Ngoma za kisukuma special thread

Shy land

JF-Expert Member
Jul 28, 2013
6,024
1,959
Nyimbo za kisukuma zimekuwa zikipigwa sana maeneo mbalimbali na kona zote za nchi, na kwenye maharusi, kumbi za starehe na kwenye ndoa za watu wote nchini.

Huu uzi utakuletea majina ya wasanii na ngoma zote nzuri zinazopedwa mda Wote. wasanii kama GUDEGUDE, LIMBU LUCHANGULA, BHUNDAGALA, BAHATI BHUGALAMA, KISIMA, MAMA USHAURI, MWANAKANG'WA, NGELELA. nakuja
 
Nilikua shule fln hv huko mikoa ya pwan kwenye mahafali ya kidato cha sita. Kumbe bwana wanafunzi wameandaa ngoma ya kisukuma kama burudanj mojawapo. Kuna ngoma fln hv maarufu sana, goma lilipoanza tu nlishangaa kuona wageni waalikwa wawili wenye nyadhifa za juu tu, mmoja wa kike na mwingine wa kiume kwa timing tofauti tofauti wanaingia jukwaani pale kuimba na kucheza pamoja na wale wanafunzi.

Ilikua ni bonge la vibe, hizi ngoma za kitamaduni zina vibe fln asikwambie mtu especially kama ulizisikiliza kpnd unakua.


Kwa wahaya kuna hiii "Mtoro" ikiwepo kwenye sherehe watu husahau hata vyeo vyao na kujirusha
 
Nyimbo za kisukuma zimekuwa zikipigwa sana maeneo mbalimbali na kona zote za nchi, na kwenye maharusi, kumbi za starehe na kwenye ndoa za watu wote nchini.

Huu uzi utakuletea majina ya wasanii na ngoma zote nzuri zinazopedwa mda Wote. wasanii kama GUDEGUDE, LIMBU LUCHANGULA, BHUNDAGALA, BAHATI BHUGALAMA, KISIMA, MAMA USHAURI, MWANAKANG'WA, NGELELA. nakuja
Nyimbo za Gude Gude na Ntemi O'Mabala ndo zimenifanya nikijue vizuri Kisukuma. Mwingine ninayempenda ni Kisima (Nyanda Majaba) ila Kisukuma chake kigumu, huwa ananiacha jangwani...
 
Wabeja sana ongwise..huwa nafurahi nikienda home ni mwendo wa nyimbo za kisukuma tu..nimezimis sana huku pwani tunasikiliziswa singeli kwa lazima.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kisima, Gude Gude, Nelemi Mbasando, Bahati bhugarama, Ng'wana kang'wa, Limbu, Bhudagala ila kwa Sasa tuko Nzuki, Lugulu na Mwana majaliwa
 
Back
Top Bottom