hili kwamba ni la muhimu kwa ustawi wa wanufaika na waathirika.
1. Kwanza kwenye barua hii imenukuu ibara ya 23(1) ya katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuipa nguvu hoja inayosadifu mtu kupata ujira kulingana na kazi yake,; kwamba baada ya serikali kufanya marekebisha ya sheria inayohusu mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ya mwaka 2016 imesababisha uvunjifu wa makubakliano ya mktaba kati ya mwanafunzi na mtoa mkopo (Student's Loan Agreement). Hata hivyo hapa umeshindwa kutaja ni vifungu gani vya sheria vimeleta athari kuliko kupiga kulalamika kiujumla ikiimaanisha sheria nzima ifutwe!!! Haya ni maajabu, kweli hakuna mwanasheria bora wa kubaini upungufu huu kabla ya kuandika barua ndefu isyo na kigoda cha kuketia kitako?

2. Pili, kwenye barua hiyo anbayo imekosa uvuvio inadai kwamba utungwaji wa sheria yoyote huwa haifanyi kazi kinyume yaani kwa kiingereza chako "..The Law doesn't work retrospectively", isipokuwa tu huanzia pale inapopitishwa na watunga sheria na kusainiwa na Rais kwa matumizi.

*Nakupa pole sana kudhani kwamba siku zote sheria huwa haifanyi kazi kinyume nyume kwa matendo yaliyotenda kabla ya uwepo wake, huo ni uwongo kwa mantiki ya kwamba hiyo kauli hujaipa nguvu ya ushahidi (There is no substantative evidence with objective case study reference attached to reasonably support the argument being merited). Ili sheria iendane na nadharia ya uelewa wako mdogo kwamba sheria haifanyi kazi kinyume nyume ni sharti sheria mpya itamke kwenye kifungu kwamba sheria hiyo kuanzia muda huo ilipoidhinishwa na kuendelea mbele, lakini kama iko kimya itatekelezwa kwa kugusa matendo yaliyotokea kabla ya uwepo wa sheria hiyo.

The retrospective perception as it was envisaged in the letter was an absolute disinformative, misinformative and malinformative misleading the addressee and readers on social media audience because it targetedly focussed to define on one side only as taking away or impairing any vested right acquired under existing laws, or creating a new obligation, or imposing a new duty, or attaching a new disability in respect to transactions or considerations already in the past.

Kwa taarifa yako hata huko USA federal laws, UK & Wales wana sheria retrospective/retroactive ambazo zipo kwa nia ya kurekebisha matendo yaliyotokea nyuma kabla ya sheria mpya. Wanaharakati kama wewe walishawahi kupeleka mashauri kama haya katika mahama za juu kupata tafsiri na kwa ombi la kufutwa kwa madai ya kukiuka Article 1 section 9 & 10. Lakini Mahakama ya juu (Supreme Court ilitupilia mbali madai hayo na sababu za mantiki zilitolewa naomba ninukuu kwa uchache kwa ung'eng'e "...‘nova constitutio futuris formam imponere debet, non prœteritis’, that is unless there be clear words to the contrary statutes ‘do not apply to a past, but to a future, state or circumstance3......."

From the very beginning the author of the USA constititution clearly found out that it was abhorent to pass any legislation that was retrospective becuase it woukld violate the article I section 9 & 10 that prohibited the federal government and state governments to enact any ex post facto law, and section 10 specifically imposes the ban on passing any law 'impairing the obligation of contracts', however, the Supreme Court ruled that despite Article I, retrospective/retroactive legislation is not necessarily UNCONSTITUTIONAL.........A.D.Woozley

Barua imeheni malalamiko ya makato mengi na ukosefu wa ajira kwa kuituhumu serikali kushindwa kutengeneza mazingiara wezeshi upatikanaji wa ajira kwa vijana wanaohitimu vyuo vikuu. Hapa nafikiri ninyi wanaharakati mnafanya utani wa kisiasa uchwara kama kwaida zenu kwa nia ya kutafuta uungwaji mkono na wadau wa suala husika.

Tuweke kipengele kilichomo kwenye mkataba kati ya mwanafunzi kama mnufaika mkopo na mkopeshaji yaani serikali ambacho kinataka endapo kuna mabadiliko yoyote ya sheria ni sharti wakutane kujadiliana kama kulikuwa na ulazima wa kupandisha asilimia ya makato baada ya miaka miwili tangu mnufaika ahitimu chuo ili tujue kumbe kweli kulikuwa na ukiukwaji wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo. Kinyume na hapa ni kupiga mbinja zisizo na lengo jema ila kuleta taharuki kwa manufaa binafsi.
 
Kijana acheni kumsumbua Seif
Ngome ya vijana Act-Wazalendo tumeendelea kuchukua hatua kadhaa wa kadhaa juu ya changamoto iliyopo katika marejesho ya mikopo elimu ya juu pamoja na sheria yake kuhusu viwango na masharti ya marejesho ya mikopo ya elimu ya juu.

Kama ambavyo mwenyekiti wa Vijana taifa Ndg Abdul Nondo alizungumza na vyombo vya habari kuhusu hili tarehe 14 /Januari/2021, akisema Ngome tumeazimia kuandika barua kwenda katika mamlaka za serikali ili serikali kuchukua hatua stahili.

Mnamo tarehe 20 Januari 202. Katibu wa Ngome ya vijana act wazalendo Ndg Mwanaisha Mndeme aliandika barua kwenda wizara ya Elimu-Dodoma yenye kichwa cha barua,

Serikali kufanya marejeo na tathimini mpya juu ya viwango na masharti ya marejesho ya mikopo elimu ya juu kupitia bodi ya mikopo na sheria yake

Nakala za barua hii zilipelekwa pia Ofisi ya Rais-Ikulu(kupitia Katibu mkuu kiongozi),Ofisi ya Waziri mkuu na Bodi ya mikopo elimu ya juu.Barua hizo zilipelekwa na viongozi wa Ngome ya vijana Petro Ndolezi Amir Khamis na Julius Massabo.

Mbali na barua hizo kupelekwa ofisini ,Ngome ya vijana ilizituma pia barua hizo kupitia email yake actwazalendovijana@gmail.com kwenda katika ofisi zote na kupokelewa.

Hizi ni hatua za awali tuu Ngome ya vijana tunafanya.Ikiwa hakuna hatua zozote zitakazo chukuliwa na serikali bado kuna njia ya ziada tutaifanya ya kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya sheria ya bodi ya mikopo kuvunja mkataba wa msingi (Student's Loan Agreement) kati ya muombaji (Mwanafunzi) na Bodi ya mikopo kwa kushirikiana na wadau ,Azaki na wahanga wa sheria hii.

Tunaendelea kupongeza Azaki mbalimbali ikiwemo kituo cha sheria na haki za binadamu, Wanaharakiti ,wahanga na wanafunzi kwa pamoja wanavyoendelea kupaza sauti kwa pamoja dhidi ya sheria hii .

Ngome ya vijana Act wazalendo tutaendelea kupigania,maslahi ya msingi ya vijana na jamii kwa ujumla dhidi ya uonevu na hata kupokonywa haki.

Imetolewa Na
Idara Ya Habari Uenezi na Mawasiliano kwa Umma
Ngome ya Vijana Taifa.
22/01/2021.

 
Back
Top Bottom