Uchaguzi 2020 Ngome kuu za CCM (Kanda ya Kati na Kanda ya Ziwa) walizokuwa wakizitegemea zimetikiswa

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Kwenye uchaguzi mkuu uliopita wa 2015 CCM ilipata kura 8,882,935 za urais, karibu nusu ya kura zote zilitoka kanda ya Ziwa na kanda ya Kati.

CCM ilipata kura 3,638,623 kutoka mikoa 9 tu ya Dodoma, Singida, Tabora, Mwanza, Geita, Mara, Simiyu, Kagera na Shinyanga, huku CHADEMA ikiambulia kura 1,724,569 kwenye kanda hizo kati ya kura 6,072,848 za urais walizopata 2015.

Pamoja na kuwa ngome kuu za CCM, lkn mwaka huu hadi sasa kupitia kampeni zake, CHADEMA imeonekana kufanya vizuri kwenye mikoa hiyo, huku ikiwa bado na uhakika wa kupata kura zaidi kwenye ngome zake za mikoa ya Kanda ya Kaskazini (Kilimanjaro, Arusha, na Manyara) na Mikoa ya nyanda ya juu Kusini (Mbeya, na Iringa).

Hadi sasa kimikakati bado CHADEMA inaongoza kwa kushambulia ngome za mpinzani wao wa karibu CCM kwa muda mrefu, nafikiri ‘strategist’ wao aliwashauri vizuri.

Nyanda zingine za Mashariki (DSM, Pwani, Morogoro na Tanga), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma, Katavi) na Zanzibar ni kanda ambazo kura zake bado zimegawanyika kwa vyama vyote vikuu yaani CCM, CHADEMA na ACT.

Hii ni tathimini yangu kwa mikakati inayoonekana wazi ya awamu ya kwanza ya kampeni iliyofikisha mwezi mmoja tangu kuzinduliwa trh 26/8. Matarajio mabadiliko machache kutokea tunapokaribia siku ya uchaguzi.

DODOMA,
CCM (516,317); CHADEMA (157,623).
SINGIDA,
CCM (290,899); CHADEMA (112,342).
TABORA,
CCM (413,492); CHADEMA (181,213).
MWANZA,
CCM (584,184); CHADEMA (311,532).
KAGERA,
CCM (475,910); CHADEMA (287,538).
GEITA,
CCM (377,051); CHADEMA (157,440).
SIMIYU,
CCM (318,358); CHADEMA (163,319).
MARA,
CCM (335,476); CHADEMA (221,382).
SHINYANGA,
CCM (326,936); CHADEMA (132,180).
 
Pamoja na kuwa ngome kuu za CCM, lkn mwaka huu hadi sasa kupitia kampeni zake, CHADEMA imeonekana kufanya vizuri kwenye mikoa hiyo, huku ikiwa bado na uhakika wa kupata kura zaidi kwenye ngome zake za mikoa ya Kanda ya Kaskazini (Kilimanjaro, Arusha, na Manyara) na Mikoa ya nyanda ya juu Kusini (Mbeya, na Iringa).
Kaskazini kwa sasa hawana Chao ilikuwa ngome ya Slaa,Lowasa na Ndesamburo ambao wote kwa sasa hawapo .Ndesamburo mwamba wa Kilimanjaro alifariki Lowasa na Slaa na makundi yao walisharudi CCM

Mbeya na Iringa unaongelea mbeya mjini na iringa mjini tu wilaya zingine hamna kitu
 
Umeandika nilichokuwa nakiwaza wiki nzima hii. Nimekuwa nikitafakari route ya Lissu, nikajiuliza, tangu alivyotoka Mbeya kwa nini jamaa amejikita kuzunguka nchi kupitia mipakani, Mbeya, akapita kwa Pinda, akapanda hadi Kigoma, akaenda Kagera, kapita Mwanza, Mara na sasa anamalizia Tarime. Kwa ufupi kaizunguka nchi. Kama ni vitani, basi ameamua kumzunguka adui yake ambaye amejificha hapo Dodoma.
 
Kaskazini kwa sasa hawana Chao ilikuwa ngome ya Slaa,Lowasa na Ndesamburo ambao wote kwa sasa hawapo .Ndesamburo mwamba wa Kilimanjaro alifariki Lowasa na Slaa na makundi yao walisharudi CCM

Mbeya na Iringa unaongelea mbeya mjini na iringa mjini tu wilaya zingine hamna kitu
Kaskazini bado itabaki kuwa ngome ya Chadema hata baada ya Slaa, Lowassa mwenyewe aliikuta na ameiacha kama ilivyo.
 
Kaskazini bado itabaki kuwa ngome ya Chadema hata baada ya Slaa, Lowassa mwenyewe aliikuta na ameiacha kama ilivyo.
Sio kweli Watu watatu ndio walikuwa mhimili wa hiyo kanda Lowasa, Slaa na Ndesamburo mtakiona cha mtema kuni tarehe 28 October

Dar es salaam wana Dar wameshawashia Taa za hazard na ving'ora kuwa chadema hamna chenu Dar

Uzinduzi wenu mliona ulivyodorora Dar hadi aibu
 
Umeandika nilichokuwa nakiwaza wiki nzima hii. Nimekuwa nikitafakari route ya Lissu, nikajiuliza, tangu alivyotoka Mbeya kwa nini jamaa amejikita kuzunguka nchi kupitia mipakani, Mbeya, akapita kwa Pinda, akapanda hadi Kigoma, akaenda Kagera, kapita Mwanza, Mara na sasa anamalizia Tarime. Kwa ufupi kaizunguka nchi. Kama ni vitani, basi ameamua kumzunguka adui yake ambaye amejificha hapo Dodoma.
Sasa akivamia dodoma singida tabora ndo Basi tena,

Nashauri wiki ya mwisho atumie chopa kwa majimbo ambayo hakufika
 
Umeandika nilichokuwa nakiwaza wiki nzima hii. Nimekuwa nikitafakari route ya Lissu, nikajiuliza, tangu alivyotoka Mbeya kwa nini jamaa amejikita kuzunguka nchi kupitia mipakani, Mbeya, akapita kwa Pinda, akapanda hadi Kigoma, akaenda Kagera, kapita Mwanza, Mara na sasa anamalizia Tarime. Kwa ufupi kaizunguka nchi. Kama ni vitani, basi ameamua kumzunguka adui yake ambaye amejificha hapo Dodoma.
Kazunguka nchi au kazunguka mijini?
 
Sio kweli Watu watatu ndio walikuwa mhimili wa hiyo kanda Lowasa, Slaa na Ndesamburo mtakiona cha mtema kuni tarehe 28 October

Dar es salaam wana Dar wameshawashia Taa za hazard na ving'ora kuwa chadema hamna chenu Dar

Uzinduzi wenu mliona ulivyodorora Dar hadi aibu
Dar itawashangaza tangu kuanza kwa uchaguzi wa vyama vingi haijawahi kuwa CCM.
 
Huna tofauti na yule anayetaka kuwekeza shilingi laki nne na apate faida milioni kumi na nane kwenye kilimo cha matikiti maji.pole sana.
 
Sio kweli Watu watatu ndio walikuwa mhimili wa hiyo kanda Lowasa, Slaa na Ndesamburo mtakiona cha mtema kuni tarehe 28 October

Dar es salaam wana Dar wameshawashia Taa za hazard na ving'ora kuwa chadema hamna chenu Dar

Uzinduzi wenu mliona ulivyodorora Dar hadi aibu
Kabla ya campaign mlikuwa mnasema Cdm imekufa !!. Leo unaipa baadhi ya mikoa ! Kulikoni ?!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom